Vyama vya siasa ni vya msimu-by JK-Sasa Hataki chadema wafanye siasa! Kulikoni?

George Maige Nhigula Jr.

JF-Expert Member
Mar 14, 2008
470
149
Ndugu Wana JF,

Nadhani sote tuna kumbu kumbu njema mda si mrefu mwaka jana wakati wa kampeni za uchaguzi, Mgombea wa CCM JAKAYA MRISHO KIKWETE aliwatangazia watanzania kuwa vyama vya siasa vya upinzani vinafaa kupuuzwa na kuto aminiwa na wananchi kwani ni vya msimu, yaani ni vyama vya uchaguzi tu!

Nadhani wengi wetu tulipinga sana kauli hiyo ya mgombea wa CCM JK na iliyokuwa ikipigiwa tarumbeta na makada wengi kwenye social media mbali mbali kama JF, FB, TWITER etc.

Lakini baada ya uchaguzi kumalizika CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO kimeendelea kufanya shughuli zake za kisiasa kama kawaida kwa hari na vuguvugu jipya la ukombozi kwa kudai katiba mpya na kupambana na ufisadi unaendelea kulitafuna Taifa letu, Lakini tumeshuhudia jinsi serikari ya CCM chini ya JK ikifanya kila mbinu kuhujuma CHADEMA isiweze kufanya siasa na kuendelea kujiimarisha kama chama kikuu cha upinzani bungeni.

Kitendo cha serikari kupiga marufuku mikutano kadhaa ya wabunge wa chadema nchi nzima na kuzuia maandamano ya amani ARUSHA ni dhahiri kabisa ni jitihada za kutaka tamko la JK wakati wa kampeni kutimia yaani vyama vya siasa vya upinzani ni vya msimu.

Tumemsikia mkuu wa kitengo cha propaganda TAMBWE HIZA akisema kuwa uchaguzi umekwisha chadema hawapaswi kufanya siasa, Je hii ina maana gani?

Ni ukweli usiopingika kuwa CHADEMA kimechukua nafasi yake kama chama kikuu cha upinzani Tanzania kwa ufanisi mkubwa na kimekuwa mstari wa mbele kupigania haki za wananchi na kuwaumbua watawala kiasi kwamba hali ya CCM ni taabani kutokana na kibano cha chadema. Hivyo mimi binafsi napenda kumwambia Raisi Jakaya Kikwete kuwa inawezekana kuna vyama vya upinzani ni vya msimu yaani wakati wa uchaguzi lakini sio chadema, kwani kibano wanachokupa nadhani unakuwa na wakati mgumu sana,

Sasa ni mda wako JK to show leadership kwani CHADEMA ni mwendo mdundo mpaka 2015
 
they didn't expect what they see now! and Tambwe political death is soon to come.

Kum discredit Tambwe inabidi uwathibitishie watanzania kuwa alipohamia CCM alilala na mama yake kwanza? kama jibu ni hapana basi ni mtu asie aminika hata kidogo kwa kauli zake za hovyo
 
Achana na fikra za kikwete mkuu huyo ndo anaizika CCM.
Ile laana ya baba wa taifa aliyoacha ikulu ya kutokuwepo kwa lowasa na kikwete kwenye madaraka makubwa ya nchi ndo inawatafuna.
HUYO NDO KABURI LA CCM.
 
Ndugu Wana JF,

Nadhani sote tuna kumbu kumbu njema mda si mrefu mwaka jana wakati wa kampeni za uchaguzi, Mgombea wa CCM JAKAYA MRISHO KIKWETE aliwatangazia watanzania kuwa vyama vya siasa vya upinzani vinafaa kupuuzwa na kuto aminiwa na wananchi kwani ni vya msimu, yaani ni vyama vya uchaguzi tu!

Nadhani wengi wetu tulipinga sana kauli hiyo ya mgombea wa CCM JK na iliyokuwa ikipigiwa tarumbeta na makada wengi kwenye social media mbali mbali kama JF, FB, TWITER etc.

Lakini baada ya uchaguzi kumalizika CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO kimeendelea kufanya shughuli zake za kisiasa kama kawaida kwa hari na vuguvugu jipya la ukombozi kwa kudai katiba mpya na kupambana na ufisadi unaendelea kulitafuna Taifa letu, Lakini tumeshuhudia jinsi serikari ya CCM chini ya JK ikifanya kila mbinu kuhujuma CHADEMA isiweze kufanya siasa na kuendelea kujiimarisha kama chama kikuu cha upinzani bungeni.

Kitendo cha serikari kupiga marufuku mikutano kadhaa ya wabunge wa chadema nchi nzima na kuzuia maandamano ya amani ARUSHA ni dhahiri kabisa ni jitihada za kutaka tamko la JK wakati wa kampeni kutimia yaani vyama vya siasa vya upinzani ni vya msimu.

Tumemsikia mkuu wa kitengo cha propaganda TAMBWE HIZA akisema kuwa uchaguzi umekwisha chadema hawapaswi kufanya siasa, Je hii ina maana gani?

Ni ukweli usiopingika kuwa CHADEMA kimechukua nafasi yake kama chama kikuu cha upinzani Tanzania kwa ufanisi mkubwa na kimekuwa mstari wa mbele kupigania haki za wananchi na kuwaumbua watawala kiasi kwamba hali ya CCM ni taabani kutokana na kibano cha chadema. Hivyo mimi binafsi napenda kumwambia Raisi Jakaya Kikwete kuwa inawezekana kuna vyama vya upinzani ni vya msimu yaani wakati wa uchaguzi lakini sio chadema, kwani kibano wanachokupa nadhani unakuwa na wakati mgumu sana,

Sasa ni mda wako JK to show leadership kwani CHADEMA ni mwendo mdundo mpaka 2015

Leo wakati nimekaa nikawa nawaza nirushe jiwe gani kwa magamba nikafikiria ana juu ya kauli aliyowahi kuitoa jamaa mmoja aliye wahi kuhongwa suti kisha akawapatia eneo waliomhonga suti lakini kabda sija ianzisha nikagoogle daa kumbe ipo banaaaaaaaa.....Kikwete upo chezea chadema wewe.....
 
sema baba hawakufaham kama CHADEMA is the STRONGEST PARTY IN TANZANIA AND AFRICAN CONTINENT.

No mkuu! Suala si chadema! Suala ni PEOPLES POWER!
Utakumbuka vema matumaini ya watanzania wakati wanampa kikwete (kijana) nchi ni kuwa atawashughulikia akina mramba, mkapa n.k. waliotajwa kwa ufisadi wakati huo.
Hakuweza, akasilimishwa DHAIFU.
Matumaini ya uongo ya maisha bora kwa kila mtanzania yametufanya tumchukie na kumwona msaliti, huku akihamia airport.
Uhuni wake wa kubaka demokrasia kwa kutesa na kuua kwa kutumia jeshi ndivyo vinavyompeleka katika kaburi la sahau milele!
Vitendo vyote hivi vitalipwa tu, na yeye mwenyewe, ama akina ridhi, ama wajukuu wake. TIME WILL TELL!
 
Alilopoka tu, hakumanisha kihivyo kama wananfunzi wanapata mimba ni vihelehele vyao, ukitaka cheo lazima na wewe ukubali kuliwa, sijui kwa nini tanzania ni maskini, maisha bora kwa kila mtanzania inawezekana, ni kulopoka tu asamahewe; hata kuna watanzania wengine walopokaji kama yeye ila wao sio marais.
 
Kum discredit Tambwe inabidi uwathibitishie watanzania kuwa alipohamia CCM alilala na mama yake kwanza? kama jibu ni hapana basi ni mtu asie aminika hata kidogo kwa kauli zake za hovyo

CDM haina msimu bado watapata wazimu waache wapigiane simu polisi kuwalazimu wameleta uhasimu hadi kunyweshana sumu sera zao za urasimu Savimbi ajiheshimu. Tumechoka. 'Ccm hatuitaki tena!!!'
 
kuna kauli za viongozi wa nchi hii ukizifatilia utajiuliza mara 100 huyu ni kiongozi wa kitaifa au nikiongozi wa machizi..
 
Back
Top Bottom