Wabongo wakereka na wasanii wavaa vimini

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,318
33,125
pix.gif

Licha ya kuwepo kwa jitihada za makusudi kuhakikisha filamu kutoka kiwanda cha filamu hapa bongo zinachukua chati na hatimaye kuitangaza nchi hii kimataifa, kumekuwepo na lawama nyingi kutoka kwa jamii kuhusiana na aina ya mavazi ambayo yanatumiwa na nyota kadhaa wanaoishiriki katika filamu hizo...
Hali hii ya uvaaji wa kimagharibi imeleta hofu kubwa kwa wapenzi wa filamu hizo hususani akina mama kutokana na kuhofia kuharibiwa kwa watoto wao ambao watakuwa wanaiga mambo hayo endapo watakuwa wakiangalia filamu hizo.

“Mimi ni shabiki mkubwa wa filamu za kitanzania lakini umefika wakati naogopa kununua kazi hizo kwa kuhofia kuharibu maadili ya familia yangu kutokana na uvaaji wa wasanii wetu hivi sasa wanonekana kuiga sana mambo ya Ulaya kitu ambacho kwetu hakina maana yoyote” alisema Sikudhani Said, mkazi wa Chango’mbe jijini Dar es Salaam.

Katika kutafuta ukweli wa jambo hilo Risas Wikiendi Vibes ’ liitembelea duka kubwa la kusambaza filamu Kibongo ‘Tollywood’ na kukutana muuzaji wa bidhaa hizo aliyejitabulisha kwa jina la Michael Mzee, ambaye alikiri kukumbwa na tatizo la kupungua kwa idadi ya wanunuzi wa muvi za Tanzania kutokana na kile wazazi wanadai ni kulinda maadili ya watoto wao.
 
Hapa nadhani tunadanganya, tunapenda kukwepa ukweli wa suala hili, hayo maadili ni yepi?Umalaya au kuvaa nguo fupi?
Tuna mifano hai ya wanawake wanaheshimika na kupewa nyadhifa muhimu za serikali ambao wanao vaa kiheshima tena na wengine kujifunika ushungi lakini utakuta ndio wa kwnza kufanya umalaya kisiri, je ni hayo maadili unayo zungumzia yani mambo yafanyike kisiri ?.

Kuto nunua hizo DVD isiwe sababu ya kuwanyima kipato wasanii, kwani hao watoto wako wako kwnye utandawazi , haya mambo watayaona tuu na kuyaiga haswa ya uvaaji, Kikubwa unachotakiwa kufanya ni wewe mzazi kujituma zaidi chapa kazi uwe na kipato kizuri , hakikisha watoto wako wanapata mahitaji yote muhimu na pia hakikisha malezi yako ni bora , kwa kuka na watoto wako kuwa elezea kuhusu maadili mema ni yepi tena kwa upendo,pamoja na kuhakikisha unahishi eneo ambalo ni zuri na haliwezi changia kuharibu watotot wako.
Kumbuka kuharibika kwa watoto kunachangiwa zaidi na wewe mzazi na sio nini wana watch kwnye TV.
 
Back
Top Bottom