Wabunge wazoa Sh 90mil kila mmoja kujinunulia Magari

mwingine akasema "viongozi wasijilimbikizie mali".. walichosahau ni kuwa kulikuwa na semina ya siku kumi ambapo kila mbunge alilipwa elfu 80 kwa siku kama posho!
 
Vipi yale maandamano ya nchi nzima ya kupinga hali ngumu ya maisha,niliwahi kusikia kamati kuu CDM ikitoa tamko,maana hii hali sasa inatisha CCM ndio wanaosababisha umaskini jamani tuwatoe kinguvu Mil. 90 ni nyingi sana kwa mbunge
 
Hakuna kurudisha kila mmoja achukue tu maana hii ni nchi ya wajinga. Tutakoma! Najua hata kingekuwa chama gani lazima haya yangekuwapo tu wala watu wasitake kujikosha hapa.
 
Nimetafakari na kuona kwamba uamuzi waliofanya watu wa visiwa vya Sheli Sheli ni uamuzi wa busara sana. Wao baada ya kuona viongozi wao wanawadidimiza waliamua kuwaita Wafaransa wawe wakoloni ili mradi tu walete maendeleo. Kwangu nafikiri ni wakati mwafaka hapa kwetu pia tuwaite wakoloni waje watutawale. Hawa watu tunaowaita viongozi siyo kabisa. Hakuna wanachofanya kabisa.

Mfano badala ya kununua magari 300 kwa bei ya shilingi milioni 90 wakanunua mitambo ya umeme tunaweza kutibu kabisa tatizo la mgao wa umeme hapa Tanzania. Kwani thamani ya hela zote ni dola za Kimarekani milioni 18. Nimefanya utafiti wa generator na nimeona kwamba kuna generator yenye uwezo wa kuzalisha MW 307 inauzwa $ milioni 18. Tukipata generator hii tutakuwa na upungufu wa umeme wa megawatt 43 tu. Tukifikiri zaidi ni kwamba kama mawaziri wangetumia magari ya bei ndogo tungeweza kutatua tatizo la umeme mwaka huu bila shaka.

Lakini hawa jamaa wametuasi. Mimi nasema viongozi wetu ni waasi, tunapaswa kuwapinga kwa namna zozote.

Power Plants and Generators - Equipment and Turnkey Installation
 
quote_icon.png
Originally Posted by TUKUTUKU
Mh. Lema mbunge wa Arusha akatatae hizo milioni 90 ili iwe mfano kwa wabunge wengine na wananchi kwa ujumla!!

Colleagues,

Hoja ya kukataa au kupokea pesa hizo kwa wabunge walionauchungu wa hali halisi ya wa-Tanzania maskini yaweza kuwa si ya msingi sana. Nionavyo mimi ni kuwa hata kuthubutu kutoa taharifa hiyo ni ujasiri tosha wa kimabadiliko. Yapo mambo mengi bungeni ambayo wananchi wakiyajua yatasaidia kuelimisha na kutoa mwamko wa mabadiliko kote nchini.

Wito wangu kwa wabunge jasiri ni kuwa waendelee kutoa taharifa na 'privileges' nyingine nyingi sizostahiki kwa kundi dogo la watu kama hawa ili watu wajue .
 
ivi ni kweli hizi pesha zilipitishwa kwenye bajeti iliyoisha au imekuwaje mimi nina wasi wasi sana na hili jambo.

nadhani katiba ya JMT kuna kifungu kinasema kila raia anayo haki ya kutunza rasilimali zake na za umma kwa ujumla, kama ndio ivi mbona hawa waheshimiwa wanatumia fedha zetu mimi na wewe kujinunulia magari ya kifahari wakati kuna hospitali hazina madawa hakuna wodi za kufanyia upasuaji kama hapa mawenzi hospital .

by the way bob marley once said. Emancipate your self from memntaly slsvery non but ourselves can free our mind.

we need to know wabunge wako kwa ajili yao au kwa ajili yetu sisi na tuliowapigia kura. inasikitisha kuona mbunge mmoja anapewa gari then watu wa jimbo lake wanatumia bajaji kwenda hospitalini
 
Watawala Tz!
Hawaishi kwa uwezo wa mifuko yao
Hawaishi katika uhalisia wa maisha ya raia wake
Hawaoni sababu kwa nini wasiendelee kutumbua
Hawana utu wala maono ya kuitoa nchi ktk umaskini
Ni wabinfasi, walafi na wanafiki wakubwa.

Ee MUNGU inusuru Tz!
 
haya wapinzani wa kweli huu ndio muda wa kususia hizo fedha kama mnavyo susia vikao vya bunge na kuitisha maandamano makubwa kupinga ulipwaji wa mil 90 kwa manunuzi ya magari ya kifahari wakati wagonjwa wanalazwa mzungu wa nne hospitalini.
 
Watawala Tz!
Hawaishi kwa uwezo wa mifuko yao
Hawaishi katika uhalisia wa maisha ya raia wake
Hawaoni sababu kwa nini wasiendelee kutumbua
Hawana utu wala maono ya kuitoa nchi ktk umaskini
Ni wabinafsi, walafi na wanafiki wakubwa.

Ee MUNGU inusuru Tz!
 
Nasubiri kwa hamu kweli kweli msimamo wa Chadema kuhusu hii inconsistence ya sera na vitendo. Kwamba wanataka kuondoa umaskini uliokithiri kwa wananchi na wakati huo huo wanatumia rasilimali za wananchi kujilimbikizia huku wakitutangazia kwamba viongozi wasijilimbikizie!
 
Tuache porojo za kwenye majukwaa na dhana ya "staki nataka".Wabunge wa CDM kama kweli ni Wazalendo na njaa zao haziwazibi macho wafanye yafuatayo na wathibitishie umma wa Watanzania kuwa si sawa na CCM Club:
1.Kuamua kwa kauli moja kuzikataa ama kurudisha pesa hizo kama wamekwisha chukua.
2.Kuchukua na kuzielekeza kwenye matatizo ya Wananchi (Elimu,Afya & Ajira).
3.Kuzigawa kwa wao kupata usafiri wa bei nafuu(RAV 4) na kiasi kingine kuelekeza kwa Wananchi.

Ni mbunge mmoja wa CCM(Lameck Airo) ndiye aliyetamka kubadili matumizi ya hizo fedha kwa kununua katapila ya kuchonga barabara jimboni kwake.

Tunaomba CDM watoe tamko kati ya hayo na si porojo za "ndumilakuwili".
 
lakini hlo mbona ni swala la kawaida kabisa kila baada ya uchaguzi ma MP wote hupewa?
CDM ni wachache sana zaidi ya hao wababe CCM , hivyo hata wakizikataa wale jamaa wataendelea kuzitanua tu
sasa bora kipi?
pia kumbuka kuwa hata wakizikataa hizo pesa hazitzrudishwa HAZINA ng'o zinaishia tu mikononi mwa wajanja.
Nasubiri kwa hamu kweli kweli msimamo wa Chadema kuhusu hii inconsistence ya sera na vitendo. Kwamba wanataka kuondoa umaskini uliokithiri kwa wananchi na wakati huo huo wanatumia rasilimali za wananchi kujilimbikizia huku wakitutangazia kwamba viongozi wasijilimbikizie!
 
Tuache porojo za kwenye majukwaa na dhana ya "staki nataka".Wabunge wa CDM kama kweli ni Wazalendo na njaa zao haziwazibi macho wafanye yafuatayo na wathibitishie umma wa Watanzania kuwa si sawa na CCM Club:
1.Kuamua kwa kauli moja kuzikataa ama kurudisha pesa hizo kama wamekwisha chukua.
2.Kuchukua na kuzielekeza kwenye matatizo ya Wananchi (Elimu,Afya & Ajira).
3.Kuzigawa kwa wao kupata usafiri wa bei nafuu(RAV 4) na kiasi kingine kuelekeza kwa Wananchi.

Ni mbunge mmoja wa CCM(Lameck Airo) ndiye aliyetamka kubadili matumizi ya hizo fedha kwa kununua katapila ya kuchonga barabara jimboni kwake.

Tunaomba CDM watoe tamko kati ya hayo na si porojo za "ndumilakuwili".

mkuu... mbona unaelekeza kwa CDM tuu... si kuna KAFU, NCCR na UDP ...hao huwaoni ..bado sikuelewi
 
Tatizo ni kwamba hao wabunge hawana mawazo endelevu kama hayo, wao wanajali tu matumbo yao
leo wakishiba yatosha, kwnai kesho hawana shida nayo kabisa.
Wangelikuwa wanafanya vitu kwa ajiri ya kizazi kijacho basi wasingekuwa wanafanya upuuuzi huo
Nimetafakari na kuona kwamba uamuzi waliofanya watu wa visiwa vya Sheli Sheli ni uamuzi wa busara sana. Wao baada ya kuona viongozi wao wanawadidimiza waliamua kuwaita Wafaransa wawe wakoloni ili mradi tu walete maendeleo. Kwangu nafikiri ni wakati mwafaka hapa kwetu pia tuwaite wakoloni waje watutawale. Hawa watu tunaowaita viongozi siyo kabisa. Hakuna wanachofanya kabisa.
Mfano badala ya kununua magari 300 kwa bei ya shilingi milioni 90 wakanunua mitambo ya umeme tunaweza kutibu kabisa tatizo la mgao wa umeme hapa Tanzania. Kwani thamani ya hela zote ni dola za Kimarekani milioni 18. Nimefanya utafiti wa generator na nimeona kwamba kuna generator yenye uwezo wa kuzalisha MW 307 inauzwa $ milioni 18. Tukipata generator hii tutakuwa na upungufu wa umeme wa megawatt 43 tu. Tukifikiri zaidi ni kwamba kama mawaziri wangetumia magari ya bei ndogo tungeweza kutatua tatizo la umeme mwaka huu bila shaka.
Lakini hawa jamaa wametuasi. Mimi nasema viongozi wetu ni waasi, tunapaswa kuwapinga kwa namna zozote.
Power Plants and Generators - Equipment and Turnkey Installation
 
mkuu... mbona unaelekeza kwa CDM tuu... si kuna KAFU, NCCR na UDP ...hao huwaoni ..bado sikuelewi
Hapo umesema ukweli,
wabunge karibu wote ni uozo tu.
Ila CDM wakifanya basi itakuwa ni fundisho kwa wengine wote.
 
lakini hlo mbona ni swala la kawaida kabisa kila baada ya uchaguzi ma MP wote hupewa?
CDM ni wachache sana zaidi ya hao wababe CCM , hivyo hata wakizikataa wale jamaa wataendelea kuzitanua tu
sasa bora kipi?
pia kumbuka kuwa hata wakizikataa hizo pesa hazitzrudishwa HAZINA ng'o zinaishia tu mikononi mwa wajanja.

Aaaa Mallaba bana, there must be an impact. Pinda alikataa shangingi ilikuwa ni milestone ingawa wengi walibeza nadhani kuna impact katika uamuzi wa serikali kupanga kununua mashangingi in the future.

Sina uhakika sana kwamba hizo pesa hazitarudi hazina, zingatia Zitto ni waziri wa fedha kivuli bwana atafuatilia.

Lakini jiulize pia impact itakayowapata Chadema kama wakikubali hayo mashangingi. Yaani waswahili wanasema heri nusu shari kuliko shari kamili au siyo mkuu.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom