Wachumi tuambieni

Sanda Matuta

JF-Expert Member
May 9, 2007
949
134
Mods,kama hii haipaswi kuwa hapa mataiweka mahara husika.

Je wachumi embu tuambieni,Uchumi wa Marekani umezidi kushuka kiasi cha kuathiri kwa kiasi kikubwa shughulri zao za ki-bank.
Lakini inashangaza hapa nyumbani kwamba hiyo Hela yao yaani US DOLLAR $ imekua inapanda thamani kinyume na mambo yalivyo yaani kwa leo hii habari nilizo nazo imefika Dolla 1 =Tshs. 1220
Je Wachumi haya mambo hapa yakoje?maan hata mafuta huko kwenye soko la dunia yamefika nusu ya bei kwa pipa,ukilinganisha bei ya nyuma,sasa je? Tanzania tunaishi dunia ipi,hii hii wanayoishi wenzetu au.................?
 
Dah, kaazi kwel kweli, kiswahili kimeniacha hoi, japo umeeleweka ila jitahidi kutukuza lugha yetu hii adhimu.
 
Kwa nadhani ni the other way around, benki zina matatizo ambazo ndo zimeathiri uchumi kwa kuwa watu hawana confidence na a lot of "assets" za mabenki hayo, ambayo imesababisha kutopeana credit.
Hilo la dola kupanda TZ kweli sijui why, I guess inamaanisha dola inashuka but Shilling inashuka zaidi, hata Rand ya South Africa ni hivyo hivyo.

Mafuta nadhani ni demand and supply hapo, kama wauza mafuta wanaweza kuuza yote kwa 2000/litre hakuna haya ya kupunguza bei, kwa kuwa vyombo vya kudhibiti bei havina nguvu. Pia inawezekana bado wanauza stock ya gharama zaidi.
 
Kwa ujumla thamani ya dolla inaongezeka sio kwetu Tanzania tu hata katika nchi za EU zote. Serikali ya USA, UK,France,Germany,Italy na kadhalika zimekopesha benki zao fedha nyingi sana ili uchumi wa ulimwengu usiharibike au kuvunjika kabisa. Ndio maana utaona sasa kidogo kuna nafuu hata huko Asia.

Lakini bei ya mafuta umepungua katika nchi zote za EU kwa hiyo ni kinyume sasa kuona bei ya mafuta huko Tanzania bado iko juu sana.

Vile rasi J.K kusema kwamba serikali ya Tanzania inampango wa kuondoa fedha zake katika benki za Ulaya au Amerika si kitu cha maana sasa hivi kwa vile itakuwa ni hasara tupu. Kwanza kwa nini fedha zetu zinawekwa nje ya Tanzania. Kwa nini hatuweki fedha zetu katika bar za dhahabu katika benki yetu ya Tanzania (BOT).
Tanzania ina dhahabu ya kutosha ya kuweza kuweka uchumu wake katika gold bars benkini kwetu. Mara nyingi thamani ya dhahabu haishuki sana na kukiwa na vita inapanda.
 
Dah, kaazi kwel kweli, kiswahili kimeniacha hoi, japo umeeleweka ila jitahidi kutukuza lugha yetu hii adhimu.

Sawa nakubari,kiswahili changu hakija tulia hapo.
Naomba fanya marekebisho ya hiyo text yangu (kwa idhini yangu) hapo juu ili nione knimekosea wapi!
 
Kwa nini hatuweki fedha zetu katika bar za dhahabu katika benki yetu ya Tanzania (BOT).
Tanzania ina dhahabu ya kutosha ya kuweza kuweka uchumu wake katika gold bars benkini kwetu. Mara nyingi thamani ya dhahabu haishuki sana na kukiwa na vita inapanda.

..kwa sababu Tanzania haina dhahabu...dhahabu yote Tanzania inamilikiwa na jamaa zetu wa Kanada, Australia na Afrika Kusini!
 
..kwa sababu Tanzania haina dhahabu...dhahabu yote Tanzania inamilikiwa na jamaa zetu wa Kanada, Australia na Afrika Kusini!

Tell me you are just kidding...!!!!???
Haiwezekani dhahabu yote nchii hii iwe inamilikiwa na hao wazungu,si tunaambiwa makampuni yana milikiwa kwa ubia?
,sasa ile nusu yetu si tungeweka huko au hata hiyo nusu tuna wauzia wao?

Basi kama ni hivyo nchi hii,imeshauzwa siku nyingi na hata sisi wabongo labda ni wa-majatari wa marekani.
 
Tell me you are just kidding...!!!!???
Haiwezekani dhahabu yote nchii hii iwe inamilikiwa na hao wazungu,si tunaambiwa makampuni yana milikiwa kwa ubia?
,sasa ile nusu yetu si tungeweka huko au hata hiyo nusu tuna wauzia wao?

Basi kama ni hivyo nchi hii,imeshauzwa siku nyingi na hata sisi wabongo labda ni wa-majatari wa marekani.

Habari ndiyo hiyo.
 
Back
Top Bottom