Gurudumu
JF-Expert Member
- Feb 5, 2008
- 2,349
- 261
Wabunge wazoa Sh90mil kila mmoja
Tuesday, 15 February 2011
Mwandishi Wetu, Dodoma
JUMLA ya Sh3.24 bilioni zimelipwa kwa wabunge ili kuwawezesha kununua magari binafsi kwa ajili ya shughuli za kibunge, imeelezwa.
Kwa mujibu wa habari hizo kila mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amelipwa Sh90 kwa ajili ya kujinunulia gari.
Aidha, wabunge hao wapatao 360 wamekatiwa bima ya afya inayotarajiwa kuanza kutumika kabla ya mwezi Juni mwaka huu.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika uzinduzi wa Tawi la Chadema, Mipango Kata ya Miyuji mkoani Dodoma wabunge wa Chadema, walisema kuwa wanashangazwa na hatua ya Rais Kikwete kuweka pikipiki za matairi matatu (Bajaji) kama moja ya vipaumbele vyake ili zitumike kubeba wajawazito wakati wabunge wanalipwa mamilioni.
Katika hotuba yake ya kulizindua bunge Kikwete alieleza mpango wa serikali yake kununua pikipiki hizo 400 zitakazosambazwa maeneo mbalimbali hasa vijijini kwa ajili ya kuwabebea wajawazito kama njia ya kupunguza matatizo ya usafiri kwenye maeneo hayo.
"Ndugu zangu hali ni mbaya, siku moja tutafanya maandamano bungeni, sio kutoka nje ya ukumbi. Inashangaza, tumepewa Sh90 milioni za magari kwa wabunge wote, huku bungeni tunajadili bajaji kuwa 'ambulance'(gari ya kubebea wagonjwa),'" alisema mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema.
Alisema mbali na hilo katika hali inayoonyesha kuwa hospitali za serikali ni mbaya, katika semina iliyofanyika Dar es Salaam hivi karibuni, wabunge waliomba kuwekewa bima za afya, kutibiwa nje ya nchi na katika hospitali binafsi hapa nchini.
Aliongeza kuwa: Ndoto ya kuiondoa CCM ni 'serious' (thabiti), lakini mkifanya noma ya kupata haki, hiyo imebarikiwa. Kama (CCM) wanafikiri wanaweza kuendesha nchi watakavyo, sasa hawawezi, ninyi vijana msipojitoa kwa sasa nchi itakufa."
Alikwenda mbali zaidi akisema anaomba wake za viongozi wapate ujauzito na kupakiwa katika bajaji hizo wakati wa uchungu kwenda kujifungua ili waone adha ya usafiri huo itakavyokuwa.
Akiongea katika mkutano huo naye mbunge Tundu Lissu aliwataka wananchi kutoogopa mabadiliko na kwamba historia haiheshimu watu wanaoogopa.
""Historia haiheshimu wanaoogopa, tusije kusahau bei ya mabadiliko, bei yake ni kupigwa, kufungwa hata bei kubwa zaidi ya kifo," alisema Lissu.
My take: Nakubaliana na uchungu walionao hawa makamanda, nasubiri kuona watafanyaje kuhusu hizo Sh 90mil
Tuesday, 15 February 2011
Mwandishi Wetu, Dodoma
JUMLA ya Sh3.24 bilioni zimelipwa kwa wabunge ili kuwawezesha kununua magari binafsi kwa ajili ya shughuli za kibunge, imeelezwa.
Kwa mujibu wa habari hizo kila mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amelipwa Sh90 kwa ajili ya kujinunulia gari.
Aidha, wabunge hao wapatao 360 wamekatiwa bima ya afya inayotarajiwa kuanza kutumika kabla ya mwezi Juni mwaka huu.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika uzinduzi wa Tawi la Chadema, Mipango Kata ya Miyuji mkoani Dodoma wabunge wa Chadema, walisema kuwa wanashangazwa na hatua ya Rais Kikwete kuweka pikipiki za matairi matatu (Bajaji) kama moja ya vipaumbele vyake ili zitumike kubeba wajawazito wakati wabunge wanalipwa mamilioni.
Katika hotuba yake ya kulizindua bunge Kikwete alieleza mpango wa serikali yake kununua pikipiki hizo 400 zitakazosambazwa maeneo mbalimbali hasa vijijini kwa ajili ya kuwabebea wajawazito kama njia ya kupunguza matatizo ya usafiri kwenye maeneo hayo.
"Ndugu zangu hali ni mbaya, siku moja tutafanya maandamano bungeni, sio kutoka nje ya ukumbi. Inashangaza, tumepewa Sh90 milioni za magari kwa wabunge wote, huku bungeni tunajadili bajaji kuwa 'ambulance'(gari ya kubebea wagonjwa),'" alisema mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema.
Alisema mbali na hilo katika hali inayoonyesha kuwa hospitali za serikali ni mbaya, katika semina iliyofanyika Dar es Salaam hivi karibuni, wabunge waliomba kuwekewa bima za afya, kutibiwa nje ya nchi na katika hospitali binafsi hapa nchini.
Aliongeza kuwa: Ndoto ya kuiondoa CCM ni 'serious' (thabiti), lakini mkifanya noma ya kupata haki, hiyo imebarikiwa. Kama (CCM) wanafikiri wanaweza kuendesha nchi watakavyo, sasa hawawezi, ninyi vijana msipojitoa kwa sasa nchi itakufa."
Alikwenda mbali zaidi akisema anaomba wake za viongozi wapate ujauzito na kupakiwa katika bajaji hizo wakati wa uchungu kwenda kujifungua ili waone adha ya usafiri huo itakavyokuwa.
Akiongea katika mkutano huo naye mbunge Tundu Lissu aliwataka wananchi kutoogopa mabadiliko na kwamba historia haiheshimu watu wanaoogopa.
""Historia haiheshimu wanaoogopa, tusije kusahau bei ya mabadiliko, bei yake ni kupigwa, kufungwa hata bei kubwa zaidi ya kifo," alisema Lissu.
My take: Nakubaliana na uchungu walionao hawa makamanda, nasubiri kuona watafanyaje kuhusu hizo Sh 90mil
Asante kwa kuwatetea ila naomba nikuulize tuseme mshahara wa mbunge ni milioni 2 kama alivyosema mh Sitta:-
a. Unsecured loan yenye lowest risk ni ile ya miezi kumi na mbili so 2,000,000 x 12 = 24,000,000 (hatujaweka interest ya 20% walalahoi wanalipa kule katika mabenki)
b. Loan za kawaida zinategemea na mapato na biashara unayofanya.
Turejee katika mkopo wa wabunge:-
a. Tukicalculate Pay Back Period milioni 90 = 90,000,000/ 2,000,000 = 45 months = 3.75 almost 4 years
b. Wabunge muda wao bungeni ni 5 years.
c. Wakimaliza wanapata kiinua mgongo bungeni cha milioni kama 60,000,000.
Sasa tuulizane je wanahaki ya kupata hizo milioni 90?? for 4 years? Ni wafanyakazi wangapi wanapata mikopo hiyo? Tena mbaya zaidi ni zero interest for 4 years wakati walalahoi wanakatwa na interest inakuwaje? Vilevile nikuulize ahadi za JK za bajaji na ambulance bajaji kwa wamama wajawazito wewe unahisi ni sahihi halafu wabunge wachukue milioni 90 za kununulia mikoko ambayo tayari wanayo??
Ushauri wangu:-
a. Wabunge wasipewe mkopo wa magari wakitaka wakachukue mkopo benki wa kununua gari.
b. Wabunge wasipewe nyumba bali wapewe allowance ya nyumba ambayo hiyo ni rahisi kuwa audited na inasaidia kusave hela.
c. Wabunge wapewe allowance ya petrol na sio kujaziwa mafuta tupate kusave hela.