Wabunge wa Chadema wekeni contacts zenu kwenye website ya bunge tuwasiliane nanyi kwa urahisi

George Maige Nhigula Jr.

JF-Expert Member
Mar 14, 2008
470
149
Ndugu Zangu wana JF,

Nimejaribu kupitia kwenye website ya bunge kutafuta namba ya Mbunge wangu wa Nyamagana Bwana Dibongo Wenje lakini nimekuta profile yake hainna contacts zozote na nikaenda mbali zaidi kwa kuangalia namba za wabunge wengine wa chadema karibu wabunge wote hawana contacts ya aina yoyote kwenye website ya bunge, sasa sijui ni uzembe wa mbunge ameshindwa kuwasilisha contacts zake kwa katibu wa bunge au ni uzembe wa katibu wa bunge kuhakikisha contacts za wawakilishi wetu zinapatikana kwa urahisi zaidi ili tuweze kuwasiliana nao hususani hivi sasa kuna mchakato wa hii draft bill ya katiba.

Hata baadhi ya wabunge wa ccm pia hawana contacts kwenye profile zao nilitegemea wabunge wetu wao karibu nasi watu wanaotuwakilisha ikiwa pamoja na kutuwezesha kuwapata kwa urahisi pindi tunapohitaji mawasiliano nao.

Naomba kuwasilisha hoja yangu nadhani kuna baadhi ya wabunge hupitia hapa JF naomba walifanyie kazi kwa uharaka hili swala.
 
Kwenye website ya Chadema kwenye sehemu ya "Tuwasiliane" kuna mawasiliano ya viongozi mbali mbali wa Chadema ikiwa pamoja na wabunge. pale una pata anuani pepe zao na simu zao.

Anuani za Wanachama wa CHADEMA

Nadhani hapo ni mwanzo mzuri japo Bunge nalo lina takiwa kuweka mawasiliano ya hawa waheshimiwa.
 
Kwenye website ya Chadema kwenye sehemu ya "Tuwasiliane" kuna mawasiliano ya viongozi mbali mbali wa Chadema ikiwa pamoja na wabunge. pale una pata anuani pepe zao na simu zao.

Anuani za Wanachama wa CHADEMA

Nadhani hapo ni mwanzo mzuri japo Bunge nalo lina takiwa kuweka mawasiliano ya hawa waheshimiwa.


Nashukuru kwa link ya Chadema but still contacts za mbunge wangu hazipo na hiyo list ni ya siku nyingi haijawa updated, kwa sababu Halima Mdee anaonekana bado mbunge wa viti maalum na sio mbunge wa kuchaguliwa kawe, na wabunge wengi wapya hawapo kwenye orodha ya viongozi na wabunge wa chadema, chama makini kinahakikisha information zake zinakuwa up to date nadhani kuna uzembe wa ku up to date information kwenye website ya chama. huyo webmaster hafanyi kazi yake inavyopaswa
 
Jamani naomba kama tutaupata ule muswaada wa MOI tupachikieni hapa jukwaani kama ulivyo ingekuwa bora sana.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom