Tanzania: Vyeti bandia, elimu za kununua na watumishi vihiyo

Naomba kutoa hoja kwa wanafamilia wa JF,mimi naona kuna ulazima kwa mamlaka husika kuunda tume itakayoshirikisha wakuu wa vyuo vyote vilivyopo hapa nchini na kuwasiliana na wale wa vyuo vya nje ili kufahamu au kujilizisha na vyeti vya baadhi ya waajiriwa serikalini, juzi tumesikia waheshimiwa wawili tena wenye vyeo vya juu wakituhumiwa kwa kuwa na vyeti bandia na hivyo elimu yao kutilia shaka, mimi naamini si hao tu wapo wengi wenye vyeti bandia au vya marehemu wakivitumia kujipatia ajira isiyowahusu, Tanzania haiwezi kuendelea, mtu mwenye cheti bandia hata kazi zake nazo ni bandia tuuu...

Yaani hii ndivyo inavyoonekana si ajabu tunabaki tunashangaa taifa limejaa viongozi wasomi mbona amna maendeleo kumbe wengi bandia tu.

Ndio maana wasomi wa-kweli huwekwa kwenye mabalozi yetu ugenini na hawa bandia ndio wame jaa humo serikalini. Its about time nakubaliana na mapendekezo yako moja kwa moja, lakini je is it possible kwetu kufanya hilo jambo.
 
Digrii ya mlimani haitambuliki Marekani.Kama mtu ameridhika kupata digrii yake mahali popte kinachowauma ni nini.Mimi nina digrii ya mlimani haikuweza kukubalika hapa USA.Naombeni mnieleze maana ya digrii kukubalika au kutokubalika.
 
Kuhusu hizo digrii mnazozita feki naomba pigeni simu 1-877-566 7226 .Muwaulize dukuduku zenu.
 
Matata,

Inabidi nikupe picha kamili ya biashara hii ya Elimu nchi hizi za magharibi. Virgin Islands bado dunia ya tatu kwa hiyo vitu kama hivi lazima watu wanaona kama miujiza ya Mussa.

Kuna kitu kinaitwa University without walls (UWW). Hapa labda nikupe mfano kwa nyumbani.

Mfanyabiashara mmoja aamuwe kuwakusanya maprofesa wetu ktk masomo mbali mbali toka baadhi University na kuweka utaratibu wa mafundisho, nidhamu na n.k kwa kuzingatia ngazi zote za ufundishaji toka Universities nyingine. Kisha kundi hili wasajiri kampuni hiyo ktk wizara ya Elimu kama wanavyosajili hizo zahanati hapo Dar hali madaktari wake ni wafanya kazi wa Muhimbili au Hindu Mandal...

Kwa hiyo usajiri unakuwa kama Open university yaani masomo kwa njia ya Mtandao! hapa nadhjani ndipo wengi wanapote kwani tumezoea kuona zahanati nje ya hospital.. lakini nchi hizi kuna madaktari ambao wamesajiri Udaktari na huendesha shughulki zao nje ya Hospital au Zahanati. Hospital yake ipo mkobani, na address ni nyumbani kwake...na simu yake. Anywaya kufupisha story nirudi ktk mada, Baada ya usajiri wa hii Association hawa jamaa waitangazaeTZ nzima kama University ambayo huna haja ya kukaa darasani lakini maprofesa wote wakali wa UDSM wapo ndani kukusomesha kwa kupitia Mtandao. Hapa mshikaji hakuna majengo ila software yao yenye kila hatua ya mafunzo (publishers of materials) pia kuna huduma za online, multimedia, text kwa mtanzao na video, pia e-learning.

Yote haya yanatengenezwa hususan kwa elimu fulani na wataalam kwa kushirikiana na hao walimu wake. Sijui kama bado nipo na wewe?...

Sasa nirudi ktk swala la COU. Mwenye kila kitu hapa ni British learning Association (BLA) toka Uingereza ambao ndio wenye vitu vyonse!.. kisha wao huuza membership kwa mtu yeyote duniani mwenye kutaka kuwasaidia watu ktk elimu... iwe ngumbaru ama wale ambao hawakujaliwa kuwa na uwezo wa kulipia elimu. Yaani iwe na malengo ya kutoa huduma ya elimu kwa wananchi.. imekuwa kama mfano wa franchise kwa hiyo COU wao wamejiunga na BLA ili kupata ile UWW... kisha wanauza elimu hiyo kwa watu dunia nzima. Unaweza kukuta COU ina wanafunzi 200,000 across the world kila mwaka, na wote wanasoma kupitia mtandao na hupewa kasha la -CD (software) ambazo zitakuchukua wewe hatua kwa hatua na pia utajadili muda wa mafunzo yako toka hapo ulipo. Mathalan ukisema wewe upo Dar basi wao huwa na profesa wao ktk mitaa hii ambaye huchukua muda kukusaidia. Na kila anapokusaidia huingiza zake inategemea.

Kwa hiyo, COU kweli wamesajiri Virgin Islands kwa sababu ya kodi maanake wanazichota kishenzi. Mapato kama yao Uingereza, Marekani na nchi yeyote ile ya Kibepari wangeshika adabu maanake hawa jamaa hawana matumizi zaidi ya kulipia software ambayo BLA wameitengeneza. Hizi software zinauzwa kwa mamillioni sio kama windows na kila mwaka hufanyiwa marekebisho ama kutolewa toleo jipya. Huwezi kuipata software hiyo unless wewe ni member wa hiyo association.

Kwa hiyo COU wao hawana haja ya kuwepo Virgin Islands kwani lecturer wote wapo karibu na wewe popote duniani. Na kinachokuunganisha wewe na hao lecturer ni hiyo software kama vile unavyoingia MSN ama yahoo! Hapo COU hawapo tena wameisha kusanya mapeni na kazi yao ni kuwalipa hao maprofesa kwa kila kazi wanayoifanya...

Nadhani haya yametosha kwa lleo.


Mkandara kadigrii kako feki nini????????

Issue iko wazi, chuo hakitambuliki,watu wameenda mele zaidi kuwa hicho chuo hakipo wewe unakomalia. Kuna vyuo vinavyotoa distance learning na vanatambulika. Chuo lazima kiwe na ofisi hata kama hakina madarasa otherwise ndipo kinakuwa feki.

Kama elimu itakuwa hivyo basi kutakuwa hakuna umuhimu wa kusoma. Elimu lazima iwe regulated,hatuwezi kuwa na chuo kikuu ambacho hakiwi regualated na taasisi yoyote.

Mfano open university of Tanzania watu wanasoma distance learning lakini wana ofisi zao na wanakuwa regulated. Vinginevyo basi hata mimi ningeanzisha chuo kesho tu kwenye mtandao halafu naanza kula pesa za watu,kwani elimu ni biashara inayolipa sana ukichukulia watu wengi wanataka elimu.
 
Ahsante ndugu mjumbe kwa taarifa hii, naomba pia utoe maoni yanu kuhusu matokeo ya kidato cha nne mwaka huu hapa Tanzaia ukizingatia kwa makini na kwa upeo ulitukuka kuwa ni 17.53% tu ya watahiniwa ndo wana daraja la kwanza mpaka la tatu hao wengine ni daraja la nne na sifuri!!! je taifa linaelekea wapi katika elimu???
 
mungu wangu hawa watu wanacheza na taaluma za watu ila hawatafika mbali mana aliyenunua degdee hata thinking capacity yake na performance ni ndogo na hata akipewa uwaziri atabofoa hahahaaaaaaaa wapo wengi wafichueni jamani wenye sifa wanakosa ajirasababu yao na ndio wanaoturudisha nyuma kila siku
 
Jamani ajira imekuwa ngumu sana hapa nchini na vijana wengi tuna Degree na Adv Diploma au Diploma na hatuna kazi, lakini bado Serikali inawakumbatia Wanajeshi na Mapolisi wenye vyeti vya kugushi. Ukiwa kama mkeleketwa ambae unapinga UFISADI wa Elimu, Tupia majina ya watu au watoto wa vigogo wanaotumia Vyeti vya ndugu, marehemu au marafiki ili waanze kukimbia kabla ya sisi ambao hatuna kazi na degree zetu hapa mtaani hatujaanza kuwachomoa maofisini. Na hapo hawajawafikia Walimu na Manesi! Hapo itakuwa balaa

Naomba muweke hayo majina bila uoga maana bila kulikomalia litazimika kama Richmond, Kagoda a.K.a EPA, na wamesitisha kutoa hivyo vitambulisho ili wachakachue watoto wao waendelee kupeta mawizarani, inakera na inauma sanaaa.

Tanzania tunaelekea wapi? Usije shangaa hata mawaziri wanatumia vyeti vya watu!

Changia bila matusi

Mimi ya kwangu nitayaweka baada ya watu kuchangia, ninao watatu na wapo Serikalini
 
Mkuu Ta Kamugisha,kama sijakuchanya basi utanisahihi wewe si ndio huwa unashadadia CCM? Sasa unakuaje unakosa kazi hawajakupa mshahara?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Ta Kamugisha,kama sijakuchanya basi utanisahihi wewe si ndio huwa unashadadia CCM? Sasa unakuaje unakosa kazi hawajakupa mshahara?

Kaka nadhani wewe si msomaji wa nakala zangu katika Jf, niliweka wazi kuwa nimejiondoa CCM na nabaki mwanachama huru, kwa sasa sina chama na niliorodhesha sababu za kutoka CCM
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom