Mwanajamii
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 7,063
- 68
Wabunge wa CHADEMA wanahitaji kujua kwamba Katiba nzuri itapatikana kwa mchakato utakaofanyika Bungeni si kwenye jukwaa la Katiba kama wanavyofanya wanaharakati. Wananchi tuliowachagua tuna matarajio makubwa kutoka kwenu maana ndiyo mnaotuwakilisha katika masuala mbalimbali ikiwemo kupatikana Katiba inayokidhi mahitaji ya wananchi wa majimboni yenu na Taifa kwa ujumla. Igeni Mbunge MACHALI, MREMA, na wabunge wa CUF walioamua kupambana kwa hoja Bungeni kwa maslahi ya wananchi wa majimbo yao na Taifa kwa ujumla. Tambueni kuwa siyo tu mnategemewa na wananchi waliowapigia kura majimboni bali watanzania kwa ujumla wetu. Kama mnayo mazuri mnayodhani ni muhimu kwa taifa hili myasema Bungeni na siyo kutoka kama mnavyoendelea kufanya.
Hivi mnaleta picha gani kwa wananchi tulio wachagua mnapotoka nje ya Bunge na kutuacha hatuna wawakilishi kwenye suala hili muhimu la Katiba na mengineyo. Au hizi ni dalili za woga kwa Wabunge wa CCM mnayoituhumu kuwa haijafanya lolote huku nyie mnawakimbia? Mnatupa wasi wasi na kutufanya tuamini kuwa mnatusaliti na kutupotezea nafasi ya uwakilishi tuliyowakabidhi ambayo ni dhamana ya maisha yetu. Mnashindwa nini kupambanisha hoja zenu mpaka mkimbie? Hii inatia mashaka na kutufanya tujiulize la kufanya mwaka 2015.
Acheni fujo zenu, tutumikieni kama tulivyowatuma.
Hivi mnaleta picha gani kwa wananchi tulio wachagua mnapotoka nje ya Bunge na kutuacha hatuna wawakilishi kwenye suala hili muhimu la Katiba na mengineyo. Au hizi ni dalili za woga kwa Wabunge wa CCM mnayoituhumu kuwa haijafanya lolote huku nyie mnawakimbia? Mnatupa wasi wasi na kutufanya tuamini kuwa mnatusaliti na kutupotezea nafasi ya uwakilishi tuliyowakabidhi ambayo ni dhamana ya maisha yetu. Mnashindwa nini kupambanisha hoja zenu mpaka mkimbie? Hii inatia mashaka na kutufanya tujiulize la kufanya mwaka 2015.
Acheni fujo zenu, tutumikieni kama tulivyowatuma.