Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Binamu yangu alimdekeza mtoto wake wa kwanza hadi kufikia karibu miaka minne mtoto alikuwa anakimbia kwa mama na kutaka nyonyo! Kwa kawaida viumbe karibu wengi tu huchukua jukumu la kulea vichanga vyao na katika muda wa malezi ya miaka ya mwanzo basi vinakuwa karibu sana na hao watoto wao. Kwa kadiri siku zinavyoendelea ndivyo wazazi wanajitahidi kuanza kuwafunza watoto wao kuanza kujitegemea.
Hata hivyo katika ya vitu vyote ambavyo ni vichungu kwa mtoto na mama lakini ni vya lazima ni siku ya kumkatisha mtoto kunyonya au kumletea chakula na kumlisha. Ni wakati ambapo mtoto anatakiwa aanze kutafuta chakula yeye mwenyewe na mara kadhaa chini ya uangalizi wa wazazi ambao watahakikisha anakula chakula kizuri na bora na ambacho mwili wake mchanga unaweza kuhimili.
Katika kuhakikisha mtoto anaacha kunyonya wanyama wanatumia namna mbalimbali. Mbwa kwa mfano, hufikia mahali humbwakia mtoto wake kila akikaribia nyonyo, na ng'ombe wao hurusha hata mateke na kumfukuza mtoto kwa pembe. Hawa wote wawili hawajifunzi mahali popote na wala hakuna tathmini ya kujua kama mtoto yuko tayari kujitegemea. Wanachofanya kimo ndani ya hulka yao kama wanyama.
Ninapofikiria hili ninaona jinsi gani Tanzania (siwezi kuzisemea nchi nyingine) ilivyodekezwa na kuendekezwa na wafadhili kiasi kwamba hata wakati wa kuacha kunyonya ulipofika bado hatutaki kuachia nyonyo!! Meno yameshakuwa makubwa na mwili una nguvu lakini hatutaki kucheza mbali na nyonyo za "wazazi wetu" ambao tumewaita "wafadhili".
Wafadhili hawa bahati mbaya hawatoi maziwa mazuri bali wanatoa dawa ikamatayo ya misaada ya kigeni. Sasa hivi hatuwezi kuamini au kufikiria hata kwa kidogo nini kitatokea endapo misaada hiyo itasitishwa. Cha kuudhi zaidi ni kuwa wafadhili hawa hawawezi hata kutubwekea au kutufukuza kwa pembe na kututaka tutafute chakula sisi wenyewe!
Wafadhili hawa wanaamini kabisa kuwa tunawahitaji na ya kuwa pasipo wao "our survival chances are dim". Na sisi wenyewe hatuwezi kufikiria hata kidogo kuweza kuishi bila misaada ya kigeni na hivyo hata tukitaka kufanya lolote lile ni lazima tujiulize kama wafadhili wako tayari kutusaidia. Hakuna mradi mkubwa, na hakuna mpango mkubwa wa maendeleo ambao sisi wenyewe tunaweza kusema tutauanzisha, kuusimamia, kuufanikisha na kuuendeleza bila ya msaada wa wafadhili. Tumedekezwa tukadeka, na sasa bado tunataka nyonyo!!
Ninachosema ni kuwa, wakati wa kutukatisha kunyonya umefika. Tayari tuna wasomi wa kutosha, tuna raslimali ya kutosha, tuna watu wa kutosha na tuna sababu za kutosha kujitegemea. Lakini zaidi ya yote tunaweza kujitegemea kwa kiasi kikubwa katika kujiletea maendeleo. Hadi hivi sasa ninachokiona ni importation of development ambapo kile tunachokiita "maendeleo" kwa kweli ni vitu tulivyocopy and paste kutoka ng'ambo! Juzi nilimsikia Waziri Mkuu akitaka watu wanunue vitunguu vya Tanzania!!! Yaani kwa maneno mengine Tanzania inaagiza hadi vitunguu kutoka ng'ambo ambayo wenyewe tunaviona ni 'bora'!
Hatuwezi kuendelea kuagiza maendeleo kutoka ng'ambo na kuyaaita ni 'maendeleo yetu'. Development of a people can never be imported, it has to be brought forth from the people, by the people for the people!
Napendekeza hatua zifuatazo zianze kuchukuliwa ili hatimaye na sisi tuwe katika mahali pa kutoa misaada ya kigeni kwa nchi nyingine na kuacha kusaidiwa tunavyosaidiwa sasa.
1. Programu ya kuondoa kwa utaratibu misaada ya kigeni kwenye serikali kuu (Systematic phasing out of foreign aid).
Tuangalie ni maeneo gani (sekta) ambayo tunaweza kuhakikisha tunayaendesha moja kwa moja kwa fedha zetu wenyewe. Binafsi naamini upande wa Ulinzi, Elimu, na Miundo Mbinu ni maeneo ambayo tunaweza kuanza nayo. Kutoka hapo tuangalie mengine na kuweka malengo yanayojulikana wazi ili ifikapo sema 2015, asilimia 100 ya bajeti ya Tanzania inatokana na fedha za ndani.
2. Kukataa baadhi ya misaada
Mara nyingi tumekuwa tukipokea misaada mbalimbali kwenye maeneo ambayo kwa hakika hatuhitaji. Msaada wa kuchimba visima, kujenga kliniki, au kuongeza madarasa ni misaada ya kudumaza. Kama Taifa tuwaambie wafadhili kuwa misaada yoyote ya kigeni haitapewa kwenye maeneo haya. Misaada ya mtu kuja nyumbani kwako kukuchimbia choo wakati una uwezo, sababu na raslimali za kuchimba choo hicho wewe mwenyewe ni misaada ya dharau! Misaada ya wageni kuja kutuonesha jinsi ya kusafisha miji yetu ni misaada ya kututweza!
3. Kuelekeza misaada kwenye maeneo nyeti
Binafsi naamini kuwa kama wafadhili kweli wanataka kutusaidia basi watusaidie katika maeneo ambayo kwa hakika tunahitaji misaada hiyo.
- Wafungue Vyuo Vyao Vikuu kwa kutoa bid discounted tuition kwa wananchi wetu. Najua baadhi zinafanya hivyo, lakini hapa nazungumzia programs ambazo Tanzania inahitaji wasomi wengi. Zaidi ya yote, nchi wafadhili zitiwe shime pamoja na taasisi za kwao kuanzisha vyuo vyao vikuu au matawi yao nchini ili kusaidia katika kile kinachoitwa "transfer of knowledge". Na hapa nafikiria taasisi za kimataifa za utafiti wa Sayansi na Technolojia. Kwa mfano COSTECH ikiiwa na uhusiano na NASA, MIT n.k
Hapa pia nafikiria suala la kusomesha madaktari wetu katika vyuo vyao vikuu. Au sisi wenyewe kuwa na utaratibu utakaochochea madaktari na mabingwa wa afya kuja Tanzania kufanya kazi na hawa wa kwetu, kutusaidia katika vifaa vya kisasa, na mbinu za kisasa za tiba.
- Tatizo kubwa tulilonalo hadi hivi sasa ni kwenye udhibiti wa fedha za umma na usimamizi wa sheria. Maeneo haya kwa kweli tumeshindwa (and I mean that) kuyasimamia vizuri. Hapa kwa hakika tunahitaji msaada. Kwa hakika, ningependa kuona tunapata timu kama ya watu kutoka Japani au moja ya marafiki zetu kuiendesha Benki Kuu ya Tanzania, kuisafisha, na kuweka misingi ya kuhakikisha kuwa chembe la wingu wa ufisadi haliwezi kusikika tena.
Yapo mambo mengine ambayo naamini pia yanawezekana. Lakini katika vyovyote tutakavyofanya, ni lazima tuweze kufika mahali kuwa "tunajitegemea". Ushirikiano wowote uliopo kati yetu na nchi za kigeni, uwe ni ushirikiano wa "walio sawa".
Tusipofanya hivyo kwa haraka tutajikuta kuwa misaada hii ya kigeni ambayo tumeing'ang'ania katika nyonyo za wafadhili wetu inaendelea kututweza, kutudekeza na kwa hakika inatishia uhuru wetu, inabeza utu wetu, na kwa kadiri ya kwamba tunazidi kuishabikia na kuogopea kukatiwa ndivyo hivyo hivyo inaongeza utegemezi wetu wa kifikra. Ni lazima kama tunataka kupata nafasi ya kuendelea, tusimame kwa miguu yetu hata kama inatetemeka kwa kutokujiamini.
Jamani, hata wanyama wanaachishwa kunyonya!! Nani kwetu atakuwa wa kwanza kusema "sitaki nyonyo, nataka nile chakula changu mwenyewe?"!
Hata hivyo katika ya vitu vyote ambavyo ni vichungu kwa mtoto na mama lakini ni vya lazima ni siku ya kumkatisha mtoto kunyonya au kumletea chakula na kumlisha. Ni wakati ambapo mtoto anatakiwa aanze kutafuta chakula yeye mwenyewe na mara kadhaa chini ya uangalizi wa wazazi ambao watahakikisha anakula chakula kizuri na bora na ambacho mwili wake mchanga unaweza kuhimili.
Katika kuhakikisha mtoto anaacha kunyonya wanyama wanatumia namna mbalimbali. Mbwa kwa mfano, hufikia mahali humbwakia mtoto wake kila akikaribia nyonyo, na ng'ombe wao hurusha hata mateke na kumfukuza mtoto kwa pembe. Hawa wote wawili hawajifunzi mahali popote na wala hakuna tathmini ya kujua kama mtoto yuko tayari kujitegemea. Wanachofanya kimo ndani ya hulka yao kama wanyama.
Ninapofikiria hili ninaona jinsi gani Tanzania (siwezi kuzisemea nchi nyingine) ilivyodekezwa na kuendekezwa na wafadhili kiasi kwamba hata wakati wa kuacha kunyonya ulipofika bado hatutaki kuachia nyonyo!! Meno yameshakuwa makubwa na mwili una nguvu lakini hatutaki kucheza mbali na nyonyo za "wazazi wetu" ambao tumewaita "wafadhili".
Wafadhili hawa bahati mbaya hawatoi maziwa mazuri bali wanatoa dawa ikamatayo ya misaada ya kigeni. Sasa hivi hatuwezi kuamini au kufikiria hata kwa kidogo nini kitatokea endapo misaada hiyo itasitishwa. Cha kuudhi zaidi ni kuwa wafadhili hawa hawawezi hata kutubwekea au kutufukuza kwa pembe na kututaka tutafute chakula sisi wenyewe!
Wafadhili hawa wanaamini kabisa kuwa tunawahitaji na ya kuwa pasipo wao "our survival chances are dim". Na sisi wenyewe hatuwezi kufikiria hata kidogo kuweza kuishi bila misaada ya kigeni na hivyo hata tukitaka kufanya lolote lile ni lazima tujiulize kama wafadhili wako tayari kutusaidia. Hakuna mradi mkubwa, na hakuna mpango mkubwa wa maendeleo ambao sisi wenyewe tunaweza kusema tutauanzisha, kuusimamia, kuufanikisha na kuuendeleza bila ya msaada wa wafadhili. Tumedekezwa tukadeka, na sasa bado tunataka nyonyo!!
Ninachosema ni kuwa, wakati wa kutukatisha kunyonya umefika. Tayari tuna wasomi wa kutosha, tuna raslimali ya kutosha, tuna watu wa kutosha na tuna sababu za kutosha kujitegemea. Lakini zaidi ya yote tunaweza kujitegemea kwa kiasi kikubwa katika kujiletea maendeleo. Hadi hivi sasa ninachokiona ni importation of development ambapo kile tunachokiita "maendeleo" kwa kweli ni vitu tulivyocopy and paste kutoka ng'ambo! Juzi nilimsikia Waziri Mkuu akitaka watu wanunue vitunguu vya Tanzania!!! Yaani kwa maneno mengine Tanzania inaagiza hadi vitunguu kutoka ng'ambo ambayo wenyewe tunaviona ni 'bora'!
Hatuwezi kuendelea kuagiza maendeleo kutoka ng'ambo na kuyaaita ni 'maendeleo yetu'. Development of a people can never be imported, it has to be brought forth from the people, by the people for the people!
Napendekeza hatua zifuatazo zianze kuchukuliwa ili hatimaye na sisi tuwe katika mahali pa kutoa misaada ya kigeni kwa nchi nyingine na kuacha kusaidiwa tunavyosaidiwa sasa.
1. Programu ya kuondoa kwa utaratibu misaada ya kigeni kwenye serikali kuu (Systematic phasing out of foreign aid).
Tuangalie ni maeneo gani (sekta) ambayo tunaweza kuhakikisha tunayaendesha moja kwa moja kwa fedha zetu wenyewe. Binafsi naamini upande wa Ulinzi, Elimu, na Miundo Mbinu ni maeneo ambayo tunaweza kuanza nayo. Kutoka hapo tuangalie mengine na kuweka malengo yanayojulikana wazi ili ifikapo sema 2015, asilimia 100 ya bajeti ya Tanzania inatokana na fedha za ndani.
2. Kukataa baadhi ya misaada
Mara nyingi tumekuwa tukipokea misaada mbalimbali kwenye maeneo ambayo kwa hakika hatuhitaji. Msaada wa kuchimba visima, kujenga kliniki, au kuongeza madarasa ni misaada ya kudumaza. Kama Taifa tuwaambie wafadhili kuwa misaada yoyote ya kigeni haitapewa kwenye maeneo haya. Misaada ya mtu kuja nyumbani kwako kukuchimbia choo wakati una uwezo, sababu na raslimali za kuchimba choo hicho wewe mwenyewe ni misaada ya dharau! Misaada ya wageni kuja kutuonesha jinsi ya kusafisha miji yetu ni misaada ya kututweza!
3. Kuelekeza misaada kwenye maeneo nyeti
Binafsi naamini kuwa kama wafadhili kweli wanataka kutusaidia basi watusaidie katika maeneo ambayo kwa hakika tunahitaji misaada hiyo.
- Wafungue Vyuo Vyao Vikuu kwa kutoa bid discounted tuition kwa wananchi wetu. Najua baadhi zinafanya hivyo, lakini hapa nazungumzia programs ambazo Tanzania inahitaji wasomi wengi. Zaidi ya yote, nchi wafadhili zitiwe shime pamoja na taasisi za kwao kuanzisha vyuo vyao vikuu au matawi yao nchini ili kusaidia katika kile kinachoitwa "transfer of knowledge". Na hapa nafikiria taasisi za kimataifa za utafiti wa Sayansi na Technolojia. Kwa mfano COSTECH ikiiwa na uhusiano na NASA, MIT n.k
Hapa pia nafikiria suala la kusomesha madaktari wetu katika vyuo vyao vikuu. Au sisi wenyewe kuwa na utaratibu utakaochochea madaktari na mabingwa wa afya kuja Tanzania kufanya kazi na hawa wa kwetu, kutusaidia katika vifaa vya kisasa, na mbinu za kisasa za tiba.
- Tatizo kubwa tulilonalo hadi hivi sasa ni kwenye udhibiti wa fedha za umma na usimamizi wa sheria. Maeneo haya kwa kweli tumeshindwa (and I mean that) kuyasimamia vizuri. Hapa kwa hakika tunahitaji msaada. Kwa hakika, ningependa kuona tunapata timu kama ya watu kutoka Japani au moja ya marafiki zetu kuiendesha Benki Kuu ya Tanzania, kuisafisha, na kuweka misingi ya kuhakikisha kuwa chembe la wingu wa ufisadi haliwezi kusikika tena.
Yapo mambo mengine ambayo naamini pia yanawezekana. Lakini katika vyovyote tutakavyofanya, ni lazima tuweze kufika mahali kuwa "tunajitegemea". Ushirikiano wowote uliopo kati yetu na nchi za kigeni, uwe ni ushirikiano wa "walio sawa".
Tusipofanya hivyo kwa haraka tutajikuta kuwa misaada hii ya kigeni ambayo tumeing'ang'ania katika nyonyo za wafadhili wetu inaendelea kututweza, kutudekeza na kwa hakika inatishia uhuru wetu, inabeza utu wetu, na kwa kadiri ya kwamba tunazidi kuishabikia na kuogopea kukatiwa ndivyo hivyo hivyo inaongeza utegemezi wetu wa kifikra. Ni lazima kama tunataka kupata nafasi ya kuendelea, tusimame kwa miguu yetu hata kama inatetemeka kwa kutokujiamini.
Jamani, hata wanyama wanaachishwa kunyonya!! Nani kwetu atakuwa wa kwanza kusema "sitaki nyonyo, nataka nile chakula changu mwenyewe?"!