Kaa la Moto
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 7,903
- 1,053
Ukanjanja na changamoto inayoukabili uandishi nchini
Na Prudence Karugendo
Zimekuwepo juhudi za makusudi zinazodaiwa ni za kutaka kuilinda taaluma ya uandishi zinazoonekana kufanywa na wana taaluma wakereketwa. Wanataaluma hao wanaona kwamba ni kama taaluma yao inaingiliwa. Majina mbalimbali ya kibaguzi yamebuniwa yakiwalenga wanaodaiwa kuivamia fani. Yanatajwa majina kama makanjanja, makanjakanja nakadhalika, bila shaka mengine yako mtamboni yanaundwa.
Binafsi nakubaliana na hoja ya kuwepo kwa taaluma ya uandishi na umuhimu wa kuiheshimu taaluma hiyo. Kinachonipa utata, na mahali ninapotofautiana na wanataaluma, ni katika namna taaluma hiyo inavyopaswa kulindwa. Sikubaliani na wanaotaka taaluma hiyo ilindwe kwa mabavu na vitisho dhidi ya wale wasiotakiwa ambao kwa namna moja au nyingine ndio wanaoonekana kuivamia taaluma, japo wao wanajiweka karibu kutokana na mapenzi yao kwenye taaluma hiyo na hivyo kuamua kuiunga mkono.
Ili taaluma iheshimike haina budi kujilinda yenyewe kwa wana taaluma kuonyesha kile kinachoifanya ikaitwa taaluma, ambacho kwa tafsiri nyingine kinapaswa kiwe nje ya upeo wa wale wasio na taaluma. Mathalan, maadishi yenye kufikirisha ambayo si kila mmoja mwenye kuelewa kuandika anaweza kuyarukia na kujaribu kuyaandika.
Kinyume chake wana taaluma ya uandishi wanashindwa kukifanya kile ambacho kingeifanya taaluma yao ikaheshimika na kuogopeka, badala yake wanafanya mambo ambayo kila mmoja anajiona ana uwezo nayo. Kwa hilo wa kujilaumu ni wana taaluma ya uandishi wenyewe. Wanapaswa wajiulize kwa nini taaluma nyingine hazivamiwi? Badala ya wana taaluma kutumia ujuzi wa kitaalamu kuihami taaluma yao wanaishia kupiga piga makelele ya kuvamiwa kwa kutaka kuishawishi dola itunge sheria ya kuwalindia taaluma yao. Wana taaluma wameshindwa kuilinda taaluma, wanataka ilindwe na sheria na bunduki (?).
Kushindwa huko kwa wana taaluma kutumia njia za kitaalamu kuilinda taaluma yao kunaifanya taaluma ya uandishi kubaki kama haina mwenyewe, na matokeo yake ni kila mtu mwenye kujiona ana uwezo wa kuandika kushawishika kujiingiza kwenye taaluma hiyo kwa vile wahusika wanakuwa hawawezi kujitofautisha na wasio wahusika.
Haitoshi kuilinda taaluma kwa kutaja tu muda ambao mtu anakuwa ameutumia kuisotea taaluma husika au mrundikano wa shahada. Kinachotakiwa ni kuonyesha mabadiliko katika taaluma kwa kuifanyia vitu ambavyo hasiye mwana taaluma atajionea aibu kuisogelea taaluma ya watu. Hapa nchini ni wana taaluma wangapi wanafanya hivyo?
Wapo watu ambao naamini kwamba wanaendelea kuilinda taaluma ya uandishi bila kutumia mabavu pamoja na kwamba watu hao hawapo tena duniani, ingawa kulingana na mpangilio wa madai yanayotolewa na watetezi wa taaluma wa kipindi hiki, watu hao wanaweza wakaonekana nao hawakuwa wana taaluma kwa vile wasingeweza kutaja miaka waliyotumia wakiisotea taaluma hiyo ya uandishi wala kuonyesha vyeti vya kuwatambulisha kama wana taaluma.
Mmoja wa watu ninaoamini kuwa bado wanailinda taaluma ya uandishi ni marehemu Shaaban Robert. Uandishi wa mzee yule, ambao mwingine aliufanya zaidi ya miaka 50 iliyopita, bado mpaka sasa unailinda taaluma ya uandishi kwa kumfanya kila mtu aliye makini asiweze kujipendekeza kuwa anaweza kuimudu taaluma hiyo. Wala Shaaban Robert hatumii majivuno, vitisho na majigambo katika kuilinda taaluma yake. Yeye anaiwezesha taaluma kujionyesha uadhimu na uzito wake na kisha yenyewe kujijengea heshima.
Uandishi wa Shaaban Robert wa kuonya, kuhadharisha, kukanya, kusifia pamoja na kuelimisha, bila kukosa kuhabarisha kwa namna ya pekee ni kielelezo tosha cha uadhimu wa taaluma ya uandishi na manufaa inayoyachangia katika jamii.
Aina ya uandishi wa Shaaban Robert inawafanya watu kuitamani taaluma ya uandishi. Hii ni kwa sababu wapo watu wanaotumia aina ya uandishi wake kama mwongozo wa maisha yao. Hivyo ndivyo taaluma inavyopaswa kuinufaisha jamii. Na papo hapo jamii inajenga heshima kwa taaluma hiyo kwa wanajamii kuamini kwamba si wote wenye uwezo wa kufanya kama alivyofanya yeye. Kwa mantiki hiyo sitegemei kama zingekuwepo kelele za kutaka taaluma ya uandishi iheshimiwe. Yenyewe ingekuwa inajitosheleza.
Mtu mwingine aliyeitumia taaluma ya uandishi kuinufaisha jamii ni Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere. Tangu kabla ya uhuru wa Tanganyika, alipoingia kwenye harakati za kutafuta uhuru, alitumia zaidi taaluma ya uandishi na kuifanya silaha yake kuu katika mapambano yale. Tunakumbuka alivyonusurika kwenda jera baada ya kudaiwa kuwakashfu wakoloni akiwa mhariri wa gazeti la chama cha TANU. Hata baada ya uhuru bado Nyerere aliendelea kuitumia taaluma hiyo kuwaelimisha wananchi juu ya maana ya nchi kuwa huru. Tunafahamu machapisho aliyoyatoa, sina haja ya kuyataja hapa. Na alipokuwa ameisha staafu uongozi bado Mwalimu aliendelea kujikita katika taaluma ya uandishi na kuitumia kufikisha nasaha zake kwa jamii. Mwanzoni mwa miaka ya 1990 pale lilipoibuka kundi la wabunge la kuidai serikali ya Tanganyika, Mwalimu alitumia taaluma ya uandishi kuutuliza mzuka huo. Aliandika vitabu viwili kwa mkupuo navyo vikawafanya wabunge wale kufyata mkia. Ni taaluma ya uandishi iliyofanya kazi.
Ingekuwa sasa hivi si ajabu Mwalimu angetakiwa aonyeshe vyeti vya uandishi kwanza na wale wanaoamini kwamba taaluma hii ni mali yao, kabla ya maandishi yake hayajakubalika kwa wana taaluma. Na nisingeshangaa kama naye angekumbwa na jina la ukanjanja.
Nataka nieleweke, nilichokilenga hapa ni uandishi kama waleta hoja wanavyopendelea kuliweka. Maana najua kuna watakaonibadilikia wakidai kwamba kinachopaswa kulengwa ni uandishi wa aina fulani, mfano uandishi wa habari. La uandishi wa habari linaeleweka ila kwa makusudi kabisa wameamua kulipanua suala hilo ili liweze kuwameza wote wanaojihusisha na uandishi kwa lengo la kutaka kuwadhibiti. Ndiyo maana hata mimi hoja zangu nikawa nazielekeza kwenye uandishi kwa ujumla.
Kwa mtizamo wangu, wapo baadhi ya waandishi ambao wangependa kuihodhi taaluma ya uandishi, bila shaka kwa kutaka iwanufaishe wao tu bila jamii kuambulia chochote. Hawa ndio wanaowaona wale wanaojitokeza kuipanulia wigo taaluma hiyo kama wavamizi katika fani. Huko ndiko mashambulizi yanayoongozwa na majina yenye kila dalili za matusi, kama hilo la makanjanja, yanakoanzia, lakini bila wenyewe kuyaweka bayana manufaa yanayotokana na wale wasio makanjanja katika jamii yetu.
Majuzi mwandishi mmoja mkongwe hapa nchini alikuwa anajaribu kunipa darasa la uandishi baada ya mimi kuwa nimemchokoza. Alisema kwamba mwandishi anapaswa kuwa kama mwamuzi wa mchezo, kwamba hapaswi kuhukumu nani ashindwe ila kuuachia mchezo wenyewe ndio utoe hukumu. Akasema kwamba mwandishi anatakiwa kutoa kitu jinsi kilivyo bila dalili za upendeleo hata kama anao upande anaoupendelea. Nilipomuuliza juu ya waandishi wanaokiuka kanuni hiyo wakati wakijidai kuwa mahiri katika fani, akasema yeye sasa anatamani kufanya kazi katika vyombo vya ughaibuni maana kwa hapa nchini watu hawaambiliki. Kwa maana hiyo inaonyesha kwamba yanayofanywa na waandishi wa hapa nchini mengi hayaungi mkono, na si ajabu anawaona wale wanaowaita wenzao makanjanja ndio makanjanja wenyewe ila hasemi kwa kubanwa na kanuni za taaluma anazoonekana kuziheshimu na kuzizingatia, anaiachia jamii itoe hukumu.
Zimetafutwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwasakama hao makanjanja, ila ukweli ni kwamba kudorora kwa taaluma ya uandishi hapa nchini kunachangiwa zaidi na baadhi ya wana taaluma kukubali kuzianika wazi bei zao, kitu kilichoifanya taaluma ipimwe thamani yake kulingana na inavyotaka kutumiwa. Watumiaji ndio wamebaki wameishikilia thamani nzima ya taaluma Kwa hapa kuwasakama makanjanja ni kuwaonea.
Mwandishi anayeandika kwa maelekezo ya kumchafua mtu fulani au kumpamba mtu fulani tayari anakuwa ameishabandika alama ya bei yake usoni mwake. Na kamwe siwezi kuamini kama anafanya hivyo kwa malengo ya kuboresha taaluma. Dhahiri huko ni kuiua taaluma. Thamani ya taaluma inabaki mikononi mwa wale wanaotaka kuitumia taaluma kwa manufaa yao. Hivi kweli waandishi wa aina hii wanataka tuamini kwamba wanapowashambulia wanaowaita makanjanja wanakuwa wamedhamiria kwa dhati kuisafisha taaluma yao? Ni kitu gani cha kutufanya tusiwaone wao kuwa ndio makanjanja?
Tumewashuhudia wahariri kadhaa, ambao baadhi yao ndio vinara wa kuushambulia unaoitwa ukanjanja, ama wakitishiwa kuburuzwa mahakamani au wakati mwingine kulazimika kuomba misamaha nje ya mahakama kutokana na vyombo wanavyovihariri kutowatendea haki baadhi ya watu, kama vile kuwakashfu, kuwapaka matope nakadhalika, ili kuzifurahisha nafsi fulani ambazo zinakuwa zimewatuma au kuwanunua. Katika hali hiyo nani anayo haki ya kusimama na kumnyooshea mwingine kidole kuwa ni kanjanja? Kwa nini ukanjanja usionekane kuanzia hapo?
Hii inapaswa itukumbushe kwamba vita inapokuwa ngumu wasio na fani ya kijeshi hulazimika kuingia katika mapambano hata kama ni kwa kutumia silaha duni kama manati, ili kujaribu kuokoa jahazi. Wanaoitwa makanjanja inabidi tuwatambue kwa kukiona kile kinachofanywa na wasiokuwa makanjanja na kiwe kimejitofautisha, vinginevyo siuoni ubora unaowasababishia watu viburi vya kuwapachika wenzao majina ya ajabu ajabu.
Inabidi tujenge utamaduni wa kuifanya taaluma ya uandishi kujisimamia, kwa kufanya hivyo tutakuwa tumeijengea heshima inayoistahiki.
prudencekarugendo@yahoo.com
0784 989 512
Na Prudence Karugendo
Zimekuwepo juhudi za makusudi zinazodaiwa ni za kutaka kuilinda taaluma ya uandishi zinazoonekana kufanywa na wana taaluma wakereketwa. Wanataaluma hao wanaona kwamba ni kama taaluma yao inaingiliwa. Majina mbalimbali ya kibaguzi yamebuniwa yakiwalenga wanaodaiwa kuivamia fani. Yanatajwa majina kama makanjanja, makanjakanja nakadhalika, bila shaka mengine yako mtamboni yanaundwa.
Binafsi nakubaliana na hoja ya kuwepo kwa taaluma ya uandishi na umuhimu wa kuiheshimu taaluma hiyo. Kinachonipa utata, na mahali ninapotofautiana na wanataaluma, ni katika namna taaluma hiyo inavyopaswa kulindwa. Sikubaliani na wanaotaka taaluma hiyo ilindwe kwa mabavu na vitisho dhidi ya wale wasiotakiwa ambao kwa namna moja au nyingine ndio wanaoonekana kuivamia taaluma, japo wao wanajiweka karibu kutokana na mapenzi yao kwenye taaluma hiyo na hivyo kuamua kuiunga mkono.
Ili taaluma iheshimike haina budi kujilinda yenyewe kwa wana taaluma kuonyesha kile kinachoifanya ikaitwa taaluma, ambacho kwa tafsiri nyingine kinapaswa kiwe nje ya upeo wa wale wasio na taaluma. Mathalan, maadishi yenye kufikirisha ambayo si kila mmoja mwenye kuelewa kuandika anaweza kuyarukia na kujaribu kuyaandika.
Kinyume chake wana taaluma ya uandishi wanashindwa kukifanya kile ambacho kingeifanya taaluma yao ikaheshimika na kuogopeka, badala yake wanafanya mambo ambayo kila mmoja anajiona ana uwezo nayo. Kwa hilo wa kujilaumu ni wana taaluma ya uandishi wenyewe. Wanapaswa wajiulize kwa nini taaluma nyingine hazivamiwi? Badala ya wana taaluma kutumia ujuzi wa kitaalamu kuihami taaluma yao wanaishia kupiga piga makelele ya kuvamiwa kwa kutaka kuishawishi dola itunge sheria ya kuwalindia taaluma yao. Wana taaluma wameshindwa kuilinda taaluma, wanataka ilindwe na sheria na bunduki (?).
Kushindwa huko kwa wana taaluma kutumia njia za kitaalamu kuilinda taaluma yao kunaifanya taaluma ya uandishi kubaki kama haina mwenyewe, na matokeo yake ni kila mtu mwenye kujiona ana uwezo wa kuandika kushawishika kujiingiza kwenye taaluma hiyo kwa vile wahusika wanakuwa hawawezi kujitofautisha na wasio wahusika.
Haitoshi kuilinda taaluma kwa kutaja tu muda ambao mtu anakuwa ameutumia kuisotea taaluma husika au mrundikano wa shahada. Kinachotakiwa ni kuonyesha mabadiliko katika taaluma kwa kuifanyia vitu ambavyo hasiye mwana taaluma atajionea aibu kuisogelea taaluma ya watu. Hapa nchini ni wana taaluma wangapi wanafanya hivyo?
Wapo watu ambao naamini kwamba wanaendelea kuilinda taaluma ya uandishi bila kutumia mabavu pamoja na kwamba watu hao hawapo tena duniani, ingawa kulingana na mpangilio wa madai yanayotolewa na watetezi wa taaluma wa kipindi hiki, watu hao wanaweza wakaonekana nao hawakuwa wana taaluma kwa vile wasingeweza kutaja miaka waliyotumia wakiisotea taaluma hiyo ya uandishi wala kuonyesha vyeti vya kuwatambulisha kama wana taaluma.
Mmoja wa watu ninaoamini kuwa bado wanailinda taaluma ya uandishi ni marehemu Shaaban Robert. Uandishi wa mzee yule, ambao mwingine aliufanya zaidi ya miaka 50 iliyopita, bado mpaka sasa unailinda taaluma ya uandishi kwa kumfanya kila mtu aliye makini asiweze kujipendekeza kuwa anaweza kuimudu taaluma hiyo. Wala Shaaban Robert hatumii majivuno, vitisho na majigambo katika kuilinda taaluma yake. Yeye anaiwezesha taaluma kujionyesha uadhimu na uzito wake na kisha yenyewe kujijengea heshima.
Uandishi wa Shaaban Robert wa kuonya, kuhadharisha, kukanya, kusifia pamoja na kuelimisha, bila kukosa kuhabarisha kwa namna ya pekee ni kielelezo tosha cha uadhimu wa taaluma ya uandishi na manufaa inayoyachangia katika jamii.
Aina ya uandishi wa Shaaban Robert inawafanya watu kuitamani taaluma ya uandishi. Hii ni kwa sababu wapo watu wanaotumia aina ya uandishi wake kama mwongozo wa maisha yao. Hivyo ndivyo taaluma inavyopaswa kuinufaisha jamii. Na papo hapo jamii inajenga heshima kwa taaluma hiyo kwa wanajamii kuamini kwamba si wote wenye uwezo wa kufanya kama alivyofanya yeye. Kwa mantiki hiyo sitegemei kama zingekuwepo kelele za kutaka taaluma ya uandishi iheshimiwe. Yenyewe ingekuwa inajitosheleza.
Mtu mwingine aliyeitumia taaluma ya uandishi kuinufaisha jamii ni Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere. Tangu kabla ya uhuru wa Tanganyika, alipoingia kwenye harakati za kutafuta uhuru, alitumia zaidi taaluma ya uandishi na kuifanya silaha yake kuu katika mapambano yale. Tunakumbuka alivyonusurika kwenda jera baada ya kudaiwa kuwakashfu wakoloni akiwa mhariri wa gazeti la chama cha TANU. Hata baada ya uhuru bado Nyerere aliendelea kuitumia taaluma hiyo kuwaelimisha wananchi juu ya maana ya nchi kuwa huru. Tunafahamu machapisho aliyoyatoa, sina haja ya kuyataja hapa. Na alipokuwa ameisha staafu uongozi bado Mwalimu aliendelea kujikita katika taaluma ya uandishi na kuitumia kufikisha nasaha zake kwa jamii. Mwanzoni mwa miaka ya 1990 pale lilipoibuka kundi la wabunge la kuidai serikali ya Tanganyika, Mwalimu alitumia taaluma ya uandishi kuutuliza mzuka huo. Aliandika vitabu viwili kwa mkupuo navyo vikawafanya wabunge wale kufyata mkia. Ni taaluma ya uandishi iliyofanya kazi.
Ingekuwa sasa hivi si ajabu Mwalimu angetakiwa aonyeshe vyeti vya uandishi kwanza na wale wanaoamini kwamba taaluma hii ni mali yao, kabla ya maandishi yake hayajakubalika kwa wana taaluma. Na nisingeshangaa kama naye angekumbwa na jina la ukanjanja.
Nataka nieleweke, nilichokilenga hapa ni uandishi kama waleta hoja wanavyopendelea kuliweka. Maana najua kuna watakaonibadilikia wakidai kwamba kinachopaswa kulengwa ni uandishi wa aina fulani, mfano uandishi wa habari. La uandishi wa habari linaeleweka ila kwa makusudi kabisa wameamua kulipanua suala hilo ili liweze kuwameza wote wanaojihusisha na uandishi kwa lengo la kutaka kuwadhibiti. Ndiyo maana hata mimi hoja zangu nikawa nazielekeza kwenye uandishi kwa ujumla.
Kwa mtizamo wangu, wapo baadhi ya waandishi ambao wangependa kuihodhi taaluma ya uandishi, bila shaka kwa kutaka iwanufaishe wao tu bila jamii kuambulia chochote. Hawa ndio wanaowaona wale wanaojitokeza kuipanulia wigo taaluma hiyo kama wavamizi katika fani. Huko ndiko mashambulizi yanayoongozwa na majina yenye kila dalili za matusi, kama hilo la makanjanja, yanakoanzia, lakini bila wenyewe kuyaweka bayana manufaa yanayotokana na wale wasio makanjanja katika jamii yetu.
Majuzi mwandishi mmoja mkongwe hapa nchini alikuwa anajaribu kunipa darasa la uandishi baada ya mimi kuwa nimemchokoza. Alisema kwamba mwandishi anapaswa kuwa kama mwamuzi wa mchezo, kwamba hapaswi kuhukumu nani ashindwe ila kuuachia mchezo wenyewe ndio utoe hukumu. Akasema kwamba mwandishi anatakiwa kutoa kitu jinsi kilivyo bila dalili za upendeleo hata kama anao upande anaoupendelea. Nilipomuuliza juu ya waandishi wanaokiuka kanuni hiyo wakati wakijidai kuwa mahiri katika fani, akasema yeye sasa anatamani kufanya kazi katika vyombo vya ughaibuni maana kwa hapa nchini watu hawaambiliki. Kwa maana hiyo inaonyesha kwamba yanayofanywa na waandishi wa hapa nchini mengi hayaungi mkono, na si ajabu anawaona wale wanaowaita wenzao makanjanja ndio makanjanja wenyewe ila hasemi kwa kubanwa na kanuni za taaluma anazoonekana kuziheshimu na kuzizingatia, anaiachia jamii itoe hukumu.
Zimetafutwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwasakama hao makanjanja, ila ukweli ni kwamba kudorora kwa taaluma ya uandishi hapa nchini kunachangiwa zaidi na baadhi ya wana taaluma kukubali kuzianika wazi bei zao, kitu kilichoifanya taaluma ipimwe thamani yake kulingana na inavyotaka kutumiwa. Watumiaji ndio wamebaki wameishikilia thamani nzima ya taaluma Kwa hapa kuwasakama makanjanja ni kuwaonea.
Mwandishi anayeandika kwa maelekezo ya kumchafua mtu fulani au kumpamba mtu fulani tayari anakuwa ameishabandika alama ya bei yake usoni mwake. Na kamwe siwezi kuamini kama anafanya hivyo kwa malengo ya kuboresha taaluma. Dhahiri huko ni kuiua taaluma. Thamani ya taaluma inabaki mikononi mwa wale wanaotaka kuitumia taaluma kwa manufaa yao. Hivi kweli waandishi wa aina hii wanataka tuamini kwamba wanapowashambulia wanaowaita makanjanja wanakuwa wamedhamiria kwa dhati kuisafisha taaluma yao? Ni kitu gani cha kutufanya tusiwaone wao kuwa ndio makanjanja?
Tumewashuhudia wahariri kadhaa, ambao baadhi yao ndio vinara wa kuushambulia unaoitwa ukanjanja, ama wakitishiwa kuburuzwa mahakamani au wakati mwingine kulazimika kuomba misamaha nje ya mahakama kutokana na vyombo wanavyovihariri kutowatendea haki baadhi ya watu, kama vile kuwakashfu, kuwapaka matope nakadhalika, ili kuzifurahisha nafsi fulani ambazo zinakuwa zimewatuma au kuwanunua. Katika hali hiyo nani anayo haki ya kusimama na kumnyooshea mwingine kidole kuwa ni kanjanja? Kwa nini ukanjanja usionekane kuanzia hapo?
Hii inapaswa itukumbushe kwamba vita inapokuwa ngumu wasio na fani ya kijeshi hulazimika kuingia katika mapambano hata kama ni kwa kutumia silaha duni kama manati, ili kujaribu kuokoa jahazi. Wanaoitwa makanjanja inabidi tuwatambue kwa kukiona kile kinachofanywa na wasiokuwa makanjanja na kiwe kimejitofautisha, vinginevyo siuoni ubora unaowasababishia watu viburi vya kuwapachika wenzao majina ya ajabu ajabu.
Inabidi tujenge utamaduni wa kuifanya taaluma ya uandishi kujisimamia, kwa kufanya hivyo tutakuwa tumeijengea heshima inayoistahiki.
prudencekarugendo@yahoo.com
0784 989 512