FairPlayer
JF-Expert Member
- Feb 27, 2006
- 4,145
- 716
Wakuu,
Siku nyingi sijawahi kuanzisha topic humu.
Nimekua nikifuatilia kwa makini vurugu za hivi karibuni, nikajaribu kuzifikiria kwa mapana na marefu.
Ninachoweza kusema ni kuwa Serikali yetu imefeli kwenye USALAMA na AJIRA. Nitaelezea kidogo hapo chini.
Kuna kiongozi aliwahi kusema ukosefu wa ajira kwa vijana ni a TIME BOMB. Watu tukabeza...
Naelezea, Timing ya Mtoto alietenda kosa Mbagala na vurugu ni vitu viwili vya kufikiriwa.
Vijana hawana ajira, anasikia kuna kufanya vurugu sehemu akiangalia hana BUKU mfukoni anafanyaje?, anaenda kubahatisha huko kwenye vurugu angalau anaweza kupata hata Buku (shs elfu moja).
Kumbe basi vurugu, maandamano mengi ni "AJIRA" kwa hawa vijana! mie nafikiria hivyo. Haiingii akilini mtu yupo BIZE na shughuli zake halafu umuondoe eti akaandamane tena akavunje amani?, labda uwe na akili ndogo kama yangu ndo utasema uende.
UAMSHO Zanzibar. Hainiingii akilini kwakweli kua serikali imeshindwa kudhibiti hili GENGE. Ukiangalia kwa makini utagundia kuwa hiki kikundi hakikuanza leo. Kilikuwepo kabla. Ni nini basi kinachochea haya mambo?. Kwa hakika ni PESA. Uhamsho wanapata RUZUKU. Hili msiniambie UWT (TISS) hawajui, hawa jamaa wanafadhiliwa kufanya haya wanayofanya. Nani anawafadhili? mbona simpo, hata gari analotumia kiongozi wao kasema kasaidiwa atumie..... Of coz tunahitaji CIA kuja kugundua wafadhili wao.
Vurugu zote zinazotumia UDINI ni Hatari kama vurugu zote zitumiazo UKABILA. Lazima tuzipinge kwa nguvu zote.
Siamini kua mifano tulionayo tumeisahau... siamini kua kuna TISS au intelijensia ya Polisi haioni haya.
Ila Serikali ikiweka mambo sawa na maisha bora kwa kila mtanzania ambayo tuliwahidi hawa watu mwaka 2005 basi hizi vurugu zitatokomea. Na wafadhili wa hizi vurugu wakitembelewa na TRA mara kwa mara watatulia. Hela wanaiba serikalini (kutolipa kodi) kisha wanazipeleka kuishambulia same govt.
AU KUNA WANAOFAIDIKA NA HIZI VURUGU SERIKALINI??
Mrisho Mpoto: Chocheeni kuni mbichi moto ukolee.....
Ni hayo tu
Fairplayer
Siku nyingi sijawahi kuanzisha topic humu.
Nimekua nikifuatilia kwa makini vurugu za hivi karibuni, nikajaribu kuzifikiria kwa mapana na marefu.
Ninachoweza kusema ni kuwa Serikali yetu imefeli kwenye USALAMA na AJIRA. Nitaelezea kidogo hapo chini.
Kuna kiongozi aliwahi kusema ukosefu wa ajira kwa vijana ni a TIME BOMB. Watu tukabeza...
Naelezea, Timing ya Mtoto alietenda kosa Mbagala na vurugu ni vitu viwili vya kufikiriwa.
Vijana hawana ajira, anasikia kuna kufanya vurugu sehemu akiangalia hana BUKU mfukoni anafanyaje?, anaenda kubahatisha huko kwenye vurugu angalau anaweza kupata hata Buku (shs elfu moja).
Kumbe basi vurugu, maandamano mengi ni "AJIRA" kwa hawa vijana! mie nafikiria hivyo. Haiingii akilini mtu yupo BIZE na shughuli zake halafu umuondoe eti akaandamane tena akavunje amani?, labda uwe na akili ndogo kama yangu ndo utasema uende.
UAMSHO Zanzibar. Hainiingii akilini kwakweli kua serikali imeshindwa kudhibiti hili GENGE. Ukiangalia kwa makini utagundia kuwa hiki kikundi hakikuanza leo. Kilikuwepo kabla. Ni nini basi kinachochea haya mambo?. Kwa hakika ni PESA. Uhamsho wanapata RUZUKU. Hili msiniambie UWT (TISS) hawajui, hawa jamaa wanafadhiliwa kufanya haya wanayofanya. Nani anawafadhili? mbona simpo, hata gari analotumia kiongozi wao kasema kasaidiwa atumie..... Of coz tunahitaji CIA kuja kugundua wafadhili wao.
Vurugu zote zinazotumia UDINI ni Hatari kama vurugu zote zitumiazo UKABILA. Lazima tuzipinge kwa nguvu zote.
Siamini kua mifano tulionayo tumeisahau... siamini kua kuna TISS au intelijensia ya Polisi haioni haya.
Ila Serikali ikiweka mambo sawa na maisha bora kwa kila mtanzania ambayo tuliwahidi hawa watu mwaka 2005 basi hizi vurugu zitatokomea. Na wafadhili wa hizi vurugu wakitembelewa na TRA mara kwa mara watatulia. Hela wanaiba serikalini (kutolipa kodi) kisha wanazipeleka kuishambulia same govt.
AU KUNA WANAOFAIDIKA NA HIZI VURUGU SERIKALINI??
Mrisho Mpoto: Chocheeni kuni mbichi moto ukolee.....
Ni hayo tu
Fairplayer