Kama hawawezi ku 'manage' finances zao sasa tutawasaidiaje. Wao wamekalia kushindana. Kwanza lazima tuwakumbushe kuwa kazi ya ubunge walituomba tuwape kura. Wengine walituhonga na wengine wakatupigia magoti. Sasa wasilinganishe na kada nyingine ambazo wao waliajiriwa kwa kazi zao, ingawa pia napinga posho katika sekta zote. Kama pesa haziwatoshi ni kubwaga manyanga aje yule anayejitolea na sio kuwaongezea pesa. Wabunge wetu wengi wamelimbuka kwahio wanataka kujaribu kila wanachokiona mtaani
Posho zinakatika?sijakusoma please. Au unamaanisha kuwa matumizi yao ni makubwa kuweza kwenda sambamba na posho hizo? Lakini amenitisha zaidi alipodai kuwa. Mbunge anamaliza muda wake february anakata kamba. April. Ina maana kipindi hicho kifupi cha miezi miwili tu kimetosha kukwangua viji faranga vyake vyote?nna shaka! Au kuna man made issue
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.