Kabla ya Mwangosi kumetokea mambo mengi ya kuashiria manyanyaso kwa wandishi wa habari kama vile kumwagiwa tindikali kwa Saed kubenea jambo ambalo lilikuwa kiashiria kibaya na endapo mngeungana na kupaza sauti kama mnavyofanya sasa pengine haya yasingetokea. Nadhani mlifukiri yeye ni yeye na nyie ni nyie. Matokeo yake mmeyaona.
Gazeti la Mwanahalisi limefungiwa wakati ambapo linahitajika mno kwa watanzania lakini wandishi wa habari mmeshindwa kupaza sauti kwenye vyombo vyenu na ninahisi kuna watu wamefurahia kufungiwa kwake ili muuze yenu jambo ambalo mimi naona si haki. Mungekuwa kitu kimoja naamini leo hii polisi wasingethubutu kuwachezea.
Nawashauri kifo cha Mwangosi kiwe chachu ya mabadiliko muungane zaidi, mudai gazeti la Mwanahalisi lifunguliwe. Kuna wale waandishi walipewa tuzo wakati fulani lakini kutokumuona Kubenea akipewa tuzo nilijiridhisha kuwa zile tuzo hazikuwa na mshiko kwa upande wangu kwani makala zake zilikuwa nzuri na ziliibua uozo mwingi.
Nawaomba badilikeni kuweni kitu kimoja kama mlivyoonyesha umoja kwenye maandamano ya jana japo mmechelewa ndiyo maana yametokea yaliyotokea.
Au wadau mnasemaje?
Gazeti la Mwanahalisi limefungiwa wakati ambapo linahitajika mno kwa watanzania lakini wandishi wa habari mmeshindwa kupaza sauti kwenye vyombo vyenu na ninahisi kuna watu wamefurahia kufungiwa kwake ili muuze yenu jambo ambalo mimi naona si haki. Mungekuwa kitu kimoja naamini leo hii polisi wasingethubutu kuwachezea.
Nawashauri kifo cha Mwangosi kiwe chachu ya mabadiliko muungane zaidi, mudai gazeti la Mwanahalisi lifunguliwe. Kuna wale waandishi walipewa tuzo wakati fulani lakini kutokumuona Kubenea akipewa tuzo nilijiridhisha kuwa zile tuzo hazikuwa na mshiko kwa upande wangu kwani makala zake zilikuwa nzuri na ziliibua uozo mwingi.
Nawaomba badilikeni kuweni kitu kimoja kama mlivyoonyesha umoja kwenye maandamano ya jana japo mmechelewa ndiyo maana yametokea yaliyotokea.
Au wadau mnasemaje?