Dhana ya upinzani ni ngeni, bado haijaeleweka vizuri kwa wapinzani wenyewe na kwa Serikali zilizo madarakani. Wengi wa wapinzani wametoka kwenye vyama tawala kwa maana ya Serikali kwa kutokubaliana na viongozi waliokuwa maswahiba wao kwa maana hiyo wanafahamiana kila mtu na mapungufu yake. Aidha, wanakuwa na chuki binafsi kwa sababu ya kutokelewana kulikokuwepo baina yao kabla ya kuachana na kwa maana hiyo kunakuwepo na kulipiziana visasi. Vile vile Serikali zilizo madarakani ni ni matokeo ya Chama au wamelelewa ndani ya chama kimoja na walishazoea kufanya mambo yao bila kuhojiwa, kwa maana hiyo wapinzani wakihoji Serikali zinaona kama wanawakosea adamu.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.