Wabunge wa CCM wasioiunga mkono Bajeti ya Serikali wakwepa kupiga kura!

Raia Fulani

JF-Expert Member
Mar 12, 2009
10,773
2,544
Mbunge wa Kisesa ameingia mitini, hasa ikizingatiwa kuwa aliipinga bajeti waziwazi.
 
Ni muoga tu. kwa nini asiwepo na akatae kama kweli alikuwa na nia ya kukataa.
 
Baadhi ya Wabunge wa CCM wasioiunga mkono bajeti ya serikali akiwemo Filikujombe na Mpina wamekacha kupiga kura ya kuiunga mkono bajeti ya serikali yao ya CCM. Hii inaashiria nini katika siasa ya chama hicho?.
 
Ni kazi ya adrenaline hormone inakuweza uchukue moja kati ya F tatu (Fight,Flight or Fear) ok luhaga mpina kachukua ya kati kasepa
 
Hizi ni nidhamu za woga, mkuu. Alikuwa na hoja nzuri tu. Kadhalika watu kama Mbatia tulihofia wangepiga kura ya NDIYO, kumbe siyo
 
baadhi ya wabunge wa ccm wasioiunga mkono bajeti ya serikali akiwemo filikujombe na mpina wamekacha kupiga kura ya kuiunga mkono bajeti ya serikali yao ya ccm. Hii inaashiria nini katika siasa ya chama hicho?.

udikteta.
 
Kwa mtazamo wangu hakuna mbunge wa CCM aliyeikacha bajeti.Walioikacha bajeti ni wale waliopiga kura za hapana na wala hakuna mbunge wa CCM aliyepiga kura ya hapana achilia mbali huyo Mpina.Kukimbia kupiga kura kwa hofu ya kuzua sintofahamu sio kukacha bajeti bali ni kuogopa kuikacha bajeti kwa uoga usio na dhamira ya kweli kutoka moyoni.
 
Mimi niliamini zilikuwa mbwembwe tu za jukwaani asingeweza ikataa. Sasa tunamsubiri jimboni tumhoji alikuwa na maana gani kuikataa hadharani halafu siku ya kura asepe? Mchumia tumbo huyo!
 
mimi huwa siamini kama kuna mbunge msafi ssiem..yaezekana walikua wammenda short call wakati wa kura za ndiooooo
 
Mimi niliamini zilikuwa mbwembwe tu za jukwaani asingeweza ikataa. Sasa tunamsubiri jimboni tumhoji alikuwa na maana gani kuikataa hadharani halafu siku ya kura asepe? Mchumia tumbo huyo!

Hata hivyo ni haki yake, na kuwepo kwake kusingebadili lolote. Bado tunawapongeza japo kwa kuonyesha misimamo yao juu ya hili
 
Hata hivyo ni haki yake, na kuwepo kwake kusingebadili lolote. Bado tunawapongeza japo kwa kuonyesha misimamo yao juu ya hili[/QUOTE]

Mkuu, nakushauri usiwasifie. hiyo siyo misimamo ya kishujaa, ni misimamo ya kinafiki.
Mpamabanaji wa kweli hupigana hadi hatua ya mwisho, na siyo kutafuta visingizio vya kuondoka ulingoni ili hali mapambano uliyoyaanzisha bado yanaendelea.
 
Hata hivyo ni haki yake, na kuwepo kwake kusingebadili lolote. Bado tunawapongeza japo kwa kuonyesha misimamo yao juu ya hili[/QUOTE]

Mkuu, nakushauri usiwasifie. hiyo siyo misimamo ya kishujaa, ni misimamo ya kinafiki.
Mpamabanaji wa kweli hupigana hadi hatua ya mwisho, na siyo kutafuta visingizio vya kuondoka ulingoni ili hali mapambano uliyoyaanzisha bado yanaendelea.
kiukweli sio kama naafiki kiasi hicho bali katika mazingira ya chama kile bora uwe na alibi. Cha msingi hapa ni kubadili taratibu ya upigaji kura
 
wanafiki kama wao ni wanaume wangekaa bungeni kupinga hadi mwisho ....wana shughuli zao binafsi
 
Ccm bado wanawaza mapinduzi ya kisiasa kwa kulindana sasa wamesahau km nchi niya wananchi.
 
Ndugu zangu, mimi natumaini ni mapema sana kuwaita wanafiki!
Kwa upande Filiku'njombe, hii ni mara pili kasimama hadharani kupinga waziwazi. Kumbukeni bunge llilopita,ktk wizara ya Uchukuzi. Kwa upande wa Mpina(Mbunge wa kisesa), Kabla ya Bunge la Bajeti halijaanza, alitangaza dhamira yake mapema na kudhihirisha wakati wa kuchangia kwa uthabiti mkubwa. Ni kweli ushujaa wao ungedhihirika dhahiri leo endapo wangepiga kura ya HAPANA. Natumaini lazima kuna JAMBO/SABABU ya msingi kwa wote kuona si vyema kuwepo mjengoni.

Hawa jamaa ni MAKAMANDA, wamevaa MAGWANDA, ila tu tatizo eneo la msitu ni kubwa mnoooooooooooooooooo:yield:
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom