Wabunge na mfumo wa udhibiti wao

GY

JF-Expert Member
Nov 2, 2009
1,279
126
Samahani kama hoja hii ilishawai kujadiliwa kabla

Nilitaka kujua, katiba inasemaje ikiwa mbunge aliyechaguliwa na wananchi hafanyi yale aliyoahidi na/au yaliyotarajiwa kutoka kwake, je wananchi wanauwezo wa kumuondoa kabla ya kipindi cha uchaguzi mwingine au laa

Na ikiwa inawezekana, ni utaratibu gani unatakiwa kufuatwa?

Na Ikiwa haiwezekani, je ni haki kwa wananchi kumchagua mtu awawakilishe kwa miaka mitano, lakini yeye kwakuwa labda alihitaji ubunge kwa ajili ya masuala yake binafsi, basi asifanye hata moja aliloahidi au analoombwa na wananchi wake, wananchi wasubiri mpaka miaka mitano ndio wamuadhibu mtu huyo

Naomba kutoa hoja
 
Back
Top Bottom