Wabunge wa CCM hawana mamlaka ya kumwachisha kazi Waziri; JK awatosa!

Huelewi maana ya Caucuss.
Caucuss ni hiyari ya mtu , siyo lazima na haxziundwi kisheria.
kwa maneno mengine ni kukaa chemba kabla ya kuja na uamuzi wa pamoja. Ila naona uelewa wako upo mbali kidogo.
Wanaweza wakawa hawana guts, ila uwezo wanao.
Naomba uangalie maana ya caucuss, ni dhahiri kabisa huelewi maana yake.

Kama wana uwezo mbona walimshinikiza rais kuwaachisha kazi akina Ngeleja, Dr Mponda na Dr. Nkya lakini bado wakaendelea kuwepo madarakani? Halafu hapa naongelea caucus in the context of Tanzania na sio Marekani. CCM caucus is like a toothless hag working on a slice of white bread. It's all a sham.
 
Wabunge wa CCM kupitia vikao vyao nje na ndani ya Bunge wanao uwezo wa kuwalazimisha Mawaziri wao wajiuzulu. Kinachokosekana hapa ni ujasiri wa kufanya maamuzi!

No hawana uwezo huo. Ibara ya 55 inaweka wazi ni nani anateua mawaziri. Lakini pia Ibara ya 58 ya katiba inaweka wazi pia kazi ya uwaziri itafanywa na mtu kwa ridhaa ya Rais. Maana yake ni kwamba hakuna mamlaka ingine ambayo inaweza kupinga ridhaa ya rais. Hii ni katiba yetu ambayo inamfanya rais kuwa mungu mtu. Ndiyo maana ninasema kuwa wabunge wa CCM na bunge hawana uwezo wa kuondoa mawaziri kwa kuwataka wajiuzulu kwani si kazi yao. Kazi yao wao ni ile inayofanywa na Zitto ya kukusanya sahihi na baadae kura 51% ya kura za kutokuwa na imani na waziri mkuu au 70% kutokuwa na imani na rais. Wabunge wa CCM wafuate katika waache kitchen parliament (caucus). Katiba inawapatia more than kumg'oa ngeleja, wanaweza kumg'oa pinda. Hapo ndipo kwenye urefu wa rungu lao tena wakiwa bungeni siyo kwenye vikao vya jikoni.


55.-(1) Mawaziri wote ambao ni wajumbe wa Baraza la Mawaziri kwa mujibu wa ibara ya 54 watateuliwa na Rais baada ya kushauriana na Waziri Mkuu.

(2) Pamoja na Mawaziri waliotanjwa katika ibara ndogo ya (1), Rais aweza, baada ya kushauriana na Waziri Mkuu, kuwateua Naibu Mawaziri. Naibu Mawaziri wote hawatakuwa wajumbe wa Baraza la Mawaziri.

(3) Rais aweza kuteua idadi yoyote ya Naibu Mawaziri ambao watawasaidia Mawaziri katika utekelezaji wa kazi na shughuli zao.

(4) Mawaziri na Naibu Mawaziri wote watateuliwa kutoka miongoni mwa Wabunge.

(5) Bila ya kujali masharti ya ibara ndogo ya (1) ikitokea kwamba Rais anahitajiwa kumteua Waziri au Naibu Waziri baada ya Bunge kuvunjwa, basi aweza kumteua mtu yeyote ambaye alikiwa Mbunge kabla ya Bunge kuvunjwa.

58. Mawaziri na Naibu Mawaziri watashika madaraka yao kwa ridhaa ya Rais, na watalipwa mshahara, posho na malipo mengineyo kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge.
 
No hawana uwezo huo. Ibara ya 55 inaweka wazi ni nani anateua mawaziri. Lakini pia Ibara ya 58 ya katiba inaweka wazi pia kazi ya uwaziri itafanywa na mtu kwa ridhaa ya Rais. Maana yake ni kwamba hakuna mamlaka ingine ambayo inaweza kupinga ridhaa ya rais. Hii ni katiba yetu ambayo inamfanya rais kuwa mungu mtu. Ndiyo maana ninasema kuwa wabunge wa CCM na bunge hawana uwezo wa kuondoa mawaziri kwa kuwataka wajiuzulu kwani si kazi yao. Kazi yao wao ni ile inayofanywa na Zitto ya kukusanya sahihi na baadae kura 51% ya kura za kutokuwa na imani na waziri mkuu au 70% kutokuwa na imani na rais. Wabunge wa CCM wafuate katika waache kitchen parliament (caucus). Katiba inawapatia more than kumg'oa ngeleja, wanaweza kumg'oa pinda. Hapo ndipo kwenye urefu wa rungu lao tena wakiwa bungeni siyo kwenye vikao vya jikoni.

Tena Zitto aliliweka wazi kabisa hili

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kutoa taarifa kwamba; mimi na Bunge hili halina mamlaka ya Mkurugenzi wa Shirika, Katibu Mkuu wa Wizara au Mkurugenzi wa Halmashauri. Mawaziri ambao wametajwa kwa njia moja au nyingine kutokuwajibika ipasavyo na kuliingizia hasara taifa wamekuwa wagumu sana kuwajibika, wanampa kazi Rais ya kuwafukuza.

Lakini sisi hatuwezi kuwaazimia hapa ila sisi tuna mamlaka na mtu mmoja tu humu ndani ya Bunge; na naomba mnisikilize kwa makini sana. Tuna mamlaka na mtu mmoja tu, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, bila kumwajibisha Waziri Mkuu hawa Mawaziri waliotajwa hawatatoka na wasipotoka madudu haya yatarudia. Kwa hiyo Mbunge yoyote mwenye uchungu na ubadhirifu, Mbunge yoyote ambaye anakereka na watoto kwenye Jimbo lake kukaa chini, Mbunge yoyote anayekereka na madawa kuharibiwa na MSD na MSD kushindwa kupeleka madawa kwenye vijiji vyetu, nampa taarifa kwamba kuanzia kesho tunakusanya sahihi za Wabunge 70, ili siku ya Jumatatu tutoe hoja hapa Bungeni ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na kipindi hiki tunakitoa Mawaziri wote ambao wapo implicated kwenye taarifa hizi waweze kuona ama wao, au wamtoe rehani Waziri Mkuu. (Makofi)
 
Kama wanashindwa kuzungunza kwa sauti kuu bungeni ni kitu gani kinachowafanya waweze kuzungunza kwa sauti kuu wakiwa huko caucus? Why someone can sit "with someone in a room yesterday and told him to his face that he has messed and must go for the good of the country" lakini anashindwa kufanya hivyo bungeni? Kweli hiyo tunaweza kuita ni "Courage" kama January Makamba anavyodai?

Kama nilivyoeleza katika post yangu hapo juu,BUNGENI wana hatari ya kupoteza serikali na wanahisi,kwa usahihi kabisa,kuwa, itakuwa sababu ya kukataliwa na wananchi mwaka 2015.Ndio maana ,mara zote, hawaoni kama Bunge ni mahali muafaka kufanyia siasa(misuguano ya kihoja)..Hoja hii inapata nguvu tunaporejea ukweli kuwa baadhi ya wapiganaji dhidi ya ufisadi mfano Selelii ,Shelukindo hawakurudi bungeni mwaka 2010.Kadhalika,Spika Sita hakurudi katika nafasi yake kwa mizengwe ya Kamati kuu ya CCM.Hawajaweza kujenga utamaduni wa kisiasa unaotambua umuhimu na nafasi ya tofauti za mawazo..kwa muda mrefu wameendesha siasa za zidumu fikra za mwenyekiti.
Kwa sasa tuna FILIKUNJOMBE.Kwa kweli itakuwa ngumu kwake kurudi bungeni mwaka 2015 maana ni dhahiri wakuu wa chama hawafurahii misimamo yake.
 
Kama nilivyoeleza katika post yangu hapo juu,BUNGENI wana hatari ya kupoteza serikali na wanahisi,kwa usahihi kabisa,kuwa, itakuwa sababu ya kukataliwa na wananchi mwaka 2015. Ndio maana ,mara zote, hawaoni kama Bunge ni mahali muafaka kufanyia siasa(misuguano ya kihoja)..Hoja hii inapata nguvu tunaporejea ukweli kuwa baadhi ya wapiganaji dhidi ya ufisadi mfano Selelii ,Shelukindo hawakurudi bungeni mwaka 2010.Kadhalika,Spika Sita hakurudi katika nafasi yake kwa mizengwe ya Kamati kuu ya CCM.Hawajaweza kujenga utamaduni wa kisiasa unaotambua umuhimu na nafasi ya tofauti za mawazo..kwa muda mrefu wameendesha siasa za zidumu fikra za mwenyekiti.
Kwa sasa tuna FILIKUNJOMBE.Kwa kweli itakuwa ngumu kwake kurudi bungeni mwaka 2015 maana ni dhahiri wakuu wa chama hawafurahii misimamo yake.

Hata waliomkaanga Zitto kwenye Sakata la Buzwagi nao hawakurudi Bungeni, mmojawao ni Mzee Malecela, Mudhihir Mudhihir, Ruth Msafiri, wengine siwakumbuki. Hypothesis yako haiko sahihi.

Katiba Mpya inakuja, mgombea binafsi ngazi ya Ubunge na Kushuka chini wataruhusiwa, kwa hiyo mwisho wa mizengwe ya CCM unakaribia. Wananchi wanaona na kusikia sarakasi zote za unafiki wa wabunge wa CCM. CCM imewashika wabunge wake mateka, kwa kuaminishwa huo upuuzi kwamba ukiipinga serikali Bungeni jina lako haliwezi kurudi kwenye kura za maoni.

Selelii na Shelukindo walishindwa kwenye kura za maoni. Swala la Spika hiyo ni mizengwe ya vikao vya CCM. Lakini bado haliwezi kutumika kama excuse ya mtu kutumika kama mateka ili kulinda ufisadi. Mbunge akianza kutumika kwa malengo hayo ujue kwamba ana matatizo kichwani; kipi kizuri, CCM ikukate jina kwenye vikao vyake kwa sababu ya kutetea maslahi ya wananchi Au Uwe mlamba miguu ya serikali halafu uende kukataliwa na wananchi jimboni?

CCM wanajimaliza wenyewe kwa kuwa wakiwafungia wabunge wao huko kwenye vikao vyao "caucus" wananchi hawajui nani anawatetea, maana ni vikao vya siri. Matokeo yake wanawapa promo wapinzani ambapo hujibebea ujiko mbele ya wapiga kura. Kinachowapandisha chat akina Dr. Slaa, Zitto, Mnyika, Lissu na wengineo ni kwa kuwa hawamung'unyi maneno wakiwa Bungeni na wananchi wanaona kila kitu bila chenga. Badala ya kusubiri kwenye magazeti yasiyo na vyanzo vya kuaminika kwamba Makamba alimkoromea fulani, au sijui nani afyatuka, kwanini wasifyatuke tukiwa tunawaona? Wanaficha nini? Wao si ndio wawakilishi wa wananchi Bungeni? Au ni wawakilishi wa wana CCM na ndio maana wanaenda kufyatukia kwenye caucus?
 
Nimebaini eneo linaloleta 'utata'.
Wapo ndugu zetu wanadhani tunazungumzia nani anamteua nani?kwamba wateule wa Rais hawawezi kuondolewa katika nafasi zao na wabunge.Hii si sahihi kimantiki hata kidogo tukikubaliana na mtiririko huu hapa chini:
1.Rais anachaguliwa na wananchi wa Tanzania,na anawajibika kwao.
2.Wabunge wanachaguliwa na wananchi wa Tanzania.
3.Rais huchagua MAWAZIRI kutoka wabunge wa Tanzania,na kuwa MAWAZIRI wanawajibika indirectly kwa wananchi kupitia kwa wabunge na pia wanawajibika moja kwa moja kwa RAIS.
4.Wananchi wa Tanzania ndio msingi wa utawala,mamlaka na uhalali wa serikali YOYOTE ya KIDEMOKRASIA.
Kwa hiyo,basi,
Kwa kuwa Rais,anawajibika kwa wananchi wa Tanzania,na kwa kuwa wananchi wa Tanzania huiwajibisha serikali yao kupitia wawakilishi wao ambao ni wabunge kwa njia mbalimbali ikiwemo kuuliza maswali bungeni,kujadili bajeti ya serikali, ama hata kuleta hoja binafsi bungeni,na kwa kuwa MAWAZIRI 3 walipata kujiuzulu nyadhifa zao mwaka 2008,na kuwa wabunge, vile vile, wamepata kumtia misukouko bwana David JAIRO mwaka 2011, kwa sababu za uwajibikaji,na kwa kuwa maamuzi hayo hayakubatilishwa hadi leo,na yanaweza kabisa kuchukuliwa kama rejea, basi uamuzi huo utumike tena katika hoja hii,kwa wawakilishi wa wananchi kuchukua hatua za uwajibikaji dhidi ya mawaziri ambao wanamwakilisha rais,na ambao pia kwa kawaida huchaguliwa na wananchi majimboni, kwa makosa ya uzembe na ubadhirifu.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Nimebaini eneo linaloleta 'utata'.
Wapo ndugu zetu wanadhani tunazungumzia nani anamteua nani?kwamba wateule wa Rais hawawezi kuondolewa katika nafasi zao na wabunge.Hii si sahihi kimantiki hata kidogo tukikubaliana na mtiririko huu hapa chini:
1.Rais anachaguliwa na wananchi wa Tanzania,na anawajibika kwao.
2.Wabunge wanachaguliwa na wananchi wa Tanzania.
3.Rais huchagua MAWAZIRI kutoka wabunge wa Tanzania,na kuwa MAWAZIRI wanajibika kwa wananchi kupitia kwa RAIS.
4.Wananchi wa Tanzania ndio msingi wa utawala,mamlaka na uhalali wa serikali YOYOTE ya KIDEMOKRASIA.
Kwa hiyo,basi,
Kwa kuwa Rais,anawajibika kwa wananchi wa Tanzania,na kwa kwa kuwa wananchi wa Tanzania huiwajibisha serikali yao kupitia wawakilishi wao ambao ni wabunge,kwa kuuliza maswali bungeni,kujadili bajeti ya serikali, ama hata kuleta hoja binafsi bungeni,na kwa kuwa MAWAZIRI 3 walipata kujiuzulu nayadhifa zao mwaka 2008,na kuwa vile vile wamepata kumtia misukouko bwana David JAIRO mwaka 2011, kwa sababu za uwajibikaji,na kwa kuwa maamuzi hayo hayakubatilishwa hadi leo,na yanaweza kuchukuliwa kama rejea, basi uamuzi huo utumike tena katika hoja hii,kwa wawakilishi wa wananchi kuchukua hatua za uwajibikaji dhidi ya mawaziri ambao wanamwakilisha rais,na ambao pia kwa kawaida huchaguliwa na wanachi majimboni, kwa makosa ya uzembe na ubadhirifu.

Which you simply mean that badala ya wabunge wa CCM kutaka mawaziri wafukuzwe kwa kupitia vikao vya Caucus vya CCM wafanye hivyo kwa kupitia chombo cha uwakilishi cha wananchi ambacho ni bunge. Wananchi wanawakilishwa kupitia bunge na sio caucus ya CCM.
 
Which you simply mean that badala ya wabunge wa CCM kutaka mawaziri wafukuzwe kwa kupitia vikao vya Caucus vya CCM wafanye hivyo kwa kupitia chombo cha uwakilishi cha wananchi ambacho ni bunge. Wananchi wanawakilishwa kupitia bunge na sio caucus ya CCM.

Exactly!!Ndivyo ilivyo in theory(n advanced democracies )ingawa kuna uchanga wa misingi na tunu za demokrasia katika CCM...na ni mkakati wa kuendeleza status qou.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Mkuu FortJeasus,

Hoja ya msingi ya EMT ni kwamba "caucus" ya CCM haiwezi kumuwajibisha waziri yeyote yule, hata Waziri Mkuu. Hakuna Kanuni wala Sheria inayowapa nguvu au mamlaka ya kumuwajibisha Rais, Waziri Mkuu, Spika, Naibu Spika au Waziri/Naibu Waziri yeyote. Wakishakutana huko pembeni, maamuzi yao huwa hayam-bind yeyote.

Hata maazimio ya Bunge zima bado huwa hayam-bind, na ndio maana huwa wanasema "tunapendekeza mawaziri waliohusika na kashfa wawajibike wenyewe au mamlaka inayohuka na uteuzi iwawajibishe". Wale wa skendo ya Richmond wajiondoa wenyewe, wengine waliofuata hakuna hata mmoja ambaye alishawahi kujiondoa. Si ajabu Lowassa, Karamagi na Msabaha huko waliko wanajuta kwa maamuzi ya kujiondoa.

Sasa kwa kuangalia mtiririko wa utekelezaji wa maazimio ya Bunge tangu 2008 mpaka sasa, sioni kama kuna uwezekano wa JK kutekeleza matakwa ya wabunge wa CCM.

Hajawahi kutekeleza maazimio ya Bunge kuhusu skendo ya Richmond, hajawahi kutekeleza maazimio ya Bunge ya sakata la Jairo, hajawahi kutekeleza mapendekezo ya Kamati ya Huduma za Jamii yaliyomtaka awatimue Mponda na Nkya. Skendo ya Richmond ilizikwa kienyeji. Sakata la Jairo haieleweki kinachoendelea ili hali watu wanasema kwamba jamaa bado anavuta mshiko (mshahara) kama kawa.

Kwa serikali kama hii ya JK, dawa yake ni kuiaibisha tu. Maana ambacho JK amekuwa akifanya tangu 2008 ni kiburi na kulidharau/kulidhalilisha Bunge kwa kutotekeleza maazimio yake. Nadhani kuna watu walimwambia kwamba hata asipotekeleza maazimio na mapendekezo ya Bunge, Bunge haliwezi kumfanya kitu. So, amejenga tabia ya kusema kwani watafanya nini? Dawa ya mtu ambaye anafunga mdomo ili asinywe dawa, ziba pua yake, lazima atafungua mdomo na ndipo unapoingiza dawa. Akiitema, dunga sindano.

Wabunge wa CCM wangekuwa na akili wangemuunga mkono Zitto ili kumshikisha adabu JK kwa kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, kitu ambacho kinamlazimisha JK kuvunja Baraza la Mawaziri na kuunda jipya au angewatema hao mafisadi wake (hii ndio kuziba pua). Sasa kama atawarudisha mafisadi hao hao kwenye baraza jipya (kutema dawa), then wabunge watajua kwamba Rais mwenyewe ndiye fisadi mkuu, kwa hiyo badala ya kuhangaika na Waziri Mkuu, then Bunge linapiga kura ya kukosa imani na JK mwenyewe ili kuitisha uchaguzi mwingine (dunga sindano).

Kwa ushindi wa 61% alioupata 2010 tena kwa mbinde, hawezi ku-take hiyo risk maana anajua wazi kwamba zitashuka mpaka less than 40%. Kwa hiyo angekuwa na nidhamu na asingejifanyia mambo kama anavyotaka. Sasa kwa sababu wabunge wa CCM wamedekeza ndio maana anasema hafanyi kazi kwa shinikizo, kama siyo dharau ni nini? Iwapo Bunge litatumia njia ambayo inamlazimisha, hawezi kuwa na hayo majibu ya dharau na kudhalilisha.

Kwa kuwa wabunge wa CCM ama sheria zinawapiga chenga au uelewa mdogo wa political calculations, wao wanakimbilia kwenye caucus na tayari wameishaanza kulalamika kwamba Zitto amepora hoja yao. Hoja hiyo sio ya Zitto, ni hoja ya Bunge zima, maana bila support ya wabunge wa CCM, hoja hiyo haiwezi kupata kura za kutosha. Hoja hiyo ingefanikiwa, credit ingeenda kwa Bunge zima na sio kwa chama fulani au Mbunge fulani.

Wabunge wengi wa CCM wanatakiwa kuelewa kwamba JK hii ni term yake ya mwisho, hatarudi kwenye kampeni come 2015. So, whatever wanachokifanya leo, kitakuja ku-backfire kwenye uchaguzi. Uchaguzi ni wao, kama wanataka kurudi mjengoni ni juu yao, kama wanataka kumfurahisha JK hiyo ni juu yao, lakini mwisho wa siku hasara ni ya kwao.
 
Which you simply mean that badala ya wabunge wa CCM kutaka mawaziri wafukuzwe kwa kupitia vikao vya Caucus vya CCM wafanye hivyo kwa kupitia chombo cha uwakilishi cha wananchi ambacho ni bunge. Wananchi wanawakilishwa kupitia bunge na sio caucus ya CCM.
Waziri anaweza kujiuzulu anytime, for any reason.
Anaweza kufukuzwa uwaziri na wabunge au rais.
Tunapozungumzia wabunge, wao pia ni wananchi raia wqa Tanzania.
Kama mawaziri wasingetaka kujiuzulu, halafu babu mmoja mchawi akawaloga wakajiuzulu, the end result is the same and justifiable.Hakuna sheria inayozuia.
 
Waziri anaweza kujiuzulu anytime, for any reason.
Anaweza kufukuzwa uwaziri na wabunge au rais.
Tunapozungumzia wabunge, wao pia ni wananchi raia wqa Tanzania.
Kama mawaziri wasingetaka kujiuzulu, halafu babu mmoja mchawi akawaloga wakajiuzulu, the end result is the same and justifiable.Hakuna sheria inayozuia.

Naomba unipe mfano mmoja tu wa Waziri ambaye ameishawahi kufukuzwa na caucus ya CCM kwenye hizi zama za siasa za vyama vingi.
 
wabunge wengine wa ccm wanafuata upepe2 na kutokuwa makini, hoja ya zitto ni ya kisiasa
 
Taarifa zinasema kumekuwa na mazungumzo baina ya Rais Kikwete na Pinda yaliyolenga kunusuru serikali yao lakini wametofautiana kuhusu hatua inayopaswa kuchukuliwa dhidi ya mawaziri waliotakiwa kujiuzulu.








Msimamo wa Pinda inadaiwa kuwa anataka mawaziri wanaokabiliwa na tuhuma waondoke ili kuleta uwajibikaji serikalini, lakini Rais Kikwete amesema mawaziri hao waachwe waendelee na kazi zao, kwa kuwa suala hili ni la upepo tu, liachwe litapita.

Habari zinasema Rais Kikwete na Pinda walitofautiana juu ya hatua dhidi ya mawaziri hao, hivyo kuwafanya baadhi ya mawaziri kutamba mitaani kuwa hawang'oki madarakani kwa sababu tayari bosi wao ameonyesha kutounga mkono tuhuma hizo.

Habari hizi zinasema pia kwamba Pinda amekuwa hafurahishwi na msimamo wa ‘bosi' wake, hasa katika kushindwa kutoa uamuzi mgumu.

Baadhi ya wabunge wameweka wazi kuwa kama Rais Kikwete ataamua kuwalinda na kuwatetea mawaziri wake basi watawaondoa kwa mkakati tofauti utakaomlazimisha rais kukubaliana na hoja za wabunge.


Source: Gazeti la Tanzania Daima

Kama Pinda ametoa ushauri mawaziri waondolewe na Raisi akakataa, Je hiyo siyo sababu tosha kwa Pinda kujiuzulu? Ieleweke kwamba hii siyo mara ya kwanza Pinda kupuuzwa na JK au Viongozi wengine waliokaribu na/washikaji wa JK
 
Waziri anaweza kujiuzulu anytime, for any reason.
Anaweza kufukuzwa uwaziri na wabunge au rais.
Tunapozungumzia wabunge, wao pia ni wananchi raia wqa Tanzania.
Kama mawaziri wasingetaka kujiuzulu, halafu babu mmoja mchawi akawaloga wakajiuzulu, the end result is the same and justifiable.Hakuna sheria inayozuia.

Kwa maana hiyo unakubali kuwa "caucus" ya CCM haina uwezo wa kumfukuza waziri?
Au una maana gani unaposema kuwa waziri anaweza "kufukuzwa uwaziri na wabunge"?
Wabunge kwa maana ya wabunge wa bunge la Jamhuri au wabunge wa CCM kupitia "caucus" ya CCM?
 
Wizi unafanyika raisi wa nchi(Jakaya Kikwete)anawatetea wezi wa mali ya uma kwa kauli za reja reja kama hizi(huu ni upepo utapita tu).Mhuni ndie aliepaswa kuzungumza maneno haya sio raisi wa nchi.Nnasema Leo hapa jamiiforums Kama kweli mkuu wa nchi ndie mtetea wezi wa mali ya uma basi Jakaya ni janga la kitaifa
 
Kwa maana hiyo unakubali kuwa "caucus" ya CCM haina uwezo wa kumfukuza waziri?
Au una maana gani unaposema kuwa waziri anaweza "kufukuzwa uwaziri na wabunge"?
Wabunge kwa maana ya wabunge wa bunge la Jamhuri au wabunge wa CCM kupitia "caucus" ya CCM?
EMT, hawa jamaa hata ukiwaelewesha usiku kucha hawataweza kuelewa unachosema. Caucus ya CCM si mbadala wa Bunge, na hakina uwezo wala ubavu wa kumlazimisha waziri ajiuzulu labda aamue mwenyewe. Na hata akiamua hivyo bado Raisi kama anamhitaji anaweza kumkatalia kama alivyowahi kumkatalia Dr. Idris Rashid wa TANESCO huko nyuma. Bunge pekee ndilo lenye uwezo wa kupiga kura ya kutokuwa na imani kwa ama Waziri Mkuu au Raisi ndani ya kikao rasmi cha bunge na siyo uchochoroni eti kwenye caucus ya CCM.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Vipi rais akikataa kuitikia wito wao wa kuwafukuza kazi hao wabunge? Wako tayari kula matapishi yao?

Ni dhahiri Wabunge watakula matapishi yao,kwani wameshiriki nyakati tofauti bungeni kukubaliana na matakwa au malengo hafifu ya serikali kwa asili mia mmoja,na hivyo watakubali yaishe ili wasimuudhi Raisi.Imekula kwao,wameuza utu wao siku nyingi na mara nyingi,vipi wanakumbuka shuka asubuhi?
 
The logic behind ni kuwavua madaraka mawaziri ambao ni wana-CCM wenzao kistaarabu. Wasiopotaka, basi baraza la mawaziri lote litaondoka!!! CCM ina majority, so only CCM caucus can do this!!!.... trust me, they can do it. Hata rais anaweza kuondolewa na wabunge wa CCM wakiamua kwa pamoja.
kobello, unaishi katika nchi ya kusadikika siyo Tanzania and very soon you will come back to earth only a little wiser!
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: EMT
Back
Top Bottom