Vyuo vikuu Chadema waja na `washa taa mchana`

kweleakwelea

JF-Expert Member
Nov 29, 2010
3,066
1,535
Vyuo vikuu Chadema waja na `washa taa mchana`




Na Gideon Mwakanosya



22nd March 2011


email.png

B-pepe



printer.png

Chapa



comment_bubble.png

Maoni




Chadema%2858%29.jpg

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)



Vijana wasomi wa vyuo vikuu mbalimbali nchini wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wamezindua kampeni waliyoipa jina la ‘washa taa mchana’, itakayoendeshwa nchi nzima, yenye lengo la kuleta ukombozi wa kifikra kwa wananchi.
Akizungumza kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni hiyo uliofanyika jana mjini hapa, Mratibu wa kampeni hiyo mkoa wa Ruvuma, Likapo Bakari, alieleza kuwa taa hiyo itawashwa rasmi Machi 26 mwaka huu, ikiwa na lengo la kumulika na kuangaza katika kila mkoa nchini ili kuleta ukombozi kwa Watanzania
Alisema kuwa, ukombozi huo utakuwa katika nyanja za kiuchumi, kijamii na kisiasa na kwamba itaanzia mkoa wa Ruvuma kwa kufanya mikutano mbalimbali ya hadhara katika kata zote za Manispaa ya Songea, kwa kutoa elimu ya uraia kwa wananchi wa eneo husika ili waweze kuzijua haki zao, kuzitetea na kuzidai.
Aliongeza kusema kuwa, kupitia mikutano hiyo pia watahamasisha jamii namna ya kutumia vizuri rasilimali za taifa katika kujiendeleza na kujiongezea kipato na kuwaelimisha maana ya katiba ya nchi na umuhimu wa kudai katiba mpya.
Akizindua kampeni hiyo, Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Ruvuma, Joseph Fuime, alisema maendeleo yoyote hayawezi kufikiwa bila ya kuwepo kwa siasa safi, hivyo wameanzisha kampeni hiyo itakayoendeleza, kukuza na kukitangaza chama kila kona ya nchi na kufungua matawi mapya.



CHANZO: NIPASHE
 

Well done wasomi wetu.......mna deni kubwa kwa taifa hili and this is atleast the least you can do.

Never give up, the Dawn is so near
 
Nimeipenda sana! CCM wanasema tusubiri mpaka 2015 wakati kiza kitakapokuwa kimetanda ili wafunge magoli kiurahisi. Ila hii ya kuwasha taa mchana ni safi sana. Kama wachaga biashara asubuhi, jioni unahesabu faida.
Go CDM go go go goooooo ...
 
Saaafi sana....
Taifa hili halina mkombozi zaidi ya vijana wasomi....mapambano daima...na nguvu isambae hadi ngazi ya Masekondarini....ndio ukombozi utafikia mwisho...taifa ni la nguvu mpya na kizazi kipya...
PAMOJA DAIMA....DAIMA TUNAWEZA...NA PAMOJA TUTAFIKA....WITH PEOPLE'S POWER...YES WE CAN!
 
Thats perfect! Kazi ya vijana ni kukijenga chama. Tunamikakati ya kuhakikisha tunashinda ushindi wa kushtusha mwaka 2015. This is the right move to the right direction! Tuwaache wenzetu wakiendekeza majungu na kugombana wao kwa wao sisi tukijenga chama. Wakishtuka itakuwa jioni ishaingia! Tuwashe taa mchana ili tuwachunge wasichakachue tena kura zetu!
 
Vyuo vikuu Chadema waja na `washa taa mchana`




Na Gideon Mwakanosya



22nd March 2011


email.png

B-pepe



printer.png

Chapa



comment_bubble.png

Maoni




Chadema%2858%29.jpg

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)



Vijana wasomi wa vyuo vikuu mbalimbali nchini wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wamezindua kampeni waliyoipa jina la ‘washa taa mchana', itakayoendeshwa nchi nzima, yenye lengo la kuleta ukombozi wa kifikra kwa wananchi.
Akizungumza kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni hiyo uliofanyika jana mjini hapa, Mratibu wa kampeni hiyo mkoa wa Ruvuma, Likapo Bakari, alieleza kuwa taa hiyo itawashwa rasmi Machi 26 mwaka huu, ikiwa na lengo la kumulika na kuangaza katika kila mkoa nchini ili kuleta ukombozi kwa Watanzania
Alisema kuwa, ukombozi huo utakuwa katika nyanja za kiuchumi, kijamii na kisiasa na kwamba itaanzia mkoa wa Ruvuma kwa kufanya mikutano mbalimbali ya hadhara katika kata zote za Manispaa ya Songea, kwa kutoa elimu ya uraia kwa wananchi wa eneo husika ili waweze kuzijua haki zao, kuzitetea na kuzidai.
Aliongeza kusema kuwa, kupitia mikutano hiyo pia watahamasisha jamii namna ya kutumia vizuri rasilimali za taifa katika kujiendeleza na kujiongezea kipato na kuwaelimisha maana ya katiba ya nchi na umuhimu wa kudai katiba mpya.
Akizindua kampeni hiyo, Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Ruvuma, Joseph Fuime, alisema maendeleo yoyote hayawezi kufikiwa bila ya kuwepo kwa siasa safi, hivyo wameanzisha kampeni hiyo itakayoendeleza, kukuza na kukitangaza chama kila kona ya nchi na kufungua matawi mapya.



CHANZO: NIPASHE
Chadema wanahamasisha ukombozi wa kifikra. Pale ambapo wadau wanaamka kutaka kudai chao mnawatuliza. Yaani kama vile kumringishia mwanao pipi halafu humpi. Lazima atalia tu. Sasa kwa watu wazima hawa unadhani watachukua hatua gani?
 
Kwa makakati hii siku moja mtachukua dola mtatuongoza kataifa, kwa sasa mnatuongoza kwenye halmashauri zetu. Focus sasa iwe mikoa ya nyanda za juu kusini. waachie akina lipumba wahangaike na wajahidina mpaka watakapopigwa mabomu.
 
Washa Taa Mchana


Taa hii tunaiwasha itusaidie kuibua yaliyofichika,itusaidie kuhoji na itusaidie kukemea uchafu wa viongozi wasio waadilifu, Nchi yetu haitapotea...23-01-2011 Serengeti.
 
chadema songea hiyo nzuri sana. na ndicho nafikiria cdm should be doing now, kueneza/ku inject fikra za mabadiliko kwa wananchi huko waliko vijijini, mashuleni, vyuoni na si kukalia inshu ya meya arusha na kutoa 21 days!. vjana songea na mwenyekiti wenu wa wilaya safiiiiiiiii sana!!!
 
Operesheni ''washa taa mchana'' ......ikiwa na lengo la kumulika na kuangaza katika kila mkoa nchini ili kuleta ukombozi kwa Watanzania......kwa kutoa elimu ya uraia kwa wananchi wa eneo husika ili waweze kuzijua haki zao, kuzitetea na kuzidai.

Bonge la Operesheni. Limekuja Kwa kupindi sahihi, mahali sahihi na kwa watu sahihi. Na kama vipi hawa vijana wpitie na wilaya zilizo gizani sana hasa kule ambako wabunge majambazi ya CCM walipita bila kupingwa. Kule Igunga...etc.
 
Washa Taa Mchana


Taa hii tunaiwasha itusaidie kuibua yaliyofichika,itusaidie kuhoji na itusaidie kukemea uchafu wa viongozi wasio waadilifu, Nchi yetu haitapotea...23-01-2011 Serengeti.



Nilikuwa napita nikakutana na hii... Imebidi nisimame kutoa pongezi... Nimefurahia sana.... Wenye kuendekeza majungu na maneno ya taarabu watakoma wenyewe!!!! Songeni mbele na sisi tuko nyuma yenu.
 
Back
Top Bottom