SAGAI GALGANO
JF-Expert Member
- Nov 13, 2009
- 43,707
- 60,756
Hivi kwa nini huyu Mukama asiuwawe?
Ndio tunajua chama kinakufa lakini Mukama kama kiongozi lazima aonekane anakisaidia, mbona kuna wengine wamo humo humo wanaonekana?
Kufuatia wimbi la vitisho linalotolewa na Katibu Mkuu wa CCM,Wilson Mukama kwa wabunge wa chama hicho waliotia saini Waraka wa Zitto wa kutokuwa na imani na Waziri Mkuu,mbunge mmoja amedai kuwa Mukama hawezi kuwatishia nyau.Nikizungumza na mmoja wa Wabunge hao jana jioni,Mbunge huyo alinidokeza kuwa Mukama amechelewa kukarabati chama chake kinachowalea Mawaziri wezi.Mbunge huyo maarufu kwa kipato anayetokea Mkoa wa Baba wa Taifa alinidokeza kuwa Mukama ataishia kuwatisha 'wengine' na hatathubutu kumsogelea yeye.
Mbunge huyo alishangazwa na Mukama kuingilia kisichomuhusu huku yeye(Mukama) akiwa ndiye msimamizi wa sera ya kujivua gamba ya CCM.'Huyu Ndugu yangu sijui amekuwaje tena?!' aliuliza kwa mshangao Mbunge huyo.
Je,Mukama anacheza mdundo anaouelewa?