Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,216
- 113,520
Hebu niwaulize wana JF. Wewe ukiona wako wa zamani (ex) anatoka na mtu mwingine eti utajali? Kuna jamaa mmoja kwa kweli simwelewi. Sielewi kabisa mantiki yake na jinsi mchakato wake wa kufikiri ulivyo.
Eti huyu jamaa huwaga anamaindi aonapo wanawake aliowahi kutoka nao wana watu wengine. Eti kwa mtazamo wake hao ni "mademu" wake na iweje jamaa mwingine atoke nao.
Mimi nimeshindwa kabisa kumwelewa. Mtu ukishaachana na mpenzi wako na miaka ikapita bado utadai tu kuwa huyo mpenzi ni wako? Haiingii akilini kabisa. Mimi nilidhani mkishaachana ndo basi tena kila mtu anakuwa huru kutoka na yeyote yule ampendaye.
Eti huyu jamaa huwaga anamaindi aonapo wanawake aliowahi kutoka nao wana watu wengine. Eti kwa mtazamo wake hao ni "mademu" wake na iweje jamaa mwingine atoke nao.
Mimi nimeshindwa kabisa kumwelewa. Mtu ukishaachana na mpenzi wako na miaka ikapita bado utadai tu kuwa huyo mpenzi ni wako? Haiingii akilini kabisa. Mimi nilidhani mkishaachana ndo basi tena kila mtu anakuwa huru kutoka na yeyote yule ampendaye.