Barubaru
JF-Expert Member
- Apr 6, 2009
- 7,161
- 2,323
hakika kwa takriban wiki mbili nimekuwa naangali vichwa mbali mbali vya habari vinavyotawala magazeti mbalimbali ya huko Tanzania na kuona vichwa vingi vinavyotawala ni OIC, Mahakama ya kadhi na waraka wa kanisa katoliki.
katika fani ya uandishi hivi ni visa vinavyogusa imani na hisia kubwa sana katika jamii. Hususan kwa watanzania ambapo kuna dini kuu mbili yaani Ukristu na Uislamu. Hii ni sawa sawa na mpira Simba na Yanga. Kwani kama wewe ni mshabiki wa mpira huko tanzania ni lazima uwe mshabiki wa yanga au Simba kisha ukawa wa timu nyingine kama malindi au miembeni n.k.
Kwa kifupi Dhumuni kuu na ndio msingi mkuu wa waandishi wa habari ni KUIPASHA JAMII, KUIELIMISHA JAMII na KUIBURUDISHA JAMII. Nikiwa kama Mwandishi wa habari kitaaluma na mwanasheria kitaaluma pia naona WAHARIRI wa tanzania sasa wanaipeleka nchi pabaya.
Waandishi wengi huko Tanzania sasa wameweka mbele maslahi ya pesa pamoja na hisia zao binafsi na kuamua kuachana na maadili ya uandishi. Utaona Mwandishi anaandika kitu kwa matakwa yake na vile yeye anavyotaka kiwe kiasi cha kuibabaisha jamii na kuiweka jamii katika malumbano makali.
Mwandishi hatakiwi kuwa upande wowote wa shilingi. yeye anatakiwa kuripoti kitu vile kilivyo na kuiachia jamii iamue. sasa unapomwona mwandishi anaripoti kitu na kisha ku conclude yeye mwenyewe ni kinyume cha kanuni za uandishi na vile vile kinyume cha sheria kwani kwani kazi yake ni kupasha habari na sio kuiamulia jamii ifanye nini.
Siku zote tunaamini kuwa KALAMU YA MWANDISHI ina ushawishi mkubwa sana katika kuleta mtafaruku katika jamii. Kwani sana waandishi wa huko wameamua kufatilia na kuingilia mambo ya Dini na kuyaripoti vile wanavyotaka wao, kuwahoji baadhi ya mabalozi na hata kuandika kashfa kwa watu ambao wanakuwa kinyume cha matarajio yao.
Huu kiuandishi ni mwiba mkali sana katika jamii ya ndugu zetu huko Tanzania. naishauri Serikali kuthibiti mambo hayo kwani yanaweza kuvunja amani iliyopo japo ni ya woga (hata ukiangalia humu barzani hoja za kidini zimechukua sura tofauti kiasi cha watu kuanza kukashifiana na kubezana katika iimani zao).
Kuna mambo mengi huko Tanzania ambayo inabidi yaandikwe kama mauji ya albino, uchaguzi wa serikali za mitaa, vifo vya mama na watoto, ugonjwa wa ukimwi, malaria n.k ambapo waandishi wanatakiwa wafanye tafiti nyingi na kuandika makala nyingi za kuielimisha jamii.hayo ndio mambo yatakayoleta tija kwa jamii na kuimarisha usalama wa nchi.
Namaliza kwa kusema.
WAANDISHI NA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI HUKO TANZANIA TAMAA YENU YA PESA MTAIZAMISHA TANZANIA KATIKA BALAA KUBWA LA VITA VYA KIDINI.
Ni Mimi.
Nasriyah Saleh Al- Nahdi.
Qatar Petrolium Ltd
Umm Hays
Doha. Qatar
katika fani ya uandishi hivi ni visa vinavyogusa imani na hisia kubwa sana katika jamii. Hususan kwa watanzania ambapo kuna dini kuu mbili yaani Ukristu na Uislamu. Hii ni sawa sawa na mpira Simba na Yanga. Kwani kama wewe ni mshabiki wa mpira huko tanzania ni lazima uwe mshabiki wa yanga au Simba kisha ukawa wa timu nyingine kama malindi au miembeni n.k.
Kwa kifupi Dhumuni kuu na ndio msingi mkuu wa waandishi wa habari ni KUIPASHA JAMII, KUIELIMISHA JAMII na KUIBURUDISHA JAMII. Nikiwa kama Mwandishi wa habari kitaaluma na mwanasheria kitaaluma pia naona WAHARIRI wa tanzania sasa wanaipeleka nchi pabaya.
Waandishi wengi huko Tanzania sasa wameweka mbele maslahi ya pesa pamoja na hisia zao binafsi na kuamua kuachana na maadili ya uandishi. Utaona Mwandishi anaandika kitu kwa matakwa yake na vile yeye anavyotaka kiwe kiasi cha kuibabaisha jamii na kuiweka jamii katika malumbano makali.
Mwandishi hatakiwi kuwa upande wowote wa shilingi. yeye anatakiwa kuripoti kitu vile kilivyo na kuiachia jamii iamue. sasa unapomwona mwandishi anaripoti kitu na kisha ku conclude yeye mwenyewe ni kinyume cha kanuni za uandishi na vile vile kinyume cha sheria kwani kwani kazi yake ni kupasha habari na sio kuiamulia jamii ifanye nini.
Siku zote tunaamini kuwa KALAMU YA MWANDISHI ina ushawishi mkubwa sana katika kuleta mtafaruku katika jamii. Kwani sana waandishi wa huko wameamua kufatilia na kuingilia mambo ya Dini na kuyaripoti vile wanavyotaka wao, kuwahoji baadhi ya mabalozi na hata kuandika kashfa kwa watu ambao wanakuwa kinyume cha matarajio yao.
Huu kiuandishi ni mwiba mkali sana katika jamii ya ndugu zetu huko Tanzania. naishauri Serikali kuthibiti mambo hayo kwani yanaweza kuvunja amani iliyopo japo ni ya woga (hata ukiangalia humu barzani hoja za kidini zimechukua sura tofauti kiasi cha watu kuanza kukashifiana na kubezana katika iimani zao).
Kuna mambo mengi huko Tanzania ambayo inabidi yaandikwe kama mauji ya albino, uchaguzi wa serikali za mitaa, vifo vya mama na watoto, ugonjwa wa ukimwi, malaria n.k ambapo waandishi wanatakiwa wafanye tafiti nyingi na kuandika makala nyingi za kuielimisha jamii.hayo ndio mambo yatakayoleta tija kwa jamii na kuimarisha usalama wa nchi.
Namaliza kwa kusema.
WAANDISHI NA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI HUKO TANZANIA TAMAA YENU YA PESA MTAIZAMISHA TANZANIA KATIKA BALAA KUBWA LA VITA VYA KIDINI.
Ni Mimi.
Nasriyah Saleh Al- Nahdi.
Qatar Petrolium Ltd
Umm Hays
Doha. Qatar