Wabunge na Mawaziri Muungano Mmeishiwa: SMZ

Junius

JF-Expert Member
Mar 11, 2009
3,181
139
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imesema Wabunge na mawaziri wa Serikaliya Muungano wanaokejeli Maaumuzi ya Baraza la Mapinduzi juu ya kuliondoa suala la utafutaji mafuta na uchimbaji wa gesi asilia katika mambo ya Muungano wameishiwa na hoja.
Waziri wa Maji, Ujenzi,Nishati na Ardhi, Mansoor Yussuf Himid, Aliliambia Baraza la Wawakilishi wakati akijibu hoja mbali mbali zilizotolewa walipokuwa wakichangia bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka wafedha 2009/10.
Waziri Mansour, alisema kauli ya Baraza la Mapinduzi iliyoiwasilisha mbele ya Baraza la Wawakilishi, juu ya maamuzi ya haikuwa yake binafsi na ni ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar’.
“Wizara yangu inawajibika kwa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, inayoongozwa na Rais Dk. Amani Abeid Karume na Baraza hili lipo chini yake yeye Rais Karume na wewe Mheshimiwa Pandu Ameir Kificho ndie unaeliongoza na siwajibiki kwa Wabunge” alisema Waziri huyo.
Alisema kwamba “Ni hulka ya mwanadamu anapokosa hoja usishangae kwani atatukana na anaweza kutupa mawe sasa na ndio hao wabunge wamekosa hoja anapojuwa amewatendea wenzake dhambi na wizi wa mchana” alisisitiza Waziri huyo.
Alisema Baraza la Mapinduzi limeamua kutoa uamuzi huo baada ya kubaini kuwapo kwa ghilba za wizi wa mchana juu ya suala hilo zilizobainishwa na Mshauri elekezi na SMZ haijifurahishi kwani wanachokieleza wabunge hao pamoja Viongozi wa Muungano ni kutokana na kuishiwa kwa hoja juu maamuzi iliyoyachukua serikali.
Akifafanua kauli yake hiyo alisema katika baadhi maelezo ya Mshauri elekezi ambayo yamo ndani ya ripoti yake imeelezea wazi kuwa sheria zilizowekwa kusimamia mafuta na gesi asilia Tanzania, imetungwa ikiwa kama Zanzibar haimo ndani ya vipengele vyake vya sheria hiyo na ndio maana serikali haioni haja ya kuelezea kama suala hilo ni la Muungano.
“Baada ya kuona tatizo lipo ndio maana serikali mbili ilizungumzwe na serikali kama zanzibar haipo utaifa uko wapi” Alihoji Waziri huyo huku akishangiriwa na wajumbe wenzake.
Himid alisema kwamba sheria ya uundwaji wa Shirika la Kusimamia Mafuta Tanzania (TPDC) ni maoni ya muelekezi ya ambapo ameeleza kwamba halina sura ya Muungano.
“Mwelekezi alisema utaratibu tunaoutumia ni wa ajabu na haupo duniani kote na unatumika Tanzania peke yake na akaelekeza kupelekwa katika Mahakma ya Kikatiba sasa tatizo liko wapi Mheshimiwa Spika tayari njia ipo ya kufuatwa” Aliuliza Himid.
“Nilisikia hadithi moja Nyerere akielezea dhana ya Mungano ambapo alimuita Karume akamwambia waunganishe nchi, lakini siamini kama Mzee Karume, na Mzee Thabit Kombo, waliondosha watawala wawili na kukubali kuletewa watawala wengine mmoja hakuna watawala wengine tunataka kujenga umoja” alisema Waziri huyo huku akipumzika.
Baada ya kubainika hayo Mshauri Mwelekezi pia ametowa rai ya kwamba suala hilo serikali zote zielekee katika mahakama ya Kikatiba kwa vile utaratibu wake ulikuwa ni wa ajabu kabisa.
Waziri huyo alifahamisha ndio maana serikaliya Zanzibar iliyabaini hayo mapema tangu wakati wa utawala wa Dk. Salmin Amor, ambaye alitoa amri ya kuzizuia baadhi ya kampuni zilizopewa leseni na serikali ya Muungano kutafuta mafuta hapa Zanzibar.
“Hapa Mshauri elekezi alikuja katika Baraza la wawakilishi, akatuambia kwamba sheria zote za mafuta zimetungwa kama Zanzibar haipo na Mamlaka ama taasisi ya kusimamia mafuta haipo wanalazimisha hii ni dhambi kubwa Mheshimiwa Spika wanayowatendea wenzao dhambi na ni wizi wa mchana kweupe kabisa” alisema kwa hasira Waziri huyo.
Himid alisema Mshauri Mwelekezi alisema tatizo lipo na ndio maana alisema mlizungumze na ndio hatua hiyo ya Wajumbe wa Baraza hilo ilikuja baada ya Naibu Waziri wa Nishati na Madini Tanzania bara Adam Kigoma Malima kuliambia Bunge kwamba msimamo wa SMZ kupitiaBaraza lake la Mapinduzi kuliondoa suala la mafuta katika kero za Muungano ni kujifurahisha jambo ambalo baraza hilo lilieleza ni kitendo cha dharau.
Kauli hiyo ya Malima pia iliungwa na mkono na Mbunge wa Same, Samueli Sita ambaye aliliambia Bunge hiyo kwamba hatua hiyoitailazimu SMZ kuamuliwa na Bunge mambo ambayo yalisababisha kutolewa matamshi mbali mbali ya wajumbe wa baraza la Wawakilishi.
Waziri huyo alifahamisha ni vyema kwamba Wabunge kutambua kuwa hakuna watawala wawili wanoweza kumtawala mtawala mmoja na kuzingatia kwamba Muungano uliounganisha Zanzibar na Tanganyika umefanywa kutokana na kujenga umoja wa nchi mbili hizo ili kutafuta mustakabali bora wa maelewano.
“Wazanzibari wamefuta utaifa wao iliwafaidike na Muungano lakini sio kwa utaratibu wa sasa uliopo wanakejeli leo tunatafuta suluhu na njia muafaka tuna ambiwa tunajifurahisha Muheshimiwa Spika Baraza la Mapinduzi, ndio limeshaamua” alisema Waziri huyo hukuakiwa anashangiriwa na wajumbe wa Baraza hilo.
Akiendelea alisema kazi ambayo hivi sasa Wizara hiyo inakusuda kuifanya ni kuona inamalizia kutayarisha sera ya kusimamia mafuta na gesi asilia, pamoja na kuandaa sheria ambayo inatarajiwa kuwasilishwa katikakikao cha mwezi Oktoba mwaka huu.

SOURCE: ZANZIBAR YETU BLOG.
 
S
“Mwelekezi alisema utaratibu tunaoutumia ni wa ajabu na haupo duniani kote na unatumika Tanzania peke yake na akaelekeza kupelekwa katika Mahakma ya Kikatiba sasa tatizo liko wapi Mheshimiwa Spika tayari njia ipo ya kufuatwa” Aliuliza Himid.
“Nilisikia hadithi moja Nyerere akielezea dhana ya Mungano ambapo alimuita Karume akamwambia waunganishe nchi, lakini siamini kama Mzee Karume, na Mzee Thabit Kombo, waliondosha watawala wawili na kukubali kuletewa watawala wengine mmoja hakuna watawala wengine tunataka kujenga umoja” alisema Waziri huyo huku akipumzika.

SOURCE: ZANZIBAR YETU BLOG.

Kwani kilakitu lazima tuige kwa watu, kwani hakiwezi tukawa nacho sisi tu wengine wasiwe nacho duniani? Mimi namwona mwalimu alikuwa na akili aliunda kiu ambacho hata wazungu hawana?? na wanatamani wangekuwa nacho.

Vipi tukivunja muungano leo? Pemba na Unguja watabaki wamoja?? Nyie watu wa visiwani masije mkaanza tena kuomba mkahifadhiwe sumbawanga kama wakimbizi mtakapo chafuliana hali ya hewa huko znz, haya shauri yenu
 
Haya mafuta ambayo hayapo yamewapagawisha Wazenj. Sasa hivi wameamua kuumega Muungano kidogokidogo ili wasishtukiwe, leo mafuta na gesi asilia, kesho watataka kuwa na fedha yao, nk. Mwisho wa siku kutakuwa hakuna Muungano!
 
Haya mafuta ambayo hayapo yamewapagawisha Wazenj. Sasa hivi wameamua kuumega Muungano kidogokidogo ili wasishtukiwe, leo mafuta na gesi asilia, kesho watataka kuwa na fedha yao, nk. Mwisho wa siku kutakuwa hakuna Muungano!

Inani kumbusha wakati fulani nikiwa dogo tulikuwa tuna bishana bwana. kisa ilikuwa jinsi ya kugawana pesa kama tukiokota. Tukabishana wee na nusu kukunjana mashati. Kuja kuamuliwa ugomvi na kueleza kisa chenyewe yani ilibidi watu waanze kucheka. Ndiyo ninavyo ona hili swala mimi. Ni utoto. It's obvious waasisi wa muungano wasingeweza kuanticipate kila kitu. Kuna vitu vingi ambavyo havikuwepo wakati huo vitakuja kuwepo. Sasa kila kitu kipya ambacho hakikuwepo tuka barikiwa kukipata na kuunza kusema hichi ni cha huyo peke yake na kile ni cha yule peke yake muungano utadumu kweli baada ya miaka kadhaa? Hii ni dalili kwamba muungano wetu bado ni jina na haujaweza kuintergrate kisawa sawa. Sidhani kama watu ni wa nyumba moja mmoja wapo akipaa chakula atasema hiki ni changu nyie wengine hamna chenu. Kuna matatizo on both sides.
 
Wazenj huwa hawaeleweki sometimes. Kwenye share za BOT wanataka wajipachike, kwenye suala la mafuta/gesi asilia wanataka wajitenge! Chao changu, changu changu?
 
Sasa kama walishauriwa suala lifikishwe kwenye mahakama ya katiba, kwa nini wamelitolea uamuzi kabla ya kulifikisha mahakamani kama walivyoshaurowa? wanajua maana ya jambo walilolifanya?
 
Inani kumbusha wakati fulani nikiwa dogo tulikuwa tuna bishana bwana. kisa ilikuwa jinsi ya kugawana pesa kama tukiokota. Tukabishana wee na nusu kukunjana mashati. Kuja kuamuliwa ugomvi na kueleza kisa chenyewe yani ilibidi watu waanze kucheka. Ndiyo ninavyo ona hili swala mimi. Ni utoto. It's obvious waasisi wa muungano wasingeweza kuanticipate kila kitu. Kuna vitu vingi ambavyo havikuwepo wakati huo vitakuja kuwepo. Sasa kila kitu kipya ambacho hakikuwepo tuka barikiwa kukipata na kuunza kusema hichi ni cha huyo peke yake na kile ni cha yule peke yake muungano utadumu kweli baada ya miaka kadhaa? Hii ni dalili kwamba muungano wetu bado ni jina na haujaweza kuintergrate kisawa sawa. Sidhani kama watu ni wa nyumba moja mmoja wapo akipaa chakula atasema hiki ni changu nyie wengine hamna chenu. Kuna matatizo on both sides.
Kinachosumbua ni viongozi kuwa na tamaa ya madaraka.Tukumbuke kuwa mwakani ni kipindi cha uchaguzi na viongozi wengi CCM Zanzibar ili kupata umaarufu hutumia kasoro za Muungano kujijenga.Kelele zote hizi zinatangazwa na kusikika sana ni siasa za makundi katika mchakato wa kujiweka sawa kwa ajili ya Uchaguzi wa mwakani.
Muundo wa muungano una matatizo,lakini ukweli hakuna kitu hapa duniani kilichoundwa na mwanadamu kisiwe na kasoro.Tunapobaini tatizo busara inakutuma kutafuta chanzo cha tatizo na kutafuta majibu yatakayopelekea tatizo kulitatua.Sasa kinachonishangaza ni tabia ya viongozi wa CCM Zanzibar kuorodhesha matatizo bila kutoa njia sahihi ya kuyatatua.Mimi binafsi naona wanatumia njia kulalamika hadharani ili kujenga chuki kwa watu wauchukie muungano na kuonekana kama ndio chanzo cha wananchi kuwa maskini.Haya mafuta ni kikolezo tu cha kuchochea chuki na hasira za wananchi wauchukie muungano.
Hivi taratibu za kuwakilisha mapendekezo ya kutatua matatizo hayo si zipo au kama hazipo ni njia zipi za kutumia ili tuweze kuanzisha hiyo mahakama ya kikatiba kama haipo?
Nafikiri it is time watu kushirikishwa kufikia uamuzi muafaka wa suala hili kuliko kuliacha Viongozi kuwawekea maneno wananchi ambayo hayapo.
 
Kwani kilakitu lazima tuige kwa watu, kwani hakiwezi tukawa nacho sisi tu wengine wasiwe nacho duniani? Mimi namwona mwalimu alikuwa na akili aliunda kiu ambacho hata wazungu hawana?? na wanatamani wangekuwa nacho.
Hata na mimi naomuona Mwalimu alikuwa ana akili. Na waliokubali kuundwa kwa kitu hicho (Muungano wa ainan yetu) kina Mzee Karume na Sheikh Thabit Koimbo pia walikuwa na akili kwa kubali hilo. Lakini kuundwa kwa kitu ni jambo moja na kutekelezwa kwa muundo wake ni lengine. Tatizo letu lililotufikisha hapa tulipo katika muungano ni kutokubali kutekeleza kile kilochokubaliwa kuundwa wakati huo. Hayo ndiyo kwa ufupi anayoeleza Mansour. Na ujanja wa kupindisha kutekeleza kilichokubaliwa katika muungano huu ulikuwa ukifanyika tokea waasisi hao wapo hai. Na tulishuhudia mara kadha Mzee Karume akilalama kwa Mwalimu Nyerere kuhusu mambo fulani fulani ambayo Zanzibar ilikuwa inataka kunyanganywa umiliki na kuingizwa katika himaya ya Muungano. rejea historia. sasa Wazanzibari hawakatai Muungano huu wa aina yetu kinachokataliwa ni utekelezaji unaokwenda kinyume na matakwa na matakwa na misingi ya Muungano huu wa mfano.
 
CUF na CCM wataendelea kuwa kitu kimoja wakati wa uchaguzi mkuu, 2010 kwa 'maslahi ya taifa' au mafuta hewa ndio yamewaunganisha kwa kitambo?
 
kulaumu viongozi wa CCM Zanzibar peke yao hutendi haki. Kwa nini hulaumu na wabunge pamoja spika wao Sitt. Kauli ya kuwabeza wenzao wa baraza la wawakilkishi inatoka wapi? Ni ya kiungwana hiyo au ni ya kuashiria ubabe wa Spika Sitta na Bunge lake. Hizo busara ziko wapi hapo? sasa wale wa wawakilishi wanaojibu kuwa nao kama ni chombo halali cha wananchi na chenje madaraka na mamlaka kamili kwa Zanzibar kinao ubavu wa kutaka jambo fulani liliomo katika Muungano liondolewe katika orodha ya Muungano, au kwa ufupi kutaka jinsi ya vipi Muungano wetu uwe- utawasakamaje na kuwapigia makofi kina Sitta?
 
kulaumu viongozi wa CCM Zanzibar peke yao hutendi haki. Kwa nini hulaumu na wabunge pamoja spika wao Sitt. Kauli ya kuwabeza wenzao wa baraza la wawakilkishi inatoka wapi? Ni ya kiungwana hiyo au ni ya kuashiria ubabe wa Spika Sitta na Bunge lake. Hizo busara ziko wapi hapo? sasa wale wa wawakilishi wanaojibu kuwa nao kama ni chombo halali cha wananchi na chenje madaraka na mamlaka kamili kwa Zanzibar kinao ubavu wa kutaka jambo fulani liliomo katika Muungano liondolewe katika orodha ya Muungano, au kwa ufupi kutaka jinsi ya vipi Muungano wetu uwe- utawasakamaje na kuwapigia makofi kina Sitta?
SItta amesema sawa hana makosa ,mafuta ni ya Muungano na hao vitimba kwiri wanaotokeza humo kwenye serikali ya Zanzibar ni wanafiki tena wazandiki wasio na maana hata ya kuwepo madarakani, mi naunga mkono kuwa mafuta na gesi yote ni mali ya Muungano Zanzibar yao ni serikali tu ,wanakwiba kukaa madarakani sasa wasubiri wagaiwe mishahara kutokana na mauzo ya mafuta ,wasijidai kuwa vifua mbele kutetea Zanzibar ni waongo wezi.
 
Wazenj huwa hawaeleweki sometimes. Kwenye share za BOT wanataka wajipachike, kwenye suala la mafuta/gesi asilia wanataka wajitenge! Chao changu, changu changu?


kama kipi unachokiona wewe cha Tanganyika wazenji wanjivunia ?ulisha wahi kumsikia mzenji kutamka na kuwambia watu mahali popote pale ulimwenguni eti sie tuna mlima wa kilimanjaro au tunambuga za wanyama na kadhalika kwa nini hawafanyi hivyo ?sababu tunajuwa(elewa) kuwa sio vyetu ni sawa na ule msemo wa kiswahili unaosema mtegemea cha ndugu hufa masikini.ulichosema wewe hapa ni kizungu mkuti eti chao changu changu changu kwa msemo wako huo ni sawa kuwambia jamaa zako kwanini hizi gas na madini kama ya pamoja hawa jamaa wazenj hawana chao na iweje mafuta yao yawe yetu ingekuwa wewe binafsi tujalie mimi ndio mwenye mali iliyokuwepo Tanganyika na wewe ndio mwenye mali iliyokuwepo ZANZIBAR halafu tukawa na ushirikianao mali yangu ni yangu peke yangu lakini mali yako ndio tuwe tunagawana na sio yangu, ungelikubali hilo? na kweli linaingia akili hilo ?mumekuwa mnatumia msemo huo Chao changu, changu changu hata hamuoni aibu .ulimwengu wa sasa ni wa uwazi hizo propaganda za aruba fogo wali pesambili zimeshapitwa na wakati.
 
Last edited:
kulaumu viongozi wa CCM Zanzibar peke yao hutendi haki. Kwa nini hulaumu na wabunge pamoja spika wao Sitt. Kauli ya kuwabeza wenzao wa baraza la wawakilkishi inatoka wapi? Ni ya kiungwana hiyo au ni ya kuashiria ubabe wa Spika Sitta na Bunge lake. Hizo busara ziko wapi hapo? sasa wale wa wawakilishi wanaojibu kuwa nao kama ni chombo halali cha wananchi na chenje madaraka na mamlaka kamili kwa Zanzibar kinao ubavu wa kutaka jambo fulani liliomo katika Muungano liondolewe katika orodha ya Muungano, au kwa ufupi kutaka jinsi ya vipi Muungano wetu uwe- utawasakamaje na kuwapigia makofi kina Sitta?

Kaka pakacha upo ?leo nakuona unahubiri kwa unyoge kabisa ,jamaa waliokamata mapini ndio washasema serekali ya watoto wa wakulima na wakwezi hawana uwezo wa kuamuwa mambo ya kiume,full stop
 
Babylon,
Kuthibitisha zaidi msemo huo unawageukia wao unamkumbuka Mh. Daniel Yona(fisadi papa No.6) alipo kuwa waziri wa fedha, aliwaambia Wazanzibar kuwa katika umeme wetu hakuna cha Muungano wala nini, mtalipa au tutawakatia nchi nzima,"business is business.." akaishia
Mwaka 1996 SMT iliinyima makusudi Zanzibar misada ya wafadhili kwa madai kuwa eti wafadhili wamesitisha misada yao zanzibar baada mgogoro na kutoridhishwana matokeo ya uchaguzi mkuu wa 1995. Yona alisisitiza kuwa hawasingeweza kukiuka maagizo ya wahisani kwa kuipa mgao wake zanzibar kutoka na misada ya muungano kwa kuchelea hasira ya wahisani hao kwa SMT. Hebu nambieni ndo udugu gani huo kujifikiria ww tu wakati ndugu yako wa miaka zaidi ya 40 anakufa njaa? Leo akiamua yy ajitafutiea asikutegemee tena kwa roho mbaya, ww unaona vibaya?
 
Swali: Hivi Tanganyika tunafaidikaje kwa Zanzibar kujiunga nasi?

Wazenj wanataka mafuta aslia na gesi yao yawe yao wenyewe. Wadanganyika wanawapekea umeme utokanao na gesi asilia yao bila Wazenj kutambua umuhimu wake.

Wazenj wasiozidi milioni moja wanataka usawa na Wadanganyika milioni 38. Hata hakuna mkoa mmoja bara wenye wakaazi wachache hivyo. Usawa gani huu??????

Bunge la Muungano lina Wazenj 50 na Wadanganyika takriban 250. Hata Upinzani Bungeni unaongozwa na Wazenj! Na kuna mawaziri wazenj chungu mbovu. We have bent backwards for too long. Enough is enough!!!!
 
Hili la CCM- Zanzibar kweli jamaa ni wakali sio mchezo,Zanzibar uwezekano wakuwa na mafuta ni mdogo sana na wala hawana mpango nao.

Hapa dili ni kuwa ,hawa wajanja wa ccm- zanzibar wameshazichungulia nyavu za Bartez ,namna ambavyo akili ya watanzania yani wazanzibar zilikoegemea, kuwa kete mhimu kwao ni kuushambulia muungano ni kete isiyo na maslahi kwa zanzibar bali ni kete mhimu kurejea ktk viti virefu.

Hii ni sawa na huku kwetu kwa wadanganyika hawa wenye kete ya ufisadu,tunajuwa ufisadi ni mbaya ndiyo lakini kama kweli malengo yako ni kuikomboa nchi hii na si vinginevyo ,ok panda mwenge yanga sema yote ok njoo nenda mahakami kafungue kesi na nyaraka zako mhimu.

Kwanini hawaendi mahakamani japo wananyaraka mhimu ni kwasababu malengo yao makuu si hayo ya kuukomesha ufisadi,malengo ni kete ili apate pa kupandia ngazi kila mara maana akifikisha mahakamani kete hiyo itafungwa rasimi.Nakukosa umaarufu na jinsi ya kuzikonga nyoyo za wadanganyika.
 
Babylon,
Kuthibitisha zaidi msemo huo unawageukia wao unamkumbuka Mh. Daniel Yona(fisadi papa No.6) alipo kuwa waziri wa fedha, aliwaambia Wazanzibar kuwa katika umeme wetu hakuna cha Muungano wala nini, mtalipa au tutawakatia nchi nzima,"business is business.." akaishia
Mwaka 1996 SMT iliinyima makusudi Zanzibar misada ya wafadhili kwa madai kuwa eti wafadhili wamesitisha misada yao zanzibar baada mgogoro na kutoridhishwana matokeo ya uchaguzi mkuu wa 1995. Yona alisisitiza kuwa hawasingeweza kukiuka maagizo ya wahisani kwa kuipa mgao wake zanzibar kutoka na misada ya muungano kwa kuchelea hasira ya wahisani hao kwa SMT. Hebu nambieni ndo udugu gani huo kujifikiria ww tu wakati ndugu yako wa miaka zaidi ya 40 anakufa njaa? Leo akiamua yy ajitafutiea asikutegemee tena kwa roho mbaya, ww unaona vibaya?

sasa ndg unataka wanzanzibar wasilipe umeme?zanzibar wana shirika lao la umeme linalojiendesha kibiashara na linategemea umeme wa tanesco linalojiendesha kibiashara,hivyo yona alikuwa sahihi kuwaambia alivyowaambia.
sasa kama wahisani wametoa pesa kwa masharti kwanini tusifuate masharti?ni juu yao kutoa pesa na kuelekeza wapi pa kutumika,kosa la yona hapo lipo wapi?kuwaambia ukweli?mngekuwa mnataka mgao mngemwachia seif shariff kiti cha urais alichoshinda kipindi hicho.
 
sasa ndg unataka wanzanzibar wasilipe umeme?sasa kama wahisani wametoa pesa kwa masharti kwanini tusifuate masharti?ni juu yao kutoa pesa na kuelekeza wapi pa kutumika,kosa la yona hapo lipo wapi?kuwaambia ukweli?
Kwanza wakati Yona alipo sema hvyo SMZ haikusema haitaki kulipa, kilichokuwa kina tibua kuona SMT hawakuwa na soni wala uungwana kutoa vitisho vya kudai deni lao, na walii treat zanzibar kama wateja wengine wakati zanzibar ni mteja "special" nikimaanisha ana maslahi mengine kaitka chombo (smt) kinachomiliki TANESCO.
Fikiria ww tupo katika Muungano kwa muda wa miaka zaidi ya 40, tumeshakuwa ndugu wa hali na mali,shida na raha, kufa na kuzikana n.k Leo anakuja jirani au mtu mbali wakati wa shida, anakupa msaada halafu anakwambia, ndugu yako huyo wa kufa na kuzikana usimpe, na ww unakubali hutampa na kejeli juu, kweli huo ndo undugu wa kweli na si unafiki. Msifikiri wazanzibar wasahaulifu wanajua kila dhuluma na idhiliali waliyosababishiwa na Muungano tokea mapinduzi 1964, kupachikiwa viongozi mamluki, kuuliwa na kupotea kwa waasisi wao, kuteswa, mauwaji ya Jan.26/27/01 n.k na wala haitasahau walivyowavumilia wenzao wa Tanganyika katika vipindi vyote vigumu hata ikafika zanzibar inatoa fedha zake mfukoni kusaidia mambo yasiyokuwa ya muungano. Wala haitasahau roho za wazanzibar katika vita vya Kagera(vita binafsi vya Nyerere na Idd Amin) ambavyo havikuwa na sababu kupiganwa na rasilimali chungu nzima nyengine zikapotea na nchi kuingizwa katika umasikini mkubwa, sote tulilazimishwa kufunga mikanda kulipa gharama za vita visivyo tuhusu ndewe wala sikio. Leo unapo justify maneno ya Yona unapimia mizani ipi ya udugu na kustahamiliana?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom