hKichaka
Senior Member
- Apr 23, 2011
- 199
- 19
Thursday, 28 April 2011 21:04 Elizabeth Suleyman
UMOJA wa vyama vya Upinzani Mkoa wa Dodoma, umemwandikia barua Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu( Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi ukitaka ujibiwe hoja yao ya kuondolewa kwa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma(CDA) waliyodai waliitoa kwa maandishi.
Wapinzani hao walidai CDA imewekwa kwa tamko la serikali na maslahi ya wachache, huku ikiwafanya wananchi wa mkoa huo kuishi kwa hofu ya kuporwa ardhi yao.
Katika barua ya umoja wa wapinzani hayo kwenda kwa Lukuvi yenye kumbukumbu namba NCCR_ M/KM/DOM/05/011 ambayo alidai ilifikishwa ofisi ya Waziri jana hiyo jijini Dar es Salaam ilisema wanaomba kupata majibu ya hoja za kuondolewa kwa CDA.
Ilisema CDA inaonekana kuwanyima uhuru na haki wananchi wa Dodoma kwa kuwa haifanyi kazi kwa ajili ya wananchi na badala yakena kwamba wananchi wanataka wahudumiwe na Manispaa yao kama ilivyo katika maeneo mengi nchini.
Akizungumza jana na gazeti hili, Mwenyekiti wa Umoja unaovihusisha vyama vya CUF, TLP na UPDP, Kayumbo Kabutali alisema, lengo la kuandika barua hiyo ni kushinikiza, CDA iondolewe kwasababu haifanyi kazi kwa ajili ya maslahi ya wananchi bali ni ya CCM.
"Lengo la kuandika barua hii, kwa Waziri ni kuomba CDA iondolewe haraka kwa mujibu wa sheria, kwasababu iko kwa ajili ya maslahi ya CCM na sio wananchi," alisema Kabutali na kuongeza:
"Hivi sasa wananchi wameingiwa na hofu kubwa ya kutaka kuporwa ardhi yao kwa kuondolewa kwenye maeneo yao, kuvunjiwa nyumba bila kulipwa fidia kitendo ambacho kinawanyima haki zao kama binadamu,"alisema.
Kabutali aliongeza kuwa, kazi zinazofanywa na Halmashauri ya Manispaa Dodoma hazina tofauti na za CDA, hivyo uwepo wake ni kutaka kuwanyonya wananchi ardhi yao yenye ekari zaidi ya 276, 910 kwa kudai kuwa wanataka kuupanua mji huo uwe mji mkuu.
Alisema ukiangalia uwezo wa katiba ibara ya 64(5) inasema ...itakuwa nguvu ya kisheria katika Jamhuri nzima endapo sheria yoyote itakiuka masharti yaliyomo katika Katiba, hivyo sheria ya kuanzisha Manispaa na CDA kwa mujibu wa katiba ya mwaka 1977, zinaonyesha kuwa zinafanya kazi zinazofanana zikijinadi zipo kisheria.
"Kitendo cha kuwepo kwa CDA na halmashauri ni kusababisha usumbufu kwa wananchi wa Dodoma hususan masuala ya ardhi na kuwafanya kuishi maisha ya kubahatisha kwa kutofahamu ni kipi kinaendelea juu ya ardhi siku zijazo,"
"Hivyo tunalazimika kuandika barua hii, ili kuutaarifu umma kwamba kurudi katika Katiba ya nchi ya 1977, ibara 64 (5), tutaona nani hayuko kisheria zaidi na anambana mwenzake na anafaa aondolewe,"alisisitiza.
Alisema, baada ya kuwasilisha barua hiyo kama umoja uliamua kuazisha mtandao wa sauti ya wana wana Dodoma ambapo wamepanga kufanya maandamano Juni 16, mwaka huu baada ya kikao cha bajeti kuanza, ili kushinikiza CDA iondolewe.
UMOJA wa vyama vya Upinzani Mkoa wa Dodoma, umemwandikia barua Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu( Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi ukitaka ujibiwe hoja yao ya kuondolewa kwa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma(CDA) waliyodai waliitoa kwa maandishi.
Wapinzani hao walidai CDA imewekwa kwa tamko la serikali na maslahi ya wachache, huku ikiwafanya wananchi wa mkoa huo kuishi kwa hofu ya kuporwa ardhi yao.
Katika barua ya umoja wa wapinzani hayo kwenda kwa Lukuvi yenye kumbukumbu namba NCCR_ M/KM/DOM/05/011 ambayo alidai ilifikishwa ofisi ya Waziri jana hiyo jijini Dar es Salaam ilisema wanaomba kupata majibu ya hoja za kuondolewa kwa CDA.
Ilisema CDA inaonekana kuwanyima uhuru na haki wananchi wa Dodoma kwa kuwa haifanyi kazi kwa ajili ya wananchi na badala yakena kwamba wananchi wanataka wahudumiwe na Manispaa yao kama ilivyo katika maeneo mengi nchini.
Akizungumza jana na gazeti hili, Mwenyekiti wa Umoja unaovihusisha vyama vya CUF, TLP na UPDP, Kayumbo Kabutali alisema, lengo la kuandika barua hiyo ni kushinikiza, CDA iondolewe kwasababu haifanyi kazi kwa ajili ya maslahi ya wananchi bali ni ya CCM.
"Lengo la kuandika barua hii, kwa Waziri ni kuomba CDA iondolewe haraka kwa mujibu wa sheria, kwasababu iko kwa ajili ya maslahi ya CCM na sio wananchi," alisema Kabutali na kuongeza:
"Hivi sasa wananchi wameingiwa na hofu kubwa ya kutaka kuporwa ardhi yao kwa kuondolewa kwenye maeneo yao, kuvunjiwa nyumba bila kulipwa fidia kitendo ambacho kinawanyima haki zao kama binadamu,"alisema.
Kabutali aliongeza kuwa, kazi zinazofanywa na Halmashauri ya Manispaa Dodoma hazina tofauti na za CDA, hivyo uwepo wake ni kutaka kuwanyonya wananchi ardhi yao yenye ekari zaidi ya 276, 910 kwa kudai kuwa wanataka kuupanua mji huo uwe mji mkuu.
Alisema ukiangalia uwezo wa katiba ibara ya 64(5) inasema ...itakuwa nguvu ya kisheria katika Jamhuri nzima endapo sheria yoyote itakiuka masharti yaliyomo katika Katiba, hivyo sheria ya kuanzisha Manispaa na CDA kwa mujibu wa katiba ya mwaka 1977, zinaonyesha kuwa zinafanya kazi zinazofanana zikijinadi zipo kisheria.
"Kitendo cha kuwepo kwa CDA na halmashauri ni kusababisha usumbufu kwa wananchi wa Dodoma hususan masuala ya ardhi na kuwafanya kuishi maisha ya kubahatisha kwa kutofahamu ni kipi kinaendelea juu ya ardhi siku zijazo,"
"Hivyo tunalazimika kuandika barua hii, ili kuutaarifu umma kwamba kurudi katika Katiba ya nchi ya 1977, ibara 64 (5), tutaona nani hayuko kisheria zaidi na anambana mwenzake na anafaa aondolewe,"alisisitiza.
Alisema, baada ya kuwasilisha barua hiyo kama umoja uliamua kuazisha mtandao wa sauti ya wana wana Dodoma ambapo wamepanga kufanya maandamano Juni 16, mwaka huu baada ya kikao cha bajeti kuanza, ili kushinikiza CDA iondolewe.