Wafanyakazi: JK Hahitaji kura zetu

Status
Not open for further replies.
Mimi na wanaonitegemea hatopata kura zetu amesama hazihataji kwa nini tumpe na kwa mafanikio gani ya kumrudisha Ikulu.
 
Bora nipoteze haki yangu ya kupiga kura kuliko nimpe kura yangu!!
sio mimi peke yangu, hata wale wanaonitegemea nimeshawashawishi.
Dr. Slaa ana Kura zangu 6 mpaka sasa.
Naombeni na wafanyakazi wengine mfanye the same!!
Ni hayo tu.
 
Daah!!! nibora haki yangu ipotee hivi naiona kuliko kumchagua mtu aliyenidhalilisha mbele ya wanangu! inaniuma tena sana nikukumbuka maneno ya Mh. Dr.... Nadhani ni vyema kama kila mfanyakazi hatumia muda huo kumdhalilisha na yeye
 
utakuwa mpumbavu kama utampa kura wakti yeye mwenyewe kashasema hazitaki mi simpi
 
Mimi na familia, wazazi wangu, ndugu zangu, kina shangazi na mjomba na wale wote walio na uhusiano wa karibu pamoja na majirani zangu wote hatumpi.
Kumpa kura ni kujipendekeza, yeye kashasema hazitaki, kwa nini tumpe..

Nina uhakika wa kusababisha yeye kutopata kura kama 20 to 30 hivi.

Usawa huu sio wa kujipendekeza tena, lazima tumwoneshe kua tumechukizwa na maneno yake ya dharau na ujivuni..
 
Nafurahi ameyasema mwenyewe, nadhani wafanyakazi ni wakati wenu sasa kuamua ki utu uzima manake sababu mnazo, nia ipo, uwezo ndo mmepewa amueni wenyewe kumpa ASIYEZITAKA KURA ZENU au kumnyima!
 
Hahaaa, jamaa anajindanganya huyu, anafikri hao wakulima huko vijijini hawana ndugu zao wanofanyakazi?
Sasa unajipendekeza nini kumpa kula wakati amesema haitaji kula yako?????????????













 
Mipango aliyonayo ni kuiba kura. Sasa wafanyakazi tusimpigie kura halafu tulinde kura zetu asiziibe.
 
Kuna kauli aliyoitoa siku ya mkutano wao Dodoma kua hata wasiposhinda, watajishindisha....
Sijui kujishindisha ndio kuiba kura au vp....
 
Mtu kakukana hadharani na kusema hataki kura yako na wewe unalazimisha kumpa huo ndio unaitwa "UBWEGE" na Mwakyembe alisema watanzania sio Mabwege tena.
 
Inaonekana JK ana mapungufu makubwa ktk somo la historia, hana habari kuwa sehemu nyingi duniani mapinduzi yaliwashirikisha wafanyakazi kwa karibu mno, sasa ni wakati wa kumuelimisha kwa vitendo......mie na familia yangu, na kijiji chetu chote (manake mie ndio mwenye digrii kijiji kizima na wanasikiliza kwa kila jambo) hatumpi "kula" wala kura zetu, ng'o!
 
Moja ya matatizo makubwa kwa watz ni umasikini wa akili.

Wafanyakazi walio wengi ni masikini wa akili na hii ndiyo sababu tosha ya kuamini kwamba wataendelea kumpigia kura pamoja na kwamba hazihitaji.

Wafanyakazi na wakulima wamenyang'anywa chama chao (CCM) lakini hakuna anayeweza kuhoji na hawajui kwamba chama kimeporwa.

Sasa hivi mafisadi, wezi, wafanyabiashara wenye tamaa, viongozi wa dini wenye tamaa na wanaofanana na hao ndiyo wanaopigana vikumbo kusaka uongozi wa kuchaguliwa kupitia chama cha wakulima na wafanyakazi.

JK amesahau kwamba chama chake ni cha wakulima na wafanyakazi na wafanyakazi hawajui kwamba wao wamemuajiri.

Sasa tutegemee nini kwa watu wa aina hiyo?
 
Double click uweze kusoma maandishiView attachment 12088
pencil.png
 
Jamani wafanyakazi mkataeni, wakulima mkimbieni, wanafunzi mtoeni wananchi hatufai hatumtaki kaburi la umasikini.

KURA ZETU KWA Dr. Peter Slaa
 
Tatizo mbayuwayu wengi ni bora hata ya wakulima wa huko kantalamba sijui yakoje!
 
Moja ya matatizo makubwa kwa watz ni umasikini wa akili.
Wafanyakazi walio wengi ni masikini wa akili na hii ndiyo sababu tosha ya kuamini kwamba wataendelea kumpigia kura pamoja na kwamba hazihitaji.
Wafanyakazi na wakulima wamenyang'anywa chama chao (CCM) lakini hakuna anayeweza kuhoji na hawajui kwamba chama kimeporwa.
Sasa hivi mafisadi, wezi, wafanyabiashara wenye tamaa, viongozi wa dini wenye tamaa na wanaofanana na hao ndiyo wanaopigana vikumbo kusaka uongozi wa kuchaguliwa kupitia chama cha wakulima na wafanyakazi.
JK amesahau kwamba chama chake ni cha wakulima na wafanyakazi na wafanyakazi hawajui kwamba wao wamemuajiri.
Sasa tutegemee nini kwa watu wa aina hiyo?

bila shaka wewe ndo masikini wa akili. yaani wewe kuwa mwana chadema ndo unaakili sana sio?
this is politics do not pretend ignorance
 
Unakumbuka JK alisema hataki kura za wafanyakazi,t-shirt hiyo hapo kwa kumbukumbu zaid
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom