Mimtamu
JF-Expert Member
- Jan 27, 2012
- 368
- 105
Habari wana Jf wenzangu.
Mwenzenu nimeamua kufunguka baada ya kuona maji yananifika shingoni. Kila mtu anajua umuhimu wa mawasiliano hasa ya simu katika dunia yetu ya leo. Leo kero yangu naihamishia katka mtandao wa TIGO.
Kama mambo haya yananikuta mimi tu basi line yangu inamatatizo,
1. Ninapata sms zisizopungua 20 kutoka TIGO kwa siku halafu hazina kichwa wala miguu
2. Nikijiunga internet mobile na inapokwisha muda wake, wananiunganisha kila siku bila idhini yangu na wananikata hela
3. Tangu huduma ya kukopa salio lianze sijawahi kukopa lakini natumiwa sms kuwa deni langu ninalodaiwa sijalipa
4. Juzi nilinunua muda wa maongezi katika TIGO PESA lakini cha kushangaza wamenikata hela ktk Tigopesa lakini salio halikuongezwa mpaka muda huu
5. Tangu mwaka huu uanze sijawahi kupokelewa simu zangu katika huduma zao za customer care wao
6. Wamekuwa wezi wa salio, kwani hata kama hujatumia ukiangalia salio baada ya muda fulani unakuta limepungua
7. Niwasumbufu wakati wa mawasiliano.
Natamani niuache mtandao huu laki namba yangu ndio ninayoitegemea ktk biashara zangu na wateja wangu wengi wana namba ya tigo kuliko mitandao mengine. Swali langu wadau, Matatizo kama haya yanachukuliwa hatua na mamlaka ipi katika serikali yetu? Haki zangu nitazipata vipi, maana hapa wanakesi ya kujipatia pesa kwa njia ya utapeli.
Kwakweli inaniuma sana, INAKERA SAAAAAANA!!
Nawasilisha kero yangu
Mwenzenu nimeamua kufunguka baada ya kuona maji yananifika shingoni. Kila mtu anajua umuhimu wa mawasiliano hasa ya simu katika dunia yetu ya leo. Leo kero yangu naihamishia katka mtandao wa TIGO.
Kama mambo haya yananikuta mimi tu basi line yangu inamatatizo,
1. Ninapata sms zisizopungua 20 kutoka TIGO kwa siku halafu hazina kichwa wala miguu
2. Nikijiunga internet mobile na inapokwisha muda wake, wananiunganisha kila siku bila idhini yangu na wananikata hela
3. Tangu huduma ya kukopa salio lianze sijawahi kukopa lakini natumiwa sms kuwa deni langu ninalodaiwa sijalipa
4. Juzi nilinunua muda wa maongezi katika TIGO PESA lakini cha kushangaza wamenikata hela ktk Tigopesa lakini salio halikuongezwa mpaka muda huu
5. Tangu mwaka huu uanze sijawahi kupokelewa simu zangu katika huduma zao za customer care wao
6. Wamekuwa wezi wa salio, kwani hata kama hujatumia ukiangalia salio baada ya muda fulani unakuta limepungua
7. Niwasumbufu wakati wa mawasiliano.
Natamani niuache mtandao huu laki namba yangu ndio ninayoitegemea ktk biashara zangu na wateja wangu wengi wana namba ya tigo kuliko mitandao mengine. Swali langu wadau, Matatizo kama haya yanachukuliwa hatua na mamlaka ipi katika serikali yetu? Haki zangu nitazipata vipi, maana hapa wanakesi ya kujipatia pesa kwa njia ya utapeli.
Kwakweli inaniuma sana, INAKERA SAAAAAANA!!
Nawasilisha kero yangu