Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,316
- 33,125
8th July 2009
Vyandarua.
Hakuna ubishi kwamba pamoja na ukimwi kuwa ni ugonjwa hatari kuliko magonjwa yote kwa sasa kutokana na kutokuwa na chanjo wala tiba, bado ugonjwa wa malaria unaongoza kwa kuua watu wengi zaidi nchini na kwa nchi zote za ukanda wa kitropiki.
Kwa maana hiyo, juhudi za kutokomeza malaria si tu zinatakiwa ziongezwe zaidi ili kuokoa maisha ya watu wetu hasa watoto wadogo walio chini ya umri wa miaka mitano, bali pia sera za kukabiliana na ugonjwa huu inabidi zitazamwe kwa umakini zaidi ili kuleta matokeo bora zaidi kwenye jamii.
Juzi, Mganga Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Deo Mutasiwa, alitangaza programu kabambe ya serikali kwa kushirikiana na wafadhili wa Benki ya Dunia, Serikali ya Marekani na Global Fund, ya kugawa vyandarua viwili vilivyowekwa dawa ya kuua mbu kwa familia milioni 14 nchini kote.
Mpango huo unaotarajia kuanza mwakani, unalenga kupunguza maambukizi ya malaria na hivyo kupunguza vifo vinavyotokana na ugonjwa huo ambao bado ni tishio kwa uhai wa wananchi wengi.
Inakadiriwa kwamba mkakati huu wa kugawa vyandarua vya mbu utagharimu Dola za Marekani milioni 100 sawa na Sh. bilioni 120.
Tungependa kuchukua fursa hii kupongeza juhudi hizi za kugawa vyandarua kwa wananchi, hasa kwa sababu vitatolewa bure, hapana shaka uamuzi huu umezingatia uwezo wetu kwa maana hiyo kila familia kati ya hizo milioni 14 zitapata vyandarua viwili hivyo kusaidia kuwakinga wanafamilia na mbu waenezao malaria.
Pamoja na kuunga mkono juhudi hizi, tumejiuliza maswali mengi pia juu ya uamuzi huo. Tunafahamu kwa hakika kabisa kwamba ili kuondokana kabisa na malaria njia sahihi zaidi ni kuangamiza mbu wote.
Kama nguvu kubwa zaidi ikielekezwa kuangamiza mbu, kwa kuharibu mazalia yake; kama kufukia madimbwi, kuweka makazi katika mazingira ya usafi na kunyunyuzia dawa katika mabwawa ya maji machafu, uwezekano wa kupunguza mbu ni mkubwa zaidi na hivyo kupunguza madhara yake kwa binadamu.
Ndiyo maana tunapotafakari kwa kina mpango mzima wa kugawa vyandarua vyenye dawa tunapata jibu moja kwamba maambukizi ya malaria hutokea kitandani tu wakati watu wamelala.
Ni dhahiri, wapo watu wanaoumwa na mbu sehemu za kazi, wakiwa kwenye mazungumzo ukumbini nyumbani, wakiwa kwenye malindo usiku au hata wakiwa baa wakijiburidisha.
Kwa kuwa si rahisi kutembea na chandarua chenye dawa kila mahali ambako kuna uwezekano wa kuumwa na mbu, basi ni dhahiri matokeo ya kuvitumia ili kupunguza maambukizi ya maradhi hayo hayawezi kuwa ya kiwango cha juu sana.
Ni kwa kutambua ukweli huu tunadhani njia ya kweli na ya uhakika ya kukabiliana na malaria ni kuangamiza mbu kwa kuharibu mazalia yake.
Kutumia vyandarua vyenye dawa kunaweza tu kupunguza kwa asilimia kidogo maambukizi ya ugonjwa huo, lakini kwa uhakika hakuwezi kutokomeza malaria kabisa.
Kwa msingi huu basi pamoja na juhudi za kugawa vyandarua viwili bure kwa familia milioni 14, ambavyo hata hivyo havitoshi kwa wanafamilia wote kutokana na wengine kuwa na idadi kubwa ya watu; nguvu pia zielekezwe kwenye kuharibu mazalia ya mbu.
Hatutaki kuamini kwamba serikali haijui kwamba kugawa vyandarua vya bure pekee hakutatokomeza malaria nchini, inajua jambo muhimu na la msingi ni kuharibu mazalia ya mbu hivyo kuteketeza wadudu hao moja kwa moja.
Tunajua, mpango huu ni msaada na kwa maana hiyo mwenye kupewa hana chaguo, hupokea kile alichopewa, lakini tukumbuke kuwa ni vema kuwa na mipango yetu inayojitegemea katika kukabiliana na malaria tukilenga kuangamiza mbu kwanza.
Tujiepushe na mipango ambayo mwisho wa yote itatugeuza kuwa soko za bidhaa za kukabiliana na malaria kama dawa, vyandarua na vitu vingine vinavyofanana na hivyo. Tuamke sasa na kujipanga vizuri.
CHANZO: NIPASHE
Vyandarua.
Hakuna ubishi kwamba pamoja na ukimwi kuwa ni ugonjwa hatari kuliko magonjwa yote kwa sasa kutokana na kutokuwa na chanjo wala tiba, bado ugonjwa wa malaria unaongoza kwa kuua watu wengi zaidi nchini na kwa nchi zote za ukanda wa kitropiki.
Kwa maana hiyo, juhudi za kutokomeza malaria si tu zinatakiwa ziongezwe zaidi ili kuokoa maisha ya watu wetu hasa watoto wadogo walio chini ya umri wa miaka mitano, bali pia sera za kukabiliana na ugonjwa huu inabidi zitazamwe kwa umakini zaidi ili kuleta matokeo bora zaidi kwenye jamii.
Juzi, Mganga Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Deo Mutasiwa, alitangaza programu kabambe ya serikali kwa kushirikiana na wafadhili wa Benki ya Dunia, Serikali ya Marekani na Global Fund, ya kugawa vyandarua viwili vilivyowekwa dawa ya kuua mbu kwa familia milioni 14 nchini kote.
Mpango huo unaotarajia kuanza mwakani, unalenga kupunguza maambukizi ya malaria na hivyo kupunguza vifo vinavyotokana na ugonjwa huo ambao bado ni tishio kwa uhai wa wananchi wengi.
Inakadiriwa kwamba mkakati huu wa kugawa vyandarua vya mbu utagharimu Dola za Marekani milioni 100 sawa na Sh. bilioni 120.
Tungependa kuchukua fursa hii kupongeza juhudi hizi za kugawa vyandarua kwa wananchi, hasa kwa sababu vitatolewa bure, hapana shaka uamuzi huu umezingatia uwezo wetu kwa maana hiyo kila familia kati ya hizo milioni 14 zitapata vyandarua viwili hivyo kusaidia kuwakinga wanafamilia na mbu waenezao malaria.
Pamoja na kuunga mkono juhudi hizi, tumejiuliza maswali mengi pia juu ya uamuzi huo. Tunafahamu kwa hakika kabisa kwamba ili kuondokana kabisa na malaria njia sahihi zaidi ni kuangamiza mbu wote.
Kama nguvu kubwa zaidi ikielekezwa kuangamiza mbu, kwa kuharibu mazalia yake; kama kufukia madimbwi, kuweka makazi katika mazingira ya usafi na kunyunyuzia dawa katika mabwawa ya maji machafu, uwezekano wa kupunguza mbu ni mkubwa zaidi na hivyo kupunguza madhara yake kwa binadamu.
Ndiyo maana tunapotafakari kwa kina mpango mzima wa kugawa vyandarua vyenye dawa tunapata jibu moja kwamba maambukizi ya malaria hutokea kitandani tu wakati watu wamelala.
Ni dhahiri, wapo watu wanaoumwa na mbu sehemu za kazi, wakiwa kwenye mazungumzo ukumbini nyumbani, wakiwa kwenye malindo usiku au hata wakiwa baa wakijiburidisha.
Kwa kuwa si rahisi kutembea na chandarua chenye dawa kila mahali ambako kuna uwezekano wa kuumwa na mbu, basi ni dhahiri matokeo ya kuvitumia ili kupunguza maambukizi ya maradhi hayo hayawezi kuwa ya kiwango cha juu sana.
Ni kwa kutambua ukweli huu tunadhani njia ya kweli na ya uhakika ya kukabiliana na malaria ni kuangamiza mbu kwa kuharibu mazalia yake.
Kutumia vyandarua vyenye dawa kunaweza tu kupunguza kwa asilimia kidogo maambukizi ya ugonjwa huo, lakini kwa uhakika hakuwezi kutokomeza malaria kabisa.
Kwa msingi huu basi pamoja na juhudi za kugawa vyandarua viwili bure kwa familia milioni 14, ambavyo hata hivyo havitoshi kwa wanafamilia wote kutokana na wengine kuwa na idadi kubwa ya watu; nguvu pia zielekezwe kwenye kuharibu mazalia ya mbu.
Hatutaki kuamini kwamba serikali haijui kwamba kugawa vyandarua vya bure pekee hakutatokomeza malaria nchini, inajua jambo muhimu na la msingi ni kuharibu mazalia ya mbu hivyo kuteketeza wadudu hao moja kwa moja.
Tunajua, mpango huu ni msaada na kwa maana hiyo mwenye kupewa hana chaguo, hupokea kile alichopewa, lakini tukumbuke kuwa ni vema kuwa na mipango yetu inayojitegemea katika kukabiliana na malaria tukilenga kuangamiza mbu kwanza.
Tujiepushe na mipango ambayo mwisho wa yote itatugeuza kuwa soko za bidhaa za kukabiliana na malaria kama dawa, vyandarua na vitu vingine vinavyofanana na hivyo. Tuamke sasa na kujipanga vizuri.
CHANZO: NIPASHE