Cha ajabu ni kipi wabunge hao kuwa na mkutano?
Cha ajabu ni kipi wabunge hao kuwa na mkutano?
Hakuna cha ajabu wao kuhutubia ila wamefungua macho ya wengi. Kwanza waliingia kwa msafara wenye pikipiki wenye bendera za ccm akiwemo Dani Makanga kaimu DC. Mkutano ukaanza DC akaanza kuongea bila kufanya utambulisho wa wageni Rasmussen bali aliwatambulisha makatibu wa ccm wilaya na mkoa, Josephine ngenzabuke mb Viti maalum akaanza kuongea pumba huku akiwashukuru wananchi kwa kumchagua awe mbunge(viti maalum hawachaguliwi) wananchi wakamzomea akashuka kisha mb viti maalum tabora akapandana kuongea kuhamasisha uchangiaji wa katiba. Mwisho makanga akafanya majumuisho akaanza kusoma sheria ya rasimu ya katiba na adhabu za kujadili katiba. Akawaambia wananchi wajadili hiyo sheria. Mwananchi mmoja aliuliza kwa nini muswada wa sheria yenye vitisho hivyo haukuletwa kwa wananchi kabla haijasainiwa na kwa nn ina vitisho kwa wananchi pia kama mkutano huo ulikuwa wa kuhamasisha katiba kwa nini DC alianza kutambulisha makatibu wa ccm kigoma na yule wa kasulu bila ya kutambulisha viongozi wa vyama vingine. Aluminum kibabe na majibu alitoyatoa kwanza walimzuia muuliza swali asiendelee kuuliza kwani atamaliza muda wa kuuliza maswali mengine. Huyu mkuu wa wilaya hana tofauti na hao wabunge wa viti maalum kwani wote ni wa kuwekwa ili wafurahishe wakubwa Baba riz. Wanafuata upepo tu hawana lolote kichwani. Natamani viti maalum vifutwe na DC wote watimuliwe kwani hawana kazi madc kazi yao kuijenga ccm kwa hela zetu
Nakupa tano mkuu.kumbe tulikuwa wote!
Mbona hata Chadema nao huweka mikutano ?