Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,921
- 22,074
Wafanyakazi wa shirika la ndege la tanzania wapatao 181 wanatarajiwa kugawiwa barua zao za mkono wa ahsante leo hii....akionngea na mwandishi wetu katibu mkuu wa wizara ya miundo mbinu Bw omary chambo amesema leo lazima kila mfanyakazi awe ameshapata haki yake....akiulizwa swali la kuhusu mbia alisema bado hakuna aliejitokeza kuichukua atcl bali mchina amesema atajitahidi kuisaidia kwa kuwaletea ndege kadhaa...huku akikwepa kujibu baadhi ya maswali kwa nini mkataba wa trl mmesaini kihuni huku watu wakiwahasa madhara yake alisema lile shirika atuwezi kuliacha nalo siku za usoni linatarajiwa kupunguza wafanyakazi ili kuendana na hali halisi....huku baadhi ya waandishi wakimuuliza iweje mna mpango wa kuleta ndege kwenye shirika la atcl huku mkipunguza idadi kubwa hivyo Mh chambo alisema hilo alikwepeki kama zikija basi ajira zitakuwepo tu na kila mtu atakaribishwa kutuma maombi....baada ya hapo mh chambo anatarajiwa kuwa na mkutano mwingine na waandishi wa habari kuhusu wizi uliofanyika miundo mbinu ambapo alijitahidi kukwepa maswali kuhusu ulaji wa pesa za vipuri pamoja na pesa za ikulu......