Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,172
Wafanyakazi walalamikia nyongeza kiduchu ya mshahara | Send to a friend |
Thursday, 28 July 2011 21:34 |
Gedius Rwiza na Patricia Kimelemeta BAADHI ya wafanyakazi wa umma wamelalamikia nyongeza ya mishahara iliyoanza kulipwa na mwisho wa Julai, mwaka huu.Uchunguzi wa gazeti hili kutoka kwa wafanyakazi wa kada mbalimbali za utumishi wa umma ambao tayari wamelipwa mshahara wa mwezi Julai, umebaini kuwa kiasi kilichoongezwa ni kati ya Sh10,000 na Sh70,000. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili, wafanyakazi hao walisema wameshindwa kujua vigezo vilivyotumika kuwaongezea viwango hivyo ambavyo havikidhi mahitaji ya sasa kimaisha. Baadhi ya wafanyakazi wa Idara ya Kilimo ambao ni maofisa ugani, walisema kiwango chao cha elimu ni stashahada, ambao awali walikuwa wanapata Sh 230,000 baada ya makato, sasa walisema wanapata Sh300,000. Mfanyakazi mmoja ambaye yupo katika sekta ya afya ambaye ni muuguzi, alisema ana miaka 11 kazini na ameongezewa Sh40,000 ambazo alisema ni kudogo. Ni kweli tumeongezewa mshahara, lakini ni sawa na kutoongezwa ikilinganishwa na gharama za maisha zilivyopanda, alisema mfanyakazi mwingine.Kwa upande wa walimu waliohojiwa na gazeti hili, walisema baadhi yao wameongezewa Sh 20,000 na wengine Sh60,000 na kwamba, Serikali imeshindwa kukifikisha kiwango cha kima cha chini kilichopendekezwa,. Kwa mfano, walimu wa stashahada tunabakiwa Sh 250,000 baada ya makato wakati tulitegemea kima cha chini kuwa Sh350,000, hivyo kwa ngazi yetu tungepata tungepata zaidi, alisema mmoja wa walimu hao. Kauli ya CWT Chama Cha Walimu Tanzania (CWT), Gratian Mukoba, alisema kitendo cha Serikali kushindwa kufikisha kima cha chini cha Sh350,000, kitaleta mgogoro kati yake (Serikali)na wafanyakazi. Mukoba alisema: Unajua, Serikali inawakejeli wafanyakazi, kwani kumwongezea mfanyakazi Sh30,000 ni kitendo cha kumfanyia kejeli, kwani kutokana na halu maisha ilivyo sasa, hata kima cha chini kilichopendekezwa hakitoshi,alifafanua Mukoba. Msimamo wa Tucta Shirikisho la Vyama Vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), limesema nyongeza hiyo mpya ya mishahara ni ndogo na haikidhi mahitaji ya wafanyakazi nchini. Akizungumza na Mwananchi kwenye mahojiano jijini Dar es Salaam jana, Naibu Katibu Mkuu wa Tucta, Nicolaus Mgaya, alisema nyongeza hiyo ni ndogo ikilinganishwa na hali ya maisha ya sasa. Mgaya alisema, mwaka 2007 Tucta ilpendekeza kuwa kima cha chini kiwe Sh315,000, lakini Serikali imeshindwa kuongeza hadi sasa, badala yake imeongeza asilimia 11 hadi 12 ya mishahara Sasa hivi tunasubiri walaka wa mishahara mipya ili tuweze kuangalia nyongeza hiyo, lakini tunavyojua ni ndogo na kwamba, haiwezi kukidhi mahitaji ya wafanyakazi, kutokana na hali hiyo hiyo Serikali inapaswa kuliangalia suala hilo kwa undani ili kuondoa migogoro ya wafanyakazi.Alisema baada ya hapo watakusanya maoni kutoka kwa wafanyakazi wenyewe na kutoa tamko kulingana na nyongeza hiyo ili waweze kuangalia hatua zitakazofuata. Kwa mujibu wa Mgaya, migogoro ya wafanyakazi inatokana na viwango midogo na kwamba jambo hilo limechangia wafanyakazi kushindwa kufanya kazi kwa bidii na kukithiri kwa rushwa katika uwajibikaji. Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hawa Ghasia, alipoulizwa na gazeti hili kuhusu vigezo vilivyotumika kuongeza mishahara alisema kuwa, kwa sasa yeye hawezi kuzungumzia suala hilo na kuongeza kwamba, viongozi wa vyama vya wafanyakazi walishiriki katika mchakato huo. Unajua, viongozi wa vyama vya wafanyakazi walishirikishwa katika mchakato wa kuongeza mishahara, hivyo unaweza kuwahoji watakupa jibu sahihi, alisema Ghasia. |