Inanambo
JF-Expert Member
- Jun 26, 2011
- 3,975
- 2,755
Nimesikitika sana baada ya kukosa hata kibarua cha muda mfupi cha kusaidia serikali kufanya sensa mwaka huu. Nilimaliza form 6 mwaka jana niko tu home na wazazi wangu nawategemea kwa kila kitu from chakula, mavazi kunyoa na kusuka nywele, nauli ya kwenda na kurudi. Nimetafuta tempo kila pahala hata ya kuuza duka sijapata angalau na mimi nizoea kidogo kupata kwa jasho langu. Nikasikia kuna watu wanatafutwa wa kufanya sensa. Nikaenda kwa serikali za mitaa kuulizia nikaambiwa eti lazima uwe mwalimu ndio utapewa kazi hiyo. Nikajaribu kwenda wilayani nikapewa jibu hilo hilo. Nauliza hivi sisi tuliomaliza form 6 hatuwezi kusaidia serikali kufanya kazi hiyo? Waalimu tayari wana ajira yao na wanapata mshahara. Wao kila ikija sensa, uchaguzi ndio huwa wanapewa nafasi tuu. Watu wengine hata kama tuna identity zinazojulikana hutupewagi hizo nafasi. Ni bora waalimu wafunge shule wanafunzi wakose masomo ili wao wapewe kazi hizi. Mimi nimeona ingekuwa bora kwa kipindi hiki cha sensa na kuandikisha vitambulisho serikali ikawatumia vijana tuliomaliza sekondari tunaosubiri kwenda chuo
ili tusiendelee kuwa jobless wakati kuna shughuli tunaweza saidia serikali kufanya tena kwa ujira kidogo tu wa kununulia hata boxaa.
ili tusiendelee kuwa jobless wakati kuna shughuli tunaweza saidia serikali kufanya tena kwa ujira kidogo tu wa kununulia hata boxaa.