Inanambo
JF-Expert Member
- Jun 26, 2011
- 3,986
- 2,765
Juzi nilikuwa nasilkiliza Bunge wakitunga sheria na kurekebisha sheria. Mh J. Mnyika alikuwa anatoa maoni kuhusu marekebisho ya matumizi ya Bajeti ya taasisi za Serikali. Kwamba kuna makusanyo wanafanya na kutumia hizo pesa wapendavyo bila kuingiliwa na Bunge au serikali. Mnyika akataka sheria itungwe kudhibiti matumizi ya hayo mapato au kodi. Mfano Ewura, THA, TRA, TCCA, TAA na wengineo wana mapato wanakusanya ambayo hutumia wapendavyo bila kuingiliwa na serikali mfano kujilipa posho za vikao, safari na mishahara mikubwa kuliko taasisi zingine za Umma na serikali ambayo imepelekea waTz waone hakuna usawa kwenye keki ya taifa. Taasisi hizi hufanya hivyo kwa sababu sheria inawaruhusu hivyo Mh Mnyika Jembe la Ukweli akataka sheria itenguliwe wapate kudhibitiwa hakuna matumizi nje ya Bajeti. Nilishangaa hakupata Support kwa Wabunge wenzake na sheria ilipita kama ilivyoandikwa. Nauliza tutajenga lini Usawa kwenye taasisi zetu ikiwa tunawakubali pesa zikusanywe na zitumike wengine wapendavyo?