Wabunge waigeuka TANESCO

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,004
Waungwana, hawa wabunge wa CCM wanaonyesha upumbavu wao wa hali ya juu na kutaka kuwatumia lawama watendaji wa TANESCO ambao hawahusiki kabisa na matatizo ya shirika hilo.

Uendeshaji wa TANESCO ulikabidhiwa kwa makaburu wa net group ambao waliingizwa pale kwa mtutu wa bunduki za FFU enzi za fisadi Mkapa. Walilipwa mabilioni ya pesa pamoja na kuwa walikuwa hawajui chochote kuhusiana na uzalishaji na usambazaji wa umeme. Waliondooka makaburu wale waliiacha TANESCO katika hali mbaya kuliko walivyoikuta.

Mkataba wa IPTL ambao TANESCO inatakiwa kuwalipa hao jamaa bilioni nne kila mwezi hata kama hawazalishi umeme. Mkataba wa Richmond, TANESCO inawalipa hao mafisadi shilingi 152 millioni pamoja na kuwa hawazalishi chochote. Gesi toka Songo songo pamoja na kuwa ni ya kwetu lakini TANESCO wanailipia bei kubwa sana.

Yote haya hawa wabunge wanafiki hawayaoni, sasa wanawarushia watendaji wa TANESCO lawama kuhusiana na matatizo mbali mbali ndani ya shirika hilo!

Mimi nawaambia Wabunge hao wa CCM acheni unafiki na mawazo ya kifisadi! Watanzania tumechoshwa na usanii wenu!


Wabunge waigeuka Tanesco

na Salehe Mohamed, Dodoma

KATIKA hali isiyotarajiwa, baadhi ya wabunge wameligeuka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na kudai kuwa matumizi mabovu ya fedha yanayofanywa na watendaji wake, ndiyo yaliyolifikisha shirika hilo hapo lilipo kiasi cha kushindwa kuzalisha umeme wa kutosha, hivyo kutegemea ruzuku ya serikali.

Aidha, wabunge hao walisema watendaji wa Tanesco walipopata nafasi za kuliendesha shirika hilo, walifikiria zaidi kuwapeleka watoto wao shule nje ya nchi na mambo mengine, badala ya kufikiria zaidi maendeleo ya shirika.

Wabunge hao walionyesha msimamo huo jana wakati wakichangia muswada wa umeme, uliowasilishwa na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja.

Msimamo huo ni tofauti na ule waliouonyesha Februari mwaka huu, wakati walipoukataa muswada huo katika semina iliyoandaliwa na wizara kwa ajili ya kuwapatia ufafanuzi kuhusu miswada ya nishati.

Aidha, wabunge waliendelea na msimamo huo hata katika semina ya pili kuhusu miswada hiyo, iliyofanyika wiki chache zilizopita jijini Dar es Salaam.

Walikuwa wakiupinga muswada wa umeme kwa maelezo kuwa sheria hiyo itasababisha kifo kwa Tanesco, kwa kukaribisha wawekezaji binafsi wakati shirika hilo liko taabani kifedha.

Wabunge walibainisha kuwa, serikali inapaswa kwanza kuiwezesha Tanesco kuwa imara kifedha kwa sababu yenyewe (serikali) ndiyo imechangia shirika hilo kuporomoka.

Lakini kwa mshangao, tofauti na ilivyokuwa siku za nyuma wakati wa semina kuhusu muswada huo ambapo wabunge wengi walitamka maneno makali kuupinga, na kuapa kutoupitisha kwa madai una lengo la kuiua Tanesco, jana wengi walionekana kuukubali na kuliponda Shirika la Tanesco.

Kabuzi Rwilomba (Busanda-CCM) ndiye aliyekuwa wa kwanza kuelekeza mashambulizi kwa Tanesco na kuusifia muswada huo, akisema kuwa awali aliupinga kwa sababu hakuuelewa vema.

Alisema kuwa muswada huo umekuja wakati muafaka na utasaidia kiasi kikubwa kuleta mabadiliko katika sekta ya nishati ya umeme, ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikitawaliwa na Tanesco ambayo hivi sasa ipo taabani.

Rwilomba alisema kwa muda mrefu shirika hilo limekuwa likijiendesha kwa hasara pamoja na kushindwa kufikisha umeme maeneo ya vijijini, na watendaji wake wamekuwa na matumizi mabovu ya fedha zinazopatikan.

Alisema serikali imeamua kuisadia fedha Tanesco, ili iweze kujikwamua katika matatizo iliyonayo, lakini hazitakuwa na maana kama watendaji wake hawatazitumia katika maendeleo.

Rwilomba alisema historia ipo wazi kwa watendaji wa shirika hilo wanapopata fedha hufikiria zaidi kuwasomesha watoto wao nje ya nchi, badala ya kuangalia namna ya kuzalisha umeme pamoja na kuwapelekea watu wa vijijini ambao kwa muda mrefu wamekosa huduma hiyo.

"Tanesco ndugu zangu mnapobebwa na nyinyi mjibebe, fedha mtakazopewa na serikali mzitumie kuboresha shirika na wala si kwa ajili ya kujinufaisha, kwani mkifanya hivyo mtakwisha hasa baada ya kuja kwa kampuni binafsi za kuzalisha umeme," alisema Rwilomba.

Aidha, mbunge huyo aliwaonya watendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA), ambayo kwa mujibu wa muswada huo, ndio watakuwa na jukumu la kukubali wawekezaji katika sekta hiyo, kutoitumia fursa hiyo kujinufaisha kwa kupitisha watu wasio na uwezo kama ilivyotokea huko nyuma.

Alisema Tanzania ina historia nzuri na mifano ya wawekezaji wasio na uwezo wa kuwekeza katika sekta hiyo kiasi cha kulisababishia taifa hasara kubwa ambayo mpaka hivi sasa inaendelea kuibeba.

Mbunge mwingine aliyeishambulia Tanesco alikuwa ni Luhaga Mpina (Kisesa-CCM) aliyesema tatizo kubwa la Tanzania ni usimamizi mbovu wa sheria ambazo zinakuwa zimetungwa kwa malengo mazuri, ila utekelezaji wake ndio unaozua tafrani.

Alisema ni aibu kwa mashirika ya umma kushindwa kufanya kazi katika sekta husika ilhali mashirika ya watu binafsi yanafanya vizuri katika sekta hiyo hiyo.

Alisema kuwa ripoti ya ukaguzi wa hesabu iliyotolewa hivi karibuni inaonyesha Tanesco imepata hasara ya sh bilioni 183 ambazo kama wangekuwa makini zingeweza kuwasaidia kuboresha shughuli zao.

"Hasara waliyopata hawa jamaa ni kubwa na kusingekuwapo na matatizo hayo, ingewasaidia katika shughuli zao za kila siku na kupunguza tatizo la kutegemea ruzuku," alisema Mpina.

Alisema kuna haja ya kuangalia sheria iliyoanzisha mashirika ya umma na kuifanyia marekebisho ili watendaji wake waweze kufanya kazi kulingana na sheria zitakazowekwa, kukomesha tabia ya kulegalega na kusababisha hasara ambazo zinaweza kuzuilika.

Mpina alisema mipango mingi ya mashirika hayo pamoja na ile ya serikali haitekelezwi hivyo kukwamisha shughuli za maendeleo ambazo zingekuwa na tija kwa taifa na wananchi wake katika harakati za kukuza uchumi na kuondokana na umasikini.

"Kutotekelezeka kwa mipango hii ni sawa na ufisadi kwa wananchi ambao wanahitaji huduma muhimu kama vile umeme, maji, barabara na mengineyo ili waweze kujikwamua kiuchumi," alisema Mpina.

Alisema haoni kama kweli serikali imedhamiria kuboresha huduma za umeme vijijini kwani mwaka 2007/08 zilihitajika sh trilioni 1.2, lakini zilizopitishwa ni sh bilioni 10 tu, jambo ambalo alisema ni mzaha kwa wananchi wenye kiu ya kupata umeme wa uhakika.

Naye Jeanista Mhagama, (Peramiho-CCM), alisema ni vema EWURA ikajiepusha kuwapatia leseni wawekezaji wanaotaka kuwekeza mjini pekee, kwani maeneo hayo tayari yana umeme wa uhakika.

Alishauri mamlaka hiyo iwabane wawekezaji wapya kuwekeza maeneo ya vijijini ambako kuna shida kubwa ya kutopatikana kwa umeme.

"Hapa ni lazima hawa ndugu zetu EWURA wawe macho katika leseni, hasa kwenye maeneo ya vijijini, lakini wasipofanya hivyo kuna hatari kila mwekezaji kukimbilia mjini na hivyo watu wa vijijini kuendelea na tatizo la kutokuwa na umeme wa kutosha," alisema Mhagama.

Aidha, alisema kama Tanesco watawezeshwa vizuri wanaweza kuwekeza vizuri maeneo ya mjini na karibu na wawekezaji wa sekta binafsi wapewe maeneo ya vijijini, hivyo kuwepo kwa mgawanyo wa umeme.

Awali, msemaji wa kambi ya upinzani, Mohamed Habib Mnyaa (Mkanyageni-CUF), alitoa angalizo kuhusu kifungu cha 11 cha muswada huo, ambacho kinahusu kuhamisha umiliki kwa mwekezaji.

Alisema Tanzania imepata fundisho kutoka kwa Richmond na Dowans, hivyo ni vema kifungu hicho kikawabana wawekezaji watakaoshindwa kuzalisha umeme mkataba wao uvunjwe na si kuhamisha umiliki.

"Kifungu hiki ni lazima kifanyiwe marekebisho, la sivyo tutawapa nafasi wawekezaji wasio makini kuja kuwekeza hapa nchini na kuwaacha wawekezaji makini kama ilivyofanyika kwa Dowans na Richmond," alisema Mnyaa.

Aidha, alisema pia ni vema muswada huo ukaangalia njia za kuwafanya wawekezaji wauze umeme wanaouzalisha hapahapa nchini na kutosheleza soko kabla ya kuuza nje.

Alisema hilo lisipofanyika, upo uwezekano wa kuwapata wawekezaji ambao watauza umeme wao wote nje ya nchi, hata kama kuna upungufu wa nishati hiyo nchini.

Muswada huo ulishindikana kuwasilishwa katika mkutano wa 10, baada ya wabunge kuupinga kwa nguvu zote, licha ya kufanyiwa semina elekezi.

Inaaminika kuwa imefanyika kazi kubwa ya kuwashawishi wabunge mmoja mmoja, hasa wale waliokuwa wameonyesha msimamo mkali, ili waukubali muswada huo ambao umeonekana kugusa hisia za wabunge wengi.

Wakati unaanza kujadiliwa jana, tayari wabunge 50 walikuwa wamejiandikisha kuomba kuchangia wakati miswada mingine iliyowasilishwa kwenye mkutano huu, ilikuwa ikichangiwa na wabunge chini ya saba.


[
Maoni ya Wasomaji
Maoni yanayotolewa na wasomaji wa safu hii ni ya kwao na sio maoni ya kampuni ya Freemedia Ltd. Aidha sio maoni ya mtunzi au mwandishi wa habari au makala husika hapo juu. Maoni haya hayajahakikiwa wala kuafikiwa na kampuni ya Freemedia Ltd.
Maoni 3 yameshatolewa. (Nawe toa maoni yako!)
Wabunge kwa kawaida hawatuwakilishi wananchi tulio wachagua,wako bungeni kwaajili ya kuganga njaa zao.Hili litaendelea kuwa tatizo kubwa kwa Tanzania kama tusipowabadili na kuleta uwiano ulio sawa na wapinzani.Serekali mara nyingi inawaonga wabunge kwa kuleta semina kabla ya kupeleka miswada bungeni hivyo bunge linakuwa kama muhuri tu.

na G KABONDE, ARUSHA,TANZANIA, - 19.04.08 @ 14:05 | #7410

Naungana na Kabonde kusema kwamba ni kweli wapo Wabunge wanaochangia hoja kwa ajili ya kuganga njaa na kujipendekeza. Ni hivi karibu gazeti moja lilitoa taarifa kwamba yasemekana baadhi ya Wabunge wa Viti Maalum walikuwa wamepewa mgao (hongo) na Rostam ili wampigie sana makofi atakapowasilisha hoja yake! Waswahili wanasema 'lisemwalo lipo na kama halipo laja'! Bunge letu hata lijikoshe vipi limeoza, maana wengi wa waliomo ndani ya Bunge hilo wameingia humo kwa kutumia pesa na si kwa utashi wa haki wa wananchi. Tunaomba Wabunge waweke maslahi ya nchi na ya wananchi mbele. Vinginevyo watapata laana na hukumu yao itakuwa hapa hapa duniani! Mwenyezi Mungu anayaona mateso ya wananchi kutokana na matendo ya Wabunge wa aina hiyo.

na Mswazi, dsm, - 19.04.08 @ 16:58 | #7445

KWA HIYO MJIULIZE KAMA MOTIVATION YA WABUNGE WETU NI 'INTELLECTUAL REASONING' AU 'EMOTIONAL EXPRESSIONISM'. KAMA NI 'INTELLECTUALISM', BASI HOJA HAIBADILIKI KAMA MUSWADA HAUJABADILIKA. KAMA NI 'EMOTIONALISM', SITASHANGAA WATU WAKIBADILKA BADILIKA. AFTER ALL, NI WACHACHE SANA WANAFANYA CRITICAL ANALYSIS YA KUTOSHA.
 
Bubu,

Hao wawili walio laumu TANESCO ni wasaliti ambao wamenunuliwa na mshiko wa "vijisenti"!

Baada ya Agenda 21 kushindwa kuwasilisha hoja ya Rostam eti kuliumbua "Bunge" sasa utaona uchumozi wa kila aina ya uyoga kubadilisha hali halisi ya kubana wale viongozi wa Serikali ambao wanashutumiwa kwa Uhujumu.
 
Kwa nini ni dhambi kuwakosoa menejimenti ya Tanesco? Kwa vile tu ni wazawa wenzetu? Get real, matatizo ya haya mashirika yetu hayakuanza na kuja kwa hao makaburu. Si Tanesco, si ATC! mimi nawa support hawa wabunge maana wakati umefika kuwaangalia hao waliopewa dhamana ya kuendesha mashirika haya ya huduma bila kujali rangi, utaifa, usomi wala jinsia!
 
Kwa nini ni dhambi kuwakosoa menejimenti ya Tanesco? Kwa vile tu ni wazawa wenzetu? Get real, matatizo ya haya mashirika yetu hayakuanza na kuja kwa hao makaburu. Si Tanesco, si ATC! mimi nawa support hawa wabunge maana wakati umefika kuwaangalia hao waliopewa dhamana ya kuendesha mashirika haya ya huduma bila kujali rangi, utaifa, usomi wala jinsia!

Kwa lipi walilolifanya mpaka wakosolewe!? Walihusika na kusani mikataba ya kifisadi?:confused:
Hawakuhusika na chochote katika kusaini mikataba ya kifisadi ya IPTL, Richmonduli, Songa na Net group ambayo ndiyo inakula asilimia kubwa ya mapato kuliko kitu kingine chochote katika shirika hilo. Kusaini mikataba ya kifisadi wafanye mafisadi Mkapa, Lowassa, Msabaha, Karamagi na wengineo halafu walaumiwe watendaji wa juu wa TANESCO! :confused: You are the one who is suppose to get real!
 
Kwa nini ni dhambi kuwakosoa menejimenti ya Tanesco? Kwa vile tu ni wazawa wenzetu? Get real, matatizo ya haya mashirika yetu hayakuanza na kuja kwa hao makaburu. Si Tanesco, si ATC! mimi nawa support hawa wabunge maana wakati umefika kuwaangalia hao waliopewa dhamana ya kuendesha mashirika haya ya huduma bila kujali rangi, utaifa, usomi wala jinsia!

Fundi Mchundo,

Tanesco kuna menejmenti mpya ambayo haina hata mwaka tangu iingie madarakani. Imekutana na vigingi elfu ambavyo vinatokana na mipango mibaya ya Serikali kuu ambayo ilipuuziwa kuwajibishwa na Bunge.

Mfano, suala la Deni sugu la Serikali (zote za Muungano na Zanzibar) kwa Tanesco, hilo ni kosa la Menejimenti au ni Serikali ambayo inatumia nguvu zake na hata mamlaka kama EWURA kuhakikisha kuwa gharama za uovu wa Serikali zinatupwa kwa Fundi Mchundo na Kishoka na kisha lawama wapewe Tanesco?

Nilichopinga si Tanesco kushikiwa bango, bali hoja zilizotolewa na hawa wabunge wawili ni za kipuuzi kabisa hasa wakati huu ambao ni dhahiri kuwa Serikali yetu na vibaraka wa Uhujumu wana nia ya kuliangamiza Tanesco kwa kudai kuletwe ushindani wa utoaji umeme, huku hujuma kubwa zilizofanya Tanesco ishindwe kufanya kazi zake vizuri zilitokana na tamaa za viongozi wa Serikali na kukosekana kwa msimamo kwa Serikali kulinda Taifa.

Labda nikuulize, je Kwa nini Serikali ilikataa kuipa fedha Tanesco kufanya marekebisho makubwa ya Mfumo wake wa Ugavi wa Umeme na badala yake kutumia nguvu za Kiserikali kulishurtisha Tanesco iingie mikataba kama IPTL na RDC ambayo tumekuja gundua kuwa ilikuwa ni bomu na fedha za mikataba hiyo zingepewa Tanesco, tusingekuwa na matatizo ya umeme ambao tumeyapata?
 
Umewahi kuomba uunganishiwe umeme hivi karibuni? Kamsome Kithuku alivyoandika upate machungu yake. Tusitumie hiyo mikataba mibovu kuwakumbatia watendaji wabovu. Hii menejimenti ndiyo iliyomkatia mteja anayelipa mamia ya mamilioni kwa mwezi kwa deni la milioni hamsini! hii menejimenti ndiyo ilienda kwa waandishi wa habari kutoa vitisho dhidi ya mteja huyo wakati wameishalipwa siku kadhaa kabla! Hii menejimenti imeshindwa kutoa ripoti ya namna wanavyopunguza gharama za uzalishaji! Hii menejimenti ndiyo imepata hasara hiyo ya mabilioni.Unataka nini zaidi? Hakuna anayesema kuwa mikataba ya IPTL, Songas n.k ina matatizo yake. La hasha, ninachokataa ni hii tabia ya kutaa kumkosoa mtu ati kwa sababu ni mzalendo mwenzetu. Kutupia hela matatizo siyo solution hata siku moja. Sasa, Mkuu, wewe niambie ni mafanikio gani ambayo tanesco wamepata tangu hao Net Group waondoke? Ah, najua, hawawezi kufanya kitu kwa sababu ya madeni ya IPTL! Haya, wameweza kueleza katika hicho kidogo wanachopata wanamipango gani ya kukiongezea? Ah, ni wakina Richmond tena! Get real, ndugu yangu, watu wengi wanaumia na utendaji mbovu wa Tanesco usio na uhusiano hata kidogo na hayo madeni.
 
Fundi Mchundo,

Tanesco kuna menejmenti mpya ambayo haina hata mwaka tangu iingie madarakani. Imekutana na vigingi elfu ambavyo vinatokana na mipango mibaya ya Serikali kuu ambayo ilipuuziwa kuwajibishwa na Bunge.

Mfano, suala la Deni sugu la Serikali (zote za Muungano na Zanzibar) kwa Tanesco, hilo ni kosa la Menejimenti au ni Serikali ambayo inatumia nguvu zake na hata mamlaka kama EWURA kuhakikisha kuwa gharama za uovu wa Serikali zinatupwa kwa Fundi Mchundo na Kishoka na kisha lawama wapewe Tanesco?

Nilichopinga si Tanesco kushikiwa bango, bali hoja zilizotolewa na hawa wabunge wawili ni za kipuuzi kabisa hasa wakati huu ambao ni dhahiri kuwa Serikali yetu na vibaraka wa Uhujumu wana nia ya kuliangamiza Tanesco kwa kudai kuletwe ushindani wa utoaji umeme, huku hujuma kubwa zilizofanya Tanesco ishindwe kufanya kazi zake vizuri zilitokana na tamaa za viongozi wa Serikali na kukosekana kwa msimamo kwa Serikali kulinda Taifa.

Labda nikuulize, je Kwa nini Serikali ilikataa kuipa fedha Tanesco kufanya marekebisho makubwa ya Mfumo wake wa Ugavi wa Umeme na badala yake kutumia nguvu za Kiserikali kulishurtisha Tanesco iingie mikataba kama IPTL na RDC ambayo tumekuja gundua kuwa ilikuwa ni bomu na fedha za mikataba hiyo zingepewa Tanesco, tusingekuwa na matatizo ya umeme ambao tumeyapata?

Mimi imani yangu na uwezo wa kujiendesha wa Tanesco ulitokana na jinsi walivyolishughulikia suala la Tanga Cement. Shirika lililo katika matatizo makubwa ya kipesa kama wote tunavyoelewa kumfanyia vile mmoja wa wateja wako wakuu, kwangu mimi ni dalili tosha ya incompetence. Kukimbila kumpandishia bei mteja bila ya kwanza kutuambia wanafanya nini kupunguza gharama za uendeshaji (na gharama zote hazitokani na hayo madeni tu! hautujaelezwa mishahara, makongamano, safari za wakubwa, vikao vya bodi na menejimenti n.k ni kiasi gani?) ni alama nyingine ya uzembe. Mimi sio kuwa nafagilia ubinafsishaji, la hasha. Ninachotaka mimi ni kuwa darubini lielekezwe kwanza kwenye utendaji wao na tukishajihakikishia kuwa wanastahili ndiyo tuanze kufikiria kuwatupia mihela mingine. La sivyo, tutarudi hapa hapa hata kama hiyo mikataba mibovu ikivunjwa. Na, Mkuu, hauhitaji mwaka mzima kumpima mtu.
 
Hata bila hayo ma-IPTL, Ricmond, Songas na mazagazaga yake, TANESCO bado ni kimeo tu. Jenga nyumba bongo ukawafuate wakuwekee umeme, uone watakavyokusumbua! Yaani hata ukinunua vifaa vyote ukafanya na wiring inavyopaswa, suala la kuungaishiwa huo umeme ni mbinde! Kampuni makini ingechangamkia sana fursa za kupata wateja wengi ili iingize hela zaidi kwa njia ya bili, lakini hawa wenzetu mteja ndiye anayebembeleza kununua huduma! Mapumbavu tu! Mie yalinisumbua sana na siyapendi kabisa haya matanesko, shenzi kabisa! Na nilishangaa mno wabunge walipopinga zisianzishwe kampuni za kushindana na TANESCO, hii nilishangaa kabisa. Tunayo EWURA, inaweza kuweka utaratibu mzuri wa kuratibu hizi kampuni, zikapewa territories na hata zikamiliki mitambo ya kuzalisha na kuuza umeme katika maeneo hayo. Huu ukiritimba wa kijinga unatuzidishia umaskini tu!

Haya ni maneno ya Kithuku hivi karibuni tu kwenye thread nyingine aliyoanzisha Bubu Ataka Kusema kuhusu Tanesco. Ni ubovu kama huu ambao nataka uangaliwe kwa darubini kali.
 
Kusema matumizi mabovu haitoshi ni lazima waainishe ili ijulikane ni wapi ulitumika uzembe ,sio kulaumu bila ya vithibitisho au wamekusudia kulekule tulikotoka kwa akina Richmonduli.
Wabunge wajifunze kuwa wawazi wa vielelezo !!
 
Umewahi kuomba uunganishiwe umeme hivi karibuni? Kamsome Kithuku alivyoandika upate machungu yake. Tusitumie hiyo mikataba mibovu kuwakumbatia watendaji wabovu. Hii menejimenti ndiyo iliyomkatia mteja anayelipa mamia ya mamilioni kwa mwezi kwa deni la milioni hamsini! hii menejimenti ndiyo ilienda kwa waandishi wa habari kutoa vitisho dhidi ya mteja huyo wakati wameishalipwa siku kadhaa kabla! Hii menejimenti imeshindwa kutoa ripoti ya namna wanavyopunguza gharama za uzalishaji! Hii menejimenti ndiyo imepata hasara hiyo ya mabilioni.Unataka nini zaidi? Hakuna anayesema kuwa mikataba ya IPTL, Songas n.k ina matatizo yake. La hasha, ninachokataa ni hii tabia ya kutaa kumkosoa mtu ati kwa sababu ni mzalendo mwenzetu. Kutupia hela matatizo siyo solution hata siku moja. Sasa, Mkuu, wewe niambie ni mafanikio gani ambayo tanesco wamepata tangu hao Net Group waondoke? Ah, najua, hawawezi kufanya kitu kwa sababu ya madeni ya IPTL! Haya, wameweza kueleza katika hicho kidogo wanachopata wanamipango gani ya kukiongezea? Ah, ni wakina Richmond tena! Get real, ndugu yangu, watu wengi wanaumia na utendaji mbovu wa Tanesco usio na uhusiano hata kidogo na hayo madeni.

Fundi,

I am not defending Tanesco or even think Net Solutions was a great idea for Tanesco. Tatizo ambalo sasa labda inabidi niwe specific nieleweke ni structure nzima ya utendaji na uongozi.

Yule fundi pale Magomeni au Ubungo na meneja wake walikuwa wachapa kazi wa kawaida. Wakaanza ingiliwa na vimemo vya katibu kata, Mjumbe wa shina, Mbunge, DDD, DC, RDD, RC, Katibu Mkuu, Mkurugenzi, Waziri na kila mtu ambaye ana madaraka au nguvu za madaraka na kushurutishwa kufanya kazi zao kwa matakwa ya vi-memo.

Hali halisi ya maisha ya fundi na meneja huyu bado ni za kusitasita. Tawi la OTTU la kampuni yao linashindwa kupata suluhisho la vipato vyao kuongezwa, lakini kila siku wanaona jinsi Shirika linavuyoongiza mapato kwa kuongeza viwango vya matumizi kwa Watumiaji umeme, wanaona na kusoma pesa zinavyotumika kiholela hata kwa menejmenti yao, wizara na Serikali yao, na mikataba ya kijinga ambalo inapunguza gawio la mapato ya kampuni kwa wao kama wafanyakazi.

Hivyo si ajabu kuona fundi huyu na meneja wake nao kuanza kutafuta njia fupi kujipatia kipato ziada kukidhi mahitaji ya lazima. Ndipo wanapokuwa na kero za makusudi ambazo zinaonekana kuwa ni ukosefu wa nidhamu, tija au motisha unaoandamana na uzembe na hivyo gharama za wao kukosa kupata kipato cha kukidhi mahitaji muhimu wanakisukuma kwa Kithuku!

Am I sympathising with this Fundi and Manager? heck NO, but I understand their plight.

Nguvu ya matatizo ya Tanzania ni Top to Bottom driven na si Bottom up kama wengi wanavyofikiri.

Ikiwa mamlaka na uongozi wa Serikali ungekuwa adilifu na makini, basi hata Tanesco wangekuwa makini na huyo Fundi pale Magomeni au yule Meneja Ubungo.

Now that is real!
 
tuko wenyewe na tunazungumzia ishu yetu haina haja kuficha mchawi, na ss wazawa tumo kulipeleka shirika monchwari kwa kujali ubinafsi kama ilivyoelezwa.

hao wengine ni kweli wametupeleka pabaya lkn wazawa wao ndio walioanza na wengine wakamaliza
 
kama hujawahi kuunganishiwa umeme na Tanesco kaa kando, hawa jamaa ni bomu kwa biashara ajabu.Ni rahisi kuunganisha umeme kwa njia ya wizi kuliko njia halali kwa kuwatumia mafundi haohao wa Tanesco.
 
Umewahi kuomba uunganishiwe umeme hivi karibuni? Kamsome Kithuku alivyoandika upate machungu yake. Tusitumie hiyo mikataba mibovu kuwakumbatia watendaji wabovu. Hii menejimenti ndiyo iliyomkatia mteja anayelipa mamia ya mamilioni kwa mwezi kwa deni la milioni hamsini! hii menejimenti ndiyo ilienda kwa waandishi wa habari kutoa vitisho dhidi ya mteja huyo wakati wameishalipwa siku kadhaa kabla! Hii menejimenti imeshindwa kutoa ripoti ya namna wanavyopunguza gharama za uzalishaji! Hii menejimenti ndiyo imepata hasara hiyo ya mabilioni.Unataka nini zaidi? Hakuna anayesema kuwa mikataba ya IPTL, Songas n.k ina matatizo yake. La hasha, ninachokataa ni hii tabia ya kutaa kumkosoa mtu ati kwa sababu ni mzalendo mwenzetu. Kutupia hela matatizo siyo solution hata siku moja. Sasa, Mkuu, wewe niambie ni mafanikio gani ambayo tanesco wamepata tangu hao Net Group waondoke? Ah, najua, hawawezi kufanya kitu kwa sababu ya madeni ya IPTL! Haya, wameweza kueleza katika hicho kidogo wanachopata wanamipango gani ya kukiongezea? Ah, ni wakina Richmond tena! Get real, ndugu yangu, watu wengi wanaumia na utendaji mbovu wa Tanesco usio na uhusiano hata kidogo na hayo madeni.

Mbona mnataka kupotosha lawama zilizotolewa! :confused:
Lawama zilizotolewa na wabunge uchwara has nothing to do na kuunganishiwa umeme

Someni hapa: KATIKA hali isiyotarajiwa, baadhi ya wabunge wameligeuka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na kudai kuwa matumizi mabovu ya fedha yanayofanywa na watendaji wake, ndiyo yaliyolifikisha shirika hilo hapo lilipo kiasi cha kushindwa kuzalisha umeme wa kutosha, hivyo kutegemea ruzuku ya serikali.

Aidha, wabunge hao walisema watendaji wa Tanesco walipopata nafasi za kuliendesha shirika hilo, walifikiria zaidi kuwapeleka watoto wao shule nje ya nchi na mambo mengine, badala ya kufikiria zaidi maendeleo ya shirika.
Rwilomba alisema historia ipo wazi kwa watendaji wa shirika hilo wanapopata fedha hufikiria zaidi kuwasomesha watoto wao nje ya nchi, badala ya kuangalia namna ya kuzalisha umeme pamoja na kuwapelekea watu wa vijijini ambao kwa muda mrefu wamekosa huduma hiyo.

"Tanesco ndugu zangu mnapobebwa na nyinyi mjibebe, fedha mtakazopewa na serikali mzitumie kuboresha shirika na wala si kwa ajili ya kujinufaisha, kwani mkifanya hivyo mtakwisha hasa baada ya kuja kwa kampuni binafsi za kuzalisha umeme," alisema Rwilomba.
 
Naomba kuwekwa sawa ndugu zangu, hivi medeni ya IPTL, DOWANS na bills za SONGAS etc yanalipwa na TANESCO kama shirika au yanalipwa na serikali (HAZINA)? katika huu UTAABANI wa TANESCO maana napata mkanganyiko niwalaumu TANESCO yenyewe au serikali
 
Wanaofanya maamuzi kuhusiana na TANESCO na kusaini mikataba hewa akina fisadi Mkapa na wengineo mikataba ya IPTL, RICHMOND, Songa na Net group ambayo imekuwa na athari kubwa katika utendaji wa shirika hilo, halafu wa kulaumiwa ni watendaji wakuu wa TANESCO eti kwa kuwapeleka watoto wao kusoma nje! :confused:

Juzi juzi wafanyakazi wa TANESCO waliandamana na kusema hadharani kwamba utendaji ndani ya shirika hilo unaathiriwa zaidi na mikataba mibovu. Hawakuzungumzia kabisa watendaji wa juu wa shirika hilo, je wana nasaba nao gani mpaka wasiwataje kwamba nao wanahusika katika kulegalega kwa shirika hilo?. Na hawa wafanyakazi wamo ndani ya TANESCO wanajua kwa undani zaidi yanayoendelea ndani ya shirika hilo kuliko wabunge wanaosema bila kujua wasemalo. GET REAL!
 
Nafikiri wapumbavu ni sisi wapiga kura tuliowapeleka pale Bungeni.
Mimi binafsi na wapiga kura wenzangu ndiyo wa kulaumiwa juu ya upuuzi wa wabunge.

Kuendelea kuwalaumu wabunge pekee yao si haki kwa sababu hawakujipeleka Bungeni bali sisi wapiga kula ndio tuliowapeleka baada ya kula masinia ya wali na finyango mbili tatu.Alaumiwe nani? Mujmbe au Bwana wa ujumbe(mpiga kura)?

Tuna mpango gani wa kuonyesha uchungu tulio nao juu ya wabunge wazembe hawa?
 
Naomba kuwekwa sawa ndugu zangu, hivi medeni ya IPTL, DOWANS na bills za SONGAS etc yanalipwa na TANESCO kama shirika au yanalipwa na serikali (HAZINA)? katika huu UTAABANI wa TANESCO maana napata mkanganyiko niwalaumu TANESCO yenyewe au serikali

Habari za kuaminika ni kwamba TANESCO na siyo hazina wanawalipa IPTL shilingi bilioni nne kwa mwezi hata kama hawazalishi umeme, wanawalipa Richmond sasa DOWANS shilingi 152 milioni kwa siku hawa hawazalishi chochote na bado wanalipwa na wanalipia gesi toka songas ambayo inasemekana ni kwa bei mbaya.
 
Habari za kuaminika ni kwamba TANESCO na siyo hazina wanawalipa IPTL shilingi bilioni nne kwa mwezi hata kama hawazalishi umeme, wanawalipa Richmond sasa DOWANS shilingi 152 milioni kwa siku hawa hawazalishi chochote na bado wanalipwa na wanalipia gesi toka songas ambayo inasemekana ni kwa bei mbaya.


Nadhania hao wabunge hawajui wanachokiongea, mi nilidhani wangeamua kusitisha ulipaji wa haya madeni ili shirika lijikwamue. Labda wanataka kusikika kuwa wameongea kitu! hawana point katika hili
 
Nadhania hao wabunge hawajui wanachokiongea, mi nilidhani wangeamua kusitisha ulipaji wa haya madeni ili shirika lijikwamue. Labda wanataka kusikika kuwa wameongea kitu! hawana point katika hili

Mama, Hicho ndicho wanachopaswa kuongelea. Malipo ya shilingi bilioni 4.5 kwa mwezi wanayolipwa DOWANS na pia malipo ya bilioni 4 kwa mwezi kwa IPTL. Viongozi wetu hawako tayari kupigania haki ya Tanzania. Nakumbuka Lowassa alipositisha mkataba wa dar city kuhusiana na utendaji wao finyu na wao kuamua kwenda kufungua mashtaka UK kwa kuvunjwa mkataba. Watanzania wengi walidhani tungeshindwa katika kesi hiyo, lakini tulishinda na hao Dar city (waingereza) kutakakiwa kulipa gharama zote za kesi ambazo Tanzania ilizilipa.

Kikwete sasa hivi ana urafiki wa karibu na Kichaka na Browns angeweza kutumia ukaribu alionao kwa viongozi hao kupata support yao ili kuutengua huo mkataba wa IPTL au malipo yakapunguzwa kwa 75% ambayo itakuwa nafuu kubwa kwa TANESCO. Hao DOWANS mimi sielewi hata kwanini wanaendele kulipwa. Sidhani kama kutakuwa na athari yoyote kama TANESCO wataamua kusimamisha malipo ya shilingi bilioni 4.5 kwa mwezi kwa kampuni hiyo.
 
LOWASSA hitting back hard boy!!!.......yaani kama namuona vile......eti naye kakamata popcorn zake anaangalia game linavyoendeshwa na vijana wake.........daahh.......anyway tuendelee kupambana......kwnai Vita na MAFISADI si ndogo ati
 
Back
Top Bottom