Wabunge wa CCM mnawachezesha Watanzania "kwata" la akili!

Wabunge wa CCM wote ni wasanii. Zikipelekwa hoja za kuziba mianya ya ufisadi, wanakuwa wa kwanza kuzipiga mawe. Juzi wote tumeona jinsi walivyoikataa hoja ya JJ Mnyika ya kutaka kuthibiti ufisadi kwenye mashirika ya umma.

Mbunge Erasto Zambi anasema, "Twende kwenye kikao cha wabunge wa CCM tukafanye uamuzi. Maana hapa Bungeni hatuwezi kumaliza". Sasa kama swala lina maslahi kwa Taifa kwanini lisimalizwe hapo Bungeni? Hata Richmond ilimalizwa kisanii hivi hivi huko kwenye vikao vya wabunge wa CCM pembeni, mjadala ukafungwa bila serikali kutekeleza maazimio ya Bunge.

Serukamba anasema, "watumie kanuni za kuwabana mawaziri wasiowajibika na wanaopindisha mambo bila ridhaa ya Bunge". Mawaziri wangapi mpaka leo hii ambao wametakiwa na Bunge wajiuzulu na hawajafanya hivyo? Kama wanataka Baraza Jipya, wapige kura ya kutokuwa na imani. Bado hata hiyo siyo suluhisho la ufisadi unaoendelea.

CCM wamekuwa wakipitisha sheria za ajabu ambazo zimejaa discretion za watendaji na hivyo kuwapa mianya ya kufanya madudu kwa jinsi wanavyojisikia na hakuna lolote linalofanyika.

Kwa hiyo wabunge wa CCM ndio ambao wamekuwa wakiilea serikali yao ambayo inajifanyia mambo yake jinsi inavyopenda na wabunge wa CCM wamebaki kuwa wacheza sarakasi. Sasa hivi tutaona sarakasi nyingi kuelekea 2015.

Chaguzi ndogo za kati ya 2006 na 2010 waliwatumia sana hawa wabunge wanaojiita wapiganaji ili ku-neutralize hoja za ufisadi. Sasa hivi wamejaribu kuwatumia Kirumba, Kiwira na Arumeru, kote huko imekula kwao. Sasa wameanza sarakasi na mazingaombwe ya kuandaa timu mpya ya "wapiganaji" kuelekea 2015 na ndio maana wamekuwa wakii-refer mara kwa mara baada ya kugundua ile timu ya mwanzo ama imepoteza mvuto au watu wameanza kuamka.

Kinachonisikitisha ni kwamba wakati mwingine watanzania ni wepesi sana wa kuwa carried away na hizi sarakasi za CCM, yaani juzi tu tumeona jamaa wanakomaa na hoja ya Mnyika, leo tayari tunasema Bungeni kumewaka moto. Hata siku ya Richmond moto uliwaka, watu tukajua sasa serikali itashikishwa adabu, matokeo yake tunajua. Baada ya hapo, kila kinachoendelea Bungeni huwa ninaona ni sanaa na mazingaombwe ya kuendelea kuwaibia watanzania ili wawe na imani na wabunge wa CCM na hivyo uchaguzi ujao CCM irejeshwe madarakani na mambo yanaendelea kama kawa.
 
yaani bunge na wabungu wa ccm linasikitisha mbunge anayo phd, wengine madocta,na elimu za kila aina ila wamekuwa kama bendera.elimu haiwasaidii.wamekuwa wanashabikia vi2 visivyo na misingi.ndo mana sasa hakuna haja ya kuangalia elimu au alikuwa na wadhifa gani.sasa ni wakati wa kupigia kura hata KICHUGUU kuliko kupigia MAGAMBA na wapambe wao na wengineo.VIVA CDM.CDM FOR 2015.
 
wanataka wakayafanye kwenye 'party caucus' kwa mujibu wa presentation ya serukamba.

Huko ndiko ambako huwa kunaua maamuzi yote muhimu ya Bunge na ndiko mikakati ya mazingaombwe hupangwa halafu mwisho wa siku, hakuna kitu, yaani wanarudi pale pale walipokuwa.

Kama hawa wabunge wangekuwa wako serious baada ya skendo ya Richmond, leo hii tusingekuwa tunaongelea ufisadi huu unaoendelea. Hili ndio linampa nguvu Lowassa kuendelea kudai kwamba Tume ya Mwakyembe iliundwa mahsusi kwa ajili ya kumng'oa yeye. Maamuzi yote 23 ya Bunge kuhusu skendo hiyo yaliishia hewani. Wabunge wa CCM ogopa sana na hasa wakikutana huko pembeni kwenye "party caucus".
 
Sipendi sana mazingaombwe:

Chama chenu
Serikali yenu
Sera zenu
Sheria mtunge nyinyi
Vyombo vya usalama vyenu
Watendaji mteue nyinyi
Majaji wote mmeteua nyiyi
Wakuu wote wa vyombo vya usalama mmewatua nyinyi
Mwanasheria Mkuu wenu
DPP wenu
Ikulu yenu
Bunge lenu
Mawaziri wote wenu
Manaibu wote mawaziri wenu

LAKINI MNA UJASIRI WA KURUKA KIMANGA KANA KWAMBA SERIKALI IMEUNDWA NA CHADEMA na wapo watu katika akili timamu kabisa wanafurahia haya maonesho yenu!! Kama kweli leo mmefunguka na kukombolewa kifikra basi fungeni kamili! Fungeni na mtoke kwenye giza na kuja kwenye mwanga. Hamhitaji kusubiri 2015! Jiuzuluni leo hii ili mjipe nafasi na kuhesabiwa! Vinginevyo, watacheza kwata wale wenye kuamini mnaweza kuwapigisha kwata la akili!!


HAYA YALIKUWA 2008 - SIKILIZENI KWA MAKINI WANAYOSEMA WABUNGE WA CCM HALAFU MSEME KAMA LEO WAMEFUNGUKA?

[video=youtube_share;Uvpaxg1ksr4]http://youtu.be/Uvpaxg1ksr4[/video]

[video=youtube_share;43uIv7_VSnY]http://youtu.be/43uIv7_VSnY[/video]

Mwanakijiji bwana, kuna wakati anasimangwaaa na kuitwa majina mengi tu......
Lakini anamsimamo mkali na ushahidi wa wazi wa anayo yaamini.

Wabunge wa CCM waache kujinafikia na kunafikia wananchi!
 
Wabunge wa CCM jana wameistrangulate serkali. Kesho wataisifia kwa nguvu zote na kuunga mkono hoja zilizoletwa na serikali kwa kusisitiza MIA kwa MIA.
They can never learn a lesson. Njaa sijui tamaa mbaya sana
 
Mkitaka kujua kama wanamaanisha waambieni wapige kura kama wanaunga mkono hoja muone watakavyoishia "pamoja na kusema hayo Mhe. Spika napenda kuunga mkono hoja!"!!!
 
Sipendi sana mazingaombwe:

Chama chenu
Serikali yenu
Sera zenu
Sheria mtunge nyinyi
Vyombo vya usalama vyenu
Watendaji mteue nyinyi
Majaji wote mmeteua nyiyi
Wakuu wote wa vyombo vya usalama mmewatua nyinyi
Mwanasheria Mkuu wenu
DPP wenu
Ikulu yenu
Bunge lenu
Mawaziri wote wenu
Manaibu wote mawaziri wenu

LAKINI MNA UJASIRI WA KURUKA KIMANGA KANA KWAMBA SERIKALI IMEUNDWA NA CHADEMA na wapo watu katika akili timamu kabisa wanafurahia haya maonesho yenu!! Kama kweli leo mmefunguka na kukombolewa kifikra basi fungeni kamili! Fungeni na mtoke kwenye giza na kuja kwenye mwanga. Hamhitaji kusubiri 2015! Jiuzuluni leo hii ili mjipe nafasi na kuhesabiwa! Vinginevyo, watacheza kwata wale wenye kuamini mnaweza kuwapigisha kwata la akili!!


HAYA YALIKUWA 2008 - SIKILIZENI KWA MAKINI WANAYOSEMA WABUNGE WA CCM HALAFU MSEME KAMA LEO WAMEFUNGUKA?

[video=youtube_share;Uvpaxg1ksr4]http://youtu.be/Uvpaxg1ksr4[/video]

[video=youtube_share;43uIv7_VSnY]http://youtu.be/43uIv7_VSnY[/video]

I do not agree with your opinion, however I will not respond because I need not to waste my time of working for my country and just to respond to your biased opinion.
 
Kura ya kutokuwa na imani itatu cost sisi wananchi pia, inamaana bunge lote linavunjwa tunaanza moja. Hapana sikubaliani na hoja ila noana kuna haja rais avunje hii baraza abadilishe safu tena.
 
It is like a tale,
Told by an idiot,
Full of sound and fury,
Signifying nothing!

- Shakespeare, Macbeth

Nina jina moja tu ninaloweza kuwaita hawa wabunge wa CCM: 'Vinyonga'...Hapa wanapima uelekeo wa upepo ndi wanasema haya, lakini suala la msingi: Je, wana udhati toka mioyoni mwao kuwa wanataka kuipindua serikali yao dhalimu? Tusubiri leo mjengoni...nadhani CCM wataenda kumwita yule mama 'aliyewezeshwa lakini hawezi' anayesimamia shughuli za bunge kwa manufaa ya CCM ili mjadala usiwe mkali leo ukapitiliza hadi kwenye vitabu vya historia...
 
Kura ya kutokuwa na imani itatu cost sisi wananchi pia, inamaana bunge lote linavunjwa tunaanza moja. Hapana sikubaliani na hoja ila noana kuna haja rais avunje hii baraza abadilishe safu tena.

Hapana, kura ya kutokuwa na imani inapigwa dhidi ya Waziri Mkuu kwa kufuata Katiba ilivyo. Ikipigwa haivunji bunge inamuondoa waziri mkuu na baraza la mawaziri. Rais analazimishwa kumtafuta waziri mkuu mpya na kuunda serikali mpya chini ya Ibara ya 53 ya Katiba ya sasa kama sikosei. Haiwezekani kupiga kura ya "kutokuwa na imani na waziri" labda kama ni symbolic.
 
kama kweli wanaona serikali haiendi si wapige kura ya kutokuwa na imani na wazirimkuu ili ajiuzulu na baraza la mawaziri libadilishweu keus?
Ajabu! halafu wanasema Wabunge wa CCM turudi kwenye kikao cha ndani tuzungumze jinsi ya kuwawajibisha mawaziri? huo si ni wehu.woga na usanii? walichaguliwa ili wakafanye vikao vya ndani?
Hawana ubavu wa kufanya hivyo maana wengi wao hawakuchaguliwa kwa nguvu ya wananchi bali ngovu ya dola na mafisadi hivyo wanatuchezea kekundu keusi
 
Nani asiyejua kwamba hawa wabunge wa CCM wamepata kiwewe baada ya kuona mwelekeo wa muanguko wa CCM, na kwamba ubenge ndio basi tena ndani ya CCM. Kiwewe hiki kimewachanganya vibaya sana. Sasa vyombo vya usalama vinadanganya havifanyi kazi kwa uwazi na kisayansi, Wakuu wa mikoa, wilaya, wakurugenzi ni maswhiba wa hawa wabunge wa CCM, mwanasheria mkuu ndio huyo huwa wanamshangilia sana kwa kuvurunda, DPP na kesi zake ndio hivyo tena, leo tunasikia richmond tu, hatusikii epa, zile bilioni 50 za kampeni vipi? hazitajwi kwa sababu zinawakuna. Hiyo Takakuru si ndio inawabeba hata wagombea wa CCM (Makamba amesema rushwa ilitawala). Mawaziri wenyewe ni wanachama wa CCM. Leo mnatoka pofu kutudanganya watanzania. Tutaamini kwenye hitimisho lenu. Tutajua kama sio unafiki tu. Ngoja tuone. M4C itawashughulikia tu, saa imefika. Tena msije mkachelewa maana kuna dalili za wananchi kubadilika kwa kasi hata bila kujali itikadi.
 
Mi nadhani muda umefika tuamke na kuitetea nchi yetu na vizazi vijavyo against dhuluma hii,.kama hata wenye serikali wanaona uozo wao kwa nini tusiwe sisi walipa kodi jamani?..tusupport na tuwe sehemu ya mabadiliko jamani.
 
Kwa hali ilivyo sasa hakuna namna mtu mwenye akili timamu na anayejua yaliofanyika Richmond, Wizi wa wanyama pori hai, Jairo na na wizi mwingine ndani ya serikali anaweza kukubaki kinachoendelea bungeni ni halisi.

Mimi nasema kinachoendelea ni sarakasi tupu! Hakuna udhabiti wa nia wakuacha kuifilisi nchi ndani ya watawala waliopo madarakani na mfumo uliopo. Wanapiga kelele ili kujisafisha na kusadikisha wajinga wengi kuwa wana nia.

Uongozi uliopo madarakani hauna uwezo wa kuondoa na kudhibiti wizi unaoendelea kuididimiza hii nchi kwenye dimbwi la umaskini na hatimaye utumwa. Kila mmoja anaogopa kuchukua hatua sahihi za kuondoa wezi na kuwaadibisha.

Nathubutu kusema viongozi wa serikali wanaujasiri na nia dhabiti ya kuiba, kudhulumu, kuangamiza taifa kuliko kutenda haki.

Tusubiri tuone kama kutakua na hatua zozote zitakazochukuliwa. Na maanisha HATUA sio upuuzi wa waziri kujiuzulu halafu anateuliwa kuwa balozi.

Naamini ipo siku tunaotaka haki na ustawi wa taifa hili tutakua na ujasiri na tutasubutu kama wanavyofanya wezi
 
Hapana, kura ya kutokuwa na imani inapigwa dhidi ya Waziri Mkuu kwa kufuata Katiba ilivyo. Ikipigwa haivunji bunge inamuondoa waziri mkuu na baraza la mawaziri. Rais analazimishwa kumtafuta waziri mkuu mpya na kuunda serikali mpya chini ya Ibara ya 53 ya Katiba ya sasa kama sikosei. Haiwezekani kupiga kura ya "kutokuwa na imani na waziri" labda kama ni symbolic.
Mi bado naona pamoja na kuwa na serikali dhaifu sana kwa ujumla wake lakini tunae waziri mkuu ambaye ni very very weak indeed.....i think the weakest of all PMs we have had before.....yaani jamaa yupo yupo tu....anadhihirisha kuwa alipopewa u PM aliuchukua kama favour..na si jukumu la kuwatumikia watanzania...maana hakemei chochote....mambo yako hovyo hovyo serikalini ye yupo yupo tu....hana msimamo......mbona huwa hawajifunzi kwa wenzao kama marehemu Sokoine?????..hata juzi eti walikwenda kuenzi alipopata ajali!!!.....sasa report zote za utendaji mbovu wa serikali ameziona.....anatakiwa achukue hatua na watu waone...lakini i don't expect it from him......huyu PM mi ana ni piss off mbaya sana..........
 
Sipendi sana mazingaombwe:

Chama chenu
Serikali yenu
Sera zenu
Sheria mtunge nyinyi
Vyombo vya usalama vyenu
Watendaji mteue nyinyi
Majaji wote mmeteua nyiyi
Wakuu wote wa vyombo vya usalama mmewatua nyinyi
Mwanasheria Mkuu wenu
DPP wenu
Ikulu yenu
Bunge lenu
Mawaziri wote wenu
Manaibu wote mawaziri wenu

LAKINI MNA UJASIRI WA KURUKA KIMANGA KANA KWAMBA SERIKALI IMEUNDWA NA CHADEMA na wapo watu katika akili timamu kabisa wanafurahia haya maonesho yenu!! Kama kweli leo mmefunguka na kukombolewa kifikra basi fungeni kamili! Fungeni na mtoke kwenye giza na kuja kwenye mwanga. Hamhitaji kusubiri 2015! Jiuzuluni leo hii ili mjipe nafasi na kuhesabiwa! Vinginevyo, watacheza kwata wale wenye kuamini mnaweza kuwapigisha kwata la akili!!


HAYA YALIKUWA 2008 - SIKILIZENI KWA MAKINI WANAYOSEMA WABUNGE WA CCM HALAFU MSEME KAMA LEO WAMEFUNGUKA?

[video=youtube_share;Uvpaxg1ksr4]http://youtu.be/Uvpaxg1ksr4[/video]

[video=youtube_share;43uIv7_VSnY]http://youtu.be/43uIv7_VSnY[/video]
Wanafiki tu hawa lakini sisi hatudanganyiki na maigizo yao hata kidogo
 
kama kweli wanaona serikali haiendi si wapige kura ya kutokuwa na imani na wazirimkuu ili ajiuzulu na baraza la mawaziri libadilishwe?

Nilitamani kuwacharaza viboko kwa maigizo yao. Kila wakiambiwa udhaifu wa serikali yao huja na propaganda za kumsifia rais, sasa ndo wanajua kuwa Ccm na serikali yake ni wezi. Wanatuchezea akili. Kama ulivyosema MM, wapige kura ya kutokuwa na imani na serikali ya JK ndo tuamini kuwa wanamaanisha wanayosema.

Hawa mwisho wao uko karibu, wajiandae kuumizwa 2015. Natumaini watanzania watakuwa tayari kufanya maamuzi sahihi.
 
Back
Top Bottom