GHOST RYDER
JF-Expert Member
- Jun 10, 2011
- 1,025
- 475
Wabunge acheni Ushamba wa Madiwani Momose Cheyo
Asubuhi leo katika mjadala wa Kipindi cha Tuongee Asubuhi Star TV nimefuatilia kwa ukaribu na tafakuri kubwa mjadala uliokuwa ukiendeshwa na Chilala kuhusu Michango ya Wabunge huko Mjengoni na Studioni alikuwepo Mbunge wa Bariadi Mashariki Mh. John Momose Cheyo na Mwenyekiti wa Chama Kipya cha CHAUMA kijana Paschal Kahangala (nitapenda tumjadili kijana huyu na Chama chake katika Thread tofauti ntakayoipost soon pia)
Nikirejea kwa Mzee Cheyo ambaye alikuwa kitoa mtazamo wake kuhusu mijadala na changamoto zilizopo Bungeni, Cheyo amesema inawezekana kabisa kundi kubwa la hoja na mivutano ya sasa inalenga zaidi katika wabunge kusaka umaarufu na kuwa kuna mchanagnyiko wa akili za ujana, umachachari, uelewa na bangi wote katika kundi moja.
Nilipolisikia hilo nikavutika kumsikiliza mzee wa Mapesa licha ya Star kukamata kwa tabu kidogo huku Bunju, Mapesa anadai kuna matumizi mabaya ya kanuni namba 68 inayotoa nafasi kwa mbunge kuomba taarifa na muongozo wakati anapohisi mambo haypo sawa.
Cheyo anadai kuwa katika sintofahamu hili wabunge wamekuwa kakijikuta katika sekeseke la kukwamishana kujadili Hoja za msingi tena za maana kwa masilahi ya Taifa kwa kuitumia kanuni hii vibaya huku upinzani ukiathiriwa zaidi na Chama Tawala.
Anadai ujanja na ushamba kama huo wamekuwa wakitumia madiwani katika vikao vyao vya halmashauri kuonyeshana ujuzi wa kutumia kanuni na ujuaji wa kishamba ambao hauna tija kwa umma.
Katika kupigilia msumari katika jeneza Cheyo kasisitiza kuwa ni vema wabunge wakajenga utaratibu wa kutumia vikao vya kamati ambapo ni nafasi nzuri kutoa hoja kwa nafasi bila kipimo na kuwa na uezo mkubwa wa kushawishi mabadiliko ya Hoja au mswaada wowote kwa masilahi ya Taifa kuliko kuendelea kutumia jukwaa la kuuza kinyago katika chupa na kusaka ujiko ambao hauna masilahi kwa Taifa.
Akibariki utetezi na Hoja yake Cheyo kasema hasiti kumpongeza Mwenyekiti wa Kamati ya Uchukuzi ambae kupitia vikao vya kamati walifanikiwa kufanya mageuzi makubwa katika kamati hiyo na kupata nyongeza ya fungu la kuhudumia mipango katika bajeti ya Wizara hiyo na kuwa huu ni uzalendo na Hoja ambazo ni kwa masilahi ya Umma.
Akiuma na kupuliza katika nyakati tofauti hakusita kutupa kombora kwa jirani zake wa upinzani akikejeli kwa mzaha kidogo kuwa hataki ifike pahala kwa wazee kama yeye mwenye upara kulazimika kuingia bungeni wakiwa wamevaa helmet kuhofia akili za wabunge ambao wanataka milango ifungwe ili wapigane.
Baada ya mzaha huo karejea tena kukazia kuwa hapa hoja si kupigana ukitaka kupigana nenda uwanjani katika mieleka ambapo pia yupo refarii mwenye kudhibiti mambo huko uwanjani, lakini kubwa hapa ni wabunge vijana kutumia maarifa, mbinu na ujuzi wao wa kitaaluma kujenga hoja katika kamati kuhakikisha mabadiliko yanapatikana kwa mtanzania mnyonge na sio ushabiki wa kutunishiana misuli kwa kukiuka kanuni za Uendeshaji wa shughuli za Bunge na kuishia kuomba miongozo na Taarifa zisizokuwa na masilahi kwa watanzania.
My TAKE:
Asubuhi leo katika mjadala wa Kipindi cha Tuongee Asubuhi Star TV nimefuatilia kwa ukaribu na tafakuri kubwa mjadala uliokuwa ukiendeshwa na Chilala kuhusu Michango ya Wabunge huko Mjengoni na Studioni alikuwepo Mbunge wa Bariadi Mashariki Mh. John Momose Cheyo na Mwenyekiti wa Chama Kipya cha CHAUMA kijana Paschal Kahangala (nitapenda tumjadili kijana huyu na Chama chake katika Thread tofauti ntakayoipost soon pia)
Nikirejea kwa Mzee Cheyo ambaye alikuwa kitoa mtazamo wake kuhusu mijadala na changamoto zilizopo Bungeni, Cheyo amesema inawezekana kabisa kundi kubwa la hoja na mivutano ya sasa inalenga zaidi katika wabunge kusaka umaarufu na kuwa kuna mchanagnyiko wa akili za ujana, umachachari, uelewa na bangi wote katika kundi moja.
Nilipolisikia hilo nikavutika kumsikiliza mzee wa Mapesa licha ya Star kukamata kwa tabu kidogo huku Bunju, Mapesa anadai kuna matumizi mabaya ya kanuni namba 68 inayotoa nafasi kwa mbunge kuomba taarifa na muongozo wakati anapohisi mambo haypo sawa.
Cheyo anadai kuwa katika sintofahamu hili wabunge wamekuwa kakijikuta katika sekeseke la kukwamishana kujadili Hoja za msingi tena za maana kwa masilahi ya Taifa kwa kuitumia kanuni hii vibaya huku upinzani ukiathiriwa zaidi na Chama Tawala.
Anadai ujanja na ushamba kama huo wamekuwa wakitumia madiwani katika vikao vyao vya halmashauri kuonyeshana ujuzi wa kutumia kanuni na ujuaji wa kishamba ambao hauna tija kwa umma.
Katika kupigilia msumari katika jeneza Cheyo kasisitiza kuwa ni vema wabunge wakajenga utaratibu wa kutumia vikao vya kamati ambapo ni nafasi nzuri kutoa hoja kwa nafasi bila kipimo na kuwa na uezo mkubwa wa kushawishi mabadiliko ya Hoja au mswaada wowote kwa masilahi ya Taifa kuliko kuendelea kutumia jukwaa la kuuza kinyago katika chupa na kusaka ujiko ambao hauna masilahi kwa Taifa.
Akibariki utetezi na Hoja yake Cheyo kasema hasiti kumpongeza Mwenyekiti wa Kamati ya Uchukuzi ambae kupitia vikao vya kamati walifanikiwa kufanya mageuzi makubwa katika kamati hiyo na kupata nyongeza ya fungu la kuhudumia mipango katika bajeti ya Wizara hiyo na kuwa huu ni uzalendo na Hoja ambazo ni kwa masilahi ya Umma.
Akiuma na kupuliza katika nyakati tofauti hakusita kutupa kombora kwa jirani zake wa upinzani akikejeli kwa mzaha kidogo kuwa hataki ifike pahala kwa wazee kama yeye mwenye upara kulazimika kuingia bungeni wakiwa wamevaa helmet kuhofia akili za wabunge ambao wanataka milango ifungwe ili wapigane.
Baada ya mzaha huo karejea tena kukazia kuwa hapa hoja si kupigana ukitaka kupigana nenda uwanjani katika mieleka ambapo pia yupo refarii mwenye kudhibiti mambo huko uwanjani, lakini kubwa hapa ni wabunge vijana kutumia maarifa, mbinu na ujuzi wao wa kitaaluma kujenga hoja katika kamati kuhakikisha mabadiliko yanapatikana kwa mtanzania mnyonge na sio ushabiki wa kutunishiana misuli kwa kukiuka kanuni za Uendeshaji wa shughuli za Bunge na kuishia kuomba miongozo na Taarifa zisizokuwa na masilahi kwa watanzania.
My TAKE:
- Sikujua hasa nini lengo la nyuma ya Pazia la Mzee mapesa.
- Lakini kama ndivyo kuna haja gani ya wapiganaji wetu kutobana hoja katika kamati na kuturahisishia maisha kuliko kuishia kutolewa nje na kukosa muda wa kututetea.
- Ipo haja tujipange vema kumbe zipo dimension nyingi ambazo tunawez kuzitumia kupaza sauti zetu na kusaka unafuu wa maisha kuliko ilivyo sasa.
- Nakamailisha Thread kuhusu chama Kipya CHAUMA Chama cha Ustawi na Maendeleo.A