Izack Mwanahapa
JF-Expert Member
- Apr 21, 2011
- 497
- 236
Bunge la sasa limekuwa moto kutokana na ongezeko la wabunge vijana, lakini vijana hawa wapo mbioni kupoteza viti vyao 2015 kama tabia ya kulewa sifa haitaondoka miongoni mwao. Kimsingi Tanzania inahitaji wabunge vijana wenye uwezo wa kufikiri na kufanya maamuzi yao kwa busara kwa kutumia vizuri elimu waliyonayo. Vitendo vya uropokaji na kujiamini kupita kiasi na kuonge kwa sababu tu mdomo unao kama ilivyokuwa kwa Ndugu Kafulila vitapelekea umma wa watanzania kupoteza imani kwa wagombea vijana. Tunaomba mjitahidi kufanya kazizenu kwa ufasaha madaraka makubwa mtayapata tu uasi si lazima