Sijaona bado yeyote aliyekataa kuwa vyama vya upinzani visikosolewe. Kumbuka hapa hii ni forum na watu wanachangia mawazo yao na kujibu hoja kwa hoja. Mtu akitoa hoja hapa inakubaliwa au kupingwa accordingly.
Mtu akileta hoja kwa kuna vyama feki basi anapewa to the face swali la kwa nini anafikiri kuna vyama feki na kisha anapewa vyama vyote ambavyo ni feki. Kama ulifikiri hii ni kuzuia vyama kukosolewa basi inabidi wewe ufanyiwe uchunguzi wa huo upeo wako "mkubwa"
MWK
Unajua kuwa ile taskforce ya BOT inachunguza how to act on kipengele cha EPA...
Hivi ile ripot ya Ernst & Young inahusu EPA pekee??? kuna uhalifu wa kimaadili wa kila aina ktk ripoti ile...
Pia hawa hawa CCM wanajua sana kulindana ktk ufujaji. Naomba ushahidi kuwa kuna mrejesho wowote wa fungu lisilotumika ktk bajeti zilizopita. Na utakuta miradi mingi waliyoipanga wao wenyewe haifanyiki na hela hairudi...
Kwa vyama-shindani hiki ndicho kipindi pekee cha kujijenga kwa uchaguzi ujao... INAWEZEKANA labda wakuu wa majeshi waape kama walivyoapa wa Zimbabwe
MWFK, Msanii, na wengine...
Chama Cha Mapinduzi nakichukia kuzidi shetani mwenyewe.
Lakini naomba kuuliza hili: mnadhani ni chama gani kinaweza kuleta mabadiliko?
Ha ha ha ...wewe kama kawaida yako na upeo wako unaishia kwa
Mwafrika wa kike,mimi huwa sipendi unafiki na unazi wa kijinga.Penye kusifia nitasifia hata kama simpendi ninayemsifia na Penye kukosoa nitakosoa hata kama nampenda ninayemkosoa.
Wewe kama unayaona hayo maoni yangu ni ya kifisadi ni hiyari yako na sikulazimishi uyakubali.Lakini ukweli ni kuwa watanzania walio wengi hasa wa vijijini bado wana imani na ccm kuliko upinzani.Kwanini?nikisema mimi utaniita fisadi,labda ukipata muda ujaribu mwenyewe kufuatilia hili.Sasa wakitokea watu wa kuyasema haya kwa faida ya upinzani ili wapange mikakati mizuri ya kwenda kuchukua kura nyingi kule vijijini,wewe unawaita mafisadi.
Unaweza kunionyesha mahali kwenye katiba au ilani ya ccm panaposema kuwa sera ya ccm ni ufisadi?
Chama hakiwezi kutoka mbinguni hata siku moja.Chama lazima kitoke tanzania na kitengenezwe na watanzania.Kitapatikana,mimi bado nina imani hiyo.Lakini kwa sasa bado hakipo.
Sasa kama hiyo altarnative haipo nitailazimishaje?maanake mimi bado sijaiona hiyo alternative unayoing'ang'aniza hapa. Mimi sizumgumzii uzuri wa website ya chama.Nazungumzia umakini wa chama.Na umakini unaweza kuonekana hata katika vitu vidogo kabisa.Kwa mfano ile website ya richmond aliyotuonyesha siku zile Mwakyembe.Yaani ukiangalia ilivyo tu unagundua kabisa hawa watu wana walakini.Sasa unaweza kulinganisha na ule mfano mwingine hapa.
Wenzako wanakwepa kujadili suala la watanzania ambao hawana madawa hospitali wala maji safi, barabara za kueleweka, nishati, bei za juu za vyakula na mengine mengi tu ambayo vijisenti ccm na viongozi walivyokwiba vingeweza kugharimia na jinsi ambavyo ccm imeshindwa kurekebisha hilo au jinsi inavyohusika moja kwa moja na hili.
So wameamua kujadili websites ambazo ziko kwenye matengenezo kuwa eti ndio sign za ufeki wa vyama.
Hivi mwenye mcho ataammbiwa tazama?? Kwanza chaguzi za ndani za ccm ni zengwe kuliko la mlingotini...
Rushwa, kuchafuana hata muda mwingine hutishia uhai wa watu... kisa? MADARAKA
Hawa ccm watatawala mpaka watakapoondolewa kwa kura zetu kwani kuongoza waliacha zamani sana....
ABC.... Any-party But CCM.
Unajua hapa Marekani, watu wengi hawategemei kuwa Democrats ni tough enough kwenye masuala ya security. Lakini ukiangalia exit polls za uchaguzi wa mwaka 2006, wananchi walisema anything but republicans na democrats wakachukua house na senate.
Kuna wakati ambapo chama kinakaa kwenye uongozi muda mrefu na kinadhani kuwa kinaweza kufanya chochote kile. Kwa sasa kwangu mimi any-party but ccm ni sera yangu.
\Ahsante, Mwafrika wa Kike.
Na na mimi mara nyingi najisikia kutapika neno 'Sisiemu' likitajwa. Natamani nijichimbia ardhini mpaka nisikie CCM imeondoka juu ya uso wa dunia ndo niibuke tena duniani kama Michael Jackson kwenye filamu ya Threaller!
Lakini naomba kupata wazo lako jingine kuhusu sera inayosema "chochote ila CCM."
Ni sahihi nikitafsiri kwamba sera yako inasema "upinzani unafaa kwa sababu CCM haifai"?
Una hakika kuwa hupendi unafiki na unazi wa kijinga?
Huwa natenda ninalohubiri.Afterall kigumu kiko wapi?Kwani wewe mwkike huwezi kuishi bila unafiki na unazi wa kijinga?
Unaongelea vijiji gani hapa, vya pemba, tarime, kigoma au vya wapi?
Hayo ya pemba yaache kabisa.siasa za zanzibar zina historia yake hivyo ni tofauti kabisa na za bara.Na wenyewe idadi yao ni ndogo sana kuwafanya ccm bara wakose ushindi.Kwahiyo ushindi wa wapemba usikufariji sana.
Vitendo vinaongea zaidi kuliko maneno.
Nilishasema kuwa matendo ni suala la mtu mmoja mmoja na si la kila mwanachama.Mbona hutaki kuelewa hapa?
Nilidhani labda kuna sehemu kwenye katiba ya ccm inayosema ufisadi ni sera.Hapa ningethibitisha kwamba wanachama wote wa ccm ni mafisadi maana katiba yao inasema ufisadi ndiyo sera yao.
na hao watanzania wewe ni miongoni mwao, je umeanzisha chama karibuni?
Sina uwezo wa kuanzisha chama cha siasa.
Hiyo siku inakuja na si mbali sana.. jitihada zinazofanyika hapa na msaada wote tunaopata kwa wenye magazeti nyumbani na ambao wanaandika uozo wa ccm day after day wanasaidia kuelemisha watanzania taratibu.
Kwa kadri mafisadi wanavyoishiwa hapa JF na kubaki kuweka viroja, wataishiwa hata huko nyumbani one of these days. Malalamiko na vilio vya watoto wachanga vinamfikia MUNGU na kuna siku ataamua kukomesha ufisadi wa ccm.
Hiyo siku inakuja na haiko mbali!....
Huwa natenda ninalohubiri.Afterall kigumu kiko wapi?Kwani wewe mwkike huwezi kuishi bila unafiki na unazi wa kijinga?
Hayo ya pemba yaache kabisa.siasa za zanzibar zina historia yake hivyo ni tofauti kabisa na za bara.Na wenyewe idadi yao ni ndogo sana kuwafanya ccm bara wakose ushindi.Kwahiyo ushindi wa wapemba usikufariji sana.
Nilishasema kuwa matendo ni suala la mtu mmoja mmoja na si la kila mwanachama.Mbona hutaki kuelewa hapa? Nilidhani labda kuna sehemu kwenye katiba ya ccm inayosema ufisadi ni sera.Hapa ningethibitisha kwamba wanachama wote wa ccm ni mafisadi maana katiba yao inasema ufisadi ndiyo sera yao.
Sina uwezo wa kuanzisha chama cha siasa.
Mungu achagui anawaona mafisadi wote, wa ccm, chadema nk.
kusaini mkataba mbovu wa Buzwagi, Richmonduli, wizi BoT, Kiwira, IPTL, Bulyanhulu, na kununua rada feki, ndege ya bei ya kutupwa, na kupelekea ukosefu wa huduma muhimu nchini kwa watanzania - wana ccm
Especially mafisadi waliiofanya yafuatayo
Hilo ni swali ambalo una jibu lake kwa vile wewe ndio umeleta hapa maneno hayo - unazi wa kijinga
Naamini ujumbe umefika barabara!
Ukishaanza kutenganisha sehemu fulani na kuzihesabu kuwa sio sehemu ya Tanzania au kuwa sio vijijini basi unarudi pale kwenye suala la upeo wako wa kuelewa!
Wewe ndiye mwenye upeo finyu wa kuelewa.Wapi nilipoitenganisha pemba na kusema siyo sehemu ya tanzania?Kusema kwamba zanzibar ina historia tofauti na bara ndiyo kuitenga?
Rudi tena usome statements zako maana inaonekana short memory yako ina matatizo kidogo.
statements zangu zote zinafanana na wala hazijipingi.Nashindwa kuelewa una matatizo gani kichwani yanayokufanya usizielewe.
Kama huna uwezo wa kuanzisha chama then unategemea nani akuanzishie huyo mwenye uwezo wa kuanzisha vyama?
Na mafisadi waliokabidhi uongozi wa chama kwa wakwe zao?
na ulikuta nini kuhusu Buzwagi, Richmonduli, wizi BoT, Kiwira, Bulyanhulu, rada feki, ndege ya bei ya kutupwa, na ukosefu wa huduma muhimu nchini?
Kuwa na uwezo wa kuanzisha chama isiwe sababu ya kutuletea vyama chungu nzima visivyo na kichwa wala miguu vilivyojaa wababaishaji,waganga njaa,wanafiki,mamluki nk nk
kusaini mkataba mbovu wa Buzwagi, Richmonduli, wizi BoT, Kiwira, IPTL, Bulyanhulu, na kununua rada feki, ndege ya bei ya kutupwa, na kupelekea ukosefu wa huduma muhimu nchini kwa watanzania - wana ccm