Wabunge wa NCCR Mageuzi na CHADEMA ndio wenye hoja nzuri Bungeni

REBEL

Senior Member
Dec 15, 2010
166
64
habari zenu wakuu,hii ni thread yangu ya kwanza hapa jamiiforums.
Bunge linaisha leo nimefanya kautafiti kangu kadogo na nimegundua kuwa wabunge wa Chadema na NCCR MAGEUZI ndio walikuwa wanatoa hoja nzuri ndani na nje ya bunge.
Sijakata kuwa kuna wabunge kidogo wa CUF kama Sakaya,Mnyaa na Hemedi wanatoa hoja na mambo mazito lakini ni wachache sana .Pia, Magamba wako wachache sana wenye hoja nzito lakini wengi wao sana sana wanapiga meza na kuzomea wabunge wa upinzani.Labda Makufuli,Pinda na Tibaijuka ndio waliong'ara kwa upande wa magamba.

Lakini wabunge wa chadema na NCCR Mageuzi kwa ujumla wake ndio waliokonga nyoyo za watanzania wengi sana.Hata kama unabisha jiulize swali dogo tu,
Unajua wabunge wangapi wa CCM au CUF?
pili,unajua wabunge wangapi wa NCCR na CHADEMa?
Jibu la hapo juu ni rahisi sana kila mtu mtaani anamjua mnyika,zito,wenje,machali,mkosamali,lema,mdee,Silinde na wengine wengi.
Lakini CCM ni mzigo,wanafiki na janga la taifa na ni watu wa ajabu sana kama sitta,lowassa,wassira.Wengine upeo wao unatia shaka na nadhani elimu yao ni ndogo sana kama Lusinde na Maji Marefu.
Nawasilisha.
 
Ndivyo ilivyo tunampango wa kuongeza wabunge wafike kama 200 ili ukombozi ufikie hii nchi.
 
Kwa ripoti hii nami nasema kula tano. Ni ukweli usiopingika kuwa wabunge wa vyama hivi viwili pamoja na ucghache wao wameacha mwangwi kwenye mjengo. Spika na naibu wake na wenyeviti wa mkutano huu wa nne wa wa bunge la kumi ni mashahidi pamoja na kwamba kukubali hili ni vigumu. Hotuba zao zao mbadala (za mawazirii Kivuli) zilisheni mikakati mingi ya kushughulikia kero za wananchi ambalo ndiyo jukumu la mbunge yeyote. Upande wa chama tawala (magamba) ni wachache waliweza kutimiza hili. Mawaziri ndio kwanza walipoteza mvuto kwa kutokuwa na majibu ya kero hizo. Wengi wanafanya kazi kimazoea bila kutafakari aina ya wawakilishi walioingia bungeni ktk uchaguzi ukliopita. Vijana wachapakazi wasiolala kama mawaziri wa serkali ambao walinaswa na kamera wakiwa wanachapa usingizi. Madhambi ya wizi, rushwa na ufisadi yaliibuliwa na kuifanya serkali kuhaha. Mafanikio ya kikao hiki ni rasharasha kazi ndio inaanza na wabunge wanarudi kwa wapiga kura kuwaeleza yale yaliojiri ili wajipange sawasawa. Pale ambapo walikuwa sahihi lakini wakazomewa kwa wingi wa magamba watakata rufaa kwao ili waihukumu serlkali. Mungu awajalie afya njema kufanikisha azma hiyo.
 
Ebwana we unaakili sana!!!! Atakae Pinga hapo basi ni Gamba au Mwanga!!! Lakini kwa mtu ambaye ni neutral hawez kubisha hapo mkuu!!
 
Upo sawa mkuu, ila najua wanaotumia masaburi wataku-dc tu, we wala usipaniki coz masaburi will be on work
 
habari zenu wakuu,hii ni thread yangu ya kwanza hapa jamiiforums.
Bunge linaisha leo nimefanya kautafiti kangu kadogo na nimegundua kuwa wabunge wa Chadema na NCCR MAGEUZI ndio walikuwa wanatoa hoja nzuri ndani na nje ya bunge.
Sijakata kuwa kuna wabunge kidogo wa CUF kama Sakaya,Mnyaa na Hemedi wanatoa hoja na mambo mazito lakini ni wachache sana .Pia, Magamba wako wachache sana wenye hoja nzito lakini wengi wao sana sana wanapiga meza na kuzomea wabunge wa upinzani.Labda Makufuli,Pinda na Tibaijuka ndio waliong'ara kwa upande wa magamba.

Lakini wabunge wa chadema na NCCR Mageuzi kwa ujumla wake ndio waliokonga nyoyo za watanzania wengi sana.Hata kama unabisha jiulize swali dogo tu,
Unajua wabunge wangapi wa CCM au CUF?
pili,unajua wabunge wangapi wa NCCR na CHADEMa?
Jibu la hapo juu ni rahisi sana kila mtu mtaani anamjua mnyika,zito,wenje,machali,mkosamali,lema,mdee,Silinde na wengine wengi.
Lakini CCM ni mzigo,wanafiki na janga la taifa na ni watu wa ajabu sana kama sitta,lowassa,wassira.Wengine upeo wao unatia shaka na nadhani elimu yao ni ndogo sana kama Lusinde na Maji Marefu.
Nawasilisha.
ni kweli kuwa wabunge hao wameongoza kwenye kutoa hoja nzuri na nzito ambazo zote kwa pamoja ni muhimu sana kwa uchumi wa nchi na wananchi.
lakini nimeona utafiti wako una vikasoro vidogo kama ule wa sinovate ya mwaka jana.
hujutaja vigezo ulizotumia kukamililsha utafiti wako.
mfano hoja zipi zilikuwa muhimu na nzito, nani alitoa, nani ameongoza ndani ya kila chama mfano chadema nani alikuwa kinara, nccr nani alikuwa kinara, na ccm nani alikuwa kinara. then unakuja kwenye majumuisho kwa pamoja ni mbunge gani ameng'ara kuliko wabunge wote, na chama gani kimeng'ara kuliko vyama vyote.
ni mawazo yangu tu
 
mkuu umenena kweli kabisa. wabunge wa magamba wapo kujaza idadi tu na kusema ndiooooooooooo. but the days for liberation are around the corner. soon.
 
Upo sawa piwa ni wazi spika anawajua zaidi wabunge wa upinzani kuliko wa CCM.mfano mzuri ni ktk kupitisha mafungu ktk bajeti kwani spika pamoja na wenyeviti wao ushindwa kuwatambua wabunge wa magamba mpaka wanapata usaidizi wa wafanyakazi wa bunge lakini anaposimama wa chadema au nccr alaka utamsikia akitaja majina bila msaada.
 
Kweliiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii tupu Hawa wa CDM na NCCR ndio waliokuja na hoja hot na pia wameonesha kuwa ni wawakilishi wa wananchi wa Tanzania. Siyo wale wa magamba wanawakilisha maslahi yao na wawekezaji.
 
1. zitto kabwe 2. sakaya cuf 3. habib mnyaa cuf 4. mnyika cdm 5. tundu Lissu cdm 6. stela manyanya ccm. 7. ole sendeka ccm 8. filikunjombe ccm. 9. mbowe cdm 10. Hamad Rashid cuf hii ndio top 10 iliyong'ara bungeni.
 
Kwenda zako stella manyanya katoa point gan bungeni sasa hivi?si afadhali ungesema anna kilango
 
1. zitto kabwe 2. sakaya cuf 3. habib mnyaa cuf 4. mnyika cdm 5. tundu Lissu cdm 6. stela manyanya ccm. 7. ole sendeka ccm 8. filikunjombe ccm. 9. mbowe cdm 10. Hamad Rashid cuf hii ndio top 10 iliyong'ara bungeni.
<br />
<br />
huo utafiti wako uliufanyia baa gani? Inaonyesha ulikuwa umelewa
 
Wabunge wote wa Tanzania hawana maana yoyote ile....mi naona tusiwe na bunge tunapoteza muda na fedha.
 
Mbunge kama Tundu Lisu amechangamsha bunge ktk upande wa sheria. Befor walikuwa wanatumia uzoefu. Igunga watuongezee kamanda mwngne sio gamba.
 
Back
Top Bottom