msnajo
JF-Expert Member
- Jan 20, 2011
- 3,066
- 1,136
Wakuu salaam.
Naomba tujadili kama GT. Tuweke tofauti zetu za kiitikadi pamoja na vyama pembeni.
Vyombo vya dola hasa mahakama na polisi, wapo kwa ajili au faida ya nani?? Je, ni sisi wananchi au ni wenye uwezo, au watawala? Nimelazimika kuleta huu mjadala kutokana na ukandamizaji na uonevu unaofanywa na vyombo husika kwa wananchi ama waliomaskini au wasiokuwa watawala. Mara nyingi kwa watu wa kawaida (ordinary people) wanapofanya makosa, polisi wanawakamata "fasta" na watuhumiwa nao wanakamatwa "fasta" itakapodhibitika hawana hatia wanaachiwa huru. Mfumo huu umejikita kwa watu wachini! Kwa wakubwa hasa watawala na wenye uwezo wa fedha, polisi wamekuwa wakijishauri kumkamata mtuhumiwa au kuacha kabisa hata kuzungumzia habari zake ili kumlinda. Huyu "Ahmed Msangi", (I dont wish to know him) ametajwa sana kwenye swala la uhalifu wa kumteka na kumjeruhi Dr Uli. Masikitiko yangu, kama ni mtuhumiwa kwa nini polisi wasimhoji walau kuupata ukweli? Huyu Kova, huu mchezo wa kudanganya watanzania, kwa nini asimdanganye mkewe na watoto wake ili kufanikisha mambo fulani kwa faida ya familia yake? Iramba kumetokea fujo na mtu mmoja karipotiwa kufa, kuna watuhumiwa saba kati ya kumi na mbili inasemekana wametoka Dar na wamelipwa ili kuweza kuleta madhara. Cha kushangaza hawajahojiwa pamoja na kwamba kinadharia wanaonekana kuhusika kwa namna moja au nyingine katika fujo zile. Badala yake unapikwa uwongo na kuwahoji watu wa chama fulani ili kuwabambikia kesi! Kwa nafasi yangu kama Mtanzania, haya ndo mambo nina uhakika kwamba yatatowesha amani yetu. Watanzania tumechoka kuonewa na vyombo vya dola, je vinamtumikia nani? Mahakama nazo zinapindisha kesi ili kuwa-favour watu fulani, wanamtumikia nani? Serikali kama chombo kinachotawala watu hakioni umuhimu wowote wa kujali wananchi/watu wake, hata kama wanateseka "no problem" watajua wenyewe!! Wenye uwezo wa kudai haki wanauawa au kujeruhiwa vibaya, wananchi nasi tunatazama. Lakini ni hadi lini? Bob Marley aliwahi kusema "how long shall they kill our prophet while we stand side and look". Tujiulize, serikali na vyombo vyake vya dola vipo kwa ajili ya nani??
Hebu tupeane hoja.
Naomba tujadili kama GT. Tuweke tofauti zetu za kiitikadi pamoja na vyama pembeni.
Vyombo vya dola hasa mahakama na polisi, wapo kwa ajili au faida ya nani?? Je, ni sisi wananchi au ni wenye uwezo, au watawala? Nimelazimika kuleta huu mjadala kutokana na ukandamizaji na uonevu unaofanywa na vyombo husika kwa wananchi ama waliomaskini au wasiokuwa watawala. Mara nyingi kwa watu wa kawaida (ordinary people) wanapofanya makosa, polisi wanawakamata "fasta" na watuhumiwa nao wanakamatwa "fasta" itakapodhibitika hawana hatia wanaachiwa huru. Mfumo huu umejikita kwa watu wachini! Kwa wakubwa hasa watawala na wenye uwezo wa fedha, polisi wamekuwa wakijishauri kumkamata mtuhumiwa au kuacha kabisa hata kuzungumzia habari zake ili kumlinda. Huyu "Ahmed Msangi", (I dont wish to know him) ametajwa sana kwenye swala la uhalifu wa kumteka na kumjeruhi Dr Uli. Masikitiko yangu, kama ni mtuhumiwa kwa nini polisi wasimhoji walau kuupata ukweli? Huyu Kova, huu mchezo wa kudanganya watanzania, kwa nini asimdanganye mkewe na watoto wake ili kufanikisha mambo fulani kwa faida ya familia yake? Iramba kumetokea fujo na mtu mmoja karipotiwa kufa, kuna watuhumiwa saba kati ya kumi na mbili inasemekana wametoka Dar na wamelipwa ili kuweza kuleta madhara. Cha kushangaza hawajahojiwa pamoja na kwamba kinadharia wanaonekana kuhusika kwa namna moja au nyingine katika fujo zile. Badala yake unapikwa uwongo na kuwahoji watu wa chama fulani ili kuwabambikia kesi! Kwa nafasi yangu kama Mtanzania, haya ndo mambo nina uhakika kwamba yatatowesha amani yetu. Watanzania tumechoka kuonewa na vyombo vya dola, je vinamtumikia nani? Mahakama nazo zinapindisha kesi ili kuwa-favour watu fulani, wanamtumikia nani? Serikali kama chombo kinachotawala watu hakioni umuhimu wowote wa kujali wananchi/watu wake, hata kama wanateseka "no problem" watajua wenyewe!! Wenye uwezo wa kudai haki wanauawa au kujeruhiwa vibaya, wananchi nasi tunatazama. Lakini ni hadi lini? Bob Marley aliwahi kusema "how long shall they kill our prophet while we stand side and look". Tujiulize, serikali na vyombo vyake vya dola vipo kwa ajili ya nani??
Hebu tupeane hoja.