Wafanyakazi wa kitanzania wa mgodi wa Buzwagi watakiwa kufukuzwa kwa vyovyote vile

MAGAMBA MATATU

JF-Expert Member
Jul 2, 2011
646
1,174
Kwa hali isiyo ya kawaida kwa migodi iliyoko chini ya kampuni ya uchimbaji madini ya Barrick wafanyakazi wake wamekuwa kwenye msuguano mkubwa na VIONGOZI (MANAGEMENT) waliowekwa kwa ajili ya kusimamia migodi hiyo.

Mgodi wa Barrick BUZWAGI ulioko Kahama kwa sasa umetokea kuwa na kashfa kubwa sana mara baada ya wamiliki wa huo mgodi kuamua kutumia maneno machafu kwa wafanyakazi wake kitu ambacho kimekuwa na uonevu mkubwa sana kwa hao wafanyakazi , imefikia hadi wakati watanzania hao kuhoji kama serikali inajua kile kinachofanyika kwa hao wafanyakazi wa kitnzania,
Hivi karibuni kuna taarifa ilitolewa na gazeti la TAIFA LETU kwa tuhuma nzito dhidi ya wafanyakazi wa kitanzania zinazofanywa na wageni(MAKABURU) kutoka afrika ya kusini, gazeti hilo lilinukuliwa likimnukuu katibu wa TAMICO wa Buzwagi pale alipoitwa mbwa wadogo pamoja nawafanyakazi wenzake, hivyo hivyo wafanyakazi hao wa kitanzania wamekuwa wakiitwa (MONKEY) kitu ambacho kimeafanya taarifa itolewe polisi pale kahama ili uchunguzi ufanywe lakini mambo yamekuwa tofauti kwani kinachoonekana polisi wanahongwa na wale wageni(MAKABURU) na kuamua kutofatilia madai ya wafanyakazi wa kitanzania.

Kwa sasa baada ya wageni hao(MAKABURU) hao kuona hawachukuliwi hatua za kinidhani wameamua kuweka mkakati wa kuhakikisha kuwa wanawafukuza watanzania kwa kigezo cha kuwa wanalala kazini,. kuna mpango unaoendelea kwa sasa ambapo kuna wageni(makaburu) kadhaa wamepewa kamera ili watimize kazi hiyo ili wawalete wafanyakazi wa kigeni, Kiukweli mpango wao umeisha anza kazi kwani kwa hii wiki zaidi ya wafanyakazi 8 wamefukuzwa kazi kwa kupigwa picha hata kama mtu ataonekana kuwa ameinama hiyo picha wataitunga kuwa alikuwa anaokota dhahabu, JUZI tarehe 26 wafanyakazi watano tena wamepigwa picha na wameamuliwa kumuona afisa mwajili KESHO TAREHE 28 kwa ajili ya kuchukuliwa hatua zitakazofaa, hadi sasa hali imekuwa ni ngumu sasa kwa wafanyakazi wa kitanzania kitu kinachofanya wajiulize kama wana serikali au hapana.

KIUKWELI HALI SI NZURI NA SERIKALI ISIPOLIANGALIA HILI SWALA BASI IJUE WANANCHI WAKE WAMEISHAGEUZWA WATUMWA JAPO UHURU TULIISHA UPATA.
 
Mambo haya yanakera, yanatokea kwenye nchi ambayo ina viongozi wanaoruhusu upuuzi kama huu kutokea na wao kuendelea kuneemeka na vipande kiasi vya fedha.

Ole wao siku yaja...!
 
huyo john comer mining engenieer ndo aliita waafrica wote mbya....na hilo li hr garth lipohapo kwa ajili ya makaburu..usitegemee ocs haway anaweza kufanya lolote hapo maana naye nikibaraka tu anaomba moaka mafuta ya gari lapolisi mgodini buzwagi unategemea nini..

meneja wa mgodi boyd timler ndo matapishi matupu hanaga akili za kufikiria akitoa maamuzi...meneja wa mahusiano ya jamii richard sherinhtin ndo bure anakazi ya kufanya ngono na vibinti vya kahama mjini...yaaani huu mgodi umeoza
 
Mambo haya yanakera, yanatokea kwenye nchi ambayo ina viongozi wanaoruhusu upuuzi kama huu kutokea na wao kuendelea kuneemeka na vipande kiasi vya fedha.

Ole wao siku yaja...!
Mkuu hii kitu imeniuma sana kwa sababu nchi ambayo nipo hayo ambayo wanafanyiwa watanzania hapo nyumbani kwa huku wanafanyiwa wageni.. Mgeni ni marufuku kuwa hata kwenye menejiment zenye maamuzi kuhusu mwenyeji.

...sasa kwa hapo Tz ni upumbavu..

Ok..ole wao siku yaja unamaanisha nini? Siku gani? Au baada ya miaka 50 tena ya uhuru..inasikitisha sana aisee...kama maigizo vile
 
huyo john comer mining engenieer ndo aliita waafrica wote mbya....na hilo li hr garth lipohapo kwa ajili ya makaburu..usitegemee ocs haway anaweza kufanya lolote hapo maana naye nikibaraka tu anaomba moaka mafuta ya gari lapolisi mgodini buzwagi unategemea nini..

meneja wa mgodi boyd timler ndo matapishi matupu hanaga akili za kufikiria akitoa maamuzi...meneja wa mahusiano ya jamii richard sherinhtin ndo bure anakazi ya kufanya ngono na vibinti vya kahama mjini...yaaani huu mgodi umeoza

serikali yetu ni ya kipumbavu...mtz anaitwa mbwa au nyani na mgeni then huyo mgeni anaendelea kudunda nchini? Dah??..maajabu ya dunia haya...inabidi tuazime vichwa wa wa egypt ili kuiondoa hii serikali.
 
Viongozi wa Tanzania wanaogopa sana wazungu. Sijui ni lugha au confidence ! Nachelea kusema ni confidence kwa sababu ingekua wanaenda kwenye mikutano na wakalimani sidhani kama uozo huu ungetokea.
 
huyo john comer mining engenieer ndo aliita waafrica wote mbya....na hilo li hr garth lipohapo kwa ajili ya makaburu..usitegemee ocs haway anaweza kufanya lolote hapo maana naye nikibaraka tu anaomba moaka mafuta ya gari lapolisi mgodini buzwagi unategemea nini..

meneja wa mgodi boyd timler ndo matapishi matupu hanaga akili za kufikiria akitoa maamuzi...meneja wa mahusiano ya jamii richard sherinhtin ndo bure anakazi ya kufanya ngono na vibinti vya kahama mjini...yaaani huu mgodi umeoza


Mkuu kiukweli kwa sasa inasemekana meneja mkuu amekaimu kaburu na kuna kaburu hawana hata utaalamu wowote na wanalipwa pesa nyingi kuliko hali yenyewe, naamini serikali isipochukua hatua kuna siku mauaji yatatokea hapo mgodini maana watu watachoka kunyanyaswa
 
Viongozi wa Tanzania wanaogopa sana wazungu. Sijui ni lugha au confidence ! Nachelea kusema ni confidence kwa sababu ingekua wanaenda kwenye mikutano na wakalimani sidhani kama uozo huu ungetokea.

uko sahihi kwani mwezi mmoja uliopita kuna waziri wa mambo ya ndani SHAMSA VUAI NAHODHA alikuja pale BUZWAGI cha ajabu hakuweza kuruhusiwa kuingia sehemu inayoitwa process plant zaid yake walimpeleka juu ya kifusi cha mawe na hapo ndo walitumia kumuonyesha jinsi mgodi unavyofanya kazi huku akiwa nje.
 
uko sahihi kwani mwezi mmoja uliopita kuna waziri wa mambo ya ndani SHAMSA VUAI NAHODHA alikuja pale BUZWAGI cha ajabu hakuweza kuruhusiwa kuingia sehemu inayoitwa process plant zaid yake walimpeleka juu ya kifusi cha mawe na hapo ndo walitumia kumuonyesha jinsi mgodi unavyofanya kazi huku akiwa nje.
Ni haki yao kutokumpeleka hata Mimi nikija kwako una hiari kuniingiza chumbani kwako
Na sisi Wa TZ tuache utegaji kazini,tuache kulala kazini na uzembe tuache tuwajibike vilivyo Ama sivyo tutaishia kupigwa PICHA na kulalamika ovyo.
 
Haya mambo tumeyakubali wenyewe. Serikali yenu mnaijua, ya nn mnaisubir ifanye maamuz? Choma moto ofisi zote. Mbona shule zenu mwazichoma? Chukueni hatua. Au mnaogopa njaa? Basi vumilien manyanyaso ndani ya nchi yenu. Eti mko huru. Huru? Labda hururuu.
 
Ni haki yao kutokumpeleka hata Mimi nikija kwako una hiari kuniingiza chumbani kwako Na sisi Wa TZ tuache utegaji kazini,tuache kulala kazini na uzembe tuache tuwajibike vilivyo Ama sivyo tutaishia kupigwa PICHA na kulalamika ovyo.
KULIKO UWE MTUMWA WA AKILI KAMA WEWE BORA UNYWE SUMU UFE!i
 
Mambo haya yanakera, yanatokea kwenye nchi ambayo ina viongozi wanaoruhusu upuuzi kama huu kutokea na wao kuendelea kuneemeka na vipande kiasi vya fedha.

Ole wao siku yaja...!

ulivyotoa ule uzi wa Shimbo nikaacha kukuamini. Acha mkwara.
 
huyo john comer mining engenieer ndo aliita waafrica wote mbya....na hilo li hr garth lipohapo kwa ajili ya makaburu..usitegemee ocs haway anaweza kufanya lolote hapo maana naye nikibaraka tu anaomba moaka mafuta ya gari lapolisi mgodini buzwagi unategemea nini..

meneja wa mgodi boyd timler ndo matapishi matupu hanaga akili za kufikiria akitoa maamuzi...meneja wa mahusiano ya jamii richard sherinhtin ndo bure anakazi ya kufanya ngono na vibinti vya kahama mjini...yaaani huu mgodi umeoza

hawa jamaa si muwashtaki kwa yale majembe ya CHADEMA pale Kahama kama mwenyekiti wa Wilaya, akina Abbas. Wakiweka vikao vyao pale California wawalipue. Wakilipuliwa wataacha.
 
Viongozi wa Tanzania wanaogopa sana wazungu. Sijui ni lugha au confidence ! Nachelea kusema ni confidence kwa sababu ingekua wanaenda kwenye mikutano na wakalimani sidhani kama uozo huu ungetokea.

haya yote ni madhara ya 10%
 
Mkuu kiukweli kwa sasa inasemekana meneja mkuu amekaimu kaburu na kuna kaburu hawana hata utaalamu wowote na wanalipwa pesa nyingi kuliko hali yenyewe, naamini serikali isipochukua hatua kuna siku mauaji yatatokea hapo mgodini maana watu watachoka kunyanyaswa

mauaji hayawezi kutokea kwa kuwa mmetengwa na kutawaliwa. Hamuwezi hata kuchangia magari wakati wote mnakaa mjini. Mabasi mengine yanarudi na watu wa4 huku wengine wakisubiri ya kwao!
 
uko sahihi kwani mwezi mmoja uliopita kuna waziri wa mambo ya ndani SHAMSA VUAI NAHODHA alikuja pale BUZWAGI cha ajabu hakuweza kuruhusiwa kuingia sehemu inayoitwa process plant zaid yake walimpeleka juu ya kifusi cha mawe na hapo ndo walitumia kumuonyesha jinsi mgodi unavyofanya kazi huku akiwa nje.

Mzanzibar hawezi kuwasaidia kwenye 10% za wakubwa zake, wekeni umoja wenu muwe na mwanasheria wenu. Poleni sana kaka zangu
 
Haya mambo tumeyakubali wenyewe. Serikali yenu mnaijua, ya nn mnaisubir ifanye maamuz? Choma moto ofisi zote. Mbona shule zenu mwazichoma? Chukueni hatua. Au mnaogopa njaa? Basi vumilien manyanyaso ndani ya nchi yenu. Eti mko huru. Huru? Labda hururuu.

kaka hawa watu hawawezi kuchukua hatua yoyote. Hawana umoja!! Mna pesa nyie anzisheni umoja wenu. Mi niko Kahama na si mgodini, nitawasaidia. Wakisikia tu watatia adabu
 
Haya mambo yanauma sana na si hapo mgodini tu, njoo Arusha uone wabongo wanavyonyanyaswa kwenye mahoteli, na position zote walizopewa wabongo ni zile za chini kabisa, kufuta madirisha, kusafisha vyumba, udereva, ulinzi na kuwabebea wageni mabegi wakifika reception.
 
Mi huwa nashangaa sijui kwanini waafrika huwa wanakasirika sana wakiitwa majina kama mbwa na nyani. Waafrika wote tabia zao ni kama MBWA na MANYANI tu wala hawana cha kulaumu hapo. Viongozi wao, kwa mfano, wapo tayari hata kuona waafrika wenzao wanateseka ili wao waendelee kunufaika na wizi wa mali wanazoziiba. Huku uswahilini nako mtu anadiriki kubaka mtoto wake wa kumzaa kwa imani za kishirikina tu. Sasa mnataka wazungu wawaite jina gani kama siyo MBWA na MANYANI.
 
Ahsante Karamagi! Yale matokeo ya kamkataba kako pale hotelini, matunda tunayaona, we endelea kula kuku tu.....
 
Back
Top Bottom