clemence
JF-Expert Member
- Mar 31, 2011
- 594
- 212
Kwanza nianze kwa kusema kuwa Watanzania wa leo sio wale wa miaka hiyo ambao walikuwa wanaitikia kila kitu kinachosemwa na viongozi wao, wakiamini kuwa kila neno litokalo kwa kiongozi ni sahihi na ni mwiko kupinga.
Leo hii kiongozi unapoamua kuongea ili uma wa Watanzania wakusikie wakuelewe na hatimaye wakuamini inabidi ujipange sawasawa, kwani watu wa leo wanapenda kuzitafakari kauri za viongozi wao.
Jana sikuamini kama ni Mh ANNA KILANGO huyu ninae mfahamu ambaye alikuwa aliishikia bango issue ya Richmond au ni mwingine? Kwamba Mh KILANGO hajui tume ya kusimamia mchakato wa kukusanya maoni juu ya katiba mpya pamoja na bunge la katiba vitachaguliwaje kama raisi asipopewa hayo mamlaka.
Je Kilango nafasi aliyo nayo aliteuliwa na raisi au alichaguliwa na wananchi? Nadhani hakumsikia prf Shivji, vinginevyo asinge hoji hao wajumbe wanaweza kupatikana vipi kama raisi atapunguziwa mamlaka katika uundwaji wa katiba mpya.
Kweli ANNA KILANGO umeniangusha kuwa hauna dhamira ya kweli ya kumsaidia Mtanzania bali kuisaidia CCM. Na huyu naye mbunge wa cCUF KHALIFA kama sijakosea jina lake, anawataka wabunge waaendelee na mjadala kwa madai kuwa hizo kasoro zitahojiwa na Wananchi na hivyo kuja kurekebishwa kwa kuondoa ama kuongeza wanachokitaka Wananchi.
Jamani wana JF kweli huyu na ubunge wake hajui ni nini ambacho upinzani unataka? Utakuja kubadiri nini wakati tayari umeshapitisha bungeni mswada unaompa mamlaka makubwa raisi ya kuteua kila kitu.
Je kwa fikra zake kutakuwa na uhuru wa kweli katika kuifikia katiba tunayoitaka, nani atakuwa kinyume na raisi wakati wote ni wateule wake?
Leo hii wabunge wa CCM hawako huru japo wamechaguliwa na Wananchi na japo wao wenyewe wanasema wana wawakilisha Wananchi, lakini ukweli ni kuwa kutokana na mfumo tulionao wabunge hawa wanajikuta wanawakilisha serikali ya CCM hata kama nafsini mwao hawapendi.
Watafanyaje ili hali wakiwa kinyume na serikali wanafukuzwa uanachama na ubunge unakoma. Inashangaza sana kwa wabunge wa ccm pamoja na kupata nafasi hii ya kuweza kubadilisha mifumo mibovu kandamizi.
Inasikitsha sana tena sana kwa usaliti huu wa wabunge wa ccm na hawa baadhi wa upinzani.
Leo hii kiongozi unapoamua kuongea ili uma wa Watanzania wakusikie wakuelewe na hatimaye wakuamini inabidi ujipange sawasawa, kwani watu wa leo wanapenda kuzitafakari kauri za viongozi wao.
Jana sikuamini kama ni Mh ANNA KILANGO huyu ninae mfahamu ambaye alikuwa aliishikia bango issue ya Richmond au ni mwingine? Kwamba Mh KILANGO hajui tume ya kusimamia mchakato wa kukusanya maoni juu ya katiba mpya pamoja na bunge la katiba vitachaguliwaje kama raisi asipopewa hayo mamlaka.
Je Kilango nafasi aliyo nayo aliteuliwa na raisi au alichaguliwa na wananchi? Nadhani hakumsikia prf Shivji, vinginevyo asinge hoji hao wajumbe wanaweza kupatikana vipi kama raisi atapunguziwa mamlaka katika uundwaji wa katiba mpya.
Kweli ANNA KILANGO umeniangusha kuwa hauna dhamira ya kweli ya kumsaidia Mtanzania bali kuisaidia CCM. Na huyu naye mbunge wa cCUF KHALIFA kama sijakosea jina lake, anawataka wabunge waaendelee na mjadala kwa madai kuwa hizo kasoro zitahojiwa na Wananchi na hivyo kuja kurekebishwa kwa kuondoa ama kuongeza wanachokitaka Wananchi.
Jamani wana JF kweli huyu na ubunge wake hajui ni nini ambacho upinzani unataka? Utakuja kubadiri nini wakati tayari umeshapitisha bungeni mswada unaompa mamlaka makubwa raisi ya kuteua kila kitu.
Je kwa fikra zake kutakuwa na uhuru wa kweli katika kuifikia katiba tunayoitaka, nani atakuwa kinyume na raisi wakati wote ni wateule wake?
Leo hii wabunge wa CCM hawako huru japo wamechaguliwa na Wananchi na japo wao wenyewe wanasema wana wawakilisha Wananchi, lakini ukweli ni kuwa kutokana na mfumo tulionao wabunge hawa wanajikuta wanawakilisha serikali ya CCM hata kama nafsini mwao hawapendi.
Watafanyaje ili hali wakiwa kinyume na serikali wanafukuzwa uanachama na ubunge unakoma. Inashangaza sana kwa wabunge wa ccm pamoja na kupata nafasi hii ya kuweza kubadilisha mifumo mibovu kandamizi.
Inasikitsha sana tena sana kwa usaliti huu wa wabunge wa ccm na hawa baadhi wa upinzani.