nderingosha
JF-Expert Member
- Mar 20, 2011
- 4,281
- 3,243
Kwa kuwa imeshadhihirika kwamba pamoja na kelele za chadema za kutaka posho zifutwe kugonga mwamba na matokeo yake ni posho kuwa zimezidi kuongezwa.......hii inadhihirisha kuwa wabunge wa ccm na spika wao wameamua kujali matumbo yao...huku wakijua kuwa come 2015 wengi wao hawatarudi bungeni hivyo bora wawavune watanzania kwa kipindi hiki cha miaka 4 iliyobaki kuelekea mwisho wao 2015.Inasikitisha na inaonyesha mkakati wa chadema wa kususa posho hauna tija tna hivyo.....ushauri wa tija kwa chadema ni:
- Badilisheni mkakati -chukueni posho zenu zote na mkae chini mzipangie mkakati wa kuzitumia kuwasaidia wananchi vijijini. Hili linawezekana kwani posho ya laki 2 mkijichanga wote kwa vikao vya bunge vinavyokuja zinaweza kuleta tija sana vijijini.......haswa kule kwenye vijiji ambavyo bado chadema haijulikani vizuri mfano vijiji vya mikoa ya mtwara,lindi, ruvuma,dodoma....taboara n.k....(.nyie mnajua wapi mna wafuasi wachache).Kwa kufanya hivyo mtaweza kujitangaza kisera na pia kupata wafuasi tosha kuwa support come 2015.Mnaweza kuchagua sekta za kusaidia mfano:afya(kununua madawa au kujenga zahanati), maji(kujenga visima),elimu(madawati au baiskeli za waalimu),na pia mnaweza kujenga ofisi zenu huko.Haya mambo ni huduma za msingi kwa raia na vijiji vingi tz bado wana shida tele baada ya hii miaka 50......haya mambo mnaweza kuyafanya kimkakati.....tena kwa mda mfupi tu wa miaka 4 kuelekea 2015 mtakuwa mnawapiga bao kubwa ccm...maana wao wamekaa dar wakijaza matumbo yao....
- Kama mtaamua kubadili mkakati wa posho na kuzichukua.....hamuhitaji wala kuweka foot prints kwa misaada yenu(maana ccm hawatakubali)......nyie kusanyeni hizo posho....fungueni mfuko(account) maalum benki....(mnaweza kuita chedema development fund).....alafu kila baada ya muda mnaamua kwenda mkoa fulani (e.g mtwara)huku mkitumia mikutano(operation sangara version).......mnaenda na misaada hii intact....msiende mikono mitupu....watu watawasikiliza na hakika mtavuna wafuasi wa kweli.........kwa kufanya hivi mtaonekana kwa kweli mnajali maisha ya watu vijijini kuliko kuendelea kugomea posho ambazo zitandelea kuchukuliwa na waganga matumbo wa ccm....these are important decisions people.........haswa viongozi wa chadema........just change the strategy...take the money and put it to people in the villages.....