Wadada mbona kwenye hili mnajiweka nyuma kulikoni?

Phlagiey

JF-Expert Member
Oct 26, 2013
3,487
1,651
Muda wingi huwa najiuliza mbona watoto wakike wanakuwa wagumu linapokuja swala la kujitegemea kimaisha kwa maana ya kupanga nyumba na kuanzisha maisha? pengine nikafikiri labda ni waoga wa maisha, lakini jibu likaja hapana maana kuna wengine unakuwa wamemaliza masomo, wanakazi nzuri mishahara safi lakini bado wanang'ang'ania kuishi majumbani mwao, sikuishia hapo nikawaza na kuwazua labda swala la umri ndiyo tatizo jibu pia nikapata hapana kwa vile wapo amboa ni wakubwa kiumri wapo mpaka wenye miaka 25-34 na kwendelea wana kazi lakini bado hawafikiri kwenda kujipangia kachumba kake.

Baada ya maswali yote hayo nikaamua kuchukua hatua ya kutafuta majibu kwa wahusika wenyewe nilizungumza na wadada kadhaa kupitia mtandao fulani fulani hivi majibu niliyopewa yalinipa wasiwasi kidogo, wengi wao walisema wana subiri kuolewa ndiyo maana wanaamua kukaa majumbani mwao pia ukiolewa kutokea nyumbini inaongeza heshima kuliko mwanaume akikukuta ukiwa umepanga, wengine wakasema mtoto wakike akijitegemea ni rahisi kushawishika na mambo ya starehe, jibu hili likanifanya nijiulize inamaana wale wadada tunaokutana nao club za starehe wote wamepanga? na kama hawajapanga huwa wanaondokaje majumbani wao.


Mwisho nikajibiwa kwamba wazazi ndiyo wanawakatalia watoto wakike kupanga basi nikauliza sababu napewa zile zile za kushawishika kujiingiza kwenye maswala ya starehe, nikamua kuachia hapo lakini majibu ya hoja zao yako wazi kabisa nikilinganisha na mazingira halisi tunayoishi kila siku, kama ilivyo ada naomba hili swala nilirudishe kwenu wadau wa jamii forums nahitaji kusikia mawazo yenu, unakifikiri ni kwanini mtoto wakike hastahili kupanga na kuanza maisha ya kujitegemea mapema? mzazi, kaka na dada mnalizungumziaje hili.


Karibuni kwa michango yenu.

 
Phlagiey ukiwa na mtoto wakike utaelewa, wengi wanakaa na wazazi au ndugu sio kwa kupenda ni shinikizo toka kwa wazazi/ndugu. Na mtu anaona ili kupunguza maneno ngoja nikae home tu.
 
Last edited by a moderator:
Huu haukuwa utamaduni wetu,lakini hili jambo lina mapana yake!
 
Phlagiey Binti yangu kama hajaolewa nitakaa naye hata kama ni Executive Director, labda awe na kazi mbali ninapoishi ila wakiume akishapata kibarua tu anaondoka home "a man's gotta do what a man's gotta do"
 
Last edited by a moderator:
mmmhh hakuna lolote hao wanaokaa nyumbani ni waoga wa maisha tuu... wengi washazoea vya nyumbani..
Wasichana weengi sasa wanajitegemea...Je ukikaa nyumbani usipoolewa utakaa tu nyumbani hadi uzeeke? Baba na mama wakigombana umo, chochote nyumbani umo tuu?

Kuna muda wa kukaa nyumbani huo muda ukifika hata kama hujaolewa unatakiwa kutoka nyumbani uanze maisha yako upate heshima ya kujitegemea...na kutafuta vyako kwani wengi wanaoishi nyumbani hawana experience ya kutafuta vyao vingi wanavyotumia ni vyawazazi..

Pili kutoka usiku yategemea na ulivyokuzwa...Kama ni mtoto wa geti kali ukiwa kwa wazazi hutatoka ila km si wageti mbona wengi tuu hutoka night na wakitokea kwa wazazi wao? Basi wenye kuishi kwao wangekuwa BIKIRA



Muda wingi huwa najiuliza mbona watoto wakike wanakuwa wagumu linapokuja swala la kujitegemea kimaisha kwa maana ya kupanga nyumba na kuanzisha maisha? pengine nikafikiri labda ni waoga wa maisha, lakini jibu likaja hapana maana kuna wengine unakuwa wamemaliza masomo, wanakazi nzuri mishahara safi lakini bado wanang'ang'ania kuishi majumbani mwao, sikuishia hapo nikawaza na kuwazua labda swala la umri ndiyo tatizo jibu pia nikapata hapana kwa vile wapo amboa ni wakubwa kiumri wapo mpaka wenye miaka 25-34 na kwendelea wana kazi lakini bado hawafikiri kwenda kujipangia kachumba kake.

Baada ya maswali yote hayo nikaamua kuchukua hatua ya kutafuta majibu kwa wahusika wenyewe nilizungumza na wadada kadhaa kupitia mtandao fulani fulani hivi majibu niliyopewa yalinipa wasiwasi kidogo, wengi wao walisema wana subiri kuolewa ndiyo maana wanaamua kukaa majumbani mwao pia ukiolewa kutokea nyumbini inaongeza heshima kuliko mwanaume akikukuta ukiwa umepanga, wengine wakasema mtoto wakike ajitegemea ni rahisi kushawisha na mambo ya starehe, jibu hili likanifanya nijiulize inamaana wale wadada tunaokutana nao club za starehe wote wamepanga? na kama hawajapanga huwa wanaondokaje majumbani wao.


Mwisho nikajibiwa kwamba wazazi ndiyo wanawakatalia watoto wakike kupanga basi nikauliza sababu napewa zile zile za kushawishika kujiingiza kwenye maswala ya starehe, nikamua kuachia hapo lakini majibu ya hoja zao yako wazi kabisa nikilinganisha na mazingira halisi tunayoishi kila siku, kama ilivyo ada naomba hili swala nilirudishe kwenu wadau wa jamii forums nahitaji kusikia mawazo yenu, unakifikiri ni kwanini mtoto wakike hastahili kupanga na kuanza maisha ya kujitegemea mapema? mzazi, kaka na dada mnalizungumziaje hili.


Karibuni kwa michango yenu.
 
wewe ukisikia dada yako au binti yako kapanga chumba tandale au manzese anaishi mwenyewe utafurahia?
alafu nyumba yenyewe vyumba vingine wamepanga wanaume ambao hawajaowa,hakina umeme, wana share bafu na choo na jioni.

utafurahia?
 
Phlagiey Binti yangu kama hajaolewa nitakaa naye hata kama ni Executive Director, labda awe na kazi mbali ninapoishi ila wakiume akishapata kibarua tu anaondoka home "a man's gotta do what a man's gotta do"
Mkuu kimsingi hakuna sababu yoyote ya kukufanya ung'ang'ane kukaa na binti yako ilihali uwezo wa kujietegemea anao na pengine yuko radhi kufanya hivyo, kwa maamuzi hayo ni kupokonya uhuru wake.
 
wewe ukisikia dada yako au binti yako kapanga chumba tandale au manzese anaishi mwenyewe utafurahia?
alafu nyumba yenyewe vyumba vingine wamepanga wanaume ambao hawajaowa,hakina umeme, wana share bafu na choo na jioni.

utafurahia?
Hizo ndiyo changamoto za kimaisha zenyewe ambazo zitamuongezea upeo wa kufikiria zaidi juu ya maisha, swala kubwa ni yeye kukubaliana na maisha aliyoyachagua.
 
Huu haukuwa utamaduni wetu,lakini hili jambo lina mapana yake!
Kama huu ukiwa utamaduni wetu inamaana kwa wale ambao wamepanga wanavunja na kutoheshimu utamaduni wetu?

Hayo mapana yake haswa ndiyo nahitaji kusikia kutoka kwako.
 
Hizo ndiyo changamoto za kimaisha zenyewe ambazo zitamuongezea upeo wa kufikiria zaidi juu ya maisha, swala kubwa ni yeye kukubaliana na maisha aliyoyachagua.

namaanisha kwa wale ambao wanakaa wilaya moja, yaani nyumbani kwenu ni magomeni alafu binti yako hajaolewa ndio ana miaka 22 alafu anaenda kupanga manzese chumba cha namna hiyo eti ndio kuanza maisha au kuchakarika? amepanga chumba kwenye nyumba ambayo vyomba vingine wamejaa wanaume ambao hawajaowa?

kupanga kwa wadada wengi ni hapa mjini anamaliza chuo anahangaika kutafuta ajira kwao ni mkoani anapanga au akipata kazi mbali anapanga hilo ni sawa kabisa au kama katoka mkoa kuja kutafuta huku hilo sawa.

ila kama mimi baba mtu niko ubungo alafu binti miaka 20 anasema anaenda kupanga chumba mtaa wa wi pili hana mume ana anaenda kuchanganyika ovyo siwezi ruhusu.
 
wewe huzijui one night stand??? zinawapata sana hawa waliopanga na kuishi wenyewe
 
Mbona wengi wanajitegemea?
Swala hapa sio wangapi wanajitegmea na wangapi hawajitegemei, hapa tunahitaji kujua sababu zote kwa ujumla wake kama mada husika ivyozungumza juu ya swala hili.
 
mmmhh hakuna lolote hao wanaokaa nyumbani ni waoga wa maisha tuu... wengi washazoea vya nyumbani..
Wasichana weengi sasa wanajitegemea...Je ukikaa nyumbani usipoolewa utakaa tu nyumbani hadi uzeeke? Baba na mama wakigombana umo, chochote nyumbani umo tuu?

Kuna muda wa kukaa nyumbani huo muda ukifika hata kama hujaolewa unatakiwa kutoka nyumbani uanze maisha yako upate heshima ya kujitegemea...na kutafuta vyako kwani wengi wanaoishi nyumbani hawana experience ya kutafuta vyao vingi wanavyotumia ni vyawazazi..

Pili kutoka usiku yategemea na ulivyokuzwa...Kama ni mtoto wa geti kali ukiwa kwa wazazi hutatoka ila km si wageti mbona wengi tuu hutoka night na wakitokea kwa wazazi wao? Basi wenye kuishi kwao wangekuwa BIKIRA

Aisee illu...mi nakupendaga sana yan......umemaliza kila kitu...unabaki kukaa nyumbani hadi uolewe? Loh....na ndugu wakiona huolewi wakakusimanga ni haki yao kabisa..ndio si unakula vya kwao? Hakuna kitu nlikuwa nakitamani katika maisha yangu kama KUJITEGEMEA... Ndio maana miezi mitano tu baada ya kumaliza UE nishapanga niko kwenye kageto kangu ka mbavu mbili
 
Last edited by a moderator:
Woman hawajiamini na niwaoga sana.
Just fikiria tu changamoto za kuishi mwenyewe na angalia namna ke wanavyoshindwa kutumia nguvu kukabiliana na tukio mbele yao.

I hope unajua kuwa si matukio yote yahitaji akili tupu.
 
wewe ukisikia dada yako au binti yako kapanga chumba tandale au manzese anaishi mwenyewe utafurahia?
alafu nyumba yenyewe vyumba vingine wamepanga wanaume ambao hawajaowa,hakina umeme, wana share bafu na choo na jioni.

utafurahia?

Aiseee kwa hiyo we binti yako hutaki ashee choo na bafu....sie wengine ndo maisha tuliyokulia so kawaida tu yan
 
Back
Top Bottom