MAGAMBA MATATU
JF-Expert Member
- Jul 2, 2011
- 646
- 1,174
Kwa hali isiyo ya kawaida kwa migodi iliyoko chini ya kampuni ya uchimbaji madini ya Barrick wafanyakazi wake wamekuwa kwenye msuguano mkubwa na VIONGOZI (MANAGEMENT) waliowekwa kwa ajili ya kusimamia migodi hiyo.
Mgodi wa Barrick BUZWAGI ulioko Kahama kwa sasa umetokea kuwa na kashfa kubwa sana mara baada ya wamiliki wa huo mgodi kuamua kutumia maneno machafu kwa wafanyakazi wake kitu ambacho kimekuwa na uonevu mkubwa sana kwa hao wafanyakazi , imefikia hadi wakati watanzania hao kuhoji kama serikali inajua kile kinachofanyika kwa hao wafanyakazi wa kitnzania,
Hivi karibuni kuna taarifa ilitolewa na gazeti la TAIFA LETU kwa tuhuma nzito dhidi ya wafanyakazi wa kitanzania zinazofanywa na wageni(MAKABURU) kutoka afrika ya kusini, gazeti hilo lilinukuliwa likimnukuu katibu wa TAMICO wa Buzwagi pale alipoitwa mbwa wadogo pamoja nawafanyakazi wenzake, hivyo hivyo wafanyakazi hao wa kitanzania wamekuwa wakiitwa (MONKEY) kitu ambacho kimeafanya taarifa itolewe polisi pale kahama ili uchunguzi ufanywe lakini mambo yamekuwa tofauti kwani kinachoonekana polisi wanahongwa na wale wageni(MAKABURU) na kuamua kutofatilia madai ya wafanyakazi wa kitanzania.
Kwa sasa baada ya wageni hao(MAKABURU) hao kuona hawachukuliwi hatua za kinidhani wameamua kuweka mkakati wa kuhakikisha kuwa wanawafukuza watanzania kwa kigezo cha kuwa wanalala kazini,. kuna mpango unaoendelea kwa sasa ambapo kuna wageni(makaburu) kadhaa wamepewa kamera ili watimize kazi hiyo ili wawalete wafanyakazi wa kigeni, Kiukweli mpango wao umeisha anza kazi kwani kwa hii wiki zaidi ya wafanyakazi 8 wamefukuzwa kazi kwa kupigwa picha hata kama mtu ataonekana kuwa ameinama hiyo picha wataitunga kuwa alikuwa anaokota dhahabu, JUZI tarehe 26 wafanyakazi watano tena wamepigwa picha na wameamuliwa kumuona afisa mwajili KESHO TAREHE 28 kwa ajili ya kuchukuliwa hatua zitakazofaa, hadi sasa hali imekuwa ni ngumu sasa kwa wafanyakazi wa kitanzania kitu kinachofanya wajiulize kama wana serikali au hapana.
KIUKWELI HALI SI NZURI NA SERIKALI ISIPOLIANGALIA HILI SWALA BASI IJUE WANANCHI WAKE WAMEISHAGEUZWA WATUMWA JAPO UHURU TULIISHA UPATA.
Mgodi wa Barrick BUZWAGI ulioko Kahama kwa sasa umetokea kuwa na kashfa kubwa sana mara baada ya wamiliki wa huo mgodi kuamua kutumia maneno machafu kwa wafanyakazi wake kitu ambacho kimekuwa na uonevu mkubwa sana kwa hao wafanyakazi , imefikia hadi wakati watanzania hao kuhoji kama serikali inajua kile kinachofanyika kwa hao wafanyakazi wa kitnzania,
Hivi karibuni kuna taarifa ilitolewa na gazeti la TAIFA LETU kwa tuhuma nzito dhidi ya wafanyakazi wa kitanzania zinazofanywa na wageni(MAKABURU) kutoka afrika ya kusini, gazeti hilo lilinukuliwa likimnukuu katibu wa TAMICO wa Buzwagi pale alipoitwa mbwa wadogo pamoja nawafanyakazi wenzake, hivyo hivyo wafanyakazi hao wa kitanzania wamekuwa wakiitwa (MONKEY) kitu ambacho kimeafanya taarifa itolewe polisi pale kahama ili uchunguzi ufanywe lakini mambo yamekuwa tofauti kwani kinachoonekana polisi wanahongwa na wale wageni(MAKABURU) na kuamua kutofatilia madai ya wafanyakazi wa kitanzania.
Kwa sasa baada ya wageni hao(MAKABURU) hao kuona hawachukuliwi hatua za kinidhani wameamua kuweka mkakati wa kuhakikisha kuwa wanawafukuza watanzania kwa kigezo cha kuwa wanalala kazini,. kuna mpango unaoendelea kwa sasa ambapo kuna wageni(makaburu) kadhaa wamepewa kamera ili watimize kazi hiyo ili wawalete wafanyakazi wa kigeni, Kiukweli mpango wao umeisha anza kazi kwani kwa hii wiki zaidi ya wafanyakazi 8 wamefukuzwa kazi kwa kupigwa picha hata kama mtu ataonekana kuwa ameinama hiyo picha wataitunga kuwa alikuwa anaokota dhahabu, JUZI tarehe 26 wafanyakazi watano tena wamepigwa picha na wameamuliwa kumuona afisa mwajili KESHO TAREHE 28 kwa ajili ya kuchukuliwa hatua zitakazofaa, hadi sasa hali imekuwa ni ngumu sasa kwa wafanyakazi wa kitanzania kitu kinachofanya wajiulize kama wana serikali au hapana.
KIUKWELI HALI SI NZURI NA SERIKALI ISIPOLIANGALIA HILI SWALA BASI IJUE WANANCHI WAKE WAMEISHAGEUZWA WATUMWA JAPO UHURU TULIISHA UPATA.