Ndani ya CUF kunafuka moshi mweusi unaotishia uhai wa chama hicho...kikubwa kinachosababisha mgogoro huo ni ulafi na uroho wa madaraka. Hamad Rashid anasigana na viongozi wakuu wa chama akiwamo katibu mkuu wake SEIF SHARIFF HAMAD baada ya Hamad Rashid kutangaza kuutaka ukatibu mkuu. Hali kama hiyo inaendelea ndani ya NCCR ambapo David Kafulila na wenzake wamefukuzwa uanachama baada ya kumtaka mwenyekiti wao aachie ngazi kwa kuwa amekidhoofisha na amekosa mvuto.kikubwa hapa ni baada ya Kafulila kuonekana kuutaka uenyekiti wa NCCR.kafulila alinyang'anywa madaraka CHADEMA akaamua kutimkia NCCR.Mwenyekiti wa TLP Augostino Lyatonga Mrema nae hivi karibuni amemtimua katibu mkuu wake JESSE Makundi pamoja na naibu katibu mkuu Hamad Tao.Katika CHADEMA siku za hivi karibuni tumeshuhudia chama hicho kikiwafukuza uanachama madiwani wake watano huko Arusha kitendo kilichowafanya wakose nafasi hizo.yote haya yanatokea huku kila mhusika katika mgogoro akidai ndie ana haki lakini upande unaopingana nae unamuonea.
My take; Je vyama vya upinzani ni taasisi za kujipatia madaraka ili kujipatia ulaji?
My take; Je vyama vya upinzani ni taasisi za kujipatia madaraka ili kujipatia ulaji?