Wabunge CHADEMA, Posho mliyoikataa, mnaifanyia nini?

Jumakidogo

R I P
Jul 16, 2009
1,851
417
Kwa bahati nimeamua kuwa siyo mwanachama wa chama chochote cha siasa bali ni shabiki wa siasa na baadhi ya wanasiasa. Mfano halisi wanasiasa ninao wakubali bila kujali itikadi zao ni Mbowe, Slaa, Mnyika, Lissu, Magufuli, Lowassa nk. Napata fursa ya kuwa makini na kauli za wanasiasa wa nchi hii bila kujali chama atokacho. Wabunge wa CDM Wamekuwa na msimamo wa kutopokea posho zao katika vikao vya bunge. Msimamo ambao wananchi tulio wengi tunauunga mkono mia kwa mia. Lakini utaratibu wa malipo ya posho hizo ni halali kwa mujibu wa kanuni za bunge. Na bahati mbaya hawapewi mkononi hivyo huingizwa moja kwa moja kwenye akaunti zao. Kwa maana ya kwamba watake watapata, wasitake watapata. Ule msimamo wa dhati upo kweli? Manake sijasikia tena wakija na mpango hasi kuhusu posho hizo kuwa, kwa sababu tulizikataa lakini mnatulazimisha. Tunaziingiza katika mradi fulani wa wananchi. Vinginevyo tunarudi kulekule kuwa. Kauli zitokazo midomoni mwa wanasiasa ni tamu masikioni mwa wananchi, lakini kuna dhamira tofauti katika mioyo yao.
 
kama wanalazimishwa kupokea unataka wafanyeje? mi nadhani kitendo chao cha kupinga hizo posho waziwazi kinatosha kuonyesha nia yao ya dhati ktk kupunguza matumizi serkali yasiyo na tija
 
kama wanalazimishwa kupokea unataka wafanyeje? mi nadhani kitendo chao cha kupinga hizo posho waziwazi kinatosha kuonyesha nia yao ya dhati ktk kupunguza matumizi serkali yasiyo na tija

Mkuu, wewe ukilazimishwa kuuwa utauwa?
 
Tatizo hamna kiongozi yeyote aliyetoa maelezo yanayoeleweka kuhusu mgomo wa hizo posho.Wananchi tunashindwa kuelewa msimamo wao ni upi katika posho hizo,na wengine ni lazima tuamini kuwa wanazipokea kwa kuwa hamna msimamo wowote uliotolewa!kwa maana hiyo inabaki kuwa ni sanaa tu ya wanasiasa kuwapumbaza wananchi.Kama kweli mna huruma na mtanzania anayeteseka na maisha magumu onyesheni kweli mna nia ya dhati katika hilo!
 
Why swali hili ni kwa wabunge Wa CHADEMA tu and why not to Wabunge wengine????
 
kama wanalazimishwa kupokea unataka wafanyeje? mi nadhani kitendo chao cha kupinga hizo posho waziwazi kinatosha kuonyesha nia yao ya dhati ktk kupunguza matumizi serkali yasiyo na tija

Kwa hiyo ukilazimishwa kula haramu unakula?
 
Wote wale ni wanafiki walikuwa wanatafuta cheap popularity.
 
CHADEMA.......!
sometimes huwa siwaelewi,
Bado nawamaind kukubali kufikia makubaliano na JK halafu wanakuja kutulilia kwamba Rais aliwachuuza..!
Hili la posho usishangae wakija na kauli kuwa hawakuwa na namna ya kukataa manake walilazimishwa kuzipokea...!
 
Mkuu, wewe ukilazimishwa kuuwa utauwa?

Kama utatumia nguvu kunishikisha trigger ya bunduki na kisha ukatumia nguvu kunivutisha hiyo trigger na risasi ikafyatuka mimi nitakuwa na kosa gani? we unaambiwa hizo posho huwa zinatangulia wiki moja kabla hata ya kuanza kikao na zinaingia kwenye akaunti moja kwa moja unategemea watazizuiaje?
 
Wote wale ni wanafiki walikuwa wanatafuta cheap popularity.

Huyu naye ni mnafiki? He is refusing to accept this allowance in order to gain cheap popularity for 2015!?

~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*

Makamba ashtushwa
Mbunge wa Bumbuli, January Makamba, alieleza kushangazwa na ongezeko hilo la ghafla akisema kamwe wabunge wasifikiri kuwa wanaweza kumaliza matatizo yao au ya wapigakura wao kwa fedha ya posho.
Alisema kitendo cha wabunge kuongezewa posho za vikao kwa asilimia 185.7, kinaleta jazba kwa wananchi ambao wanahangaika kila kukicha kwa ugumu wa maisha.

"Kwenye jamii lazima kuwe na usawa, kama watu tupo kwenye hali mbaya (ugumu wa maisha) lazima wote tuenende sawa. Wabunge kuongezewa posho kwa asilimia 185 siyo sawa kabisa, tunajiweka mbali na wananchi na wanatuona tunafaidika sana wakati wao wanateseka kwa ugumu wa maisha," alisema Makamba.

Alisema kuwa, kutokana na msimamo wake huo, Juni mwaka huu alikataa posho iliyotolewa na Wizara ya Nishati na Madini baada ya kuhudhuria semina iliyoandaliwa na wizara hiyo.

"Tulikaa kwenye semina kwa saa mbili, tunamaliza naletewa karatasi nisaini posho ya Sh280,000. Nilikataa. Nilikataa kwa sababu nilitambua kuwa ile ni kazi yangu kama mbunge, sasa unanilipa hela ya kazi gani?" alihoji Makamba.

Habari hii imeandaliwa na Fredy Azzah, Frederick Katulanda, Mwanza, Patricia Kimelemeta, Fidelis Butahe na Ellen Manyangu

SOURCE: Mwananchi.


 
Kama utatumia nguvu kunishikisha trigger ya bunduki na kisha ukatumia nguvu kunivutisha hiyo trigger na risasi ikafyatuka mimi nitakuwa na kosa gani? we unaambiwa hizo posho huwa zinatangulia wiki moja kabla hata ya kuanza kikao na zinaingia kwenye akaunti moja kwa moja unategemea watazizuiaje?

Sasa mbona wakizikuta wanakaa kimya? Hawasemi wanazitumia vipi kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wao.
 
Back
Top Bottom