komedi
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 204
- 17
Kutokana na matukio haya mawili abiria kutoka tanzania ambao ni wanasiasa wamekuwa wakizuiwa kusafiri kwa shirika la ndege la Afrika kusini.
Tukio la kwanza.
Wabunge wawili wa CHADEMA wakiwa wanasafiri kwa ndege kuelekea Johannesburg ghafla ndege ikiwa angani na huku wakiwa wanatazama picha za video alionekana mheshimiwa Jakaya Kikwete akihutubia kwenye moja ya matangazo ya biashara. Mara waliinuka kutoka kwenye viti na kutaka kutoka nje ya ndege na ndipo Airhostess alipofanya kazi ya ziada kuwakumbusha kuwa hawako Bungeni bali ndani ya ndege tena angani.
Tukio la Pili
Hii ilikuwa siku nyingine ambapo mheshimiwa mmoja mbunge wa CCM alikuwa usingizini mpaka ndege ilipotua Johannesburg. Ghafla akazinduka kutoka usingizini wakati abiria wengine wakiwa wanashuka na wengine kutoa mizigo yao. Ghafla akapiga kelele kwa sauti kubwa ''haooo... tumewazoea....haooooo, nendeni, wahuni, tokeni''. Safari hii Airhostess alifanya kazi kubwa kumzuia mzungu mmoja ambaye anasikia kiswahili vizuri na alidhani anatukanwa na alitaka kumpasua pua kwa ngumi. ''Hey good passenger this person is still dreaming...''
Tukio la kwanza.
Wabunge wawili wa CHADEMA wakiwa wanasafiri kwa ndege kuelekea Johannesburg ghafla ndege ikiwa angani na huku wakiwa wanatazama picha za video alionekana mheshimiwa Jakaya Kikwete akihutubia kwenye moja ya matangazo ya biashara. Mara waliinuka kutoka kwenye viti na kutaka kutoka nje ya ndege na ndipo Airhostess alipofanya kazi ya ziada kuwakumbusha kuwa hawako Bungeni bali ndani ya ndege tena angani.
Tukio la Pili
Hii ilikuwa siku nyingine ambapo mheshimiwa mmoja mbunge wa CCM alikuwa usingizini mpaka ndege ilipotua Johannesburg. Ghafla akazinduka kutoka usingizini wakati abiria wengine wakiwa wanashuka na wengine kutoa mizigo yao. Ghafla akapiga kelele kwa sauti kubwa ''haooo... tumewazoea....haooooo, nendeni, wahuni, tokeni''. Safari hii Airhostess alifanya kazi kubwa kumzuia mzungu mmoja ambaye anasikia kiswahili vizuri na alidhani anatukanwa na alitaka kumpasua pua kwa ngumi. ''Hey good passenger this person is still dreaming...''