Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,906
- 22,050
Wafanyabiashara wa mafuta waikosesha TRA mapato
Na Lulu George
27th November 2009B-pepeChapaMaoni
Mamlaka ya Mapato (TRA).
Mamlaka ya Mapato (TRA) Mkoa wa Tanga imeshindwa kufikia malengo ya ukusanyaji wa kodi kwa kipindi cha miezi minne kutokana na waingizaji wa mafuta nchini kuacha kutumia Bandari ya Tanga.
Kauli hiyo ilitolewa juzi na Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga, Nyonge Juma Mahanyu wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na Wiki ya mlipa kodi iliyoanza Novemba 23 hadi 26, mwaka huu.
Mahanyu, alisema katika kipindi hicho cha kuanzia Julai hadi Oktoba, mwaka huu ilikusanya kiasi cha Sh bilioni 27 badala ya lengo walilojiwekea la kupata Sh bilioni 30.3.
Alisema katika kipindi hicho mwaka jana ilikusanya kiasi cha Sh bilioni 30.7 badala ya Sh bilioni 35.5.
Mahanyu hakuelezea sababu za wafanyabiashara hao kuacha kupitisha mafuta yao kwenye bandari hiyo na kusisitiza kuwa TRA haina mamlaka ya kumlazimisha au kumchagulia mtu bandari ya kupitisha mzigo wake.
Nayo TRA Mkoa wa Morogoro, imeweka mikakati ya kukusanya zaidi ya Sh bilion 23.6 katika kipindi cha mwaka wa fedha 2009/10 .
Kaimu Meneja wake, Kilomba Kanse aliitaja mikakati hiyo kuwa ni pamoja na kutoa elimu ya kodi kwa walipakodi, kuwatembelea sehemu zao za biashara.
Alizitaja changamoto zinazijitokeza katika utendaji wao wa kazi kuwa ni wafanyabiashara wengi kushindwa kutofautisha kodi ya mapato na ushuru kutokana na uelewa mdogo wa sheria za kodi.
Nyingine ni wafanyabiashara kutotoa stakabadhi kwa wanunuzi ambao nao wamekuwa wakishindwa kuwadai na kuikosesha Serikali mapato kutokana na wafanyabiashara hao kukwepa kulipa kodi.
Vilevile, alisema wafanyabiashara hao wamekuwa wakiwakimbia maofisa wa TRA kwa kufunga maduka yao wanapokwenda kufuatilia ulipaji kodi.
CHANZO: NIPASHE
Na Lulu George
27th November 2009B-pepeChapaMaoni
Mamlaka ya Mapato (TRA).
Mamlaka ya Mapato (TRA) Mkoa wa Tanga imeshindwa kufikia malengo ya ukusanyaji wa kodi kwa kipindi cha miezi minne kutokana na waingizaji wa mafuta nchini kuacha kutumia Bandari ya Tanga.
Kauli hiyo ilitolewa juzi na Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga, Nyonge Juma Mahanyu wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na Wiki ya mlipa kodi iliyoanza Novemba 23 hadi 26, mwaka huu.
Mahanyu, alisema katika kipindi hicho cha kuanzia Julai hadi Oktoba, mwaka huu ilikusanya kiasi cha Sh bilioni 27 badala ya lengo walilojiwekea la kupata Sh bilioni 30.3.
Alisema katika kipindi hicho mwaka jana ilikusanya kiasi cha Sh bilioni 30.7 badala ya Sh bilioni 35.5.
Mahanyu hakuelezea sababu za wafanyabiashara hao kuacha kupitisha mafuta yao kwenye bandari hiyo na kusisitiza kuwa TRA haina mamlaka ya kumlazimisha au kumchagulia mtu bandari ya kupitisha mzigo wake.
Nayo TRA Mkoa wa Morogoro, imeweka mikakati ya kukusanya zaidi ya Sh bilion 23.6 katika kipindi cha mwaka wa fedha 2009/10 .
Kaimu Meneja wake, Kilomba Kanse aliitaja mikakati hiyo kuwa ni pamoja na kutoa elimu ya kodi kwa walipakodi, kuwatembelea sehemu zao za biashara.
Alizitaja changamoto zinazijitokeza katika utendaji wao wa kazi kuwa ni wafanyabiashara wengi kushindwa kutofautisha kodi ya mapato na ushuru kutokana na uelewa mdogo wa sheria za kodi.
Nyingine ni wafanyabiashara kutotoa stakabadhi kwa wanunuzi ambao nao wamekuwa wakishindwa kuwadai na kuikosesha Serikali mapato kutokana na wafanyabiashara hao kukwepa kulipa kodi.
Vilevile, alisema wafanyabiashara hao wamekuwa wakiwakimbia maofisa wa TRA kwa kufunga maduka yao wanapokwenda kufuatilia ulipaji kodi.
CHANZO: NIPASHE