Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,955
- 22,130
na Amos Nyaigoti
WAFANYAKAZI tisa waliokuwa waajiriwa wa Kampuni ya simu za mikononi ya Zain, wameishitaki menejimenti ya kampuni hiyo katika Mahakama ya Kazi jijini Dar es Salaam, wakidai fidia ya sh milioni 412, kama malipo ya stahili zao pamoja na malipo ya adhabu kwa kampuni hiyo.
Wakizungumza jana na Tanzania Daima Jumatano, kupitia wakili wao, Tundu Lissu, alisema kuwa wateja wake waliachishwa kazi kwa madai ya kuyumba kwa uchumi na shauri hilo linapingwa vikali na wafanyakazi hao ambao waliamua kuishitaki kampuni hiyo mahakamani.
Sheria inamtaka mwajiri mara tu anapofikiria kuwapunguza wafanyakazi wake ni lazima awataarifu kwa maandishi na kuwapa vigezo vya upunguzaji huo, ikiambatana na malipo yao, ambapo hilo halikufanyika, alisema Lissu.
Lissu alidai kuwa wateja wake walifukuzwa si kwa sababu za kiuchumi kama walivyodai bali chuki ya kumpuni kwa wafanyakazi hao, kwa kuwa mwaka jana Zain iliongeza asilimia 50 ya wafanyakazi.
Alisema mapato ya kampuni hiyo yaliongezeka kwa asilimia 30 mwaka jana kama faida na kuifanya kampuni hiyo iongoze kwa mapato barani Afrika kwa kampuni zote za Zain.
Alisisitiza kuwa wateja wake walifukuzwa kwa chuki kwani siku ya tukio, watano kati yao walikuwa wamepangiwa safari za mikoani na waliporipoti ofisini walipewa barua za kufukuzwa kazi, huku wawili kati yao wakipewa taarifa ya kufika makao makuu Dar es Salaam kutoka Iringa kwenye mkutano na walipofika walipewa barua za kufukuzwa kazi.
Lissu alieleza zaidi kuwa wateja wake walituhumiwa kukiuka taratibu za ofisi ambapo kampuni ilishindwa kuthibitisha hilo na kumfukuza kazi mmoja wa watumishi hao.
Wote kwa pamoja baada ya kupewa barua hawakuruhusiwa kuingia ofisini na malipo yao yalienda kulipia madeni yao katika Benki ya Kenya Commercial Bank (KCB) ambapo ni kinyume cha sheria za kazi. Wafanyakazi hao wanaiomba mahakama itoe tamko kuwa walifukuzwa kazi kinyume cha sheria, warudishwe kazini kwa nafasi zilezile na mahakama iamuru walipwe mishahara na malipo yote kwa kipindi chote walichosimamishwa kazi. Kesi hiyo namba 34/2009 imeahirishwa hadi Septemba 9, mwaka huu
WAFANYAKAZI tisa waliokuwa waajiriwa wa Kampuni ya simu za mikononi ya Zain, wameishitaki menejimenti ya kampuni hiyo katika Mahakama ya Kazi jijini Dar es Salaam, wakidai fidia ya sh milioni 412, kama malipo ya stahili zao pamoja na malipo ya adhabu kwa kampuni hiyo.
Wakizungumza jana na Tanzania Daima Jumatano, kupitia wakili wao, Tundu Lissu, alisema kuwa wateja wake waliachishwa kazi kwa madai ya kuyumba kwa uchumi na shauri hilo linapingwa vikali na wafanyakazi hao ambao waliamua kuishitaki kampuni hiyo mahakamani.
Sheria inamtaka mwajiri mara tu anapofikiria kuwapunguza wafanyakazi wake ni lazima awataarifu kwa maandishi na kuwapa vigezo vya upunguzaji huo, ikiambatana na malipo yao, ambapo hilo halikufanyika, alisema Lissu.
Lissu alidai kuwa wateja wake walifukuzwa si kwa sababu za kiuchumi kama walivyodai bali chuki ya kumpuni kwa wafanyakazi hao, kwa kuwa mwaka jana Zain iliongeza asilimia 50 ya wafanyakazi.
Alisema mapato ya kampuni hiyo yaliongezeka kwa asilimia 30 mwaka jana kama faida na kuifanya kampuni hiyo iongoze kwa mapato barani Afrika kwa kampuni zote za Zain.
Alisisitiza kuwa wateja wake walifukuzwa kwa chuki kwani siku ya tukio, watano kati yao walikuwa wamepangiwa safari za mikoani na waliporipoti ofisini walipewa barua za kufukuzwa kazi, huku wawili kati yao wakipewa taarifa ya kufika makao makuu Dar es Salaam kutoka Iringa kwenye mkutano na walipofika walipewa barua za kufukuzwa kazi.
Lissu alieleza zaidi kuwa wateja wake walituhumiwa kukiuka taratibu za ofisi ambapo kampuni ilishindwa kuthibitisha hilo na kumfukuza kazi mmoja wa watumishi hao.
Wote kwa pamoja baada ya kupewa barua hawakuruhusiwa kuingia ofisini na malipo yao yalienda kulipia madeni yao katika Benki ya Kenya Commercial Bank (KCB) ambapo ni kinyume cha sheria za kazi. Wafanyakazi hao wanaiomba mahakama itoe tamko kuwa walifukuzwa kazi kinyume cha sheria, warudishwe kazini kwa nafasi zilezile na mahakama iamuru walipwe mishahara na malipo yote kwa kipindi chote walichosimamishwa kazi. Kesi hiyo namba 34/2009 imeahirishwa hadi Septemba 9, mwaka huu