Godfrey Dilunga-Raia Mwema
NOVEMBA 14, mwaka huu, Serikali kupitia kwa Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani, iliwasilisha Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba mpya.
Muswada ambao utakaoongoza wananchi kutoa maoni yao kuhusu Katiba mpya. Tukio hilo lilitanguliwa na kazi nyingine ya uwasilishaji, mjadala na uridhiaji wa Muswada wa Sheria ya Manunuzi ya Umma.
Katika taswira ya Bunge, hasa kwa mujibu wa kanuni zake, Muswada wa Sheria ya Manunuzi na Muswada wa Mabadiliko ya Katiba, yote ni miswada. Mbele ya kanuni za Bunge, ina nguvu sawa.
Majukumu ya mbunge na Bunge ni pamoja na kutunga sheria. Mpiga kura anayekwenda kituo cha upigaji kura kumchagua mbunge, anatambua moja ya kazi ya atakayemchagua ni kutunga sheria, kwa niaba yake.
Ni makosa kwa mbunge au kundi la wabunge kudhani au kujenga dhana kwamba muswada fulani si muhimu kwa kulinganisha na muswada mwingine.
Dhana hii ni potofu kwa sababu tafsiri inayoweza kujitokeza ni kwamba, wabunge wenye mtazamo huo ni kama wanawaaminisha Watanzania kuwa zipo sheria ambazo ni mbovu wameshiriki kuzitunga. Kwamba ipo miswada wameiridhia isiyo na umuhimu kwa Watanzania.
Naam, siku hiyo ya Novemba 14, wabunge wa CHADEMA (si wote, bali waliokuwapo ukumbi wa Bunge siku hiyo) walitoka nje ya ukumbi wa Bunge, mara baada ya Waziri Kivuli wa Katiba na Sheria, Tundu Lissu, kuwasilisha maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani, kuhusu muswada huo unaohusu mchakato wa Katiba mpya.
Wabunge hawa walitoka nje katika kile kinachoelezwa kuwa kutokukubaliana na uamuzi wa Serikali kusoma muswada huo kwa mara ya pili bungeni, kwa sababu haujatoa fursa kwa maoni ya wananchi kuzingatiwa.
Maoni ambayo hata hivyo kwa namna fulani, mbunge pia anapaswa kuyajua kupitia mikutano na wananchi wake.
Ni sahihi kwa wabunge kuhimiza maoni ya wananchi kuzingatiwa katika mchakato wa kutunga sheria yoyote si tu muswada huu wa Katiba mpya. Naunga mkono, wote wanaopigania haki ya wananchi kusikilizwa.
Hata hivyo, kasoro ambayo hata Kambi ya Upinzani haijawahi kuhoji ni kwamba; je, ni wakati gani au ni vigezo gani vinatumika kulifanya Bunge kuamini kuwa wananchi wameshirikishwa au kusikilizwa kiasi cha kutosha?
Ni idadi gani ya wananchi inapaswa itoe maoni yao au kusikilizwa? Ni wakulima, wafanyakazi au wanafunzi wangapi? Nini hasa vigezo vya Bunge, kama taasisi kujiridhisha kwamba sasa wananchi wametoa maoni yao kiasi cha kutosha?
Kwa mfano, wabunge wa CHADEMA wameshiriki kikamilifu katika Muswada wa Sheria ya Manunuzi ya Umma. Sikusikia wakishinikiza kwa nini maoni ya wananchi hayakusikilikizwa kwa kiasi cha kutosha.
Hapa bado izingatiwe kuwa mbele ya kanuni za Bunge, miswada yote ni sawa na inakusudia kulinda maslahi ya wapiga kura.
Binafsi, nimesikia zaidi maoni ya wananchi kuhusu Muswada wa Katiba mpya kuliko ambavyo nimesikia kuhusu Muswada wa Sheria ya Manunuzi ya Umma. Tatizo langu kama ilivyo kwa Watanzania wengine, bado hatuna kipimo iwe kwa kanuni za Bunge au vyovyote, kujiridhisha kuwa idadi ya waliotoa maoni inatosha au la.
Na kwa hiyo, siwezi kusema waliosikilizwa wanatosha ingawa najua baadhi ya hoja za waliotoa maoni yao zimezingatiwa na nyingine kupuuzwa.
Suala la pili la kutafakari ni je, kuna udhaifu wowote uliowahi kuelezwa wazi wazi na Kambi ya Upinzani Bungeni au hata wabunge wa CCM kwamba, mchakato wa kikanuni katika kutunga sheria umekuwa na kasoro? Kwamba ni mchakato usiotoa fursa kwa mbunge kutimiza wajibu wake kikamilifu, tena usiotambua kiasi cha ushiriki wa wananchi?
Kwa hiyo, kuna mawili yanajitokeza. Mosi, miswada yote mbele ya Bunge kikanuni ina nguvu sawa kwa sababu inalenga kumlinda mwananchi. Pili, mchakato wa kutunga sheria kwa mujibu wa kanuni za Bunge bado haujalalamikiwa katika mwelekeo unaojitokeza sasa? Tuendelee na mjadala ifuatavyo.
Ombwe la uongozi wabunge wa CHADEMA
Kuna dalili za ombwe la kiuongozi katika Kambi ya Wabunge wa CHADEMA. Kama si ombwe la uongozi, inawezekana ni ombwe la busara linaloibuka kwa msimu.
Kwanza, wabunge wa CHADEMA ingawa wanaweza kuwa ni wanaharakati, lakini bungeni hawako kwa ajili ya uanaharakati. Wapo kwa sababu wamepigiwa kura na wananchi (ukiondoa vitimaalumu ambao hata hivyo, bungeni wana fursa sawa na wengine).
Kama wabunge, jukumu lao la kwanza ni wananchi, si mkakati binafsi au wa chama kisiasa, ingawa udhaifu huu unajitokeza hata kwa wabunge wa CCM.
Hivyo, walipaswa kushiriki kuandaa mchakato wa muswada wa Katiba mpya kikamilifu baada ya kubaini wananchi wao majimboni hawakushirikishwa vya kutosha.
Kwa mfano, ni matarajio ya wengi mbunge anapokwenda bungeni bila shaka na hasa katika masuala ya miswada anakuwa tayari amesikiliza maoni ya wananchi jimboni anakotoka.
Kwa hiyo, kwa sababu hoja ya msingi ya wabunge wa CHADEMA ni wananchi kutosikilizwa, angalau wao wangeonesha hao wa majimbo yao waliowasilikiza wanasemaje. Wasingekimbia na maoni ya wananchi wao na kutoka nje ya ukumbi.
Wangesema kwanza, wangepigania maoni hayo kwanza yasikike kwa Watanzania wengine wote, katika chombo rasmi (Bunge). Baada ya maoni hayo, kusikika kwa Watanzania wote na kumbukumbu rasmi za Bunge (hansard) kuhifadhi, wangekwenda kusema majukwaani. Ni busara zaidi kutumia chombo rasmi kwanza.
Wangeweza kuwasilisha mapendekezo ya mabadiliko (amendments) katika baadhi ya vifungu ambavyo wananchi wao majimbo wanataka iwe hivyo.
Uwezo huu si tu wanao kwa mujibu wa kanuni za Bunge, lakini pia tumeshuhudia Mbunge wa Ubungo, John Mnyika, akiutumia vizuri katika Muswada wa Sheria ya Manununi ya Umma, siku hiyo hiyo, Novemba 14, 2011, bungeni.
Kwa hiyo, kama ambavyo waliwasilisha maoni yao kupitia hotuba ya Tundu Lissu, ndivyo hivyo hivyo mbunge mmoja mmoja, hasa wa majimbo wangeeleza maoni ya wananchi wao na si kuyahodhi na kukimbia nayo, nje ya ukumbi wa Bunge.
Lakini hawakufanya hivyo, hawakuonesha mwelekeo kama wapinaji mahiri wenye mikakati kamili. Si tu wamehodhi na kukimbia na maoni ya wananchi wao majimboni, lakini wamewanyika fursa Watanzania kujua ili hatimaye wapime, wenzao hao wanasemaje.
Kwa hiyo, Watanzania kupitia Bunge, wameshindwa kujua maoni ya wananchi wa majimbo ya wabunge wa CHADEMA, ambayo kwa mujibu wa malalamiko yao, Bunge limeshindwa kuwapa fursa ya kusema. Hili ni kosa la kiufundi, linalohitaji mkakati mkubwa wa kisiasa kulifunika.
Binafsi ni mpiga kura wa Jimbo la Ubungo, Dar es Salaam. Nimuulize Mnyika; je, kitendo chake cha kukwepa kutumia kanuni za Bunge kupigania maoni yetu ambayo yeye na wenzake CHADEMA wanasema hatukusilizwa, kinatulinda kwa namna gani katika taswira hii ya ‘uovu' wa Serikali?
Wakati gani wangeweza kutoka nje?
Hata hivyo, kwa sababu kususa ni haki ya wabunge, lakini swali la msingi na busara zaidi ni kujiuliza; je, ni wakati gani wa kufanya kitendo hicho?
Je, ni kabla ya kupigana kwa kutumia fursa za kikanuni zilizopo? Au ni kukimbia kwa kupuuza fursa hizo ambazo ni kushiriki mjadala na hata kuwasilisha mapendekezo ya mabadiliko (amendments)?
Kwa kuzingatia matakwa ya busara, naamini wakati muafaka kwa wabunge wa CHADEMA kutoka nje ya ukumbi wa Bunge ulikuwa ni baada ya mapendekezo yao (amendments) kuwasilishwa na kupuuzwa.
Kwa sasa, hawana ushahidi wa kumbukumbu rasmi za Bunge (hansard) kwamba, wamepuuzwa kwa kuzingatia kanuni za Bunge. Kizazi kijacho miaka mingi baadaye kama si hiki, kinaweza kuwashangaa kwa kukimbia fursa za kikanuni, kama kweli wao ni wapigania haki mahiri.
Kitendo cha kutoka nje ya ukumbi wa Bunge kilipaswa kuwa hatua ya mwisho. Yaani rufaa, inayowaunganisha wao na wananchi hasa wa majimbo wanayowawakilisha.
Tunajua maana ya rufaa. Rufaa ni lazima itanguliwe na juhudi nyingine ngazi za chini. Kwa suala la utungaji sheria, ngazi za chini kabla ya rufaa ni mosi; kushiriki mjadala ili kutoa maoni ya wananchi wako; pili, kupendekeza mabadiliko ili kulinda maoni ya wananchi wako; tatu, kama yote yameshindikana nadhani ndipo hatua ya kutoka nje ya ukumbi ingefuata.
Hata hivyo, hatua hii ya kutoka nje ya ukumbi nayo inapaswa kufanyika wakati muafaka ambao kwa suala hili ni pale Spika anapomwita Waziri, kuhitimisha hoja.
Hapa, wabunge wa CHADEMA wangekuwa wameonesha si tu uvumilivu mkubwa bali busara za kiwango cha juu. Yaani watakuwa wamepigana kwa kutumia fursa zote na mwishowe, rufaa ambayo ni majukwaa ya kisiasa.
Wangekuwa wametumia fursa ya kushiriki mjadala, kupendekeza mabadiliko, lakini kubwa zaidi, kusikiliza maoni ya wananchi wengine, kupitia wabunge wenzao nje ya majimbo yao na mwishowe, wangetoka nje.
Leo hii CHADEMA wanapotangaza maandamano nchi nzima watu wenye busara wanatafakari; je, wamejipatia fursa ya kutosha kusikiliza maoni ya wananchi wengine kupitia wabunge wengine na hasa kule walikosimamisha wagombea walioshindwa kura za ubunge?
Tafakari hii inatusogeza hatua nyingine ya kuanza kujiuliza kama kuna ombwe la uongozi katika Kambi ya CHADEMA? Kama lipo, linasababishwa na nini au nani? Je, hakuna uhuru wa maoni ili kurekebishana kwenye vikao vya ndani?
Hata hivyo, nimpongeze Mbunge wa Kasulu Mjini, Moses Machali (NCCR-Mageuzi), ambaye hakuwa katika mkumbo wa ombwe la ghafla la busara.
Alibaki bungeni, ingawa mwenzake, Felix Mkosamali alitoka nje baada ya dakika chache ili kuwafuata wabunge wa CHADEMA.
Machali ametambua kuwa anaweza kupigana katika dakika za mwisho kwa kuwasilisha maoni ya wapiga kura wake. Anaweza kupigana kupitia mjadala, kupitia mapendekezo ya mabadiliko (amendments) na mwishowe, kupigana kwa kuwasilisha hisia za wananchi wake kama maoni yao yatapuuzwa kwa kutoka nje wakati Waziri akihitimisha hoja ya muswada.
Hakika, tunahitaji viongozi vijana wenye akili za kutosha kiasi hiki, watulivu wa fikra, wepesi kutoa uamuzi wa busara. Hongera ‘mseminari' Machali.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika
NOVEMBA 14, mwaka huu, Serikali kupitia kwa Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani, iliwasilisha Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba mpya.
Muswada ambao utakaoongoza wananchi kutoa maoni yao kuhusu Katiba mpya. Tukio hilo lilitanguliwa na kazi nyingine ya uwasilishaji, mjadala na uridhiaji wa Muswada wa Sheria ya Manunuzi ya Umma.
Katika taswira ya Bunge, hasa kwa mujibu wa kanuni zake, Muswada wa Sheria ya Manunuzi na Muswada wa Mabadiliko ya Katiba, yote ni miswada. Mbele ya kanuni za Bunge, ina nguvu sawa.
Majukumu ya mbunge na Bunge ni pamoja na kutunga sheria. Mpiga kura anayekwenda kituo cha upigaji kura kumchagua mbunge, anatambua moja ya kazi ya atakayemchagua ni kutunga sheria, kwa niaba yake.
Ni makosa kwa mbunge au kundi la wabunge kudhani au kujenga dhana kwamba muswada fulani si muhimu kwa kulinganisha na muswada mwingine.
Dhana hii ni potofu kwa sababu tafsiri inayoweza kujitokeza ni kwamba, wabunge wenye mtazamo huo ni kama wanawaaminisha Watanzania kuwa zipo sheria ambazo ni mbovu wameshiriki kuzitunga. Kwamba ipo miswada wameiridhia isiyo na umuhimu kwa Watanzania.
Naam, siku hiyo ya Novemba 14, wabunge wa CHADEMA (si wote, bali waliokuwapo ukumbi wa Bunge siku hiyo) walitoka nje ya ukumbi wa Bunge, mara baada ya Waziri Kivuli wa Katiba na Sheria, Tundu Lissu, kuwasilisha maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani, kuhusu muswada huo unaohusu mchakato wa Katiba mpya.
Wabunge hawa walitoka nje katika kile kinachoelezwa kuwa kutokukubaliana na uamuzi wa Serikali kusoma muswada huo kwa mara ya pili bungeni, kwa sababu haujatoa fursa kwa maoni ya wananchi kuzingatiwa.
Maoni ambayo hata hivyo kwa namna fulani, mbunge pia anapaswa kuyajua kupitia mikutano na wananchi wake.
Ni sahihi kwa wabunge kuhimiza maoni ya wananchi kuzingatiwa katika mchakato wa kutunga sheria yoyote si tu muswada huu wa Katiba mpya. Naunga mkono, wote wanaopigania haki ya wananchi kusikilizwa.
Hata hivyo, kasoro ambayo hata Kambi ya Upinzani haijawahi kuhoji ni kwamba; je, ni wakati gani au ni vigezo gani vinatumika kulifanya Bunge kuamini kuwa wananchi wameshirikishwa au kusikilizwa kiasi cha kutosha?
Ni idadi gani ya wananchi inapaswa itoe maoni yao au kusikilizwa? Ni wakulima, wafanyakazi au wanafunzi wangapi? Nini hasa vigezo vya Bunge, kama taasisi kujiridhisha kwamba sasa wananchi wametoa maoni yao kiasi cha kutosha?
Kwa mfano, wabunge wa CHADEMA wameshiriki kikamilifu katika Muswada wa Sheria ya Manunuzi ya Umma. Sikusikia wakishinikiza kwa nini maoni ya wananchi hayakusikilikizwa kwa kiasi cha kutosha.
Hapa bado izingatiwe kuwa mbele ya kanuni za Bunge, miswada yote ni sawa na inakusudia kulinda maslahi ya wapiga kura.
Binafsi, nimesikia zaidi maoni ya wananchi kuhusu Muswada wa Katiba mpya kuliko ambavyo nimesikia kuhusu Muswada wa Sheria ya Manunuzi ya Umma. Tatizo langu kama ilivyo kwa Watanzania wengine, bado hatuna kipimo iwe kwa kanuni za Bunge au vyovyote, kujiridhisha kuwa idadi ya waliotoa maoni inatosha au la.
Na kwa hiyo, siwezi kusema waliosikilizwa wanatosha ingawa najua baadhi ya hoja za waliotoa maoni yao zimezingatiwa na nyingine kupuuzwa.
Suala la pili la kutafakari ni je, kuna udhaifu wowote uliowahi kuelezwa wazi wazi na Kambi ya Upinzani Bungeni au hata wabunge wa CCM kwamba, mchakato wa kikanuni katika kutunga sheria umekuwa na kasoro? Kwamba ni mchakato usiotoa fursa kwa mbunge kutimiza wajibu wake kikamilifu, tena usiotambua kiasi cha ushiriki wa wananchi?
Kwa hiyo, kuna mawili yanajitokeza. Mosi, miswada yote mbele ya Bunge kikanuni ina nguvu sawa kwa sababu inalenga kumlinda mwananchi. Pili, mchakato wa kutunga sheria kwa mujibu wa kanuni za Bunge bado haujalalamikiwa katika mwelekeo unaojitokeza sasa? Tuendelee na mjadala ifuatavyo.
Ombwe la uongozi wabunge wa CHADEMA
Kuna dalili za ombwe la kiuongozi katika Kambi ya Wabunge wa CHADEMA. Kama si ombwe la uongozi, inawezekana ni ombwe la busara linaloibuka kwa msimu.
Kwanza, wabunge wa CHADEMA ingawa wanaweza kuwa ni wanaharakati, lakini bungeni hawako kwa ajili ya uanaharakati. Wapo kwa sababu wamepigiwa kura na wananchi (ukiondoa vitimaalumu ambao hata hivyo, bungeni wana fursa sawa na wengine).
Kama wabunge, jukumu lao la kwanza ni wananchi, si mkakati binafsi au wa chama kisiasa, ingawa udhaifu huu unajitokeza hata kwa wabunge wa CCM.
Hivyo, walipaswa kushiriki kuandaa mchakato wa muswada wa Katiba mpya kikamilifu baada ya kubaini wananchi wao majimboni hawakushirikishwa vya kutosha.
Kwa mfano, ni matarajio ya wengi mbunge anapokwenda bungeni bila shaka na hasa katika masuala ya miswada anakuwa tayari amesikiliza maoni ya wananchi jimboni anakotoka.
Kwa hiyo, kwa sababu hoja ya msingi ya wabunge wa CHADEMA ni wananchi kutosikilizwa, angalau wao wangeonesha hao wa majimbo yao waliowasilikiza wanasemaje. Wasingekimbia na maoni ya wananchi wao na kutoka nje ya ukumbi.
Wangesema kwanza, wangepigania maoni hayo kwanza yasikike kwa Watanzania wengine wote, katika chombo rasmi (Bunge). Baada ya maoni hayo, kusikika kwa Watanzania wote na kumbukumbu rasmi za Bunge (hansard) kuhifadhi, wangekwenda kusema majukwaani. Ni busara zaidi kutumia chombo rasmi kwanza.
Wangeweza kuwasilisha mapendekezo ya mabadiliko (amendments) katika baadhi ya vifungu ambavyo wananchi wao majimbo wanataka iwe hivyo.
Uwezo huu si tu wanao kwa mujibu wa kanuni za Bunge, lakini pia tumeshuhudia Mbunge wa Ubungo, John Mnyika, akiutumia vizuri katika Muswada wa Sheria ya Manununi ya Umma, siku hiyo hiyo, Novemba 14, 2011, bungeni.
Kwa hiyo, kama ambavyo waliwasilisha maoni yao kupitia hotuba ya Tundu Lissu, ndivyo hivyo hivyo mbunge mmoja mmoja, hasa wa majimbo wangeeleza maoni ya wananchi wao na si kuyahodhi na kukimbia nayo, nje ya ukumbi wa Bunge.
Lakini hawakufanya hivyo, hawakuonesha mwelekeo kama wapinaji mahiri wenye mikakati kamili. Si tu wamehodhi na kukimbia na maoni ya wananchi wao majimboni, lakini wamewanyika fursa Watanzania kujua ili hatimaye wapime, wenzao hao wanasemaje.
Kwa hiyo, Watanzania kupitia Bunge, wameshindwa kujua maoni ya wananchi wa majimbo ya wabunge wa CHADEMA, ambayo kwa mujibu wa malalamiko yao, Bunge limeshindwa kuwapa fursa ya kusema. Hili ni kosa la kiufundi, linalohitaji mkakati mkubwa wa kisiasa kulifunika.
Binafsi ni mpiga kura wa Jimbo la Ubungo, Dar es Salaam. Nimuulize Mnyika; je, kitendo chake cha kukwepa kutumia kanuni za Bunge kupigania maoni yetu ambayo yeye na wenzake CHADEMA wanasema hatukusilizwa, kinatulinda kwa namna gani katika taswira hii ya ‘uovu' wa Serikali?
Wakati gani wangeweza kutoka nje?
Hata hivyo, kwa sababu kususa ni haki ya wabunge, lakini swali la msingi na busara zaidi ni kujiuliza; je, ni wakati gani wa kufanya kitendo hicho?
Je, ni kabla ya kupigana kwa kutumia fursa za kikanuni zilizopo? Au ni kukimbia kwa kupuuza fursa hizo ambazo ni kushiriki mjadala na hata kuwasilisha mapendekezo ya mabadiliko (amendments)?
Kwa kuzingatia matakwa ya busara, naamini wakati muafaka kwa wabunge wa CHADEMA kutoka nje ya ukumbi wa Bunge ulikuwa ni baada ya mapendekezo yao (amendments) kuwasilishwa na kupuuzwa.
Kwa sasa, hawana ushahidi wa kumbukumbu rasmi za Bunge (hansard) kwamba, wamepuuzwa kwa kuzingatia kanuni za Bunge. Kizazi kijacho miaka mingi baadaye kama si hiki, kinaweza kuwashangaa kwa kukimbia fursa za kikanuni, kama kweli wao ni wapigania haki mahiri.
Kitendo cha kutoka nje ya ukumbi wa Bunge kilipaswa kuwa hatua ya mwisho. Yaani rufaa, inayowaunganisha wao na wananchi hasa wa majimbo wanayowawakilisha.
Tunajua maana ya rufaa. Rufaa ni lazima itanguliwe na juhudi nyingine ngazi za chini. Kwa suala la utungaji sheria, ngazi za chini kabla ya rufaa ni mosi; kushiriki mjadala ili kutoa maoni ya wananchi wako; pili, kupendekeza mabadiliko ili kulinda maoni ya wananchi wako; tatu, kama yote yameshindikana nadhani ndipo hatua ya kutoka nje ya ukumbi ingefuata.
Hata hivyo, hatua hii ya kutoka nje ya ukumbi nayo inapaswa kufanyika wakati muafaka ambao kwa suala hili ni pale Spika anapomwita Waziri, kuhitimisha hoja.
Hapa, wabunge wa CHADEMA wangekuwa wameonesha si tu uvumilivu mkubwa bali busara za kiwango cha juu. Yaani watakuwa wamepigana kwa kutumia fursa zote na mwishowe, rufaa ambayo ni majukwaa ya kisiasa.
Wangekuwa wametumia fursa ya kushiriki mjadala, kupendekeza mabadiliko, lakini kubwa zaidi, kusikiliza maoni ya wananchi wengine, kupitia wabunge wenzao nje ya majimbo yao na mwishowe, wangetoka nje.
Leo hii CHADEMA wanapotangaza maandamano nchi nzima watu wenye busara wanatafakari; je, wamejipatia fursa ya kutosha kusikiliza maoni ya wananchi wengine kupitia wabunge wengine na hasa kule walikosimamisha wagombea walioshindwa kura za ubunge?
Tafakari hii inatusogeza hatua nyingine ya kuanza kujiuliza kama kuna ombwe la uongozi katika Kambi ya CHADEMA? Kama lipo, linasababishwa na nini au nani? Je, hakuna uhuru wa maoni ili kurekebishana kwenye vikao vya ndani?
Hata hivyo, nimpongeze Mbunge wa Kasulu Mjini, Moses Machali (NCCR-Mageuzi), ambaye hakuwa katika mkumbo wa ombwe la ghafla la busara.
Alibaki bungeni, ingawa mwenzake, Felix Mkosamali alitoka nje baada ya dakika chache ili kuwafuata wabunge wa CHADEMA.
Machali ametambua kuwa anaweza kupigana katika dakika za mwisho kwa kuwasilisha maoni ya wapiga kura wake. Anaweza kupigana kupitia mjadala, kupitia mapendekezo ya mabadiliko (amendments) na mwishowe, kupigana kwa kuwasilisha hisia za wananchi wake kama maoni yao yatapuuzwa kwa kutoka nje wakati Waziri akihitimisha hoja ya muswada.
Hakika, tunahitaji viongozi vijana wenye akili za kutosha kiasi hiki, watulivu wa fikra, wepesi kutoa uamuzi wa busara. Hongera ‘mseminari' Machali.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika