Vyeti vya uraia na yaliyonikuta - a true story

Kiukweli hakuna wajumbe wa nyumba 10 kwa system ya serikali indugu Las Mas Bobos anatupotosha na ametumia maneno makali japokuwa ametoa point nzuri ila naungana nae pale aliposema kabla ya kujiandikisha serikali ilifanya mchakato wa kuandikisha wakazi wote wa maeneo husika hivyo mtoa hoja nae kama alikuwepo angepata room ya kutambuliwa, picha niliyopata hapa baada ya mchango wa Las Mas Bobos ni kwamba mtoa mada huenda hakuwepo wakati zoezi la utambuzi linafanyika na ndio maana akakutana na kadhia hii, all in all mwenyekiti wa mtaa ndie anaetambua wananchi wake na si vinginevyo ila yeye kwa kutumia mbinu zake za ziada ndio anatakiwa awatumia wajumbe wa serikali ya mtaa ambao kila mtaa au kijiji huwa ni wajumbe 25 ambao wanaunda serikali ya mtaa hivyo hakuna issue ya wajumbe 10 hapa. Si kila issue inahitaji degree hapa kuna vitu vingine ni kuelimishana tu mpaka tunafikia consensus tukileta issue za degree hapa wakati raia wengi wa Tanzania ni STD 7 maana yake hatuwezi kufikisha ujumbe uliokusudiwa effectively. NIDA wametumia approach hiyo ili wawanase watu ambao watajifanya raia ndio maana viambatanisho vipo kibao mpaka vya ubatizo wanachukua lakini si kwamba kwa kuwa wametumia approach hiyo ndio tuhalalishe kwamba ndio utaratibu. TUNAHITAJI ELIMU YA URAIA AMBAYO NI GENERAL KWANI MTU AKIWA ANA DEGREE VITU VYOTE ANAVIJUA MPAKA Local Government adminstration.

Mkuu asante kwa ufafanuzi mzuri. Haya hayajanikuta mimi tu kuna mtu mwingine huko naye ameshuhudia watu wanaulizwa barua za balozi wa CCM.

Tiba
 
mie naishitabata washanicharge elfu 2 ajili ya kujiandikisha sabab ya muda siku hiyo sikufanikiwa nkaenda siku mbili baada ya hapo,wakaniambia eti karatasi waliyonipa imechanika so nitoe elf 2 nyingine waibadilishe nikaondoka zango kesho ntajitutumua niende na cheti cha ubatizo ndo nilicho nacho vingine vimepotea nione wataniambia upmnbav gani wakinizingua nakula kona sijiandikishi huo mda wa mtu kuzungukia serikali aza mitaa kila mda anawatu hatuna pesa mifukoni ntaupata wapi af hawa wamama wanaongea utadhani wamekunywa ma.v pambav i hate this country kwakwli
 
Hawa ndio wale wajuaji wanaotaka kuleta kujua kwao kwenye kila jambo. Yeye kaanza na kumuuliza mjumbe wa chama gani.

Mwingine nae anasema DADA ALISHINDWA KUTOFAUTISHA KATI YA MJUMBE NA MWENYEKITI WA SERIKALI YA MTAA, hivi huyo mwenyekiti anawezaje kuwatambua wananchi wote kama mabalozi wa nyumba 10 hawatawatambulisha kwake!

Nchi yetu ina safari ndefu sana na hizi shule za kata na vyuo vya baba kanasa. Imefikia sehemu mtu anaona ni fahari kutomtambua mjumbe wake wa nyumba kumi.

Wasomi kwa faida yenu, hata Mkuu wa Wilaya anamtegemea Mjumbe wa nyumba kumi kukutambua wewe. Tusijivunie uvichwa maji eeeeeh

Wacha mawazo ya ku support a totalitalian structure. Mjumbe wa nyumba kumi ni style ya wakomunisti ya watu ku keep tabs kwa wananchi wake. Nani ana print subversive material, nani ni "enemy of the state" and some bull like that.

Na kama mjumbe wa nyumba kumi ni muhimu hivyo kwa nini asiwe neutral asiye na chama? Na CHADEMA nao wakisema wana mjumbe wao wa nyumba kumi akamtambua mtu ambaye mjumbe wa CCM hamtambui hapo itakuwaje?

Habari ya mjumbe wa nyumba kumi ilikuwa na mshiko enzi za chama kushika hatamu, ukitaka daftari la kusainiwa kupata unga wa muhogo kilo mbili kwa wiki za ugawaji shurti upitishwe na mjumbe wa nyumba kumi etc.

Sasa hivi katika mfumo wa vyama vingi, huwezi kulazimisha mtu wa CHADEMA aende kwa mjumbe wa CCM.

Ni sawasawa na kulazimisha muislamu atambulishwe na mchungaji wa kanisa la karibu.Utamkosea heshima muislamu huyu na huenda hata salamu zikagongana, muislam anasema "Wasalaam Aleikum" Mchungaji anasema "Bwana asifiwe".
 
Nadhani procedures zinazotumiwa zinaboa lakini ni za muhimu. Hata mimi ckujua kama walipita mtaani kuandikisha. Nilienda na nakala ya vyeti vyote na nikaambiwa natakiwa barua ya mjumbe. Ilibidi niifuate hiyo barua ni nipange ratiba nyingine ya cku ya kwenda kujiandikisha (nimefanikiwa)
Bila kufuata taratibu za wajumbe wa nyumba kumi nadhani kufoji kutazidi.
Passport na cheti cha kuzaliwa sio reliable sana (ukifuatilia utaratibu wa kupata hivyo vitu utagundua kuwa mtu anaweza akafoji information na kuvipata)
 
Nimezaliwa Tanzania!
Nimesoma na kumaliza shule ya msingi na secondary Tanzania!
Cheti chakumaliza masomo yangu nilichopewa nimepewa hapahapa Tanzania!
Wakati naomba maombi ya kupata Passport niliambiwa niambatanishe vyeti vyote vinavyohusu kua mimi ni Mtanzania!
Lilipofika zoezi lakujiandikisha kwenye daftari lakudumu la wapiga kura nilipewa kitambulisho cha kua mimi ni Mtanzania!

CHETI CHA URAIA KUA MIMI NI MTANZANIA NI CHA NINI????? :frusty:
 
Tiba

nenda mara ya pili kuulizia tana lakini mara hii jaribu kurekodi na kamchina kako mazungumzo yako na hao wahusika wa sensa na huyo balozi wa ccm halafu uyabandike hapa jf...hawa watu wanatakiwa waanikwe kwa sababu haiwezekani zoezi hilo hilo la aina moja likaendeshwa kwa njia tofauti tofauti...mimi sikupata shida na ilinichukua kama dk 30 hivi kumaliza zoezi lote na nilikuwa na copy ya passport na ya kitambulisho cha kupigia kura tu...!
 
Last edited by a moderator:
Inasikitisha kuona Watanzania wagume kuelewa ni wale wanaojisifu kuwa wamesoma. PASSPORT, DEGREE na sijui nini kingine ulichosema havina nafasi katika kukutambulisha wewe kama individual unaishi mtaa gani. Kwa faida yako na wasiojua wengine nitatumia muda wangu kukueleza/kuwaeleza nini nia ya NIDA kufanya zoezi, jinsi zoezi lilivyoenda na malengo ya mwisho.

Kabla ya kujaza fomu za maombi ya KITAMBULISHO, NIDA kwa kushirikiana na Serikali za Mitaa, iliandaa zoezi la utambuzi wa kaya na makazi kwa kila mtaa. Makarani wa NIDA wakiambatana na WAJUMBE WA NYUMBA KUMI walipita nyumba hadi nyumba kuwasajili wakazi kwenye DAFTARI LA WAKAZI LA MTAA. (Wajumbe wa Nyumba 10 na sio wa CCM) Nikukumbushe kuwa, wengi wa mnaojifanya mmesoma (ilhali vichwani hamna kitu) mlipuuzia zoezi hili na kuwapa wakati mgumu makarani kwa kutotoa ushirikiano kwenu. Muda uliopangwa uliisha na NIDA iliongeza siku 7 za ziada, na bado wengine mligoma kusajiliwa.

Zoezi la usajili wa kaya na wakazi lilipoisha, likaanza zoezi la ujazaji fomu. Hapa sasa na the so called wasomi mkajitokeza. Tatizo likaja kuwa, ili upate uhalali wa kujaza fomu ya maombi ya kitambulisho, inakupasa uwe umeshaorodheshwa katika daftari la mtaa. Sasa lile si daftari tu kama la rambi rambi kwamba kila anayepita na buku yake anaandika, la hasha. ILIPASA UTHIBITIKE haswa ya kwamba u-mkaazi wa eneo husika. Sasa nani anakutambua kama mkaazi, jibu linakuja MJUMBE WA NYUMBA 10.

Kumbuka kuwa, wakati wa uandikishaji wa mitaani (majumbani) mjumbe alikuwa na hao makarani kwa hiyo wote walioorodheshwa wakati huo, walidhaminiwa na mjumbe. Sasa iweje wewe leo hii uje na vyeti vyako vya shule vikutambulishe? Hivi umesoma nini ikiwa unashindwa kuelewa kuwa cheti chako cha chuo hakiwezi kueleza kama unaishi Keko au Mbagala?

Bwana Tiba, serikali ina ngazi mbali mbali za utendaji. Ngazi ya chini kabisa ni mjumbe wa nyumba 10. Ni ujinga na ni ujuha kudharau mjumbe wako wa nyumba kumi na wala kutomjua kwako hakudhihirishi usomi bali upumbavu. Hivi serikali hiyo hiyo iliyokusomesha ikikuhitaji wewe kwa maoni yako unadhani itamtumia nani kukufikia, ALIYEKUANDIKIA HAYO MAVYETI YAKO AU MJUMBE WA NYUMBA KUMI AMBAYE UPO NAYE MTAANI?

Swala la wajumbe kuwa wa nyumba kumi au wa CCM hiyo ni tafsiri tu iliyoletwa na mazoea ya wakati ule wa chama kimoja. Hapa ninapoishi, mjumbe wetu ni wa CUF na mwenyekiti wa serikali ya mtaa ni Wilbald Mlamba wa CHADEMA. Sisi tunamtambua balozi wetu kama wa nyumba kumi na sio kwa jina la chama chake.

Najua kwa mentellity ya 'KIUSOMI' hautapenda kunielewa lkn ni kwa faida yako. Wenzio waliokuwa nyumbani mjumbe alikuwapo kuwatambua wakaingizwa kwenye daftari, wewe umekuwa nani utambulishwe na vyeti? Hivi ukinionesha passport yako hiyo itanithibitishiaje kuwa unakaa mtaa husika na hukai mtaa mwingine?

Wapendwa, passport yaweza kukutambulisha umetokea nchi gani na sio mtaa gani au ni nini kigumu kuelewa hapo? Hivi leo nikikupa cheti changu cha chuo kikuu unaweza kukisoma na kuniambia ninakaa nyumba namba ngapi?

Kama humjui mjumbe wako wa nyumba kumi hiyo ni dalili hushiriki hata katika shughuli za maendeleo na kijamii mtaani. Hujui cha kukarabati barabara wala harambee ya kufanya iusafi wa mazingira, na nyie ndio wasomi njaa mnaojivunia vyeti bila kuwa na ufahamu hata mambo madogo.

Adha umeitaka mwenyewe kwa kutoandikwa nyumbani kwako. Nenda kwa mjumbe akuandikie barua ili huyo karani akutambue kuwa wewe kweli ni makazi wa eneo hilo ndio sasa atakuandika kwenye daftari na utaruhusiwa kujaza fomu. Vyeti utavitumia kuomba kazi na kujisifia kwa wajukuu zako kuwa ulimaliza madarasa, na passport utaitumia kujitambulisha utapokuwa nje ya mipaka ya Tanzania.

Halafu ni ADHA ndugu msomi na sio HADHA. Siipendi CCM lkn sio sababu ya kunifanya niwe mjinga kwa kutomtambua mjumbe wa nyumba 10.

Las Mas Bobos

mbona unatumia lugha yenye jazba?.kwani ukiongea kwa upole na unyenyekevu hatakuelewa? yote uliyojifunza hapa duniani, ungefundishwa kwa maneno makali namna hii ungelielewa?. kama unafahamu jambo, basi ujisikie fahari kumuelimisha mwingine, na hii fahari uipate pale anapokuonyesha amekuelewa. lakini unaonekana upo ktk msingi wa kumkosoa zaidi tena kwa kuonyesha namna gani hawezi kuwa kama wewe, na si namnagani ungelitaka awe kama wewe.
 
mbona unatumia lugha yenye jazba?.kwani ukiongea kwa upole na unyenyekevu hatakuelewa? yote uliyojifunza hapa duniani, ungefundishwa kwa maneno makali namna hii ungelielewa?. kama unafahamu jambo, basi ujisikie fahari kumuelimisha mwingine, na hii fahari uipate pale anapokuonyesha amekuelewa. lakini unaonekana upo ktk msingi wa kumkosoa zaidi tena kwa kuonyesha namna gani hawezi kuwa kama wewe, na si namnagani ungelitaka awe kama wewe.
nimemshangaa sana mkuu wangu hapo...angekuja huku mbezi juu watu tunakwenda kujisajili na kujaza form hapohapo na hakuna cha balozi wala nyau yeyote anayethibisha kama unaishi mtaa husika...
 
nimemshangaa sana mkuu wangu hapo...angekuja huku mbezi juu watu tunakwenda kujisajili na kujaza form hapohapo na hakuna cha balozi wala nyau yeyote anayethibisha kama unaishi mtaa husika...

ni kweli. ila tufahamu wakati tunapata matatizo au ukinzani ktkt jambo fulani, twaweza kuona kama haiwezekani kutatuliwa au tunaonewa, lakini ndo hivyo, mtu kaongea , ni swala la kumuongoza afanye nini , na si ku mshambulia, yote ya yote hata hatumjui kwa sura.
 
kama tunadhani wajumbe wa nyumba 10 ni muhimu basi waajiriwe kama wale watendaji wa mitaa na wasifungamane na chama chochote cha siasa, unadhani kila chama kikiwa na mjumbe wa nyumba 10 itakuwaje huu ni uhuni kulazimisha watu waje na barua ya mjumbe wa nyumba 10 na kama ikitokea hamuivi kiitikadi unadhani atakuhudumia ipasavyo?

Lakini nijuavyo mimi Mwenyekiti wa mtaa au kijiji anachaguliwa na wananchi wa mtaa wake
Sasa kama nyinyi mlimchagua wa chama ambacho hukipendi hiyo haimhuusu huyo karani

Tatizo letu wakati wa uchaguzi/upigaji wa kura wa hao viongozi wa chini kabisa huwa hatushiriki na wala hatutaki kuwajua na hata kujua majukumu yao
 
mie naishitabata washanicharge elfu 2 ajili ya kujiandikisha sabab ya muda siku hiyo sikufanikiwa nkaenda siku mbili baada ya hapo,wakaniambia eti karatasi waliyonipa imechanika so nitoe elf 2 nyingine waibadilishe nikaondoka zango kesho ntajitutumua niende na cheti cha ubatizo ndo nilicho nacho vingine vimepotea nione wataniambia upmnbav gani wakinizingua nakula kona sijiandikishi huo mda wa mtu kuzungukia serikali aza mitaa kila mda anawatu hatuna pesa mifukoni ntaupata wapi af hawa wamama wanaongea utadhani wamekunywa ma.v pambav i hate this country kwakwli

Pole mkuu kwa yaliyokukuta, ndio serikali ya CCM hiyo na vimbwanga vyake!!!

Tiba
 
nenda mara ya pili kuulizia tana lakini mara hii jaribu kurekodi na kamchina kako mazungumzo yako na hao wahusika wa sensa na huyo balozi wa ccm halafu uyabandike hapa jf...hawa watu wanatakiwa waanikwe kwa sababu haiwezekani zoezi hilo hilo la aina moja likaendeshwa kwa njia tofauti tofauti...mimi sikupata shida na ilinichukua kama dk 30 hivi kumaliza zoezi lote na nilikuwa na copy ya passport na ya kitambulisho cha kupigia kura tu...!

Asante mkuu kwa ushauri. Hawa jamaa wa ubungo mziwa wametengeza mradi wa kupata pesa kwani hata kwa balozi barua haitoki hivi hivi bila kutoa elfu mbili. Pamoja na passport na cheti cha kupiga kura nilikuwa na vyeti vya shule vile vile lakini binti alisisitiza anataka barua ya balozi wa CCM.

Hiyo ndio Tanzania Bwana, kila mmoja anaamua lake wakati zoezi ni hilo hilo moja!!!

Tiba
 
Lakini nijuavyo mimi Mwenyekiti wa mtaa au kijiji anachaguliwa na wananchi wa mtaa wake
Sasa kama nyinyi mlimchagua wa chama ambacho hukipendi hiyo haimhuusu huyo karani

Tatizo letu wakati wa uchaguzi/upigaji wa kura wa hao viongozi wa chini kabisa huwa hatushiriki na wala hatutaki kuwajua na hata kujua majukumu yao

Mkuu bahati nzuri mwenyekiti wa serikali ya mtaa tunafahamiana vizuri na tumeishi mitaa ile kwa zaidi ya miaka 20 sasa. Ningetakiwa nilete barua kutoka kwake isingekuwa tatizo, shida binti alisistiza nipeleke barua ya balozi tu, aliseam hiyo ya serikali ya mtaa haitaki!!!! Haya ndio maajabu ya musa!!!!

Tiba
 
Mkuu umejitahidi kueleza vizuri lakini umepoteza point ulipodai wajumbe wa nyumba 10 ni watendaji wa serikali. Hii imeanza lini? Hawa wajumbe wanapatikana vipi? Nipe hayo majibu kwanza, halafu tuendelee!!!!

Tiba

Hii inadhihirisha jinsi usivyo mshiriki wa mambo yanayoihusu jamii yako. Mjumbe wa nyumba kumi huchaguliwa na wananchi na ndio maana hapa kwetu mjumbe wetu ni mwanachama wa CUF na ofisi ya serikali ya mtaa inamheshimu regardless ya chama chake.

Tatizo letu ni kwamba, wengi wetu tuna mentality za ajabu za kudhania kwamba, kujihusisha na mambo ya jamii yako ni dalili ya kutosoma.
 
mbona unatumia lugha yenye jazba?.kwani ukiongea kwa upole na unyenyekevu hatakuelewa? yote uliyojifunza hapa duniani, ungefundishwa kwa maneno makali namna hii ungelielewa?. kama unafahamu jambo, basi ujisikie fahari kumuelimisha mwingine, na hii fahari uipate pale anapokuonyesha amekuelewa. lakini unaonekana upo ktk msingi wa kumkosoa zaidi tena kwa kuonyesha namna gani hawezi kuwa kama wewe, na si namnagani ungelitaka awe kama wewe.

Fuatilia post zake and try to read btn the lines. Kinachomsumbua ni superiority complexion. Anaamini yeye ni mtu fulani asiyehitaji kujinyenyekeza kwa mjumbe wa nyumba kumi kwa kuwa yeye amesoma na in most cases wajumbe hawa ni watu wazee ambao kwa aina ya utumishi wa kazi yenyewe, huwa ni wale wasio na shughuli.

Sina lugha nyingine ya kuongea na mtu wa namna hii ili apate kujua makosa yake.

Au na wewe una akili fupi kiasi udhanie kuwa kwa kuangalia cheti chako cha chuo, karani anaweza kufahamu uhalali wa ukaazi wako katika mtaa husika?
 
Wacha mawazo ya ku support a totalitalian structure. Mjumbe wa nyumba kumi ni style ya wakomunisti ya watu ku keep tabs kwa wananchi wake. Nani ana print subversive material, nani ni "enemy of the state" and some bull like that.

Na kama mjumbe wa nyumba kumi ni muhimu hivyo kwa nini asiwe neutral asiye na chama? Na CHADEMA nao wakisema wana mjumbe wao wa nyumba kumi akamtambua mtu ambaye mjumbe wa CCM hamtambui hapo itakuwaje?

Habari ya mjumbe wa nyumba kumi ilikuwa na mshiko enzi za chama kushika hatamu, ukitaka daftari la kusainiwa kupata unga wa muhogo kilo mbili kwa wiki za ugawaji shurti upitishwe na mjumbe wa nyumba kumi etc.

Sasa hivi katika mfumo wa vyama vingi, huwezi kulazimisha mtu wa CHADEMA aende kwa mjumbe wa CCM.

Ni sawasawa na kulazimisha muislamu atambulishwe na mchungaji wa kanisa la karibu.Utamkosea heshima muislamu huyu na huenda hata salamu zikagongana, muislam anasema "Wasalaam Aleikum" Mchungaji anasema "Bwana asifiwe".

Mimi sijakuelewa unakosoa muundo au unaukataa umuhimu wa wajumbe wa nyumba 10?

Hilo jina la WAJUMBE WA CCM ni mapokeo, lkn hapa anayezungumziwa ni Balozi wa Nyumba kumi. Hapa ninapoishi miaka mingi alikuwa ni mama mmoja wa CCM lkn mwaka juzi tulimchagua Babu Muha ambaye ni CUF. Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wetu ni CHADEMA na wajumbe wa serikali ni vyama mchanganyiko. Sasa mimi sijaelewa kinakuuma wapi mjumbe akiwa CCM.

Tuache akili za kitoto. Cha msingi hapo kwenu ni kuitisha uchaguzi mpya wa mjumbe na wewe ugombee kwa tiketi ya chama chako. Sisi tulimchagua Babu Muha wa CUF kwa mapenzi yetu na anatuwakilisha, sasa wewe usiyejua mjumbe wako alichaguliwa na nani unalalamika nini kama sio utoto?

Akili zetu ndio hizi, hatutaki kugombea, hatuendi kuchagua lkn ataechaguliwa tunampinga kwenye majukumu na kujiita wasomi, ndio nini sasa?
 
kama tunadhani wajumbe wa nyumba 10 ni muhimu basi waajiriwe kama wale watendaji wa mitaa na wasifungamane na chama chochote cha siasa, unadhani kila chama kikiwa na mjumbe wa nyumba 10 itakuwaje huu ni uhuni kulazimisha watu waje na barua ya mjumbe wa nyumba 10 na kama ikitokea hamuivi kiitikadi unadhani atakuhudumia ipasavyo?

Ujinga wetu ndio huu, kujaribu ku-complicate kila kitu kwa kuwa tu hakiko in our favor. Sasa sisi kwetu balozi wetu ni mwanachama wa CUF, ina maana na sisi wa CDM tumkatae?

Mwenyekiti wa serikali ya mtaa ni CDM, ina maana na wenzetu wa CCM na CUF wamkatae?

Kama una akili zitumie, yule mkuu wa mkoa wenu ni wa chama chako? Kama si wa chama chako, that means hamuivi kiitikadi, je umeshamkataa? Vipi kuhusu diwani na mbunge, wote ni wa chama chako?

Kabla hujabishana jaribu kufikiri. Mimi hapa nazungumzia UMUHIMU WA WAJUMBE WA NYUMBA KUMI. Hao wajumbe wa CCM unawajua wewe na wasomi wenzio ambao mnadhani cheti na passport kinaweza kukutambulisha unakaa mtaa gani.
 
Mkuu, walipita siku gani? Mimi sikai nyumbani kusubiri kuandikishwa ndugu yangu, nina mihangaiko kibao hapa mjini. Nikitoka saa 12 asubuhi narudi wakati mwingine usiku mwingi.

Tiba

Umeona sasa jinsi akili nyingi na ujuaji unavyoponza? Na haya ndio niliyoyaita majivuno na tambo za USOMI NJAA. Hivi unataka kuniambia mtaani kwenu ni wewe tu ndio mwenye ajira?

Haya ndio madhara ya kutokuwa karibu na jamii inayokuzunguka. Sawa hukuwepo, lkn una majirani na huyo mjumbe wa nyumba kumi alikuwa na makarani waliopita kuandikisha. Nijuavyo mimi, kwa maeneo ambayo watu ni washiriki wazuri wa shughuli za kijamii, hufahamiana na kupeana habari.

Nachokiona, una majivuno na kujitenga kwingi. Sawa, hukujua juu ya hili zoezi kwa kuwa huelewani na mjumbe wako, vipi kuhusu vyanzo vingine vya habari. Suala la NIDA limekuwepo hata hapa jamvini, sasa wewe ulitaka serikali ikutengee karani maalum ili akuvizie siku ambayo hujaenda kwenye shughuli zako au?
 
Mimi sijakuelewa unakosoa muundo au unaukataa umuhimu wa wajumbe wa nyumba 10?

Hilo jina la WAJUMBE WA CCM ni mapokeo, lkn hapa anayezungumziwa ni Balozi wa Nyumba kumi. Hapa ninapoishi miaka mingi alikuwa ni mama mmoja wa CCM lkn mwaka juzi tulimchagua Babu Muha ambaye ni CUF. Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wetu ni CHADEMA na wajumbe wa serikali ni vyama mchanganyiko. Sasa mimi sijaelewa kinakuuma wapi mjumbe akiwa CCM.

Tuache akili za kitoto. Cha msingi hapo kwenu ni kuitisha uchaguzi mpya wa mjumbe na wewe ugombee kwa tiketi ya chama chako. Sisi tulimchagua Babu Muha wa CUF kwa mapenzi yetu na anatuwakilisha, sasa wewe usiyejua mjumbe wako alichaguliwa na nani unalalamika nini kama sio utoto?

Akili zetu ndio hizi, hatutaki kugombea, hatuendi kuchagua lkn ataechaguliwa tunampinga kwenye majukumu na kujiita wasomi, ndio nini sasa?

Mie sina chama na kwetu hakuna upuuzi huu wa wajumbe wa nyumba kumi kwani hatuamini katika ukomunisti wa chama na serikali ku monitor wananchi kama ng'ombe.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom