Wabunge chadema tafuteni ufadhili mtimize ahadi zenu..!

Tanzaniaist

Senior Member
Nov 29, 2011
161
156
Habari zenu wana JF..,leo hii kwenye mada yangu napenda kugusia wabunge wa CHADEMA ambao wamekuwa Nguzo mhimili wa Chama pamoja kama sehemu ya serikali (Bunge)
Niwapongeze sana kwa kuweza kuhimili mikiki na mizengwe ya CCM tangia uchaguzi paka sasa hivi kwani kumekuwa na suala la hawa wabunge kufungiliwa kesi na kubambikiziwa makosa yasiyokuwa na msingi baada ya jeshi la polisi kushindwa kutimiza wajibu wao wa kusimamia haki na kushurutushwa na Siasa

Katika kampeni za Uchaguzi, wabunge wengi wa Chadema waliahidi mambo makubwa ili waweze kuchaguliwa na vile vile waweze kuzidi hoja wapinzani wao..,na kuna baadhi waliamua kufunguka kwa kuwaambia wananchi ukweli kama John Mnyika na Tundu Lissu kuhusu majukumu na wajibu wa mbunge..!

Na hili suala limekuwa tatizo sana kwa wananchi, wengi hawajui kazi ya Mbunge ni nini..? wamekuwa wakitoa tu malalamiko bila sababu za msingi hasa hapa Jamvini..

Mimi ninaamini Kazi ya Mbunge, Sio KUJENGA BARABARA, KUCHIMBA VISIMA, KUNUNUA MADAWATI, KUJENGA MADARASA, KULIPIA ADA WANAFUNZI, KUNUNUA DAWA NA VITANDA MAHOSPITALINI, KUCHIMBA MITARO, KUTOA MIKOPO, na N.K

Bali mimi naamini Kazi ya Mbunge ni kuisimamia serikali kutimiza wajibu wake kwa wananchi, kwa kuwa serikali INAKUSANYA KODI, MBUNGE KWA MSHAHARA WAKE WA MILIONI MBILI ukizingatiwa anakatwa kodi na mkopo wa gari.,na posho za bungeni hata kama wakipewa hizo 250,000 tshs Mbunge HAWEZI kujenga barabara,..au kufanya mambo makubwa hapo juu niliyoyataja ukizingatiwa wengi wana familia au wengine ndio wanaanza maisha au hata wengine walikuwa Mafukara..,TUWALAUMU wabunge ili wafanye kazi lakini TUSIWAHUKUMU..,
Serikali ndio imekuwa chanzo cha matatizo kwani inakusanya kodi na kupokea misaada toka nnje lakini pesa zinaishia kuliwa na wachache ama kutokuwa na matumizi mazuri ya pesa..,na kushindwa kujenga na kuboresha huduma muhimu za kijamii...!

Na ninawaonea sana HURUMA wabunge wa CHADEMA, wanapata sana wakati mgumu kutimiza ahadi zao kwakuwa Halmashauri nyingi wanazotoka madiwani wengi ni wa CCM, na hata watendaji wa serikali wengi wanafuata matakwa ya CCM, na saa nyingine hata shughuli zao za kibunge kuvurugwa tu kwa makusudi na jeshi la polisi ama mizengwe ya watendaji ili mbunge aonekane tu hafai mfano,.Godbless Lema, huyu mheshimiwa tangia awe mbunge kila siku ni kufunguliwa kesi,kudhalilishwa na polisi bila sababu za msingi.,na kujikuta muda mwingi akipoteza muda na kushindwa kusimamia ahadi zake pamoja na shughuli za kibunge! na ningependa kuhoji kama Godbless Lema ni mkorofi kama watu wanavyosema mbona kabla hajawa mbunge hakuwa na kesi mahakamani...!

Na ikumbukwe kwamba hawa wabunge wa CHADEMA inakuwa ngumu kutekeleza ahadi zao kwakuwa hata serikali inaongozwa na CCM kwanzia Raisi na Mawaziri..,na ili matatizo yao yasikilizwe kwa urahisi itabidi wawe mawakala wa CCM kama LYATONGA MREMA wa TLP au JOHN CHEYO wa UDP,la sivyo itakuwa ngumu kutimiza ahadi zao na hata mambo kuwa magumu zaidi jimboni kwa kubaniwa huduma muhimu za kijamii..!

Sasa imefika wakati.,,Wabunge wa CHADEMA kutumia UMMA kuchangia shughuli zao za Kimaendeleo mfano.Alivyofanya Hezekiah Wenje alivyoandaa harambee kwa ajili ya madawati..,au Hata wabunge hawa wa CHADEMA kutumia wafadhili kutoka nje kufadihili miradi yao ya kimaendeleo jimboni kwani kuitegemea tu serikali itakuwa ni sawa na kujivika kitanzi..,Kwani Serikali chini ya CCM kila siku wanatafuta njia ya kurudisha hayo majimbo mliyoyapata kwa CCM..,nimpongeze sana MH.PHILEMONE NDESAMBURO kwa kupigana kiume hadi sasa hivi lakini sidhani kama asingekuwa tajiri asingeweza kuwa mbunge hadi sasa kwani amekuwa akitumia uwezo wake kifedha kuisadia serikali kuboresha huduma za kijamii lkn kama asingekuwa na uwezo huo mambo yangekuwa tofauti na hata kutimiza ahadi zake..! sasa kwa wabunge wengine ambao sio wafanya biashara hali itakuwa vp?



Napenda kuwasilisha..!
 
Wananchi tunaelewa zengwe wanalopigwa wabunge wetu wa CDM, So, haturudi nyuma. Dunia ya leo kila kitu tunakielewa. Magamba watatulia tu hadi kitaeleweka.
 
Wewe nadhani unayako miaka amsini ya uhuni magamba wameaidi mangapi.Kwanini wao wasitimize walio aidi mwenyekiti Wa Ccm ametoa ahadi zaidi ya sabini na Saba Leo ziko wapi serekali imekuwa ya mafisadi ivi wewe aikuumi wadogo zako wanatembea peku kwenda shule mi nadhani wewe kwenu mboga Saba ugali kitenesi.wabunge Wa Cdm wako makini tuwape muda tu mambo yatanyooka baba ukiwa na familia utasubiri usaidiwe na mwanaume kulishiwa familia aiwezekani kaa chini utafakari na uo ujumbe wako uwape wabunge magamba.
 
Nitaji wa ccm aliyetimiza ahadi zake ndo uje na haya ya kwako...2najua wabunge wa chadema wanabaniwa 2waone wabaya ila hai2ingii akilini.
 
Ni mara mia uwaambie wale pesa sana, maana 2015 wabunge wote wa chama mfu(Chadema hawana chao).
.
"WASIOSOMA NI CHAKULA CHA WASOMI".
 
Wafadhili halali wa Chadema ni rasilimali za taifa hili zinazotafunwa na mchwa wa mitaa ya Shaaban Robert, Sokoine Drive, Ohio, Magogoni, Samora, Mirambo na Garden. Hicho ndicho tunachokipigania Chadema.
 
Hao wabunge ccm wangekuwa wanatimiza ajadi hii nchi ingekuwa mbali! Lakini pia nataka nikusahihishe kuhusu Gobless pamoja na Kesi ambazo zimekuwa zikimkabili: Amekuwa na jitihada binafsi za kuleta maendeleo kwa wana wa Arusha:
1. Anasomesha watoto zaidi ya 420 shule za sekondary ambao wanalipiwa ada, bima ya afya na kupewa vifaa vya shule kwa kupitia shirika aliloliazisha baada ya kuwa mbunge (Arusha Development Foundation-ArDF)
2. Kupitia uwakilishi wake bungeni amesaidia kurejesha kiwanda cha general tyre ambacho kitaanza kufanya kazi na kuajiri wananchi wa arusha muda wowote
3. Aliahidi kujenga hospitali ya mama na mtoto, tayari ameshapata kiwanja chenye thamani ya Tsh 400M kwa ajiri ya ujenzi wa hospitali hiyo
4. Amewatetea wakazi wa kaloleni ambao walikuwa wauzwe kwa mwekezaji mwarabu ili eneo hilo la makazi lililopo mjini lijengwe shoping malls na akapendekeza wawekezaji hao wapewe eneo lingine nje ya mji ili kutanua mji wa arusha na kupunguza msongamano ambao ungeletwa na uanzishwaji wa shoping malls katikati ya mji, kitendo hiko kilipokelewa vizuri sana na wananchi wa arusha
5. Jambo lililokubwa na la heshima kubwa kwetu ni UJASIRI ambao ametujengea watu wa arusha wa kutambua na kuzitetea haki zetu na haki za wengine kwa ajili ya kutetea thamani ya utu wa mwanadamu! Kwetu sisi wananchi wa arusha hata asingefanya mengine yote akafanya hili tu moja, ataendelea kuwa mbunge wa arusha mjini, maana sisi tunaamini HAKI na UTU wa MWANADAMU ndo msingi wa maendeleo ya nchi yoyote.
6. Amekuwa nguzo muhimu kuifuta CCM kwenye mkoa wa arusha, CCM ndo adui wa nne wa maendeleo ya watanzania, ukitoa wale maadui aliowataja mwalimu Nyerere, UJINGA, MARADHI, UMASIKINI adui mwingine ni CCM, huyo arusha tumeshaondokana nae!
7. Amekifanya CHADEMA kuwa chama tawala Arusha
8. Ni mwanzilishi wa Movement for Change-M4C.

Haya GODBLESS LEMA ameyafanya, ndani ya mwaka mmoja kama mbunge plus kesi zote alizokuwa nazo!
 
Ni mara mia uwaambie wale pesa sana, maana 2015 wabunge wote wa chama mfu(Chadema hawana chao).
.
"WASIOSOMA NI CHAKULA CHA WASOMI".

Ama kweli Wahenga hawakukosea, waliposema "Mfa Maji Haachi Kutapa" !!!! Baada ya huduma za afya kuimarishwa duniani, watoto wadogo hawafi kwa ugonjwa wa suarua, ila watu wazima wanakufa kwa UKIMWI. Tafakari, Chukua hatua.
 
Watanzania tunaelewa vizingiti wanayopata wabunge wa chadema....tuvumilie 2015 tuwe na halmashauri nyingi ili wabunge wetu waweze kutekeleza majukumu yao bila kupingwa pasipo sababu na madiwani wa ccm,
 
Mimi nachowaomba wabunge wa cdm waeleze wananchi majimboni mwao pesa za miradi ya maendeleo zilizotengwa na serekali kuu ili wao watoe hukumu endapo miradi husika haitatekelezwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom